Yondo Sister enzi zake...

Mkuu Invisible
Hivi yuko wapi siku hizi huyu demu? Kiuno baba kiuno, miondoko, kusasambua duh
 
Mkuu Invisible
Hivi yuko wapi siku hizi huyu demu? Kiuno baba kiuno, miondoko, kusasambua duh
Mwalimu, mi leo nimemkumbuka ghafla... Nikaanza kupitia video zake.

Hebu angalia hii na ukumbuke enzi hizi:



Nimemkumbuka SANA yani hahahaha sijui ndo kuzeeka kwangu?
 
Asante sana mkuu
Duh demu ana pumzi balaa. Huu wimbo una karibu dk 8 na inaonekana alikuwa anaukung'uta wote kwa nguvu hiyo hiyo.Wanawake ndio hawa, si hawa...nyoro nyoro
 
mkuu nashukru sana nilikuwa natafuta sana picha zake huyu dada inanikumbusha mbali sana
 
invisible asante mvina amekubali, harafu huyu binti nirajini yake au ndiyo ule usemi 'nabii hatuzwi kwao'
 
Wakuu
Bila kinyongo, kwa gwaride nampa Yondo Sister, kiuno cha Ray C. Tatizo vina na mistari ya Yondo siielewi naogopa kuwa kama majaji wa BSS
 
Huyu Yondo nakumbuka dah alikuwa anaturusha roho sana.
Hivi kwa nn Ray C kafulia moja kwa moja?
 
Hicho kibao cha Dunia taabu [aliimba Kiswahili] dah kimenikumbusha mbali sana mpaka nimemwaga uchozi,
 
Yondo Sister bado yupo mitaani. Miaka ya nyuma kidogo kulikuwa na uvumi kuwa alifariki lakini siyo kweli, bado yupo anakula maisha kama kawaida ila sasa hivi ni mama mzima kidogo kama anavyoonekana katika picha hii hapa chini:
Kwa wale walioko Uingereza nadhani walishuhudia shoo zake mwishoni mwa mwezi jana kama bango hili hapa chini linavyoonyesha
 
Nafikiri umaarufu wote wa Yondo ulikuwa ni kufanya show ila kama mwana muziki, mhh. Siku zote nyuma yake walikuwa wamesimama imara Wazee/Vijana wa Soukous Stars yaani Lokasa ya Mbongo, Dally Kimoko na Shimita El Diego ambaye kwa sasa naona kaanzisha bendi yake. Kwenye wimbo wa Bazo unasikia kabisa sauti ya Shimita iki-Rap. Hawa jamaa unaweza waona wote hapa na kwenye dakika ya 4 jamaa anaimba kwa Kiswahili. Na mwisho kwenye 7:14 jamaa wa west Africa kama sikosei Mali anakuja na hapo wanaanza kucheza Zugulu (sikumbuki wanaandikaje kifaransa).



Hapa Chini Yondo Sister kama mchezaji kwenye wimbo wa Lokasa ya Mbongo uitwao MARIE JOSE. Ninafikiri hata ni yeye aliimba kwenye background vocal ya huu wimbo.



Lazima nikubali kitu kimoja kuwa mziki wa Soukous hawa jamaa walikuwa wametawala kabisa. Chezaji ya Shimita hadi leo watu wanacheza. Mziki wao hadi kesho vijana wadogo wataiga ili wapate pa kutokea. Mwanzo nilikuwa nasikia Shimita anacheza ila nilikuwa sifahamu hadi nilipokuja kuona hii Video.



Ila nirudie tena, pamoja na mziki wao MZITO, unapokuja kwenye show, basi Yondo Sister alikuwa anafunika. Dada yake (na yeye Half cast) alikuwa akicheza kwenye kundi la Pepe Kalle and Empire Bakuba (nasikia walikuwa ndugu) sijui aliishia wapi?

Kusema kweli mie huyu dada alikuja enzi hizo nimeipenda bendi ya KASSAV na hasa huyu dada Jocelyne Beroad (aliyeimba Coupe Bibamba na Awilo). Huyu mama kwa kweli aliniuwa na hadi leo hii Kassav kwangu wako juu sana. Najuta sintakuja kuwaona LIVE. Anyway itabidi hata kufurahia video zao za LIVE.

 
Hivi Invisible huna ule wimbo wa Gato- Ngoma za kwetu.
Hiyo unaweza kuipata chini hapa...

Audio yake:



video yake (quality si nzuri):



Aaah wakati huo bana...!

Nyimbo nyingine za Ghato ni hizi:







 
Mkuu umenikumbusha mbali duh ! hahahhahah nilivyokuwa najitia stage shoo wa home nilikuwa naupenda huo mwimbo wa mbuta mbutuu mwana mamaaa mwe!
na ghato nayeee azalaki seeeawaaaa duh! si mchezo.
asanteni sana wajameniiii
 
Yaani mmenikumbusha mbali enzi hizoooo!!! za ukubwa wangu. Haswa huu mbuta mutu ulitamba sana. Kulikuwa hadi na msuko wa Yondo sister atii!!
 
Wana JF nilipoona Yondo Sister nilistika sana kwani kuna CD mmoja anapatikana maeneo ya shinyanga. Huyu Mdada ukilogwa ukakalia kiti na yeye akakajirani yako atakuomba umnunulie soda kwa utanzania wako ukafanya hivyo, ujue umeoonodoka nae piga au vinginevyo lazima umlipe. Yalimkuta mzee mmoja ilibidi akimbie kwa kwa kujifanya kwenda kujisaidia akatoweka. Tahadhari kwa mnotembelea mkoa wa shy.
 
Ray C si chochote kitandani ikimkalia kilo sabini juu anaishiwa maajabu but Yondo kwa muonekano tu ni mwanamke wa kazi hata kitandani wau mnasemaje wadau wangu?!
 
Back
Top Bottom