Yanga kutangaza utalii kwenye jezi yao kimataifa

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Jan 1, 2017
20,504
44,615
Klabu ya Yanga imeamua kutangaza utalii katika jezi zao katika mechi za kimataifa! Wamefikia makubaliano hayo na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia waziri wa wizara hiyo Dr. Damas Ndumbaro.

Yanga itatangaza bure Mlima Kilimanjaro pamoja na Visiwa vya marashi na karafuu (Zanzibar).
"Tumeamu kuunga mkono juhudi za Mh. Rais kwa kutangaza utalii kama alivyofanya kwenye royal tour" Alisema Kaimu CEO wa Yanga, Haji Mfikirwa.

Nembo hiyo ya kutangaza Utalii itakaa upande wa kushoto wa jezi hiyo!

Hii si mara ya kwanza kwa klabu ya Tanzania kutangaza utalii katika mechi za kimataifa, msimu uliopita Simba walitangaza utalii katika jezi zao walipokuwa wanashiriki hatua ya makundi ya klabu bingwa Afrika!

Hongereni Yanga, kuiga vitu vizuri sio jambo baya!!

396229DD-D93D-4671-9F5A-79F516F27FF7.jpeg
 
Ni jambo la kheri,japo haijakaa vyema sana...
Nao wangeandika Visit Tanzania sidhani kama Simba wangewakawatalia kwa kigezo cha kuiba idea

Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
Idea ilianzia ulaya huko, na zaidi tukaona kwenye jezi za Arsenal "Risit Rwanda" Simba akakwapua humo ati sasa anajiona ndio mbunifu, ujinga mtupu.
 
Hiyo project ya yanga na hao wizara ya utalii ni white elephant project..yanga na kimataifa wapi na wapi? Si wanaenda kukamilisha ratiba Nigeria kisha waanze Ruti za Namungo na ruvu
Waziri wa Utalii alisema kuwa anaamini Yanga wataenda kupindua meza Nigeria
 
Wazee wa kuiga hahaa
Mbona wabongo tunataka kuwa empty set sana vichwani mwetu?
Jambo jema lazima lifanyike, mbona kuna vist Rwanda ,ilipoanzishwa ya simba ulisijia wao wamesema wamekopy? Tumia akili kidogo msilete usimba na uyanga maandazi nyie mashabiki 2018.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom