Yehova witness kutimuliwa kwa kukataza wanafunzi kuimba wimbo wa taifa!

Kama hawa wazungu wanataka watu wasiimbe wimbo wa taifa waanzie kwao. Sio kuwadanganya watoto wetu.

Walianza kwao siku nyingi sana.

Mnamo mwaka 1943 Mahakama Kuu ya Marekani iliwapa Mashahidi wa Yehova uhuru wa kukataa kusalute bendera na kutoshiriki wimbo wa taifa (nadhani hapo hata wewe, mzee wa "miaka ya 60" hukuwepo).

11 August 1986 Mahakama Kuu ya India, iliamua kuwapa Mashahidi wa Yehova uhuru wa kukataa kuimba wimbo wa taifa ingawa walikuwa "extreme minority", na asilimia kubwa walipatikana jimbo la Kerala - mmoja wa majimbo mengi.

Namquote Supreme Judge O. Chinnappa Reddy na Justice M. M. Dutt wa India: "We are satisfied, in the present case, that the expulsion of the three children from the school for the reason that because of their conscientiously held religious faith, they do not join the singing of the national anthem in the morning assembly though they do stand up respectfully when the anthem is sung, is a violation of their fundamental right ‘to freedom of conscience and freely to profess, practice and propagate religion.'"

01 March 1993
, huko Philippines, Supreme Court yao iliuphold haki ya Mashahidi wa Yehova kukataa kusalute bendera la Phillipines na kuimba wimbo wa taifa. Hivyo waalimu wa shule za serikali au za private walikatazwa kuwafukuza wanafunzi kwa sababu hizo.


The same for Mexico, Liberia, Paraguay, Haiti, Cuba... Mashahidi wa Yehova wanakataa kuimba wimbo wa taifa ulimwenguni kote siyo TZ peke yake!
Hawa mawitness nakumbuka miaka ya 60 walifukuzwa Tanzania na Malawi kwa uhalifu huo huo.

Kumbuka, asilimia kubwa ya serikali duniani wahaoni kukataa kuimba wimbo wa taifa kuwa uhalifu, wala hakuna sheria inayomlazimisha mtu kuimba. Serikali ya Nyerere, kama serikali yeyote ya kisocialist, ilihitaji conformity, hivyo haikuwapenda Mashahidi wa Yehova kwa sababu walikataa kujihusisha kwenye siasa.

Peter G. Forster, Senior Lecturer, Department of Sociology and Anthropology, University of Hull, England anaandika kwenye kitabu chake "Race and Ethnicity in East Africa":
"R
elations between religion and the state can be particularly problematic in Africa, and recent events in Tanzania and Malawi confirm this. The first post-independence governments of both countries expected religious values to support state ideology more or less uncritically, in return for religious freedom."

Mashahidi wa Yehova ni "non-conformist" kwenye mambo ya siasa kama historia yao inavyoonyesha. Hitler na Stalin waliwachukia sana Mashahidi wa Yehova na kufunga maelfu yao gerezani na kwenye labor camps. Huko Ujerumani walifungwa kwenye concentration camps wakibandikiwa pembe-tatu ya zambarau kwenye uniform/nguo zao kama "kitambulisho" chao (wayahudi walibandikiwa nyota ya njano) kwa sababu ya kukataa kumsalute "Heil Hitler" na kukataa kujiandikisha kwenda vitani kwa kutii maandiko kama Isaya 2:4 na Mathayo 26:52. Madictator wengine wengi wenye kutamani "umoja" wamejaribu kuwatiisha Mashahidi wa Yehova na kushindwa.

Baada ya kufukuzwa wakarudishwa kwa sababu serikali za Tanzania na Malawi ziligundua kuwa walifanya makosa na wataonekana kuwa mmoja wa "oppressive regimes". In fact miaka ya 1970, Nyerere, licha ya kurisk mahusiano mabaya kati ya TZ na Malawi, aliwapa hifadhi Mashahidi wa Yehova waliokimbia Malawi kwa sababu ya siasa ya kibabe ya Kamuzu Banda.
 
Kosa lilifanyika pale tulipoutangazia ulimwengu kwamba Kambarage amefariki....maana huyo ndio waliekua wanamuogopa,,,enzi zake asingekuja Shahidi wala wakili kutuletea UPUUZI huu

Get your history right! Licha ya kuhatarisha mahusiano kati ya TZ na Malawi, Kambarage aliwapa Mashahidi wa Yehova waliokimbia Malawi hifadhi enzi za Banda. Alirealize kuwa MWY hawapose threat kwa taifa lake wala kwa ujamaa.

Pia, Kiranga put it so eloquently:
You are totally missing the point.Katika a free society watu wanaruhusiwa kufanya wanachotaka, hata kama kiko dumb, ilmuradi hakidhuru mtu.

Ndio maana ninasema wanaotaka kuabudu maji sawa, jua sawa, mti sawa.

This is not about whether the Jehovah Witness faith is flawless or not, as far as I am concerned all religions are fraudulent.

This is about freedom of worship, kila mtu awe na uhuru wa kusujudia anachotaka na kukataa kusujudia asichotaka.
 
Kiranga,
Hapana. Hakuna cha Draconian hapa. Hata Biblia inasema mpe Kaisari kilicho chake. Kama hawa wazungu wanataka watu wasiimbe wimbo wa taifa waanzie kwao. Sio kuwadanganya watoto wetu. Hawa mawitness nakumbuka miaka ya 60 walifukuzwa Tanzania na Malawi kwa uhalifu huo huo.


Ahsante sana Mkuu! I salute you!
 
Tena mimi nigekuwa ni serikali ningeisha wafukuza kitambo sana washenzi sana hawa
 
serikali haina mamlaka ya kumwambia mtu aamini nini. Mwishowe kwasababu inapata faida kwenye mabucha ya nguruwe itawalazimisha wasiokula wale.
 
je, hilo dhehebu limesajiliwa kwa mujibu wa sheria zetu?
pindi wanapewa usajili hatukujua utaratibu wao,.!?
 
Wimbo wa taifa ni wimbo wa kuliommbea taifa hili na africa kwa ujumla, Je wao hawataki kuliombea taifa lao? Hao wazungu wanaowashawishi hivyo wao hawaombei mataifa yao?
Cha msingi ni unapotamka Mungu wewe moyoni umaanishe Mungu wako unaemwabudu usimfikirie anaetamkwa na jirani yako.
 
Tatizo ukristo unaji contradict, huku kwenye amri kumi unaambiwa usimsujudie yeyote zaidi ya mungu, huku Yesu anasema mpe Kaizari ya Kaizari.

Hapa hamna anarchy, kwa sababu hamna evil intention, watu wanataka peacefully ku sit out sujuda hizi za serikali, dini yao inawakatataza.Mnaweza kuwalazimisha, lakini mtakuwa kama Nebuchadnezzar aliyewapitisha Daniel Meshack na Abednego kwenye tanuri la moto (supposedly).

Ukishaanza kuwalazimisha watu kuisujudia serikali unaanza religious persecution.

Serikali kama inafanya mambo yake murua mbona hao Witnesses hata asilimia moja hawafiki? Wawaache hao na wengine wote wasiotaka kuimba huo wimbo wachill kivyao, ama sivyo Tanzania ikubali kwamba ni nchi totalitarian inayoshurutisha watu kutenda visivyo kwa mujibu wa dini zao.

Haya mambo yashaongelewa US tangu enzi za kabla ya Vita Vikuu vya kwanza

http://en.wikipedia.org/wiki/Persecution_of_Jehovah's_Witnesses_in_the_United_States

http://en.wikipedia.org/wiki/United_States_Supreme_Court_cases_involving_Jehovah's_Witnesses

Pastor Kiranga katika ubora wake.
 
Last edited by a moderator:
Kutokana na maelezo ha mtoa post... hii ishu ilitokea 2010 na sasa ni 2016, sasa ningetegemea kuona ripoti ya uchunguzi na maamuzi ya mahakama juu ya hili suala.

Ndipo kila mtu ajitathimini juu ya mchango aliotoa juu ya hii issue.
 
Basically kuabudu, kutukuza.
Kwa mfano, wewe kama muislam kweli unaambiwa uimbe wimbo mmoja na wakristo, wimbo unaanza kwa kusema "Mungu Ibariki Afrika" lakini hausemi mungu gani (waislam wengine wakimtaja mungu ni lazima waseme S.A.W, Sasa huyu mungu asiyeeleweka huyu aliye katika wimbo wa taifa mungu gani?
Sio kweli.

S.A.W kirefu chake ni Swalla llahu Alayhi Wassalam.

Hapo kwa sisi Waislam tunamuombea Dua Mtume Muhammad.

Kwahiyo Mtume Muhammad (S.A.W) na si Mwenyezi Mungu
 
Sio kweli.

S.A.W kirefu chake ni Swalla llahu Alayhi Wassalam.

Hapo kwa sisi Waislam tunamuombea Dua Mtume Muhammad.

Kwahiyo Mtume Muhammad (S.A.W) na si Mwenyezi Mungu
Wakimtaja mtume, sorry.

Point yangu ni kwamba, Muislamu anaposema "La ila aillaha Muhammad Rasul Allah" anakuwa kashajiweka kwamba mungu anayemuamini yeye ni yule ambaye Muhammad ni mtume wake, sasa akija mtu mwingine anayesema mungu wake tofauti na huyo mungu ambaye kamfanya Muhammad kuwa mtume wake, halafu wote wawili wake pamoja na kuimba "Mungu Ibariki Tanzania" mungu huyu ni yupo?

Aliyemfanya Muhammad kuwa mtume wake au tofauti?
 
Back
Top Bottom