Yote yanayosemwa sasa na CCM kuhusu katiba mpya ni visingizio tu, hofu yao kuhusu katiba ni hii hapa

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,011
144,371
Kwa mawazo yangu,yote wanayoyasema sasa hawa wenzetu kuhususiana na madai ya wananchi ya kutaka kukamilishwa kwa mchakato wa kupata katiba mpya, ni uongo mtupu bali hofu yao kuu ni takwa lillilopo katika katiba inayopendekezwa ambalo ni kuruhusu uwepo wa Tume Huru ya Uchaguzi na si kitu kingine chochote.

Ukiruhusu kura ya maoni iendelee, basi Katiba mpya itakayopatikana pamoja na mapungufu yake yote,itatupelekea tuwe na Tume Huru ya Uchaguzi na hii ndio hofu yao kubwa na bila shaka hii ndio sababu iliyopekekea hata mchakato wa kura ya maoni kucheleweshwa ili kusubiri uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 upite.

Kwa sasa wanapima upepo na wakiona wana hali mbaya kuelekea 2020, hii Katiba inayopendekezwa wataipotezea kabisa licha ya kuwa wao wenyewe ndio walishiriki kuiandaa kwa kiasi kikubwa baada ya wapinzani kususia mchakato ule wa kuiandaa.

Wanachotaka wapinzani kwa sasa ni pamoja na kuifanyia marekebisho katiba inayopendekezwa ili iendane na matakwa ya Rasimu ya mzee Warioba lakini nina hakika maadam ina kipengele cha kuruhusu Tume Huru(kulingana na kumbukumbu zangu),basi tutarajie figisufigisu na danadana nyingi tu katika hili.

Kwa jinsi bwana fulani anavyopenda kuosha, sidhani kama kweli angekataa sifa ya kukamilisha huu mchako tena mapema kabisa.
 
Yote wanayoyasema sasa ni uongo mtupu bali hofu yao kuu ni takwa lillilopo katika katiba inayopendekezwa ambalo ni kuruhusu uwepo wa Tume Huru ya Uchaguzi.

Ukiruhusu Katiba mpya hii ya sasa pamoja na mapungufu yake yote,itatupelekea kupata Tume Huru ya Uchaguzi na hii ndio hofu yao kubwa na bila shaka hii ndio sababu iliyopekekea hata mchakato wa kura ya maoni kucheleweshwa ili kusubiri uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 upite.

Kwa sasa wanapima upepo na wakiona wana hali mbaya kuelekea 2020, hii Katiba inayopendekezwa wataipotezea kabisa licha ya kuwa wao wenyewe ndio walishiriki kuiandaa kwa kiasi kikubwa baada ya wapinzani kususia mchakato ule wa kuiandaa.

Wanachotaka wapinzani kwa sasa ni pamoja na kuifanyia marekebisho katiba inayopendekezwa ili iendane na matakwa ya Rasimu ya mzee Warioba lakini nina hakika maadam ina kipengele cha kuruhusu Tume Huru(kulingana na kumbukumbu zangu),basi tutarajie figisufigisu na danadana nyingi tu katika hili.

Kwa jinsi bwana fulani anavyopenda kuosha, sidhani kama kweli angekataa sifa ya kukamilisha huu mchako tena mapema kabisa.
Tume huru ya uchaguzi ni jina tu kwenye hiyo katiba elekezi.

Spika na Jaji mkuu na wateule wote kwa maana ya makamishna kuteuliwa na Rais wa CCM ambaye ni mgombea.

Sasa Tume huru ya uchaguzi iko wapi?
 
Tume huru ya uchaguzi ni jina tu kwenye hiyo katiba elekezi.

Spika na Jaji mkuu na wateule wote kwa maana ya makamishna kuteuliwa na Rais wa CCM ambaye ni mgombea.

Sasa Tume huru ya uchaguzi iko wapi?
Sikumbuki vizuri mashariti ya kuwapata wajumbe wa Tume lakini sidhani kama itakuwa hivyo bila kushirikisha wapinzani katika kupata hata baadhi ya wajumbe wa Tume hiyo maana itakuwa ni kama hii iliyopo sasa ambayo wajumbe muhimu wa Tume hiyo huteuliwa na Raisi kuanzia mwenyekiti wa Tume.
 
Pia inakipengere kinachoruhusu matokeo ya uchaguzi kupingwa mahakamani, na ndio maana hata jaji mkuu wanaogopa kumteua.
 
Kwa mawazo yangu,yote wanayoyasema sasa hawa wenzetu kuhususiana na madai ya wananchi ya kutaka kukamilishwa kwa mchakato wa kupata katiba mpya, ni uongo mtupu bali hofu yao kuu ni takwa lillilopo katika katiba inayopendekezwa ambalo ni kuruhusu uwepo wa Tume Huru ya Uchaguzi na si kitu kingine chochote.

Ukiruhusu kura ya maoni iendelee, basi Katiba mpya itakayopatikana pamoja na mapungufu yake yote,itatupelekea tuwe na Tume Huru ya Uchaguzi na hii ndio hofu yao kubwa na bila shaka hii ndio sababu iliyopekekea hata mchakato wa kura ya maoni kucheleweshwa ili kusubiri uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 upite.

Kwa sasa wanapima upepo na wakiona wana hali mbaya kuelekea 2020, hii Katiba inayopendekezwa wataipotezea kabisa licha ya kuwa wao wenyewe ndio walishiriki kuiandaa kwa kiasi kikubwa baada ya wapinzani kususia mchakato ule wa kuiandaa.

Wanachotaka wapinzani kwa sasa ni pamoja na kuifanyia marekebisho katiba inayopendekezwa ili iendane na matakwa ya Rasimu ya mzee Warioba lakini nina hakika maadam ina kipengele cha kuruhusu Tume Huru(kulingana na kumbukumbu zangu),basi tutarajie figisufigisu na danadana nyingi tu katika hili.

Kwa jinsi bwana fulani anavyopenda kuosha, sidhani kama kweli angekataa sifa ya kukamilisha huu mchako tena mapema kabisa.
Tatizo siyo TUME HURU, tatizo ni watumishi wa tume hiyo. Hata kama tume ingekuwa huru, watumishi wake wanaweza kuwa siyo huru kutokana na kuwa na maslahi katika vyama. Mfano mzuri ni kule nchini ZAMBIA. Tume yao ya uchaguzi ni HURU, lakini angalia jinsi ilivyoendasha zoezi la uchaguzi kwa kumpendelea Edga Lungu kuwa Rais. Tume ya MAREKANI ni HURU, lakini angalia jinsi walivyobadilisha Matokeo na kumpa ushindi TRUMP na kuwa Rais tofauti na matarajio ya wengi. Kwa hiyo, Suluhisho siyo kuwa na tume huru ya uchaguzi tu, bali pia kuwa na watumishi wenye kuwa na uzalendo wa taifa. Tume inaweza ikawa huru, lakini watumishi wake wakawa hawako huru kifikra na kimaslahi. Kwa mfano, leo hii tukiwa na tume huru ya uchaguzi halafu akateuliwa TUNDU LISSU kuwa mwenyekiti wa tume hiyo na GODBLESS LEMA akawa mkurugenzi wa hiyo tume na vyama vinavyoshindana ni CUF, CCM, CHADEMA, TLP N.K, unategemea matokeo gani?
 
Back
Top Bottom