Yu wapi Mganga Mkuu wa jiji? Matamko ya Makonda ni hatari

Rufiji dam

JF-Expert Member
Feb 20, 2020
3,803
8,786
Mkuu wa jiji la Dar es Salaam anatakiwa kupewa onyo anatakiwa akaripiwe. Huyu Makonda hana elimu ya afya. Makonda anatoa matamko hatarishi sana juu ya ugonjwa wa Korona.

Anakurupuka sana, analeta hofu. Anajenga hatari zaidi ya hatari yenyewe. Huyu afungwe speed gavana. Yupo wapi mganga mkuu wa jiji?

Nimemsikiliza Naibu Waziri wa Afya juu ya Barakoa ya kuwa leso haifai kabisa kuvaliwa kama Barakoa. Kitenge ama Khanga hazifai kuzibia pua zetu lakini Makonda kashauri zitumike Waziri Mkuu Majaliwa toa tamko.

Kuna kipindi alikusanya watu akitoa hotuba kwa vijana juu ya ugonjwa huu je hakujua kama mkusanyiko nao ni chanzo cha kukwaa gonjwa hili.

Barakoa inatakiwa kuvaliwa saa nne tu kisha unabadilisha sasa kwa bei ya Tshs. 3000 × 4= Tshs 12,000 kwa siku moja. Kwanini kusiwe na tamko la kulizima jiji la Dar es Salaam kwa wiki mbili!

Anakuja na hoja ya kufanya biashara kwa mfumo wa take away. Sijui anajua mfumo wa biashara upo vipi hasa kwa wachuuzi makasha ya kufungia bidhaa anajua yanauzwa kiasi gani? Huyu mtu anatakiwa kuonywa na kupewa elimu ya bure kuhusu madhara ya kukurupuka.

Msaada wa yule Mchina upo wapi, kwanini wanashindwa kusambaza masks bure kwa kila mkazi hasa wa jiji la Dar es Salaam kwa sababu uongozi wote wa serikali za kata na serikali za mitaa upo chini ya uongozi wa CCM.

MAKONDA AJARIBU KUWA NA UELEWA KATIKA MATAMKO YAKE HASA KIPINDI CHA UGONJWA HATARI. HII TAALUMA YA WATU SIO SIASA HIZI.
 
Yaani sisi sijuinani alituroga....tunashudia maelfu wanakufa lakini badala yake tunaendelea na ujinga...hivi katika hatari kama hii ..mpaka Sasa tunayumbishws kuhusu uvaaji wa Mask
Hivi Wizara husika inashindwa nini kuwa Firm katika Hili,au Viongozi mmeshaambiwa nani takufa na nyie hampo kwenye orodha!?Ingekuwa tupo kijiweni ningetusi .....k'n..
 
Mkuu huyo naibu waziri ndo kakurupuka kukwamisha jitihada mbalimbali za kuepusha kuenea kwa korona, mask za vitambaa bado zina msaada mkubwa kutokana na bei yake kuwa affordable kwa wengi na uwezekano wa kuitumia mara nyingi zaidi kuliko mask za N95 ambazo utatakiwa ubadilishe karibia kila siku. Ujerumani kwenyewe watu wameambiwa wanaweza kuzitumia hizo za vitambaa. Kwenye hili swala la korona kila mtu anataka aonekane mjuaji kuliko mwenzake na mwisho tunaishia kupotosha watu na kuendeleza maambukizi zaidi.....Rais aanze kuwamulika hawa wasaidizi wake wanaweza kusababisha hali ikawa mbaya zaidi kwa hizi kiki zao wanazotafuta...
 
Nilikuwa naangalia taarifa ya hbr hapa CGTN , RC anatoa maagizo ya uvaaji wa mask alafu hata yeye hajavaa. Wakati flani alisisitiza watu waondoke wakafanye kazi wala wasiogope kwamba korona ni ugonjwa mdogo, baadaye akawa anakusanya watu anawafundisha waepuke mikusanyiko, sasa anafundisha watu wavae mask. Kweli nchi yetu inafeli sana kukabiliana na hili janga, hatuna muongozo maalumu wa kukabiliana na janga, kuna wakati wataalam wetu wa afya walishauri watu wasivae mask na pia kuna utaratibu wa kuvaa mask sio kuvaa vaa tu mfano mask moja inavaliwa kwa masaa 4 tu, waziri mweny zamana amejikatia tamaa kwa kauli zake za karibuni, sasa hivi anasubiri tu watu wajipeleke wenyewe hata body temperature tu tunashindwa kufanya kweny maeneo kama stand za mabasi, sokoni nk. Ninachoshauri, ni vema ndugu mwananchi uchukue hatua mwenyewe, ukisubiri hawa viongozi huenda wakakumbuka kufuata misingi sahihi ya kujikinga na ugonjwa wakati hali imekuwa mbaya.
 
Mkuu huyo naibu waziri ndo kakurupuka kukwamisha jitihada mbalimbali za kuepusha kuenea kwa korona, mask za vitambaa bado zina msaada mkubwa kutokana na bei yake kuwa affordable kwa wengi na uwezekano wa kuitumia mara nyingi zaidi kuliko mask za N95 ambazo utatakiwa ubadilishe karibia kila siku. Ujerumani kwenyewe watu wameambiwa wanaweza kuzitumia hizo za vitambaa. Kwenye hili swala la korona kila mtu anataka aonekane mjuaji kuliko mwenzake na mwisho tunaishia kupotosha watu na kuendeleza maambukizi zaidi.....Rais aanze kuwamulika hawa wasaidizi wake wanaweza kusababisha hali ikawa mbaya zaidi kwa hizi kiki zao wanazotafuta...
Bwashee hata Marekani wameruhusiwa kutumia za vitambaa!
 
Back
Top Bottom