Yote tisa, kumi ni hili analoenda kufanya Ndalichako, mjiandae kulia na kusaga meno!

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Hivi umewahi kujiuliza kuwa ikiwa mwanao au ndugu yako wa kawaida anayesomeshwa chuo kikuu na serikali walau kwa "kamkopo" ka asilimia kadhaa na kupewa hela ya kujikimu kisha akasitishiwa ghafla hayo yote na wakati huohuo ukiwa haujajipanga na huyo ndugu/mwanao anatokea katika familia ya kawaida kabisa?

Basi pale ghafla utakapojikuta ukitakiwa kumpa siyo chini ya Tshs. Elfu hamsini tu kila wiki na ukitakiwa kuandaa ada ya siyo chini ya Tshs. 1.5 million kwa kila mwaka wa masomo kwa muda uliobaki ambao amesitishiwa hiyo huduma muhimu na serikali ndipo utakapojua hasa ni nini maana ya kujikuta ukiwajibika ili fulani aende.

Zaidi ya yote utakuta enzi za kampeni ulikuwa ukitoka jasho mpaka masikioni wakati ukiimba "CCM mbele kwa mbele" mbaya zaidi ulikuwa mbishiiii hutaki kusikia wala kuambiwa kwa Magufuli!

Usitake kujifanya kujipa moyo eti serikali itakuwa sikivu na kuwa makini katika swala hilo. Ukiwa unajipa moyo kuhusu hilo ukumbuke yule mwanao wa UDOM aliyepata Div. Two na sasa umempeleka Kleruu kusomea upya certificate ya ualimu daraja la kwanza baada ya muda kupotea na matumaini kuanza upya. Pia wakati ukijipa moyo kuhusu hilo ujiulize ni mangapi ambayo serikali hii imeyaingilia na kuyafanya kwa usahihi (Sakata la sukari? Makodi? UDOM? Lipo lingine? )

Ni hivi: Karibia nusu ya wanafunzi wote wanaoendelea na masomo yao ya elimu ya juu watasitishiwa kupewa mikopo na hela ya kujikimu kutoka serikalini baada ya serikali kutoa siku nne tu kwa vyuo vyote nchini kupeleka taarifa zote za wanafunzi wao wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi ili kuanza uhakiki rasmi ili kuwachuja rasmi wale wanaoitwa "wasiostahili kusomeshwa na serikali ambao waliingia kwa bahati mbaya"
 
Kama haya ni ya kweli kwa nini hakuna anayewajibishwa mpaka sasa!!?

haiwezekani vijana wapewe mikopo leo waambiwe hawakustahili na hakuna anayewajibishwa!!? Kama requirements zimechange kwa nini ziwaaffect waliokwishapata? Hii hali inaweza kusababisha vijana wengi kusitisha masomo hivyo kuwa hasara kubwa kwa Taifa. Imagine kama mtu alishalipiwa mwaka 1 au 2 halafu akashindwa kumaliza kwa sababu ya mkopo? Ni Kiasi gani cha pesa kitakuwa kimepotea?
 
wakome na makomeo yao waliyo yanunua wenyewe .walivyokuwa wanarubuniwa kwa vitambaa na kanga za ccm hawakujua matokeo yake? tena wabane kabisa mm uko nilishatoka isitoshe nilijisomeshaga mwenye. hapa kazi tu
Nasisi kamwe hatutawachagua mafisadi na hao wanaoendekeza ukanda. Nanyi muishie kuiona ikulu kwa nje na ufisadi wenu. Na wewe lazima ni wa pepo za kas.
 
Wakati ndugu zetu waislam wanamkataa huyo bi Joyce Ndalichako pale baraza la mitihani (Siwezi kum-adress kama profesa kwa jinsi anavyotenda), nilidhani kuna chembe za udini (Naoimba nikiri hivyo), lakini sasa nimetambua waislamu wale walikuwa sahihi sana na waliona vitu ambavyo wengine tulikuwa hatujaviona au kupofushwa na hoja ya udini!
 
wakome na makomeo yao waliyo yanunua wenyewe .walivyokuwa wanarubuniwa kwa vitambaa na kanga za ccm hawakujua matokeo yake? tena wabane kabisa mm uko nilishatoka isitoshe nilijisomeshaga mwenye. hapa kazi tu
usiwe too general jomba...sio kila mhanga wa hii serikali aliipigia kura, wengi ni wahanga kwa maamuzi yaliofanywa na wengine, tRNA vyuoni ndiko ambako ccm haikutakiwa kabisa Mkuu, so ucwalaumu hawa wenzetu wanaoyumbishwa na taarifa za mikopo
 
usiwe too general jomba...sio kila mhanga wa hii serikali aliipigia kura, wengi ni wahanga kwa maamuzi yaliofanywa na wengine, tRNA vyuoni ndiko ambako ccm haikutakiwa kabisa Mkuu, so ucwalaumu hawa wenzetu wanaoyumbishwa na taarifa za mikopo

Kweli kabisa Mkuu. Tena hao wanaojitoa ufahamu kila muda wa uchaguzi unapofika ndio wanaoisoma namba sawasawa.
 
Vyuo husika hivi hapa 1.jpg

1.jpg


2.jpg
 
Back
Top Bottom