Yawezekana JK ndiye aliyebadiliki Kesi ya DItto

Gembe

JF-Expert Member
Sep 25, 2007
2,483
159
Ndugu wajumbe,

Kwa takribani wiki mbili nimekuwa nikipitia viatbu vya sheria kuona uhallai wa kubadilishwa kwa kesi ya braza ditto kutoka kuua mpaka kuua bila kukusudia,Je ni sheria gani ilitumika?kwa utafiti wangu kwanza nilianza na katiba ya nchi..Ibara ya 45 ambayo inazungumzia uwezo wa kutoa msamaha.
45
.-(1) Bila ya kuathiri masharti mengineyo yaliyomo katika ibara hii, Rais anaweza

kutenda lolote kati ya mambo yafuatayo:-
(a) kutoa msamaha kwa mtu yeyote aliyepatikana na hatia mbele ya mahakama kwa kosa
lolote, na aweza kutoa msamaha huo ama bila ya masharti au kwa masharti, kwa mujibu
wa sheria;
(b) kumwachilia kabisa au kwa muda maalum mtu yeyote aliyehukumuwa kuadhibiwa
kwa ajili ya kosa lolote ili mtu huyo asitimize kabisa adhabu hiyo au asitimize adhabu
hiyo wakati wa muda huo maalum;
(c) kuibadilisha adhabu yoyote aliyopewa mtu yeyote kwa kosa lolote iwe adhabu
tahafifu;
(d) kufuta adhabu yote au sehemu ya adhabu yoyote aliyopewa mtu yeyote kwa ajili ya
kosa lolote au kufuta adhabu yote au sehemu ya adhabu ya kutoza, au kuhozi (au
kuchukua) kitu cha mtu mwenye hatia ambacho vinginevyo kingechukuliwa na Serikali


ya Jamhuri ya Muungano.

ukiangalia kipengele hicho hapo,unaona kabisa Mheshimiwa Rais anapewa mamlaka ya kubadilisha kosa lolote.​

nimetoa Hoja,naomba tuijadili hoja hii na nafikiri hii ni moja ya mapungufu ya katiba yetu,na nafikiri ndio maana ni vigumu hata mafisadi wa EPa kutajwa kwa majina na kushtakiwa,na hivi karibuni broza D atapewa madaraka ya kwuakilisha nchi.​
 
Kipengele hicho cha katiba kinazungumia msamaha kwa mtu ambaye tayari amehukumiwa na anatumikia kifungo gerezani.Ditopile bado ni mtuhumiwa na kesi yake bado iko mahakamani.Kwa hiyo rais hawezi kutumia kipengele kama hicho kwa Ditopile. Labda kama ilifanyika "underground movement tu".

Kesi ya Ditopile kwa sasa ni kati ya mahakama, waendesha mashitaka na mawakili wake, ninachoona hapa, kama kuna mchezo mchafu uliofanyika, basi umefanywa na DPP (Mkurugenzi wa mashitaka), ambaye ndiye huidhinisha na kuainisha aina ya mashitaka (kwa kesi za mauaji) mhalifu anapaswa kushitakiwa nayo kutegemeana na ushahidi uliokusanywa na upande wa upelelezi.

Kwa hiyo, hapa rais hausiki kabisa, japokuwa informally anaweza kuwa na influence fulani. Kwa kawaida rais anapotoa msamaha kwa mujibu wa matakwa ya kisheria aliyopewa na katiba, huwa siyo siri. Taarifa hutolewa na sababu za kutoa msamaha huelezwa pia.
 
Back
Top Bottom