Yanga kulilia Ufadhili wa Manji: Taswira ya Taifa letu, kutegemea Wafadhili!

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Ni aibu gani hii ambayo watu tunaishia kuwa ombaomba na kutegemea wafadhili mpaka tunaamua wanastahili wapewe madaraka?

Najua wengine wenu mtaliangalia jambo hili kama suala la mpira na ushabiki wa michezo, lakini kitendo cha wachezaji wa Yanga kumlilia Manji ni sawa na kile kitendo cha wale waliomlilia mkoloni na kumtukuza au wale manamba waliokuwa kwenye mashamba ya Wagiriki ambao waliwaabudu hao Wagiriki. Na nikiongezea ni jinsi Wana wa Israeli ambao waliona kuwa safari yao ya kwenda kwenye nchi walioahidiwa ilikuwa ni udhia na hivyo wakajuta kuyaacha masufuria ya Pharao!

Ni lini Tanzania tutaachana na mambo ya kuwalilia na kuwanyenyekea hawa watu tunaowaita Wafadhili?

Jambo hili si la Simba au Yanga pekee, ni LIUGONJWA kubwa na baya kuliko Malaria na Ukimwi!

NI lini jamii na jumuiya zitaanza kujituma na kubuni mbinu za kuweza kujitegemea na kujizalishia bila kutumai cha mfadhili?

Kibaya zaidi ni kuwa Manji huyu huyu, ni mtuhumiwa wa kuhujumu Uchumi wa nchi, sawa na wakati wa Gulamali na Dewji, nao walikuwa na tuhuma kibao za kuwa ni wafanyabiashara wa mambo haramu ambao walijipendekeza ndani ya klabu za mpira na hata ndani ya Siasa kiasi kufikia kwa Gulamali kuwa mbunge!

Kuna haja ya kufanyika tathmini na kampeni kubwa mno ya kupiga vita ombapmba na kutegemea Wafadhili.

Mimi ni Yanga, lakini kitendo hiki, kimenidhalilisha na kunisononesha, sawa na vile CCM inavyoendelea kukumbatia Wafadhili ambao wametuhujumu na kuangamiza uimara wa Serikali yetu na maadili ya Taifa letu.

Jambo hili linaonyesha wazi ni vipi Tanzania ilivyo mbali sana kufikia azma ya kuwa Taifa linalojitegemea na kujenga jamii ya watu wenye kujitegemea!

Narudia tena hii ni aibu kubwa sana kwetu kama Taifa, na sijali ikiwa wewe ni mshabiki wa Simba au Chadema, lakini hii ni hali halisi ya kisiasa na kijamii ya Tanzania kutegemea ufadhili kwa kila kitu.

Tanzania tunapenda sana misaada, lakini kujituma tujizalishie kwa mbinu na juhudi zetu wenyewe hakuna!

Asilimia 40 (40%) ya bajeti ya nchi inategemea Wafadhili. Wiki hii Serikali kupitia Hazina na Benki Kuu wametangaza tumefadhiliwa misaada si chini ya Dola za Kimarekani Millioni Mia Tatu!

Za nini fedha hizi? kwa nini tunaendelea kama Taifa kuwalilia kina Manji na hata kuwaomba wawe wagombea wa nafasi ya juu katika jamii yetu?

Ama tumelaaniwa!
Wachezaji Yanga wamlilia Manji‏

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 28th December 2009 Habari Leo

WACHEZAJI na wanachama wa Yanga wamesikitishwa na kitendo cha aliyekuwa mfadhili wao, Yusuf Manji, kujiondoa katika nafasi hiyo na kusema hayo yamesababishwa na viongozi wao.

Manji alitangaza uamuzi wake wa kujiondoa Yanga juzi na kusema ameamua kufanya hivyo, kwa vile klabu hiyo inaweza kujiendesha yenyewe.

Wachezaji hao ambao hawakutaka majina yao kutajwa waliulaumu uongozi wao kwamba ni chanzo cha mfadhili huyo kujitoa.

"Viongozi ndio chanzo cha yote hayo, si unaona hata kwenye taarifa yake alivyosema kwamba alichukizwa na namna usajili ulivyofanywa... usajili ulikuwa mbovu kabisa hauna kiwango chochote," alisema mmoja wachezaji mahiri katika kikosi cha Yanga.

"Tatizo viongozi wetu walikuwa kama sijui wanamuogopa Kondic (Dustan aliyekuwa kocha wa timu hiyo) alipendekeza kusajili wachezaji wabovu kwa hela nyingi matokeo yake tukawa tunafanya vibaya kwenye ligi," aliendelea kusema mchezaji huyo.

"Sasa hii imekuwa balaa tunajua huu ndio mwanzo wa kusambaratika na kuvurugana, sasa hivi utasikia sijui Yanga katiba, sijui nini," aliongeza mchezaji mwingine aliyesajiliwa msimu uliopita.

Kwa upande wa wanachama wamepanga kumuandikia Manji barua ya kumuomba arejee tena kuifadhili timu yao.

"Tutamuomba Manji akubali kurudi tena kutufadhili, uzembe wa viongozi ndio umetuponza, sasa Manji ameondoka unadhani nani tena ataifadhili klabu yetu kama alivyokuwa akifanya yeye?" alisema mmoja wa wanachama Hamisi Hassan.

Baada ya taarifa za Manji kujiengua Yanga kusambaa juzi, kundi la wanachama wa Yanga maarufu kama Yanga bomba walifunga safari mpaka kwenye ofisi za mfanyabiashara huyo na kumuomba wazungumze naye jambo ambalo lilifanyika, lakini mfanyabiashara huyo aligoma kubadilisha uamuzi wake.

"Tuna imani Manji anaipenda Yanga sema tu watu wachache kwa kujinufaisha wao ndio waliomuudhi, lakini bado sisi wanachama na mashabiki wa Yanga tunapanga tena jinsi ya kwenda kumuona na kujaribu kumuomba arudi kwenye timu yetu," alisema mwanachama mwingine Elitosha Gabriel.

Kwa muda mrefu Manji amekuwa msaada mkubwa kwa Yanga ambapo hutoa fedha za usajili, mishahara ya wachezaji na benchi la ufundi pamoja na fedha za maandalizi kwa timu inapokabiliwa na mechi ngumu, iwe ya kitaifa au ya kimataifa.

Kabla ya Manji kufikia uamuzi huo, Baraza la wazee wa Yanga lilimuomba agombee nafasi ya uenyekiti katika uchaguzi unaotarajia kufanyika hivi karibuni.

Hata hivyo Manji aliahidi angejibu ombi hilo juzi na badala yake alitoa barua ya kujiondoa kama mfadhili wa Yanga.




Manji's 'behaviour' disappoints Yanga‏


FELLEN MANOCHI, 28th December 2009 Daily News

YOUNG Africans have said that they are disappointed with the way the former sponsor, Yusuf Manji, used when announcing his exit from the club.

The club's Chairman, Imani Madega, told reporters in Dar es Salaam today that Manji was supposed to present his letter to the club leadership and not the elders' council.

"We are very disappointed with this behaviour. We had expected him to come to us and present his case instead of communicating to wrong people", he said.

Manji, who started to sponsor the team in 2006, announced on Saturday that he was stopping his financial support, citing various reasons.

He argued that Yanga is a big club that could meet its own financial obligations through its own sources of income and that depending entirely on one person to bankroll them was wrong.

However, Madega is not moved either by the reasons. He said that Manji was 'mixing' two issues at a go.

"He was asked by the elders to contest the club's chairmanship during the coming polls next month. So, he was supposed to reply the letter by saying yes or no. Period", he said.

He said that the sponsorship was not part of the requests in the letter and that he erred by bringing the two issues at a single point.

Madega said that the club leaders were still waiting for a 'formal' letter from him which explains about his exit.

"We still count him as the club's chief sponsor until he has formally written us", he said.
However, he said that the club has no ill feelings against him.

"We wish him all the best if really he has quit. Yanga is a brand name that can attract many sponsors. So, it's wrong to assume that the club will die without sponsors", he said.

He said that the challenge now is to look for new sponsors.

Currently, Kilimanjaro Premium Lager beer brand sponsors the team.
 
yanga hawajui nani hasa ni ''mfadhili wao''!wanadhani ni manji:D
 
Rev.Kishoka, Niliisikia habari hii jana kwa masikitiko makubwa sana. Hivi sisi tatizo letu kubwa katika akili zetu ni nini? Bila kuwa na neno wafadhili ndio hatuendi mbele? na mbaya zaidi ufadhili huo hatujali unatoka kwa nani. Unamtuhumu mtu kakuibia usiku na asubuhi unampigia magoti kumwomba sukari.
Natatizo hili la ombaomba haliko ktk Club tuu, hata serikali yetu ndio usiseme maana mpaka inajisifu kama vile kuomba ni SIFA.
 
Tatizo pesa, wanachama hawachangi pesa, Vilabu vingi vimekufa kwa ajili ya pesa wamekosa wafadhiri, nyie mnafikiri bila NMB na Serengeti Taifa Stars ingeng'aa hivyo? Ziko wapi Lipuli, Costal, Bandari, Pamba n.k zote zimekufa kwa ajili ya kukosa ufadhiri.
Angalieni na huko majuu Man U, Liverpool, Chelsea zinaendeshwaje?
 
Tatizo pesa, wanachama hawachangi pesa, Vilabu vingi vimekufa kwa ajili ya pesa wamekosa wafadhiri, nyie mnafikiri bila NMB na Serengeti Taifa Stars ingeng'aa hivyo? Ziko wapi Lipuli, Costal, Bandari, Pamba n.k zote zimekufa kwa ajili ya kukosa ufadhiri.
Angalieni na huko majuu Man U, Liverpool, Chelsea zinaendeshwaje?

CCM mbona wanachangisha wanachama na kuchota kutoka Serikalini lakini bado inawakimbilia Wafadhili kama kina Manji na Rostam?
 
yanga itashaini tu mwanzo mwisho!mfadhili wa yanga si MANJI!manji anatumiwa tu.....!stuka
 
watu wanaaminiwa na kupwa nafasi ili kutumikia lakini cha ajabu wanataka kutumikiwa wao badala ya wao kutumikia taifa/taasisi waliyopewa..........maslahi binafsi yalisumbua taifa hili................watu wamechoka kufikiri kwa hiyo pamoja na kupwa nafasi bado wanataka watu wengine wafikiri kwa niaba yao...............
inatia aibu..
 
Nahisi kama nimesahau mawani yangu! Ni wewe au kuna mtu kakamata pasiwedi yako?
mkuu,
yanga haiwezi kutetereka!yanga inafadhiliwa na mkuu mwenyewe!sema anamtumia manji...!naona manji amechoka KUTUMIKA!wana-yanga wasipate shida:D
 
mkuu,
yanga haiwezi kutetereka!yanga inafadhiliwa na mkuu mwenyewe!sema anamtumia manji...!naona manji amechoka KUTUMIKA!wana-yanga wasipate shida:D

Karibu msimbazi pale. Friends Of Mnyama tuna kikao leo.
 
Yanga hawajui kuwa walikuwa wanatumiwa tu. Manji aliingia kuifadhili Yanga baada ya kuona Mengi anawashauri namna ya kujitegemea pale alipowashauri wajiendeshe kibiashara baada ya kuwa amewalipia tiketi za kwenda kucheza South Africa katika mojawapo ya mashindano yaliyokuwa yakiwakabili. Manji alitaka Yanga wasiwe na hayo mawazo ya kujiendesha kibiashara ili ................
 
wanaoiua yanga TUNAWAJUA!na kwakweli leo nitamuomba mungu ujasiri niwataje hawa watu!.....
 
sisi watanzania tutaendelea kutawaliwa hadi lini sijui!!? yaani club inawanachama malaki lakini bado inategemea mtu mmoja aiongoze kifedha!! Huu ndio ukoloni mamboleo aliouita Mwalimu Nyerere...
 
Ni aibu gani hii ambayo watu tunaishia kuwa ombaomba na kutegemea wafadhili mpaka tunaamua wanastahili wapewe madaraka?

Najua wengine wenu mtaliangalia jambo hili kama suala la mpira na ushabiki wa michezo, lakini kitendo cha wachezaji wa Yanga kumlilia Manji ni sawa na kile kitendo cha wale waliomlilia mkoloni na kumtukuza au wale manamba waliokuwa kwenye mashamba ya Wagiriki ambao waliwaabudu hao Wagiriki. Na nikiongezea ni jinsi Wana wa Israeli ambao waliona kuwa safari yao ya kwenda kwenye nchi walioahidiwa ilikuwa ni udhia na hivyo wakajuta kuyaacha masufuria ya Pharao!

Ni lini Tanzania tutaachana na mambo ya kuwalilia na kuwanyenyekea hawa watu tunaowaita Wafadhili?

Jambo hili si la Simba au Yanga pekee, ni LIUGONJWA kubwa na baya kuliko Malaria na Ukimwi!

NI lini jamii na jumuiya zitaanza kujituma na kubuni mbinu za kuweza kujitegemea na kujizalishia bila kutumai cha mfadhili?

Kibaya zaidi ni kuwa Manji huyu huyu, ni mtuhumiwa wa kuhujumu Uchumi wa nchi, sawa na wakati wa Gulamali na Dewji, nao walikuwa na tuhuma kibao za kuwa ni wafanyabiashara wa mambo haramu ambao walijipendekeza ndani ya klabu za mpira na hata ndani ya Siasa kiasi kufikia kwa Gulamali kuwa mbunge!

Kuna haja ya kufanyika tathmini na kampeni kubwa mno ya kupiga vita ombapmba na kutegemea Wafadhili.

Mimi ni Yanga, lakini kitendo hiki, kimenidhalilisha na kunisononesha, sawa na vile CCM inavyoendelea kukumbatia Wafadhili ambao wametuhujumu na kuangamiza uimara wa Serikali yetu na maadili ya Taifa letu.

Jambo hili linaonyesha wazi ni vipi Tanzania ilivyo mbali sana kufikia azma ya kuwa Taifa linalojitegemea na kujenga jamii ya watu wenye kujitegemea!

Narudia tena hii ni aibu kubwa sana kwetu kama Taifa, na sijali ikiwa wewe ni mshabiki wa Simba au Chadema, lakini hii ni hali halisi ya kisiasa na kijamii ya Tanzania kutegemea ufadhili kwa kila kitu.

Tanzania tunapenda sana misaada, lakini kujituma tujizalishie kwa mbinu na juhudi zetu wenyewe hakuna!

Asilimia 40 (40%) ya bajeti ya nchi inategemea Wafadhili. Wiki hii Serikali kupitia Hazina na Benki Kuu wametangaza tumefadhiliwa misaada si chini ya Dola za Kimarekani Millioni Mia Tatu!

Za nini fedha hizi? kwa nini tunaendelea kama Taifa kuwalilia kina Manji na hata kuwaomba wawe wagombea wa nafasi ya juu katika jamii yetu?

Ama tumelaaniwa!
[/FONT]
Kumbe nchi yenyewe inategemea wafadhiri ambao ndio hao waliotutawala na kutunyonya,iweje leo ukaituhumu Yanga kukumbatia mfadhiri,au ndio ile adui yako mwombee njaa?Nina wasiwasi we si mwenzetu ila unatumiwa tuu.
 
Mimi sishangai baadhi ya wana Yanga kulilia ufadhili wa Manji kwani hii imeshakuwa sehemu ya utamaduni wa Watanzania walio wengi! Manji ameeleza vizuri sana kuhusu malengo aliyojiwekea wakati alipoamua kuisaidia Yanga na sasa ameona ni wakati mwafaka kuiacha Yanga ijiendeshe yenyewe kwani inaouwezo huo! Hoja tunayopaswa kuijadili hapa ni kuwa iweje Manji aone uwezo Yanga ilionao lakini Viongozi wa Yanga,Kundi la Wazee,Wachezaji na Mashabiki wanaogaragara mlangoni kwa Manji wasione ? Tatizo la Watanzania walio wengi hawaamini kuwa wanaweza kufanya jambo lolote kwa mipango waliojiwekea bila wafadhili,iwe ni katika siasa, michezo,uchumi,dini n.k.
Labda kitu ambacho napenda kuwajulisha Watanzania wenzangu ni kuwa kuna Watanzania wenzetu ambao wameamua kuishi katika Nchi yao iitwayo "Mediocrity Country" .Hii ni Nchi mpya inayopatikana ndani ya Tanzania na Jiografia yake iko hivi ;Upande wa kasikazini inapakana na Nchi iitwayo ''Compromise" ,upande wa Kusini inapakana na Nchi iitwayo "Indecision" ,upande wa magharibi inapakana na Nchi iitwayo "Past thinking" na Upande wa Mashariki inapakana na Nchi iitwayo "Lack of Vision".Kosa kubwa tulilofanya Watanzania ni kuwapa nafasi Watu wa Nchi hii mpya niliyoitaja kushika Madaraka makubwa katika Nchi yetu ya Tanzania kuanzia katika siasa,michezo,dini n.k.Sifa kubwa ya Watu wa nchi hiyo ya Mediocrity ni kwa wao ni "Normal People".Tusikubali kuongozwa na watu wa Nchi hiyo kama kweli tunataka maendeleo katika kitu chochote katika Nchi yetu!
 
Kama leo Yanga ikiamua kuuza hisa zake kwenye Dar Stock Exchange,watu wengi watanunua!Mnakumbuka Yanga Kampuni na Yanga Asili.Wazo la kampuni lililetwa na Mengi karibu miaka 10 iliyopita!Wahindi walipinga maana wanajua wanachokinya.Ndio hapo Mhindi na Mengi hawakai pamoja.
Mbali zaidi "waswahili" Yanga always watanunuliwa na Wahindi.

Manji anatuhuma kubwa lakini in Tanzania mambo ni big joke.
 
Yanga hawajui kuwa walikuwa wanatumiwa tu. Manji aliingia kuifadhili Yanga baada ya kuona Mengi anawashauri namna ya kujitegemea pale alipowashauri wajiendeshe kibiashara baada ya kuwa amewalipia tiketi za kwenda kucheza South Africa katika mojawapo ya mashindano yaliyokuwa yakiwakabili. Manji alitaka Yanga wasiwe na hayo mawazo ya kujiendesha kibiashara ili ................
Kichuguu, maneno yako yamenikumbusha usemi mmoja kule kwa marehemu babu yangu. Alisema, ndugu yako akiwa na shida ya chakula kama unampenda mpe jembe na mbegu na sio unga maana na kesho na siku inayofata atakuja tena huku akidhalilika kwa kuomba.
Mengi aliwapenda Yanga ndio maana aliwashauri jinsi ya kujinasua na uombaji na wajitegemee kwa kutumia rasilimali zao, lakini wao wakaona Manji anayewapa Unga wapike ndio anawapenda zaidi. Ok,Ndiyo Tanzania yetu ilipofikia
 
Kumbe nchi yenyewe inategemea wafadhiri ambao ndio hao waliotutawala na kutunyonya,iweje leo ukaituhumu Yanga kukumbatia mfadhiri,au ndio ile adui yako mwombee njaa?Nina wasiwasi we si mwenzetu ila unatumiwa tuu.
He he heee, Yanga-Bomba wewe !! Mbona Mo aliposema basi kwa Mnyama hawakuandamana? Tatizo viongozi wa Yanga (na Simba pia) hawana mikakati ya kweli, ndo maana akishatumikia miaka kadhaa anaona ameshajijengea jina, utamsikia ameenda kugombea ubunge, hayo ndio malengo yao. Kwani hukushtukia viongozi wa Yanga wanalazimisha uchaguzi wa klabu ufanyike haraka kabla ya muda wao wa madarakani haujaisha? Walishaona watachelewa kwenye maandalizi ya majimboni 2010.
 
Back
Top Bottom