Jamani mbona Yanga wanatuonea hivi? Jamaa wanataka sifa sana. Yaani pamoja na fedha zao, kila siku Yanga wanaona waishi kwa mgongo wetu sisi simba na mbaya zaidi viongozi wetu hawatoi maelezo ya kina! Nakumbuka ni Yanga hawa hawa walituibia fedha za rambi rambi ya marehemu Mutesa Mafisango hadi Simba tukaahibika kule Congo! Viongozi wetu wakakaa kimya!!! Sasa wamemchukua Twite wetu tumenyamaza. Mimi nahisi viongozi wetu ndo wanatuhujumu kwa njaa zao hasa huyu Rage!! Huyu katudanganya kuwa alimpatia Twite dola 30,000 lakini siyo, ndo maana kaufyata. Lakini mbaya zaidi wanatuhujumu kiasi hiki viongozi wanakalia kubishana tu na kutuyumbisha. Alafu hujuma hizi zinachangiwa na viongozi wetu kutaka sifa pia kwa kila kiongozi kusajili wachezaji wake. Ajabu hii yaani timu moja lkn wachezaji makundi tofauti. Hii siyo sawa.