You heard it!: Somo la rushwa kufundishwa shuleni

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,461
39,928
01.05.2008 1712 EAT

PORIS wapendekeza rushwa ifundishwe shule za msingi nchini (RAI)

SHIRIKA lisilo la kiserikali la African International Group of Political Risk Analysis (PORIS), limependekeza mitaala ya shule za msingi nchini kuhusisha somo la rushwa.

Ushauri huo ulitolewa na washiriki katika semina ya siku mbili iliyofanyika katika Hoteli ya Paradise mjini Bagamoyo wiki hii. Walisema kwa hali ilipofikia ni wazi maadili yamepotea kwa kiwango kikubwa nchini, hivyo wakaomba ikiwezekana elimu ya rushwa ianze kufundishwa kuanzia ngazi ya shule za msingi.

Mbali na shule za msingi, wameomba serikali iangalie uwezekano wa kushirikisha viongozi wa dini zote katika vita dhidi ya rushwa. "Hii iwe ajenda ya kitaifa. Masheikh misikitini wahubiri vita dhidi ya rushwa. Mapadre nao wafanye hivyo altare, wale wa CDA nao wasisite kuhubiri vita dhiti ya rushwa kila Jumamosi. Kwa njia hii pengine masikio yatazibuka," alisema Mkurugenzi Mtendaji wa FiorDIA, Bubelwa Kaiza.

Kaiza alisisitiza kuwa tatizo kubwa linalolikabili taifa hili ni uwezo (capacity) wa watendaji serikalini, wananchi na katika taasisi mbalimbali kwani wengi hawafahamu haki na wajibu wao. Alisema kazi ya kwanza inayopaswa kufanywa ni kujenga mfumo na uwezo kwa wananchi wote, ili kila mmoja ajue haki na wajibu wake na hilo litaondosha mazingira ya rushwa kwa kiwango kikubwa.

Mkurugenzi Mkuu wa PORIS, Prince Bagenda, ilisema ikibidi taifa litafute mahala pa kuazima maadili na mienendo bora kwani katika mfumo wa sasa baadhi ya watu wana nguvu kuliko sheria zilizopo. "Tupo katika mazingira ya hatari. Maafisa wanaingia mikataba na hakuna mtu mwenye uwezo wa kuiona. Hata wabunge hawaruhusiwi kuiona. Hii ni hatari. Wananchi wanapaswa kupata haki ya kuona mikataba hii," alisema Bagenda.

Mwambata wa Ubalozi wa Ubeligji nchini, Herman Boonen, alisema Serikali ya Awamu ya Nne imeanza vizuri hivyo ipewe muda katika vita dhidi ya rushwa. Alisisitiza kuwa kwa nchi yoyote kuendelea katika mapambano dhidi ya rushwa inapaswa kuhakikisha inaimarisha mifumo ya utawala bora na uwajibikaji.

Pia alisema wananchi wanapaswa kushirikishwa katika maamuzi, kupata taarifa zote ndani ya serikali na kuhusika katika maamuzi. Kwake anaona kuwa uwazi una nafasi kubwa ya kusaidia kuondoa vitendo vya rushwa. Ubeligji ndiyo iliyofadhili warsha hiyo.

Mada kuu katika warsha hiyo ilikuwa ni kupitia maazimio ya Brussels ya mwaka 2007 juu ya mapambano dhidi ya rushwa, jukumu la vyombo visivyo vya kiserikali katika mapambano dhidi ya rushwa Tanzania na mada ya mwisho ilikuwa juu ya Jinsia na Rushwa. Pia warsha hiyo ilitumika kuzindua kitabu kilichoandikwa na Bagenda kiitwacho Improving Governance
 
Nyani... hutaki sasa ndugu yangu.. "Rushwa ifundishwe shule za msingi"? Au unataka ianzie sekondari?
 
01.05.2008 1712 EAT

PORIS wapendekeza rushwa ifundishwe shule za msingi nchini (RAI)

SHIRIKA lisilo la kiserikali la African International Group of Political Risk Analysis (PORIS), limependekeza mitaala ya shule za msingi nchini kuhusisha somo la rushwa.

Ushauri huo ulitolewa na washiriki katika semina ya siku mbili iliyofanyika katika Hoteli ya Paradise mjini Bagamoyo wiki hii. Walisema kwa hali ilipofikia ni wazi maadili yamepotea kwa kiwango kikubwa nchini, hivyo wakaomba ikiwezekana elimu ya rushwa ianze kufundishwa kuanzia ngazi ya shule za msingi.

Mbali na shule za msingi, wameomba serikali iangalie uwezekano wa kushirikisha viongozi wa dini zote katika vita dhidi ya rushwa. “Hii iwe ajenda ya kitaifa. Masheikh misikitini wahubiri vita dhidi ya rushwa. Mapadre nao wafanye hivyo altare, wale wa CDA nao wasisite kuhubiri vita dhiti ya rushwa kila Jumamosi. Kwa njia hii pengine masikio yatazibuka,” alisema Mkurugenzi Mtendaji wa FiorDIA, Bubelwa Kaiza.

Kaiza alisisitiza kuwa tatizo kubwa linalolikabili taifa hili ni uwezo (capacity) wa watendaji serikalini, wananchi na katika taasisi mbalimbali kwani wengi hawafahamu haki na wajibu wao. Alisema kazi ya kwanza inayopaswa kufanywa ni kujenga mfumo na uwezo kwa wananchi wote, ili kila mmoja ajue haki na wajibu wake na hilo litaondosha mazingira ya rushwa kwa kiwango kikubwa.

Mkurugenzi Mkuu wa PORIS, Prince Bagenda, ilisema ikibidi taifa litafute mahala pa kuazima maadili na mienendo bora kwani katika mfumo wa sasa baadhi ya watu wana nguvu kuliko sheria zilizopo. “Tupo katika mazingira ya hatari. Maafisa wanaingia mikataba na hakuna mtu mwenye uwezo wa kuiona. Hata wabunge hawaruhusiwi kuiona. Hii ni hatari. Wananchi wanapaswa kupata haki ya kuona mikataba hii,” alisema Bagenda.

Mwambata wa Ubalozi wa Ubeligji nchini, Herman Boonen, alisema Serikali ya Awamu ya Nne imeanza vizuri hivyo ipewe muda katika vita dhidi ya rushwa. Alisisitiza kuwa kwa nchi yoyote kuendelea katika mapambano dhidi ya rushwa inapaswa kuhakikisha inaimarisha mifumo ya utawala bora na uwajibikaji.

Pia alisema wananchi wanapaswa kushirikishwa katika maamuzi, kupata taarifa zote ndani ya serikali na kuhusika katika maamuzi. Kwake anaona kuwa uwazi una nafasi kubwa ya kusaidia kuondoa vitendo vya rushwa. Ubeligji ndiyo iliyofadhili warsha hiyo.

Mada kuu katika warsha hiyo ilikuwa ni kupitia maazimio ya Brussels ya mwaka 2007 juu ya mapambano dhidi ya rushwa, jukumu la vyombo visivyo vya kiserikali katika mapambano dhidi ya rushwa Tanzania na mada ya mwisho ilikuwa juu ya Jinsia na Rushwa. Pia warsha hiyo ilitumika kuzindua kitabu kilichoandikwa na Bagenda kiitwacho Improving Governance

Ni ujuha kufundisha elimu ya MATATIZO badala ya elimu. Badala ya kufundisha MAADILI, unapofundisha rushwa ujue mwisho wa siku unawafundisha watoto kuwa MAFISADI. Hata kama elimu yenyewe ikiwa ni kuhusu mbinu za kukabiliana na RUSHWA. Where on hell have students being taught a subject called corruption or anti of it for that matter? This is what is called kukosa dira na mwelekeo. Next week wanafunzi wafundishwe kuhusu UBAKAJI ili mabinti wasiendelee kubakwa.

Asha
 
Ni muhimu kuifanya hii kama sehemu ya elimu ya uraia.Mitaala ihusishe pia wajibu wa raia (mmojawapo ukiwa kupigana na rushwa) pamoja na haki za raia (mambo ya kupiga na kupigiwa kura, kuwa hold viongozi accountable , haki ya kuwa na habari etc huwezi kumdanganya kwamba "mikataba hii ni siri" mbunge aliyefundishwa tangu shule ya msingi kwamba ana haki ya kupata habari za serikali ).Maswala kama majukumu na mipaka ya vyombo vya dola yataweza kusaidia kupunguza unyanyasaji wa raia, mambo kama elimu ya wajibu wa kulipa kodi na haki ya matunda ya kodi itawafanya wananchi wetu wajue kuibana serikali vizuri ielezee matumizi ya kodi na kama matokeo yake kuifanya serikali kutumia kodi vizuri zaidi.

Kuna mambo mengi zaidi ya rushwa inabidi yafundishwe katika elimu ya uraia.
 
Pundit.. you missed the point my friend... ninakupata..lakini kichwa cha habari kinapotosha sana... ni sawa na kuandika "Rais ataka anyongwe"... Ni utata usio wa lazima.
 
I must admit the presentation is a bit choppy and the headline misleading , hence partly Asha's objection to "watu kufundishwa rushwa" can be attributed rightfully, but which point did I miss?

I thought the headline zeroed in on rushwa but the issue is civic eductaion as the attempt made to elaborat in the article demonstrates. I was doing the same type of expansion which is a dear topic of mine.

Assist please, I have a feeling your mind's eye is more evolved.
 
Si tulikuwaga tunaambiwa rushwa ni adui wa haki....au siku hizi huo msamiati haupo?
 
Si tulikuwaga tunaambiwa rushwa ni adui wa haki....au siku hizi huo msamiati haupo?

Wanaokwambia "Rushwa ni Adui wa Haki" hao hao wengine ndiyo chui kwenye ngozi ya kondoo.Mara nyingine vitu hivi vinakuwa deals, gigz, warsha, talking points na hakuna cha maana kinachotokea.

Action speaks louder than words, kama tunataka kufundisha vijana wetu kuwa rushwa ni adui wa haki, in addition ya madarasa haya inabidi tuchukue hatua za kweli kuwashitaki na kuwahukumu wala rushwa wakubwa ili hata huko madarasani walimu waweze kuwa na mifano.

Siyo mwalimu darasani anaeleza ubaya wa rushwa wakati in the real world tunaona the Chenges, Karamagis and Lowassas of this world wanatanua kichizi.
 
Pundit.. upande mmoja mimi najiuliza hivi wenzetu wanafundisha masomo ya rushwa? Sidhani kama tatizo ni elimu. Nadhani bila hata ya elimu unaweza kutokomeza rushwa; pale utakapoifanya kuwa si ya lazima (when it becomes unnecessary).

NN; rushwa ni adui ya haki lakini haki ya nani? ya mtoa rushwa au mpokea rushwa? Vipi kama rushwa inasaidia kumfanya mtu mwingine aone amepatiwa haki yake..?
 
NN; rushwa ni adui ya haki lakini haki ya nani? ya mtoa rushwa au mpokea rushwa? Vipi kama rushwa inasaidia kumfanya mtu mwingine aone amepatiwa haki yake..?

By definition rushwa ni opposite ya justice.Ukitoa rushwa huwezi kupata justice, kwa mfano utanunua kitu ulichotakiwa kupata bure therefore hautakuwa umetendewa justice.

Rushwa ni adui wa haki.
 
Kuna mambo mengi nyuma ya hili .Utasema uweke Elimu lakini kijijini mtu akifikishwa kwa mjumbe wa nyumba 10 ili atoke lazima aache 200 huko.Je ataweza kuhimili mikiki ile na akumbuke mambo ya shule akubali harassment na vitisho kwa masaa ama afungiwe ? Kuna utata mkubwa wacha nione mwelekeo wa mjadala huu .
 
Pundit.. philosophically you are very right.. but practically... kuna tatizo. Angalia kauli yangu:

Vipi kama rushwa inasaidia kumfanya mtu mwingine aone amepatiwa haki yake..?

Kumbe hapa kuna suala la perception. Kama mimi haki yangu ni kupata leseni. Nikifuata njia za kawaida zilizokubaliwa(SOP) haki yangu inachukua muda mrefu kuipata. Hata hivyo, ninapoamua kutoa chochote "haki" ya leseni ninaipata ndani ya masaa machache. HIvyo basi rushwa kwangu si adui wa haki yangu kwani imenisaidia kupata haki yangu.

Sasa, inakuwa ni adui pale ambapo inatumika kama kikwazo cha mimi kupata haki hiyo au kucheleweshewa haki hiyo. Lakini kama katika fikra zangu naamini kuwa bila ya rushwa siwezi kupata haki utaona kuwa rushwa si adui wa haki kwa mtoa rushwa bali ni sehemu ya mchakato mzima wa kupata haki hiyo.

Even more, rushwa yenyewe si kinyume cha haki(justice)lakini dhulma(injustice)ndiyo. Ni mpaka tuweze kuifanya rushwa ionekane kuwa ni dhulma ndipo uhusiano wake na haki unapoweza kuonekana kama mgawanyiko wa rangikama wa kioo cha prism.
 
Kuna mambo mengi nyuma ya hili .Utasema uweke Elimu lakini kijijini mtu akifikishwa kwa mjumbe wa nyumba 10 ili atoke lazima aache 200 huko.Je ataweza kuhimili mikiki ile na akumbuke mambo ya shule akubali harassment na vitisho kwa masaa ama afungiwe ? Kuna utata mkubwa wacha nione mwelekeo wa mjadala huu .

Hapo ndipo tunakuja kwenye umuhimu wa vyombo vya sheria bora.

Kwanza mjumbe hatakiwi ku act kama detention centre, pili inatakiwa kuwe na sheria bora zinazojulikana na kila mtu, tatu inatakiwa kila mtu awe na easy access ya hizo sheria pamoja na legal representation kiasi kwamba ukiomba 200 hata kama unaomba kwa ndugu yako unajishtukia kama kuna mazingira ya rushwa.

Sisi bado sana, vijijini mgambo wananyanaysa watu na "kukusanya" kodi.Mrema alikuwa hailed as a hero kwa ku mobilize sungusungu!
 
Cha muhimu hapa ni ku enforce sheria. Kila mtu mwenye common sense anajua rushwa ni adui wa haki na ni kinyume na sheria. Utafundisha rushwa hadi level ya PhD. lakini kama hakuna enforcement ya sheria hakuna lolote la maana litakalotokea. Enforcement..enforcement...enforcement!!!!
 
Pundit.. philosophically you are very right.. but practically... kuna tatizo. Angalia kauli yangu:



Kumbe hapa kuna suala la perception. Kama mimi haki yangu ni kupata leseni. Nikifuata njia za kawaida zilizokubaliwa(SOP) haki yangu inachukua muda mrefu kuipata. Hata hivyo, ninapoamua kutoa chochote "haki" ya leseni ninaipata ndani ya masaa machache. HIvyo basi rushwa kwangu si adui wa haki yangu kwani imenisaidia kupata haki yangu.

Sasa, inakuwa ni adui pale ambapo inatumika kama kikwazo cha mimi kupata haki hiyo au kucheleweshewa haki hiyo. Lakini kama katika fikra zangu naamini kuwa bila ya rushwa siwezi kupata haki utaona kuwa rushwa si adui wa haki kwa mtoa rushwa bali ni sehemu ya mchakato mzima wa kupata haki hiyo.

Even more, rushwa yenyewe si kinyume cha haki(justice)lakini dhulma(injustice)ndiyo. Ni mpaka tuweze kuifanya rushwa ionekane kuwa ni dhulma ndipo uhusiano wake na haki unapoweza kuonekana kama mgawanyiko wa rangikama wa kioo cha prism.

Ukichukua glasi uijaze maji, kisha uchukue penseli iliyo ndefu kulko ile glasi ya maji uifanye iingie nusu kwenye maji, pale penseli inapoingia katika chupa ya maji itaonekana kama imepinda kwa sababu hewa, maji na glasi huakisi mwanga tofauti.Kwa hiyo penseli itaonekana kupinda.

Je penseli itakuwa imepinda?

Kuna kitu real na kitu apparent, kitu apparent hakibadilishi kitu real.Ni illusion tu.

Mpumbavu atafurahia kupata leseni yake kwa haraka kwa kutumia rushwa wakati ni haki yake kuwa na process iliyo efficient itakayo guarantee kila mtu kupata leseni yake kwa haraka.A fool parts with his money easily.
 
Pundit.. ndio maana nimesema "perception"... kwani hata penseli kuonekana kuwa imepinda (refraction) katika akili ya mtu inaonekana imepinda. Hiyo perception kwake ni kweli ingawa kifizikia si kweli bali ni kutokana na mwanga kupinda unapopiga maji na hivyo kufanya kilichomo kionekane hakipo pale kinapodhaniwa kipo. (of course you know that part very well my dear Pundit)

Hivyo, rushwa inaonekana kuwezesha haki kupatikana ni ukweli wa perception ingawa kihalisia sivyo. Lakini haiondoi ukweli kuwa baadhi ya watu wana perceive it as such.
 
01.05.2008 1712 EAT

PORIS wapendekeza rushwa ifundishwe shule za msingi nchini (RAI)

SHIRIKA lisilo la kiserikali la African International Group of Political Risk Analysis (PORIS), limependekeza mitaala ya shule za msingi nchini kuhusisha somo la rushwa.

Ushauri huo ulitolewa na washiriki katika semina ya siku mbili iliyofanyika katika Hoteli ya Paradise mjini Bagamoyo wiki hii. Walisema kwa hali ilipofikia ni wazi maadili yamepotea kwa kiwango kikubwa nchini, hivyo wakaomba ikiwezekana elimu ya rushwa ianze kufundishwa kuanzia ngazi ya shule za msingi.

Mbali na shule za msingi, wameomba serikali iangalie uwezekano wa kushirikisha viongozi wa dini zote katika vita dhidi ya rushwa. “Hii iwe ajenda ya kitaifa. Masheikh misikitini wahubiri vita dhidi ya rushwa. Mapadre nao wafanye hivyo altare, wale wa CDA nao wasisite kuhubiri vita dhiti ya rushwa kila Jumamosi. Kwa njia hii pengine masikio yatazibuka,” alisema Mkurugenzi Mtendaji wa FiorDIA, Bubelwa Kaiza.

Kaiza alisisitiza kuwa tatizo kubwa linalolikabili taifa hili ni uwezo (capacity) wa watendaji serikalini, wananchi na katika taasisi mbalimbali kwani wengi hawafahamu haki na wajibu wao. Alisema kazi ya kwanza inayopaswa kufanywa ni kujenga mfumo na uwezo kwa wananchi wote, ili kila mmoja ajue haki na wajibu wake na hilo litaondosha mazingira ya rushwa kwa kiwango kikubwa.

Mkurugenzi Mkuu wa PORIS, Prince Bagenda, ilisema ikibidi taifa litafute mahala pa kuazima maadili na mienendo bora kwani katika mfumo wa sasa baadhi ya watu wana nguvu kuliko sheria zilizopo. “Tupo katika mazingira ya hatari. Maafisa wanaingia mikataba na hakuna mtu mwenye uwezo wa kuiona. Hata wabunge hawaruhusiwi kuiona. Hii ni hatari. Wananchi wanapaswa kupata haki ya kuona mikataba hii,” alisema Bagenda.

Mwambata wa Ubalozi wa Ubeligji nchini, Herman Boonen, alisema Serikali ya Awamu ya Nne imeanza vizuri hivyo ipewe muda katika vita dhidi ya rushwa. Alisisitiza kuwa kwa nchi yoyote kuendelea katika mapambano dhidi ya rushwa inapaswa kuhakikisha inaimarisha mifumo ya utawala bora na uwajibikaji.

Pia alisema wananchi wanapaswa kushirikishwa katika maamuzi, kupata taarifa zote ndani ya serikali na kuhusika katika maamuzi. Kwake anaona kuwa uwazi una nafasi kubwa ya kusaidia kuondoa vitendo vya rushwa. Ubeligji ndiyo iliyofadhili warsha hiyo.

Mada kuu katika warsha hiyo ilikuwa ni kupitia maazimio ya Brussels ya mwaka 2007 juu ya mapambano dhidi ya rushwa, jukumu la vyombo visivyo vya kiserikali katika mapambano dhidi ya rushwa Tanzania na mada ya mwisho ilikuwa juu ya Jinsia na Rushwa. Pia warsha hiyo ilitumika kuzindua kitabu kilichoandikwa na Bagenda kiitwacho Improving Governance


Kitabu katunga nani? Makamba ?
 
Kitabu katunga nani? Makamba ?


Of all people you think of Makamba! Ona hapa Mnyika alivyomuumbua mwaka 2005 wakati akiwa mkuu wa mkoa kuhusu Rushwa:

http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_4.html

Na hapa:
http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_0.html

Na ona hapa David Kafulila alivyomchamba Makamba kuhusu Rushwa:

http://www.chadema.net/makala/kafulila/david_6.html


Kwa kweli Makamba naye ni mtuhumiwa wa ufisadi, ataandika vipi kitabu cha kupinga rushwa?

Asha
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom