Yona Fares Maro ( Holly Maro) akamatwa na Polisi!

Kleptomaniacs

Member
Apr 23, 2008
86
2
Nimeona ni vyema niliweke hili la huyu bwana Yona hapa JF, ni kwamba kumekuwa na taarifa mbalimbali zenye utata kuhusu kukamatwa kwa bwana Yona Fares Maro na polisi, kwa mujibu wa email iliyotumwa katika address ya wanazuoni ambao ni mtandao ama group email aliyokuwa akichangia mara kwa mara alikamatwa Jnne na taarifa hiyo ilitumwa kupitia simu yake kwa mmoja wa rafiki zake ambaye pia ni mwanachama wa kundi hilo la wanazuoni! kwa mujibu wa maelezo ambayo bila shaka si vibaya nikaya ambatanisha hapa yanasomeka kama ifuatavyo;

''Ndg wanazuoni

Habari zilizonifikia Muda mfupi uliopita zinasema kuwa Mwanazuoni Yona Maro amekamatwa na polisi tangu jumanne usiku.Kwa bahati mbaya text message iliyonifikia haijasema mahali aliko wala sababu za kukamatwa kwake.Ujumbe huo umenifikia kutoka kwa moja ya namba ambayo huwa natumia kuwasiliana na Yona.Nimejaribu mara kadhaa kupiga namba hiyo ili kuweza kupata undani wa swala hilo bila mafanikio.

Kwa wale waliokaribu sana na Yona kama wanaaltenative number ni vizuri kujaribu kumtafuta ili kuona namna ya kumsaidia.Pia wale walio Dar wanaweza kwa nafasi yao kujaribu kufatilia swala hili kwa ukaribu zaidi
.
Nawatakia kazi njema.''
( wanazuoni@yahoogroups.com)

Leo hii pia ndugu yake aliyepewa jukumu la kutafuta ukweli katika vituo vya polisi ametuma email nyingine juu ya jitihada za kumtafuta katika vituo tofauti vya polisi kutokuzaa matunda email hiyo inasomeka kama ifuatavyo;

''Wanazuoni,naandika kuwasilisha hatua ambayo nimefikia katika kumtafuta Yona,ninasikitika kuwataarifu kuwa pamoja na jitihada hizi bado hazijazaa matunda.
Nimewasiliana na Central Police wanasema wao hawana majina ya waliotiwa mbaroni lakini hata hivyo nimejaribu pia Oysterbay ambako nako sijapata jibu la uhakika.
Bado naendelea kusubiria feedback toka katika vyanzo mbali mbali ili tuwezejua huyu mwenzetu yuko wapi bila KUJALI AIDHA KATIWA NGUVUNI KWA MAKOSA BINAFSI ama ni kutokana na HARAKATI ZAKE.''


Kwasasa kuna kampeni inayoendelea inaitwa FREE YONA, sasa si vibaya kama kampeni hiyo ikiletwa hapa JF ambako pia bwana Yona amekuwa mchangiaji mkubwa katika kuendeleza hiyo kampeni ya FREE YONA. Wale wenye taarifa za ziada kuhusu huyu bwana wanaweza kuchangia hapa ama namna ya kumpata maana ndio hivyo tena polisi wanadai hawajamkamata kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari.
Nawasilisha.
 
kuna mtu anajaribu kumpiku Invisible kwa kila kitu. Hawawezi kumkamata Yona.
Mwankijiji tulishakataa Speculation.Ni nani anajaribu kumpiku Invisible?Kina nani hawawezi kumkamata Yona?Yona Yupi?

...anajaribu kumpiku Invisible kwa kila kitu. .......Hawawezi kumkamata Yona
 
Wanandugu kwa mujibu wa Invisible ni kwamba Yona yuko Barabarani anaelekea nyumbani kwake hajakamatwa.Yona mwenyewe amepigiwa simu na kuhakikisha hilo.Tunaomba ndugu aliyeanzisha thread a apologize kwa kuwa Yona mwenyewe anasema hana taarifa juu ya kukamatwa kwake.

Asanteni
 
Wanandugu kwa mujibu wa Invisible ni kwamba Yona yuko Barabarani anaelekea nyumbani kwake hajakamatwa.Yona mwenyewe amepigiwa simu na kuhakikisha hilo.Tunaomba ndugu aliyeanzisha thread a apologize kwa kuwa Yona mwenyewe anasema hana taarifa juu ya kukamatwa kwake.

Asanteni
Thats why i like Mwanakijiji
 
sasa mjumbe anauwawa tangu lini? kama amepatikana ni vyema hiyo itasaidia kuondoa uvumi wa kukamatwa kwake na kusimamisha FREE YONA campaign iliyokuwa inaendelea, mie nimewashirikisha ujumbe tu sidhani kama ni muhimu ku apologize! kwani ushahidi niliotoa hapo juu kuhusu kupotea kwa huyu jamaa toka jnne zinatoka kwa ndugu na rafiki zake. Invisible kama kampata kwa simu sio mbaya nadhani marafiki zake wanaweza mpigia pia kama kweli.
 
Nadhani pia hukusoma ujumbe wangu vyema ndg Amangk, hasa maelezo yaliyokolezwa kwa wino mwekundu ambayo ni nukuu za watu sio zangu na vyanzo vya habari hizo vimetambuliwa! na bila shaka pia ndio maana JF ipo! kusaidia pamoja na mengineyo masuala kama hayo ya uvumi kama kweli ulikuwa uvumi na sio taarifa sahihi!
 
sawa mkuu klepto nimekusoma.Ila ukweli unabaki kuwa ukweli.Kama Yona mwenyewe hajui kuwa kakamatwa hiyo Campaign aliye initiate hakua amefanya utafiti wake kiasi cha kutosha
 
Ndugu jamaa , marafiki na ndugu

Ahsanteni kwa wale wote waliokuwa wananitafuta kwa siku kadhaa ambazo nilikuwa siko hewani kwa sababu nilikuwa nimekamatwa na watu inasemekana ni jeshi la polisi wapelelezi kutoka kituo cha central

Siku hiyo nilipigiwa simu na rafiki yangu mmoja , huyu rafiki yangu sijawahi kufanya nae kazi yoyote huwa nakutana nae mara kwa mara siku hiyo akanipigia akaniambia ana tovuti yake ametengeneza anahitaji mimi kwenda kuona na kumpa ushauri zaidi na kwenda kufanya hosting na kadhalika , kabla ya hapo wiki moja iliyopita akanipigia aliniuliza kuhusu suala hili mimi nikamwelekeza aende extreme technologies na kumpa mpaka namba za simu ,baadaye akaniambia haelewi anataka maelezo ya kina .

Basi mimi sikuhiyo nilikuwa nimetoka chuoni pale mlimani , akaniambia yeye yuko mlimani city tuonane pale saa 1 usiku , nikakubali ombi laki , nikafika muda huo bila kuchelewa ili niweze kumsaidia niondoke zangu .

Kufika hapo tukaongea kwa mapana , Nilikuwa na Laptop yangu kwahiyo tulijiunga na mtandao na kumwonyesha mambo kadha wa kadha ambao anaweza kufanya kuweza kufanikisha shuguli yake , wakati naendelea na maongezi nae , ndio ghafla tu nikaona mtu ameshika tshirt yangu mwingine akanishika mkono nikapokonywa laptop halafu nikaenda kukaa katika kiti kingine kuna wazee walikuwa pale na vijana 2 ,mmoja wa askari hawa ni yule ambaye niliandika kuhusu kuhusishwa kwake na harakati za kukamata vijana mitaani yeye huwa anajifanya ni mnunuzi wa laptop na kuzichukuwa

wakasema wananitafuta sana nimekuwa nawakimbia sana nisiposema ukweli basi mimi ni halali yao ,kwanza nilianza kuulizwa maswali kuhusu majina mbali mbali ambayo huchangia mada katika majukwaa mbali mbali , majina nitaficha lakini wanasema wale ni mimi au ni mimi ambaye nawapa moyo kwa majina bandia katika kutoa propaganda na habari zingine katika hilo sikujibu chochote kwahiyo kuanzia siku ile nikafungiwa chini kule rumande chumba cha peke yangu .

simu yangu na laptop wakabaki nayo wale maaskari , pesa na vitu zingine nikaandikisha pale mapokezi kuanzia usiku huo wa jumanne saa 4 usiku nikawa kule chini katika chumba cha peke yangu , mpaka alhamisi asubuhi nikafuatwa na askari mwingine tena kuuliza maswali kadha wa kadha , kisha wakaenda kumfuata mwanamke mmoja hivi wa karibu yangu wakamfuata nyumbani kwake na yeye akaja pale nilionana nae lakini sikupata nafasi ya kuongea nae chochote alihojiwa sikujua amehojiwa nini .lakini yeye alikuja kuwekewa dhamana baada ya masaa 3 hivi akaondoka lakini alishushwa rumande kidogo .

Sasa sikuandikiwa maelezo yoyote yale , pale mapokezi polisi nililazimishwa kuandika jina tofauti sio yona maro nilitakiwa kutumia jina la Abuu Khalid , ndio maana watu wengi walipokuwa wananitafuta wakifika pale hawakuweza kuona jina langu lilibadilishwa na kupewa kesi ambayo mimi siiielewi mpaka sasa hivi .

jumamosi Yule mwanamke alikuja tena kuonana na mimi na yeye kumbe alivyotoka nje akapokea vitisho asiseme chochote wala kusema lolote kwa sababu nyumbani kwake wanapajua na mambo kama hayo dada akaogopa kusema chochote hata kwetu hakwenda kutoa taarifa zozote zile .

Ndio nimekaa mpaka asubuhi ya leo -- Mkaguzi akapita kuniuliza ninashilingi ngapi tumalizane nikasema sina kitu , akaniambia mbona mwanamke wako alivyokuja amechukuwa pesa nikamwambia amechukuwa zote kwahiyo siwezi kutoa malipo yoyote yale , baadaye sana kwenye saa 7 hivi rafiki yangu mmoja hivi ndio akaja pale tena aliambiwa na huyu mwanadada kwa siri ndio kwenda kuongea na wakubwa zao nikatolewa nje lakini walikomaa wanataka pesa akawapa alfu 10.

Pamoja na yote haya wiki hizi mbili kuna baadhi ya vitu vimetokea kwangu ambavyo ndio nahisi vinahusiana na na tukio hili

1 - NILIANDIKA KUHUSU YULE ASKARI KANZU ANAYEJIFANYA MNUNUZI WA LAPTOP NA MAMBO YAKE YA KILANGUZI KWA SABABU KATI YA WATU WALIOKUJA KUNIKAMATWA USIKU ULE YEYE ALIKWEPO ALINIULIZA KAMA NAMKUMBUKA .

2 - ANUANI YANGU YA YAHOO PAMOJA NA HOTMAIL ZILIBALISHWA PWD LAKINI NILIFANIKIWA KUIRUDISHA BAADA YA MASAA KADHAA LAKINI BAADHI YA TAARIFA KUHUSU ACCOUNT ZILIBALISHWA KAMA NCHI NAKADHALIKA

3 - KUNA KAMPUNI MOJA ILIWEKA MATANGAZO YAKE INATAFUTA ICT EXPERTS KATIKA MAGAZETI ILIANDIKA MATANGAZO HAYA KWA WIKI YA KWANZA YA MWEZI WA 6 NA WIKI YA 3 NILIWAANDIKIA KUULIZIA KUHUSU TANGAZO LAO HILI NIKAFUATILIA KAMA KAMPUNI HIYO IMESAJILIWA AU LA , KAMPUNI HII HAINA USAJILI NA JINA LILE NI BANDIA .

Mpaka sasa hivi sijajua nini kinaendelea kwa sababu nilipotoka wale walionileta pale sikuwaona hapo polisi kwahiyo wana laptop yangu , na karatasi fulani ambazo nilikuwa nimechapisha baadhi ya vitu vya kufanyia kazi zangu , simu sikuwa na wasi wasi nayo kwa sababu Line yangu ya celtel ilikuwa upande mwingine wa suruali .

Bado sijajua nini kinaendelea kwa kweli

AHSANTENI KWA WALE WALIONIPIGIA JIONI HUU KUTAKA KUJUA CHOCHOTE KILE KILICHOKUWA KINAENDELEA INGAWA SIKUWAJIBU CHOCHOTE NA KUTOA MAJIBU YA MKATO NILIKUWA NAWAHI NYUMBANI KWA SABABU NILITAKIWA KUANGALIA MASUALA MENGINE

USIKU MWEMA WASOMAJI
 
Ndugu jamaa , marafiki na ndugu

Ahsanteni kwa wale wote waliokuwa wananitafuta kwa siku kadhaa ambazo nilikuwa siko hewani kwa sababu nilikuwa nimekamatwa na watu inasemekana ni jeshi la polisi wapelelezi kutoka kituo cha central

Siku hiyo nilipigiwa simu na rafiki yangu mmoja , huyu rafiki yangu sijawahi kufanya nae kazi yoyote huwa nakutana nae mara kwa mara siku hiyo akanipigia akaniambia ana tovuti yake ametengeneza anahitaji mimi kwenda kuona na kumpa ushauri zaidi na kwenda kufanya hosting na kadhalika , kabla ya hapo wiki moja iliyopita akanipigia aliniuliza kuhusu suala hili mimi nikamwelekeza aende extreme technologies na kumpa mpaka namba za simu ,baadaye akaniambia haelewi anataka maelezo ya kina .

Basi mimi sikuhiyo nilikuwa nimetoka chuoni pale mlimani , akaniambia yeye yuko mlimani city tuonane pale saa 1 usiku , nikakubali ombi laki , nikafika muda huo bila kuchelewa ili niweze kumsaidia niondoke zangu .

Kufika hapo tukaongea kwa mapana , Nilikuwa na Laptop yangu kwahiyo tulijiunga na mtandao na kumwonyesha mambo kadha wa kadha ambao anaweza kufanya kuweza kufanikisha shuguli yake , wakati naendelea na maongezi nae , ndio ghafla tu nikaona mtu ameshika tshirt yangu mwingine akanishika mkono nikapokonywa laptop halafu nikaenda kukaa katika kiti kingine kuna wazee walikuwa pale na vijana 2 ,mmoja wa askari hawa ni yule ambaye niliandika kuhusu kuhusishwa kwake na harakati za kukamata vijana mitaani yeye huwa anajifanya ni mnunuzi wa laptop na kuzichukuwa

wakasema wananitafuta sana nimekuwa nawakimbia sana nisiposema ukweli basi mimi ni halali yao ,kwanza nilianza kuulizwa maswali kuhusu majina mbali mbali ambayo huchangia mada katika majukwaa mbali mbali , majina nitaficha lakini wanasema wale ni mimi au ni mimi ambaye nawapa moyo kwa majina bandia katika kutoa propaganda na habari zingine katika hilo sikujibu chochote kwahiyo kuanzia siku ile nikafungiwa chini kule rumande chumba cha peke yangu .

simu yangu na laptop wakabaki nayo wale maaskari , pesa na vitu zingine nikaandikisha pale mapokezi kuanzia usiku huo wa jumanne saa 4 usiku nikawa kule chini katika chumba cha peke yangu , mpaka alhamisi asubuhi nikafuatwa na askari mwingine tena kuuliza maswali kadha wa kadha , kisha wakaenda kumfuata mwanamke mmoja hivi wa karibu yangu wakamfuata nyumbani kwake na yeye akaja pale nilionana nae lakini sikupata nafasi ya kuongea nae chochote alihojiwa sikujua amehojiwa nini .lakini yeye alikuja kuwekewa dhamana baada ya masaa 3 hivi akaondoka lakini alishushwa rumande kidogo .

Sasa sikuandikiwa maelezo yoyote yale , pale mapokezi polisi nililazimishwa kuandika jina tofauti sio yona maro nilitakiwa kutumia jina la Abuu Khalid , ndio maana watu wengi walipokuwa wananitafuta wakifika pale hawakuweza kuona jina langu lilibadilishwa na kupewa kesi ambayo mimi siiielewi mpaka sasa hivi .

jumamosi Yule mwanamke alikuja tena kuonana na mimi na yeye kumbe alivyotoka nje akapokea vitisho asiseme chochote wala kusema lolote kwa sababu nyumbani kwake wanapajua na mambo kama hayo dada akaogopa kusema chochote hata kwetu hakwenda kutoa taarifa zozote zile .

Ndio nimekaa mpaka asubuhi ya leo -- Mkaguzi akapita kuniuliza ninashilingi ngapi tumalizane nikasema sina kitu , akaniambia mbona mwanamke wako alivyokuja amechukuwa pesa nikamwambia amechukuwa zote kwahiyo siwezi kutoa malipo yoyote yale , baadaye sana kwenye saa 7 hivi rafiki yangu mmoja hivi ndio akaja pale tena aliambiwa na huyu mwanadada kwa siri ndio kwenda kuongea na wakubwa zao nikatolewa nje lakini walikomaa wanataka pesa akawapa alfu 10.

Pamoja na yote haya wiki hizi mbili kuna baadhi ya vitu vimetokea kwangu ambavyo ndio nahisi vinahusiana na na tukio hili

1 - NILIANDIKA KUHUSU YULE ASKARI KANZU ANAYEJIFANYA MNUNUZI WA LAPTOP NA MAMBO YAKE YA KILANGUZI KWA SABABU KATI YA WATU WALIOKUJA KUNIKAMATWA USIKU ULE YEYE ALIKWEPO ALINIULIZA KAMA NAMKUMBUKA .

2 - ANUANI YANGU YA YAHOO PAMOJA NA HOTMAIL ZILIBALISHWA PWD LAKINI NILIFANIKIWA KUIRUDISHA BAADA YA MASAA KADHAA LAKINI BAADHI YA TAARIFA KUHUSU ACCOUNT ZILIBALISHWA KAMA NCHI NAKADHALIKA

3 - KUNA KAMPUNI MOJA ILIWEKA MATANGAZO YAKE INATAFUTA ICT EXPERTS KATIKA MAGAZETI ILIANDIKA MATANGAZO HAYA KWA WIKI YA KWANZA YA MWEZI WA 6 NA WIKI YA 3 NILIWAANDIKIA KUULIZIA KUHUSU TANGAZO LAO HILI NIKAFUATILIA KAMA KAMPUNI HIYO IMESAJILIWA AU LA , KAMPUNI HII HAINA USAJILI NA JINA LILE NI BANDIA .

Mpaka sasa hivi sijajua nini kinaendelea kwa sababu nilipotoka wale walionileta pale sikuwaona hapo polisi kwahiyo wana laptop yangu , na karatasi fulani ambazo nilikuwa nimechapisha baadhi ya vitu vya kufanyia kazi zangu , simu sikuwa na wasi wasi nayo kwa sababu Line yangu ya celtel ilikuwa upande mwingine wa suruali .

Bado sijajua nini kinaendelea kwa kweli

AHSANTENI KWA WALE WALIONIPIGIA JIONI HUU KUTAKA KUJUA CHOCHOTE KILE KILICHOKUWA KINAENDELEA INGAWA SIKUWAJIBU CHOCHOTE NA KUTOA MAJIBU YA MKATO NILIKUWA NAWAHI NYUMBANI KWA SABABU NILITAKIWA KUANGALIA MASUALA MENGINE

USIKU MWEMA WASOMAJI

Pole kwa yaliyokukuta!
 
Pole sana Shy kwa yaliyokukuta, usife moyo kwa hivyo vitisho, daima kumbuka hauko pekeyako katika hili tuko pamoja.
 
AHSANTENI KWA WALE WALIONIPIGIA JIONI HUU KUTAKA KUJUA CHOCHOTE KILE KILICHOKUWA KINAENDELEA INGAWA SIKUWAJIBU CHOCHOTE NA KUTOA MAJIBU YA MKATO NILIKUWA NAWAHI NYUMBANI KWA SABABU NILITAKIWA KUANGALIA MASUALA MENGINE
Hahaha, pole sana mwanazuoni mwenzetu... Mh, hatari kweli
 
Mwanakijiji bwana, .... .... mja hunena muungwana ni kitendo.
 
Ndugu jamaa , marafiki na ndugu

Ahsanteni kwa wale wote waliokuwa wananitafuta kwa siku kadhaa ambazo nilikuwa siko hewani kwa sababu nilikuwa nimekamatwa na watu inasemekana ni jeshi la polisi wapelelezi kutoka kituo cha central

Siku hiyo nilipigiwa simu na rafiki yangu mmoja , huyu rafiki yangu sijawahi kufanya nae kazi yoyote huwa nakutana nae mara kwa mara siku hiyo akanipigia akaniambia ana tovuti yake ametengeneza anahitaji mimi kwenda kuona na kumpa ushauri zaidi na kwenda kufanya hosting na kadhalika , kabla ya hapo wiki moja iliyopita akanipigia aliniuliza kuhusu suala hili mimi nikamwelekeza aende extreme technologies na kumpa mpaka namba za simu ,baadaye akaniambia haelewi anataka maelezo ya kina .

Basi mimi sikuhiyo nilikuwa nimetoka chuoni pale mlimani , akaniambia yeye yuko mlimani city tuonane pale saa 1 usiku , nikakubali ombi laki , nikafika muda huo bila kuchelewa ili niweze kumsaidia niondoke zangu .

Kufika hapo tukaongea kwa mapana , Nilikuwa na Laptop yangu kwahiyo tulijiunga na mtandao na kumwonyesha mambo kadha wa kadha ambao anaweza kufanya kuweza kufanikisha shuguli yake , wakati naendelea na maongezi nae , ndio ghafla tu nikaona mtu ameshika tshirt yangu mwingine akanishika mkono nikapokonywa laptop halafu nikaenda kukaa katika kiti kingine kuna wazee walikuwa pale na vijana 2 ,mmoja wa askari hawa ni yule ambaye niliandika kuhusu kuhusishwa kwake na harakati za kukamata vijana mitaani yeye huwa anajifanya ni mnunuzi wa laptop na kuzichukuwa

wakasema wananitafuta sana nimekuwa nawakimbia sana nisiposema ukweli basi mimi ni halali yao ,kwanza nilianza kuulizwa maswali kuhusu majina mbali mbali ambayo huchangia mada katika majukwaa mbali mbali , majina nitaficha lakini wanasema wale ni mimi au ni mimi ambaye nawapa moyo kwa majina bandia katika kutoa propaganda na habari zingine katika hilo sikujibu chochote kwahiyo kuanzia siku ile nikafungiwa chini kule rumande chumba cha peke yangu .

simu yangu na laptop wakabaki nayo wale maaskari , pesa na vitu zingine nikaandikisha pale mapokezi kuanzia usiku huo wa jumanne saa 4 usiku nikawa kule chini katika chumba cha peke yangu , mpaka alhamisi asubuhi nikafuatwa na askari mwingine tena kuuliza maswali kadha wa kadha , kisha wakaenda kumfuata mwanamke mmoja hivi wa karibu yangu wakamfuata nyumbani kwake na yeye akaja pale nilionana nae lakini sikupata nafasi ya kuongea nae chochote alihojiwa sikujua amehojiwa nini .lakini yeye alikuja kuwekewa dhamana baada ya masaa 3 hivi akaondoka lakini alishushwa rumande kidogo .

Sasa sikuandikiwa maelezo yoyote yale , pale mapokezi polisi nililazimishwa kuandika jina tofauti sio yona maro nilitakiwa kutumia jina la Abuu Khalid , ndio maana watu wengi walipokuwa wananitafuta wakifika pale hawakuweza kuona jina langu lilibadilishwa na kupewa kesi ambayo mimi siiielewi mpaka sasa hivi .

jumamosi Yule mwanamke alikuja tena kuonana na mimi na yeye kumbe alivyotoka nje akapokea vitisho asiseme chochote wala kusema lolote kwa sababu nyumbani kwake wanapajua na mambo kama hayo dada akaogopa kusema chochote hata kwetu hakwenda kutoa taarifa zozote zile .

Ndio nimekaa mpaka asubuhi ya leo -- Mkaguzi akapita kuniuliza ninashilingi ngapi tumalizane nikasema sina kitu , akaniambia mbona mwanamke wako alivyokuja amechukuwa pesa nikamwambia amechukuwa zote kwahiyo siwezi kutoa malipo yoyote yale , baadaye sana kwenye saa 7 hivi rafiki yangu mmoja hivi ndio akaja pale tena aliambiwa na huyu mwanadada kwa siri ndio kwenda kuongea na wakubwa zao nikatolewa nje lakini walikomaa wanataka pesa akawapa alfu 10.

Pamoja na yote haya wiki hizi mbili kuna baadhi ya vitu vimetokea kwangu ambavyo ndio nahisi vinahusiana na na tukio hili

1 - NILIANDIKA KUHUSU YULE ASKARI KANZU ANAYEJIFANYA MNUNUZI WA LAPTOP NA MAMBO YAKE YA KILANGUZI KWA SABABU KATI YA WATU WALIOKUJA KUNIKAMATWA USIKU ULE YEYE ALIKWEPO ALINIULIZA KAMA NAMKUMBUKA .

2 - ANUANI YANGU YA YAHOO PAMOJA NA HOTMAIL ZILIBALISHWA PWD LAKINI NILIFANIKIWA KUIRUDISHA BAADA YA MASAA KADHAA LAKINI BAADHI YA TAARIFA KUHUSU ACCOUNT ZILIBALISHWA KAMA NCHI NAKADHALIKA

3 - KUNA KAMPUNI MOJA ILIWEKA MATANGAZO YAKE INATAFUTA ICT EXPERTS KATIKA MAGAZETI ILIANDIKA MATANGAZO HAYA KWA WIKI YA KWANZA YA MWEZI WA 6 NA WIKI YA 3 NILIWAANDIKIA KUULIZIA KUHUSU TANGAZO LAO HILI NIKAFUATILIA KAMA KAMPUNI HIYO IMESAJILIWA AU LA , KAMPUNI HII HAINA USAJILI NA JINA LILE NI BANDIA .

Mpaka sasa hivi sijajua nini kinaendelea kwa sababu nilipotoka wale walionileta pale sikuwaona hapo polisi kwahiyo wana laptop yangu , na karatasi fulani ambazo nilikuwa nimechapisha baadhi ya vitu vya kufanyia kazi zangu , simu sikuwa na wasi wasi nayo kwa sababu Line yangu ya celtel ilikuwa upande mwingine wa suruali .

Bado sijajua nini kinaendelea kwa kweli

AHSANTENI KWA WALE WALIONIPIGIA JIONI HUU KUTAKA KUJUA CHOCHOTE KILE KILICHOKUWA KINAENDELEA INGAWA SIKUWAJIBU CHOCHOTE NA KUTOA MAJIBU YA MKATO NILIKUWA NAWAHI NYUMBANI KWA SABABU NILITAKIWA KUANGALIA MASUALA MENGINE

USIKU MWEMA WASOMAJI

wow
what a nice bedtime story....
tukupe mji???
 
Mwankijiji tulishakataa Speculation.Ni nani anajaribu kumpiku Invisible?Kina nani hawawezi kumkamata Yona?Yona Yupi?

...anajaribu kumpiku Invisible kwa kila kitu. .......Hawawezi kumkamata Yona


Mheshimiwa Gembe, (a.k.a. adui wa Wachaga) naona umefurahishwa na hili la Mchaga kutiwa nguvuni. Je chuki yako kwa wachaga imeshaanza kupungua?
 
Back
Top Bottom