Youtube na mtandao: Tanzania is more than bongo flava...

paesulta

JF-Expert Member
Mar 13, 2009
227
29
Nilikuwa naperuzi peruzi ndani ya youtube na nikagundua kuwa unapofanya search ya tanzania kikubwa utakachopata katika youtube ni bongo flavas na video za watu binafsi ambazo zinahusiana na utalii,nikimaanisha kuwa watu katika kutembelea kwao mbuga za wanyama basi walichukua baadhi ya video na kuziweka katika youtube.

hakuna official videos zozote ambazo kwa kweli zinatuonyesha kuwa watu serious.hata ukisearch kikwete unachopata ni videos ambazo zimewekwa na watu wa nje na sio watanzania hasa anapokuwa kwenye mikutano ya kimataifa.

Its really a shame kwamba katika kipindi hiki ambapo tunajidai kuwa tunataka kuwa mstari wa mbele kwenye utalii tunashindwa kutumia nafasi hii ya kujitangaza kwa bure kabisa kwa kutumia njia ambayo ni rahisi na ya bure kama mtandao wa youtube.

Idara ya utalii wangeweza kutumia njia hii kwa kujinufaisha na kufikia watu wengi dunia nzima,kwani kama tunavyojua kwa dunia ya sasa kitu cha kwanza mtu anachofanya anaposikia kitu ni kwenda kugoogle, badala ya kupoteza mamilioni ya fedha kwenda kutangaza nchi kupitia kwenye mabasi ya London tumeshindwa kuweka official video ya promortion ya nchi mtandaoni hasa katika youtube amabayo tunajua kuwa mamilioni ya watu wanatembelea kila siku.

Tulichoishia kufanya ni bongo flavas tu. I mean don't get me wrong, i love bongo flava, but we're more than that.kwa wenzetu wakenya unaweza kufuatilaia habari zakila siku zinazorushwa na vituo vya televisoin kwa kutembelea youtube kwani karibu vituo vyote vya tv vya Kenya vina ukurasa wao hapa na kila siku wanaweka video za habari zao kila siku.huwezi kupata hata habari moja si ya ITV wala TBC au kituo chochote cha Bongo mtandaoni, tumebaki kulala tu.

It's time that we wake up.......
 
Hii ndio Bongo mkuu, ninafurahi sana ukitaka habari latest za kenya ukienda Youtube unapata habari on time hii inanifurahisha sana,sijui ni nini kilichotushinda sisi wabongo.
 
Hii ndio Bongo mkuu, ninafurahi sana ukitaka habari latest za kenya ukienda Youtube unapata habari on time hii inanifurahisha sana,sijui ni nini kilichotushinda sisi wabongo.

Kinachotushinda ni kwamba kila mtu anagojea serikali na the next person afanye hiki na kile, na usually watu wanaongojea serikali na the next person wafanye this and that ndio wa kwanza kulalamika, na wa mwisho ku act.

Kwa hiyo kama limekuuma, do not be a part of the problem, be a part of the solution.
 
....kinachonishangaza ni kuwa je wahusika wa vituo vya Tv wameshindwa hata ku-assign mtu mmoja awe anamake sure kwamba habari ya siku inawekwa mtandaoni?
lakini sishangai,ni muda gani umepita tangu TBC ianzishwe na mpaka leo ukiingia mtandaoni bado wapo on construction......!?
Inatia hasira sana kwa kweli.....
 
.......... tunashindwa kutumia fulsa hii ya kutumia mtandao ambayo ni njia rahisi sana ya kujitangaza kimataifa.mfano mwingine tembelea eastafricantube,huko nako tumejaza video za mapuka,bongo flava pekee.mtandao kwetu sisi umekuwa ni sehemu ya burudani tu na si vinginevyo...

utaniambia kuwa kuna website nyingi tu za kuitangaza Tanzania nje ya youtube,lakini jaribu kutembelea website zetu nyingi,kwa kweli hazijitoshelezi na haziko kamili kwa namana yeyote ile.mara nyingi hata update hazifanyiki,wahusika wanaianzisha na baada ya hapo ndio wanasahau kabisa.

Tuamke na tujaribu ku-exploit hii opportunity ya mtandao kwa manufaa ya nchi yetu.Hongera kwa wadau wote ambao wameanzisha blog mbalimbali ingawa nyingi zinafanana katika contents na nyingi zinachukua contests za nyingine,lakini wamefungua ukurasa mpya wa uapatikanaji habari na matukio ya Tanzania kupitia mtandaoni,kitu ambacho kimeleta ushindani na challenge kwa main stream media za Tanzania kuji-engage katika suala zima la kujitangaza mtandaoni,kwani tunakumbuka kuwa miaka kama miwili hivi ya nyuma ilikuwa ukifungua kurasa zao mtandaoni unapata habari ambazo zina kama mwezi na zidi,inakuwa kama miaka ile sie tuliokulia mikoani,tulikuwa tunapata magazeti toka Dar mara moja au mbili kwa mwezi...

MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Ni kweli kwa mfano video za Youtube nyingi ni za Bongo Fleva na binafsi. za watalii. Ukitaka kujua subscribe kwa Youtube members wa Kitanzania, then wapitie kila baada ya mwezi. Utakuda video walizo-upload ni Bongo Fleva. Ziko NGOs chache zina-upload video za maana kama documentary lakini ni chache na ngumu kuzipata kwenye search.

Pia naona baadhi ya vipindi vya TV zetu wameanza kuweka baadhi ya clips za vipindi vyao, kama Daladala Show (daladalashow's Channel - YouTube) na Mimi na Tanzania (Untanzania's Channel - YouTube)
 
Back
Top Bottom