Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,399
Yaya Toure
Kuna baadhi ya watu wakizungumza kitu basi lazima dunia isimame na iwasikilize hata kama wanazungumza maneno machache sana. Mmoja wa watu wa aina hiyo ni Yaya Toure ambae ni mchezajj nyota wa zamani wa kiungo anaeweza kuitwa "Maestro".
Mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Manchester City ya Uingereza na timu ya taifa ya Ivory Coast Yaya Toure, amemshutumu vikali meneja wa timu ya Manchester City kuwa ni mmbaguzi kwa wachezaji kutoka Afrika.
Akizungumza na jarida ya France Football baada ya kuondoka rasmi kwenye timu hiyo ya Uingereza ambayo imekuwa bingwa tena kwa msimu wa 17/18, Yaya Toure ametoa shutuma hizo kwa Guadiola kwamba amekuwa mbaguzi katika timu za Barcelona na Manchester City dhidi ya waafrika na ameapa kuvunja imani hiyo ya Guadiola.
Mchezaji huyo wa kiungo wa kimataifa ambae amekaa Machester City kwa miaka nane alijiunga na timu hiyo kutoka Barcelona ya Hispania mwaka 2010 ambapo timu hiyo ilikuwa chini ya Guadiola na kwamba ni uamuzi wa Guadiola ndiyo uloruhusu yaya Toure kusajiliwa na Machester City.
Toure mwenye umri wa miaka 35 na ambae pia kwa sasa ni mchezaji wa zamani wa Ivory Coast amesema Guadiola alipokuja Machester City aliamua kwa makusudi kutomchezesha kabisa katika kampeni zote za ligi kuu na hata ile ya kombe la FA la Uingereza kwa sababu tu ya wivu dhidi yake.
Toure amedai katika mahojiano na jarida hilo la France Footbal kwamba si yeye tu kama mchezaji kutoka Afrika ambae anamfikiria hivyo Pep Guadiola bali wachezaji wengi tu kutoka barani humo wana mawazo hayo hasa kwenye ligi la Uhispania ya La Liga.
Toure anasema anataka kuvunja imani hiyo ya Guadiola na anahisi ni wivu na kutaka kumdidimiza mtu mwingine kwa makusudo ya kumvunja moyo.
Anasema kwamba, “kuna wakati huwa tulikuwa tukitizamana kwa namna ya ajabu kana kwamba tuna ugomvi na nilipomkazia macho alikuwa anaonyesha woga na wasiwasi“
Toure anaamini kwamba alitakiwa acheze msimu wote wa 17/18 bila shida lakini badala yake anasugua kiti cha wachezaji wa akiba na huku Guadiola akimsifia kwa vyombo vya habari kuwa ni mchezaji mwenye mchango mkubwa kwa timu yake huku akiwa hachezeshi.
Toure alinza mechi moja tu dhidi ya Brighton na hata kwenye fainali ya kombe la FA dhidi ya Arsenal aliachwa nje licha ya kucheza fainali nne mfululizo kabla ya Guadiola kuja City.
Yaya Toure anasema Guadiola amemnyang’anya nafasi ya kuwaaga wapenzi na mashabiki wa Machester City na alikuwa anapenda aje aagwe kama Andre Iniesta kule Barcelona au Gialuigi Buffoon pale Juventus ambao wameagwa kwa heshima zote.
Anasema “hiyo ni roho mbaya sana na ukatili, unadhani hali hiyo ingeruhusiwa kutokea kwa Iniesta pale Barcelona?”
Toure anasema kwamba ipo siku anasubiri kuona Pep Guadiola akipanga timu yake yenye wchezaji watano wa kutoka Afrika na waso raia wa nchi za Ulaya kama yeye na ikifika siku hiyo atatoa zawadi ya keki.
Akielezea tabia halisi ya Guadiola ni kwamba anapenda kutawala bila kujibiwa na kuna wachezaji ambao wanakuwa radhi kulamba mikono yao kuonyesha kumnyenyekea.
Anasema yeye hayuko tayari kwa aina hi ya uhusiano ingawa namheshimu Guadiola kama meneja wake.
Pep Guadiola ana mtindo wake wa uchezaji ambapo humtumia mchezaji mmoja tu wa kiuongo na mara nyingi katika timu alizopanga alikuwa akimtumia sana MBrazil Fernandihno kama kiuongo mkabaji wake.
NB: Mahojiano ya Yaya Toure yapo kwenye jarida ya France Football.
France Football , toute l'actualité du football