"You have been provisionally selected...." Ndio kazi ya TCU?

SHIEKA

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,244
4,258
Yaani tangu wanafunzi walipoomba kozi za degree Julai 30, mpaka leo Oktoba 13,profile hazielezi umechaguliwa kwenda wapi ila tu eti "Umechaguliwa, tunasubiri uamuzi wa mwisho wa chuo..."

Ndio maana imebidi tu-dukue tovuti za vyuo mbalimbali kujua hatma, utaratibu ambao ni kama gatecrashing vile. Kwenye tovuti za vyuo tumeyaona majina ya walioomba degree.

Je, TCU walitaka tufanye hivyo? Nilidukua tovuti ya MOCU nikaona jina la mpendwa wangu kuchaguliwa kwenye kozi ya degree, na kujisajili ni tarehe 17/10/ 2016!! TCU wanasema wanasubiri majibu toka vyuoni! What is this???

Tanzania ina maajabu mengi sana.
 
Back
Top Bottom