You don’t need “lots of money” to start a profitable online business. Most people get the basics wrong. Ndio sababu ya kushindwa

GLOBAL CITIZEN

JF-Expert Member
Jun 5, 2014
767
1,655
Greetings everybody!

Kama kawaida tunakutana tena katika darasa la leo ambapo nataka ni-share somo muhimu kabisa litakalokusaidia kuona njia bora yakuanzisha biashara ya mtandoni itakayopata wateja.

Unajua imezoeleka kutengeneza pesa mtandaoni ni vigumu.

Na hii ninaweza sema ni kweli kwasababu wengi wanaoendesha Online Business wanaanza hizi Business wakiwa weshakosea tayari.

Mara nyingi wajasiriamali wanaoanza Business Online wanawekeza muda mwingi kwneye product au service wasizofahamu hasa wanaenda kumuuzia nani.

Naongea hili kwa experience.

Tatizo kubwa ya Business nyingi zinazoanza Online kufanya vibaya ni kwasababu ya kimtazamo zaidi na si suala ya kiasi gani cha pesa chakuanza nacho kama mtaji.

Mara nyingi hapa nimeandika unaweza ukawa na product au service nzuri lakini kama watu hawahitaji maana yake utakuwa mfanyabiashara usiyeijua faida.

Trust me. Most online business are like this. They make 0 profit.

Na hasara inatokea kwasababu hizi biashara zilianzishwa vibaya.

Ngoja niseme kitu.

Ili biashara yako ya mtandaoni iwe na chance kubwa ya kukupatia faida inabidi uzingatie mambo yafuatayo.

1 • Imani (Faith)

Mmmh, vipi tena Global Citizen unataka kuingiza masuala ya Imani kwenye Business?

Jibu : Hapana

Imani nayozungumzia hapa ni wewe kuonyesha persistence.

Ukiwa na nidhamu yakufanya kitu kila siku bila kusuasua hiyo maana yake umeonyesha imani.

Haupo tayari ku-give up kisa tu hujapata sucesss ndani ya miezi michache ya mwanzo.

Unahitaji imani. Trust me, watu wengi hawana.

Wengi wamejaa shaka na wasiwasi.

Don’t be one of them.

Choose FAITH over FEAR.

Sasa ukitaka ufanikiwe kwenye Business (business yoyote ile) unatakiwa uwe na imani kwamba hatimaye huko mbele the dots will connect.

Niseme wazi.

Hakuna anayefahamu sana nini kitatokea next week au next month au few years ahead kwenye business yako. Sasa ukikosa imani ni rahisi sana ku-give up.

Utaanza kuwa doubtful.

Utaanza kusikia angry.

And guess what?

Utasema sizitaki mbichi hizi.

2 • Usiunde website, Blog au chochote kile kitakacho kutoa pesa kama hufahamu utaendae kumuuzia nani product au service yako.

Hapo vipi?

Najua watu wengi hawapendi kusikia hii.

Wanawaza aaah sasa nisipokuwa na product nitawezaje kumjua mtaja?

Ok cool.

Jibu: Inabidi uongee na potential customers kwanza na kuwauliza iwapo watapenda poduct au service yako.

Tuchukulie mfano unataka kuanzisha Digital Solution Start up kwaajili ya kusaidia Business ndogo na za kati.

Sasa kwa kawaida watu wengi watakimbilia kuanzisha website wengine hata watakodi physical office, watahangaika kwenda kujisajili Na gharama nyingine nyingi huku mwisho wa siku watashindwa kupata clients.

Hii namna yakuanzisha Online Business si nzuri sana.

Ni probability sana.

Usijidanganye kwasababu mskaji wako alianzisha Business miezi michache iliyopita na anamafanikio basi na wewe utapata mafanikio kwa urahisi tu.

Nop.

Njia nzuri ya kuanzisha biashara itakayokuja kuwa sustainable huko mbele ni kwanza kutafuta potential customers hata kabla yakuanza kuhangaika na mambo mengine.

Ongea na watu unaodhani watanunua bidhaa au huduma yako.

Labda unaweza kuanza na fariki zako, familia, ofisini?

Au kama upo active kwenye Social Platform kama hapa JF na unadhani hapa wapo potential buyers wasiliana nao.

Kama upo Facebook au Instagram do the same.

Hii ndiyo njia ya kuwa na uhakika zaidi iwapo service unayotaka kuuza Online kweli watu wapo interested kutoa pesa zao.

Hapa najua watu wangu hawapendi kwasababu kufanya hivi ni uncomfortable kwa watu wengi.

Kama umechagua kuwa entrepreneur inabidi ujiandae kwa hili.

3 • It takes Time Kuunda Imani kwa Watu. Kuwa Persistent katika Business yako.

IMG_6894.JPG


Ok.

Unapoanza Online Business inaweza ikakufurahisha sana lakini watu wengi wasichofahamu inachukuwa muda kuweza kuelewa kweli “how money is made”

Hasahasa ukiwa unajifunza mwenyewe.

Wapo watu watakwambia aaah mbona mimi sipati kazi UpWork au Online Business yangu sipati clients lakini ukiangalia walivyojiweka maaan ni very unprofessional.

Hapa simaanishi muonekano au mavazi nop.

Nazungumzia kwamfano mtu anasema yeye anataka kuwa blog writer wakati hata kuandika sentensi tano hawezi.

Na mtu huyu huyu ataka apate success ndani ya wiki ☹️

Crazy.

Hapa nikwambie kitu.

Itakuchuwa muda kuweza ku-master kila kitu kinachohusiana na Online Business unlitochagua.

Kwahiyo hapa hakuna namna. Inabidi ukibaliane na huu ukweli.

4 • Focus kwa Clients wako. Nyingine zote ni kelele tu.

Kwenye online Business kuna wateja wa aina tatu.

Number moja ni wateja walio sensitive linapokuja suala la bei. They ask so many questions kujiridhisha kweli bei uliyowatajia inalingana na service utakayompatia.

Lakini tatizo la wateja hawa wanafikiri wanafahamu kuliko wewe. Chache yao ya kununua toka kwako ni 50/50.

Inabidi uwe mindful.

Kuwa direct na muwazi kwao ili kuokoa muda.

Kwasababu unaweza ukatumia muda mwingi kwao lakini wasinunue chochote.

Number mbili ni wateja wasio fahamu lolote lakini pia hawapo na intention ya kununua chochote.

Wamefika kwako kwa bahari mbaya tu.

Don’t waste your time on this category.

Mteja anayetaka kununua kwako mara nyingi huwa na ufahamu angalau kidogo na anachotaka kununua kwako.

Number tatu ni wateja wanaojali zaidi value kwasababu wanauhakika watasaidika.

Hawa hawajali sana kuhusu bei.

Wakikutumia Email au kukupigia simu wanakuuliza “how much do you charge”

Halafu wanaendelea...

“Naomba nifanye malipo nipate huduma”

Hawa mimi ndiyo nawapenda zaidi.

Na ninawapatia high quality services.

Pia nguvu ngingi naelekeza kwako.

Wanaelewa maana ya “win win situation”

Yaani nakupatia value unanipatia pesa.

Simple.

Alright. Kwa leo naomba niishie hapa. Tukutane siku nyingine katika darasa amazing kama hili.
 
Mzee baba yule jamaa aliyekutuhumu kua ulimuahidi kumtengeneza online store akakulipa ukatokomea mpk leo,ulimalizana nae?
 
Back
Top Bottom