Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
lamwai ni dean wa kitivo cha Law pale tumaini, pia ni mwanasheria wa chama tawala. Juzi juzi nilipishana nae anaendesha gari huku anakula, (yuko busy!)
Hapana!Poa sasa nimefahamu, lakini hawa jamaa sometimes wanatuchezea akili, siamini jinsi alivyokuwa anaikandia CCM, ati leo hii naye kesha kuwa mwanasheria wao. Kweli siasa ni MCHEZO MCHAFU!
Mbona Lamwai amekuwa maarufu hata kabla ajachaguliwa Diwani wa Manzese, Kwenye Corridor za Mahakama za Tanzania jina lake si Dogo, Ni Mwalimu mzuri wa Sheria, kwamba UKIMWI unamtaiti, sina uhakika sana na hilo, mara nyingi nimetokea kufanya naye kazi kwa karibu sijaona tofauti ya Afya yake. Naona yuko fit.Kila mtu anahitaji kuombewa aliye na ........., na asiye na .............., unless kama mtu ameamua kuwa Towashi , vinginevyo huwezi kujua kesho yako.Mwaka 1994 akiwa NCCR Mageuzi tulimchagua kuwa Diwani kata ya Manzese, na hapo ndipo alianza kujulikana zaidi mitaani. Mwaka 1995 akiwa aligombea ubunge jimbo la Ubungo na alikuwa ameshinda pamoja na wenzake wa NCCR katika majimbo yote ya DSM lakini uchaguzi huo ulifutwa saa nane ya usiku baada ya tume kuona kuwa dsm yote imechukuliwa na upinzani.
Kwa kuwa NCCR haikuridhika na uchaguzi tanzania nzima, iliamua kujitoa, ila kisheria haikuwezekana. Wagombea wengine wote wa NCCR walitangaza kususia uchaguzi wa marudio dsm, lakini Lamwai alikataa na kushiriki; na tulimchagua kuwa mbunge wa jimbo la ubungo. Matokeo hayo yalipingwa mahakamani na Lamwai akashindwa kesi; na huo ukawa mwanzo wa mporomoko wake.
Baada ya hapo alifutiwa ualimu wa udsm na pia serikali ilimfutia leseni yake ya uwakili wa kujitegemea. Lamwai akadhoofu na akawa hana budi kujisalimisha kwa CCM. Ndipo Mkapa alimteua kuwa mbunge.
Kitendo cha Lamwai kurudi CCM na kuteuliwa na mkapa, kilimshushia heshima katika jamii - kama mchangiaji mmoja alivyosema 'siamini kama mtu aliyekuwa anaikandia sana ccm angeweza kurudi huko'. Wengi tulimwona kama mtu aliyekosa uvumilivu na ujasiri wa kundelea kuwa upinzani - alitusaliti. Kwa kuwa JK hakumteua tena kuwa mbunge; ikawa ndio mwisho wake katika siasa. Hana tofauti na Kabourou wa Kigoma
Katika wanasheria walioingia kwenye siasa mimi namkubali aliyekuwa katibu mkuu wa CHADEMA jaji mstaafu BOB MAKANI, jamaa ni noma!!!
nakumbuka wakati wa kesi ya uchaguzi CHADEMA vs CCM, mwaka 1995 kule Kigoma, jamaa aliwapelekesha puta majaji kinoma, hatimaye CHADEMA wakashinda ile kesi. Jamaa ana sauti nzito halafu anaongea kama anahasira halafu ana accent ya kisukuma hivi, du! ilikuwa burudani ya aina yake.