TataMadiba
JF-Expert Member
- Feb 7, 2014
- 9,866
- 5,742
Imeripotiwa katika mtandao wa jamiiforums kuwa kijana wa Kitanzania aishie Scotland, EVARIST CHAHALI kuwa amemtakia kila la heri aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana baada ya kumaliza muda wake wa kutumikia nafasi hiyo ya Katibu Mkuu.
Mbali na kumtakia kila la heri Kinana, Chahali pia amebainisha kile alichodai kuwa ni Kinana kumdhulumu kiasi cha Shilingi za Kitanzania milioni 12.5 , kiasi anachodai aliahidiwa kupewa ili kumpigia Kampeni mgombea urais wa CCM katika uchaguzi mkuu wa 2015.
Inawezekana madai ya Chahali ni ya kweli lakini ukweli zaidi unaoonekana ni kwamba Chahali anatafuta uhalali tu wa kuendelea kuichafua Serikali ya awamu ya tano ambayo kimsingi imejipambanua kupambana na ubadhilifu wa mali ya Umma Uzembe, ufisadi na Rushwa.
Baada ya Porojo za Chahali, Kijana mwingine mshika mapembe ndani ya chama kimoja cha siasa, YERIKO NYERERE ameibuka na kimshambulia CHAHALI na kusema kuwa pesa anazodai kudhulumiwa na kinana zilikuwa apewe ili kumchafua aliyekuwa mgonbea wa CHADEMA, EDWARD LOWASSA.
YERIKO anatoa tuhuma hizo dhidi ya CHAHALI na kutaka kuuonesha Umma wa Tanzania kuwa LOWASSA ni msafi na kwamba tuhuma dhidi yake mwaka 2015 zilikuwa za kumchaafua.tu. YERIKO anatoa tuhuma hizo dhidi ya CHAHLI huku alisahau kuwa mwaka. 2015 huo huo aliandika kwenye mtandao wa kijamii wa Jamiiforums kuwa LOWASSA ni muuaji na hafai hata kuwa mwenyekiti wa nyumba kumi kwa kile alichodai kuwa alianzisha wodi ya vilema wa BODABODA katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa vile ndiye aaliwanunulia vijana hao pikipi.
Kilio hiki bwana Lowassa utakilipia kabla ya 2015
Hitimisho: CHAHALI NA YERIKO wote wanasumbuliwa na njaa tofauti ni njaa zao kuuma nyakati tofauti na pengine kuwa na watu tofauti tofauti wa kutibu njaa zao.
Inawezekana mwaka 2015, Chahali alitegemea kutibu njaa zake kupitia CCM bahati mbaya mambo yakaenda ndivyo sivyo na kwa mantiki hiyo Chahali hana sababu nyingine ya kuichukia Serikali ya awamu ya tano, Serikali ambayo kamwe haiwezi kumruhusu anuse hata harufu ya kuganga njaa kipumbavu hivyo.
Mwaka 2015 Yeriko alikuwa anasumbuliwa na njaa ambayo sasa imetibiwa na LOWASSA baada ya kuhamia CHADEMA.
Nimalizie tu kwa kuwaomba Watanzania kutumia kauli za CHAHALI na YERIKO kupata somo kwamba siyo kila mtu anayejifanya kupiga kelele za kuishambulia Serikali huwa ni kelele zenye sababu za msingi bali wengine wanakuwa wamenyimwa fursa za kuganga njaa zao.
Nawatakia maandalizi mema ya kuanza kulijenga taifa kesho jumatatu baada ya mapumziko ya mwisho wa wiki.
Mbali na kumtakia kila la heri Kinana, Chahali pia amebainisha kile alichodai kuwa ni Kinana kumdhulumu kiasi cha Shilingi za Kitanzania milioni 12.5 , kiasi anachodai aliahidiwa kupewa ili kumpigia Kampeni mgombea urais wa CCM katika uchaguzi mkuu wa 2015.
Inawezekana madai ya Chahali ni ya kweli lakini ukweli zaidi unaoonekana ni kwamba Chahali anatafuta uhalali tu wa kuendelea kuichafua Serikali ya awamu ya tano ambayo kimsingi imejipambanua kupambana na ubadhilifu wa mali ya Umma Uzembe, ufisadi na Rushwa.
Baada ya Porojo za Chahali, Kijana mwingine mshika mapembe ndani ya chama kimoja cha siasa, YERIKO NYERERE ameibuka na kimshambulia CHAHALI na kusema kuwa pesa anazodai kudhulumiwa na kinana zilikuwa apewe ili kumchafua aliyekuwa mgonbea wa CHADEMA, EDWARD LOWASSA.
YERIKO anatoa tuhuma hizo dhidi ya CHAHALI na kutaka kuuonesha Umma wa Tanzania kuwa LOWASSA ni msafi na kwamba tuhuma dhidi yake mwaka 2015 zilikuwa za kumchaafua.tu. YERIKO anatoa tuhuma hizo dhidi ya CHAHLI huku alisahau kuwa mwaka. 2015 huo huo aliandika kwenye mtandao wa kijamii wa Jamiiforums kuwa LOWASSA ni muuaji na hafai hata kuwa mwenyekiti wa nyumba kumi kwa kile alichodai kuwa alianzisha wodi ya vilema wa BODABODA katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa vile ndiye aaliwanunulia vijana hao pikipi.
Kilio hiki bwana Lowassa utakilipia kabla ya 2015
Hitimisho: CHAHALI NA YERIKO wote wanasumbuliwa na njaa tofauti ni njaa zao kuuma nyakati tofauti na pengine kuwa na watu tofauti tofauti wa kutibu njaa zao.
Inawezekana mwaka 2015, Chahali alitegemea kutibu njaa zake kupitia CCM bahati mbaya mambo yakaenda ndivyo sivyo na kwa mantiki hiyo Chahali hana sababu nyingine ya kuichukia Serikali ya awamu ya tano, Serikali ambayo kamwe haiwezi kumruhusu anuse hata harufu ya kuganga njaa kipumbavu hivyo.
Mwaka 2015 Yeriko alikuwa anasumbuliwa na njaa ambayo sasa imetibiwa na LOWASSA baada ya kuhamia CHADEMA.
Nimalizie tu kwa kuwaomba Watanzania kutumia kauli za CHAHALI na YERIKO kupata somo kwamba siyo kila mtu anayejifanya kupiga kelele za kuishambulia Serikali huwa ni kelele zenye sababu za msingi bali wengine wanakuwa wamenyimwa fursa za kuganga njaa zao.
Nawatakia maandalizi mema ya kuanza kulijenga taifa kesho jumatatu baada ya mapumziko ya mwisho wa wiki.