NEW NOEL
JF-Expert Member
- May 21, 2011
- 863
- 407
Yalianza maneno,kila mtu anamrushia mwenzake,ghafla wakaanza kusukumana...watu hawajakaa sawa,milio ya risasi ikasikika.
Ilikuwa back stage kwenye tuzo maarufu za BET HIPHOP AWARDS zilizokuwa zinafanyika Atlanta ambapo Rozay na Young Jeezy walianza kurushiana maneno na ghafla kusukumana. Tukio hilo la ajabu lilipelekea risasi kusikika na inaelezwa ni mmoja wa watu wa karibu Rick Ross ndio alirusha risasi. Ingawa inaelezwa kuwa kutoweka huko kwa amani kulifanikiwa kutulizwa na watu wa usalama na shughuli nyingine kuendelea kama kawaida.
Ni takribani miaka kama miwili ambapo Young Jeezy na Rick Ross wamekuwa hawaelewani na chanzo kinaelezwa kuwa ni pale Rick Ross alipotoa wimbo wa BMF (Blowing Money Fast) na Young Jeezy kumponda Rick Ross kuwa anaimba asichokijua. Katika wimbo wa BMF rozay anamtaja Big Meech ambaye ni mmoja wa watu wa karibu wa Young Jeezy na kwa sasa yupo jela. Na ndio sababu ya Young Jeezy kumponda Rozay kuimba wimbo unaomuhusu mshikaji wake wa muda mrefu.
Hivi karibuni Rick ross alieleza kuwa yupo tayari kufanya kazi na Young Jeezy na kulikuwa na tetesi ya uwezekano wa wawili hao kufanya kazi ya pamoja.
POPOTE TZ