Nzelu za bwino
JF-Expert Member
- Jan 12, 2020
- 376
- 450
Salaam wanajamvi,
Hivi karibuni kumetokea tukio la wabunge wa CHADEMA kujiweka karantini kwa maelezo kuwa wanahofia kuambukizwa Corona. Wametoka bungeni kwa hiari yao wala hawajafukuzwa.
Kwa mujibu wa spika Mh. Job Ndugai alipoulizwa ju kitendo hicho alisema hawajafunja sheria na kanuni yoyote. Pamoja na kutovunja kanuni yoyote wapo watu wanaosema Chadema wamekosea kutohudhuria bunge muhimu na la mwisho hivyo kuwakosesha wananchi uwakilishi bungeni.
Pamoja na hayo, CCM wanakosea zaidi pale wanapowazungumzia CHADEMA muda wote ndani na nje ya Bunge, maana kwa jinsi wanavyoongelewa nikama mna watangaza (promote) zaidi kuliko kuwananga njia nzuri ilikuwa kutowazungumzia kabisa nakujikita kwenye mambo ya msingi bungeni. Kwa hili nikuwakweza sana CHADEMA maana watu wanajiuliza kwa nini wanawalazimisha sana?
Na kwanini inatumika nguvu kubwa kiasi hili? Ushauri Wangu kwa bunge achaneni kabisa na hao Chadema chapeni kazi iliyowapeleka bungeni maana wananchi wanaona ikiwezekana hili bunge la mwisho bila Chadema lingerushwa live.
Nawasilisha.
Hivi karibuni kumetokea tukio la wabunge wa CHADEMA kujiweka karantini kwa maelezo kuwa wanahofia kuambukizwa Corona. Wametoka bungeni kwa hiari yao wala hawajafukuzwa.
Kwa mujibu wa spika Mh. Job Ndugai alipoulizwa ju kitendo hicho alisema hawajafunja sheria na kanuni yoyote. Pamoja na kutovunja kanuni yoyote wapo watu wanaosema Chadema wamekosea kutohudhuria bunge muhimu na la mwisho hivyo kuwakosesha wananchi uwakilishi bungeni.
Pamoja na hayo, CCM wanakosea zaidi pale wanapowazungumzia CHADEMA muda wote ndani na nje ya Bunge, maana kwa jinsi wanavyoongelewa nikama mna watangaza (promote) zaidi kuliko kuwananga njia nzuri ilikuwa kutowazungumzia kabisa nakujikita kwenye mambo ya msingi bungeni. Kwa hili nikuwakweza sana CHADEMA maana watu wanajiuliza kwa nini wanawalazimisha sana?
Na kwanini inatumika nguvu kubwa kiasi hili? Ushauri Wangu kwa bunge achaneni kabisa na hao Chadema chapeni kazi iliyowapeleka bungeni maana wananchi wanaona ikiwezekana hili bunge la mwisho bila Chadema lingerushwa live.
Nawasilisha.