Yatokeayo Marekani yana Historia

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,883
YATOKEAYO MAREKANI YANA HISTORIA

Asiyewahi kuishi na kuijua Marekani atafikiria huko ni kama peponi. Anayeijua vema akiwaambia wabongo kheri bongo kuna amani atafikiria ni masikhara.

Matatizo yatokeayo Marekani kwa utafiti na mtazamo wangu ni kutokana na taifa hilo kuwa na tamaduni/desturi nyingi kwa vile taifa hilo limeundwa kutokana na mataifa mbalimbali duniani.

Kila wenye asili moja huishi utamaduni wao, na kama ni jamii kubwa basi wana siku yao kitaifa na ipo kwenye kalenda ya siku maalum kitaifa.

‍‍‍Kila jamii hufahamiana na hualikana, huajiriana na kuzikana.

Sehemu za starehe zinaendeshwa kadiri ya mwelelekeo wa kiasili ingawa hakuna sheria hiyo.

Jamii kubwa nchini Marekani ni wazungu, waafrika, waspanishi, waasia na wakimbizi kutoka nchi zilizovamiwa na Marekani kivita.

Wenye asili ya Marekani wahindi wekundu mfano kama kabila la Cherokee wamemezwa na sio lolote kwa Marekani.

WHITE PEOPLE

Walitokea bara la Ulaya kutoka nchi mbalimbali wakaingia Marekani kwa sababu za ukata, uhuru kiuchumi na kidini, nk.

Walipoingia Marekani Kila jamii moja ilichukua sehemu moja na kuifanya nchi/koloni lao. Waingereza, wafaransa na wajerumani ndio walikuwa makundi yenye nguvu zaidi.

Tuonavyo siku hizi state 52 kabla ya kuungana zilikuwa nchi 51 tukiiondoa Alaska iliyonunuliwa baadaye kutoka Urusi.

AFRICAN AMERICAN

Hawa waliongizwa nchini humo kwa nguvu kama watumwa. Wakati huo Marekani ilikuwa haijaungana hivyo zilikiwa nchi mbalimbali.

Hilo ni kundi linalofuata kwa wingi wa idadi baada ya wazungu.

Wamarekani weusi ni magwiji wa vurugu, uvunjaji sheria na kuzitafsiri sheria kama chombo cha kuwakandamiza.

SPANISH PEOPLE

Asili yao ni Amerika ya Kati na kusini. Waliingizwa nchini humo kwa mikataba baina ya nchi zao na Marekani.

Malengo ya kuingizwa nchini humo ni kama wafanyakazi vibarua wa mashambani, ujenzi, usafi, kutunza wazee nk.

Hilo ni kundila tatu kwa, wingi wa wakazi nchini humo.

Hawa nao ni maarufu kwa ujambazi, vurugu na uvunjaji sheria kutokana na asili ya kutoka kwenye nchi zao.

ASIAN AMERICAN

Hawa waliingia kwa mgongo wa kiuchumi. Wahindi wanaongoza kwa ubora kiuchumi na ndio kitakwimu wahindi wanaongoza kwa usomi, kiuchumi na maisha bora miongoni mwa wahamiaji wa karne ya sasa nchini Marekani.

Wapo wa kutoka China wengi pia. Waasia ni wa nne kwa population.

WAKIMBIZI

Zipo jamii nyingi zilizoingizwa nchini humo kwa title ya ukimbizi kutokana na vita kwa nchi zao kuvaniwa na Marekani. Baadhi ya nchi kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Ajabu vita ilipokuwa inaendelea kuna taasisi za kimarekani zilizoratibu kukusanya wakimbizi na kuwapeleka kwako.

Wakimbizi walipewa haraka sana uraia na kufanywa vibarua.

Wakimbizi na waspanish ndio walioziba mwanya wa kuingiza watumwa nchini humo.

Wapo wakimbizi kutoka Vietnam, Iraq, Misri, Sudan, Somalia, Ethiopia/Eritrea, Wanyarwanda nk.

MAISHA NCHINI MAREKANI

Sheria za Marekani zilivyo ni nzuri sana, lakini ukiangalia maisha sheria nyingi zipo vitabuni tofauti na kinachoendelea katika jamii mbalimbali.

Ubaguzi ni donda ndugu baina ya wazungu, weusi, waspanish, waasia na wengineo.

Weusi wanaongoza kwa violence nchini humo, ukiangalia kwa ukweli nyingi ya vurugu hazina msingi, ni kizazi chenye vurugu.

Waspanish wanafuatia kwa violence kutokana na asili za nchini zao vurugu ni asili yao.

Ubaguzi katika kazi, upendeleo wa ajira na malipo kazini kwa wazungu kupewa priority huchangia weusi na Spanish ambao ni jamii zinazofuatia kwa wingi nchini humo kujisikia minority groups.

Athari za madawa ya kulevya huchangia pia machafuko na mauaji nchini humo. Biashara hiyo ni maarufu kwa unemployed people. Ilikadiriwa kitakwimu miaka mitano iliyopita kuwa robo ya wamarekani ni waathirika wa madawa ya kulevya.

All in all, gun control wazungu wanahofu ikipitishwa watakuwa waathirika, lakini kinachoendelea maafa ndio yanaongezeka.
 
Ahsante kumbe hata wazungu huko sio kwao!!! nilikuwa sijui ila alinijuza Nyani ngabu na wewe pia umetilia mkazo, ahsanteni sana
 
kuna wale walioukana uraia wao ili wapate uraia wa huko mbona hujawataja ?
 
Back
Top Bottom