Yanga huru

Balantanda

JF-Expert Member
Jul 13, 2008
12,476
4,752
Kamati ya nidhamu ya TFF imewafungulia mabingwa wa soka wa Tanzania,Yanga kutoka katika adhabu iliyokuwa imepewa na TFF kufuatia Yanga kutopeleka timu uwanjani katika mchezo wa kombe la Kagame dhidi ya Simba..............Hata hivyo licha ya kufunguliwa Yanga imetozwa faini ya dola za kimarekani 20000(elfu ishirini) pamoja na viongozi wake kutakiwa kuomba radhi kwa TFF kwa kitendo kisichokuwa cha kiuanamichezo cha kutopeleka timu uwanjani..............Mwenyekiti wa kamati ya nidhamu ya TFF SAID HAMAD EL-MAAMRY amesema kwamba kamati yake imetengua uamuzi huo wa TFF kwa vile hakuna kifungu kinachoeleza adhabu ya miaka miwili(02) kwa timu itakayogoma kuingia uwanjani.Kwa hali hiyo TFF ilitakiwa kutumia kifungu cha adhabu cha FIFA ambacho ni adhabu hiyo (ya dola 20000) iliyotlewa na kamati ya nidhamu ya TFF
 
Kamati hiyo inadaiwa imeona kuwa TFF haikupaswa kuiadhibu Yanga kutokana na kuwa mwenyeji tu wa michuano hiyo inayosimamiwa na Baraza la soka la Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).................Hata hivyo akina El Ma-amry walijadili rufaa hiyo licha ya pingamizi kubwa toka kwa wawakilishi wa TFF katika kikao hicho Katibu Mkuu Fredrick M wakalebela na Mkurugenzi wa Ufundi Sunday Kayuni waliojenga hoja kuwa kamati hiyo haina mamlaka ya kujadili rufaa hiyo................Hali hiyo ilisababisha ubishani mkali ulioanza saa 10:10 jioni hadi 12:17 jioni nabaadae kamati ilikaa na kumaliza kikao chake kwenye saa moja na nusu usiku (www.ippmedia.com/ipp/nipashe/2008/08/120320.html
 
Ukitaka kudhitibisha mpira wa bongo 'utumbo' mtupu embu sikia ya hapo juu.....yaani hata TFF hawajui sheria zao wenyewe walizotunga?... #$%@&...
Kwa wengine tulijua tu..kwamba ile adhabu ilikuwa kama 'dua ya kuku' vile, yaani waifungie Yanga/Simba wakale wapi?

Scrap....scrap...scrap...scrap!!
 
Sasa itakuwaje wakati tunaambiwa hata CAF vilevile waifungia Yanga?

achana na magazeti ya udaku hayo.
yanga ilianzishwa 1935 hivyo hao kina tenga na mwakalebela sisi tunawaona machizi tu kwa sababu yanga ilikuwepo kabla ya wao kuzaliwa so hawawezi kukurupuka tu na kuifungia yanga.
 
na ushindi ule tulioupata yanga katika adhabu dhidi ya TFF ni salaam kwa Musonye na wajaluo wenzake wasiofahamu nini maana ya tohara....naomba kuwasilisha salaam
 
unaongelea nini, kwanini usitoe huo upuuzi wako, mimi naomaba TFF waliangalie upya tena hili swala kama hawana sheria za kuwa zibiti wahawa wanao vamia soka wazitunge ili ikitokea tena kiongozi akatoa uamzi walioutoa akina madega na wenzake wafutwe kabisa yaani wasijihusishe na soka tena.....
 
unaongelea nini, kwanini usitoe huo upuuzi wako, mimi naomaba TFF waliangalie upya tena hili swala kama hawana sheria za kuwa zibiti wahawa wanao vamia soka wazitunge ili ikitokea tena kiongozi akatoa uamzi walioutoa akina madega na wenzake wafutwe kabisa yaani wasijihusishe na soka tena.....

Unazungumzia upuuzi upi mkuu????????.....maana yameongelewa mengi sasa sijui ni upuuzi upi unataka uondolewe.....kuwa specific mkuu
 
achana na magazeti ya udaku hayo.
yanga ilianzishwa 1935 hivyo hao kina tenga na mwakalebela sisi tunawaona machizi tu kwa sababu yanga ilikuwepo kabla ya wao kuzaliwa so hawawezi kukurupuka tu na kuifungia yanga.
Haya mambo hayataisha kirahisi hivyo; angalia hii ya leo kwenye Majira

TFF haitambui kufunguliwa Yanga
*Yakataa kupokea faini hadi kamati ikutane
*El-Maamry asema amemaliza kazi yake

Na Suleiman Mbuguni

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limesema halitapokea faini ya dola 20,000 kutoka kwa uongozi wa Yanga, hadi hapo Kamati ya Utendaji ya shirikisho hilo itakapokutana Septemba mwaka huu.

Yanga ilipigwa faini ya dola 20,000 na Kamati ya Nidhamu ya TFF inayoongozwa na mwanasheria Said El-Maamry, baada ya kukata rufani kupinga adhabu ya kufungiwa miaka miwili kucheza michuano ya kimataifa iliyotolewa na Kamati ya Utendaji ya TFF, baada kugoma kupeleka timu kucheza na Simba mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu michuano ya Kagame.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa TFF, Fredrick Mwakalebela alisema Sekretarieti ya shirikisho hilo tayari imepokea rasmi uamuzi wa Kamati ya Nidhamu iliyokutana mwishoni mwa wiki, lakini suala hilo litapelekwa kwenye Kamati ya Utendaji kwa kuwa ndiyo iliyoifungia Yanga.

Katibu huyo alisema yeye hawezi kutoa uamuzi wowote juu ya faini ya Yanga na hata kama klabu hiyo ingepeleka faini jana asingeipokea hadi atakapopata mwongozo kutoka Kamati ya Utendaji.

Habari kutoka ndani ya Yanga zilieleza kuwa uongozi wa klabu hiyo, jana ulipanga kupeleka faini hiyo, lakini ikashindikana kutokana na kutokuwa na barua ya TFF ya kuwajulisha juu ya faini hiyo.

Habari hizo zilidai kuwa uongozi huo unasubiri barua hiyo, ingawa habari kutoka TFF zilieleza tayari Yanga imefahamishwa juu ya uamuzi wa Kamati ya Nidhamu kupelekwa kwenye Kamati ya Utendaji.

Alipoulizwa El-Maamry kuhusiana na uamuzi huo wa TFF, alisema tayari kamati yake ilishatoa uamuzi kuhusiana na suala la Yanga, hivyo kama TFF haitaki kupokea faini ni jukumu lao.

Alisema katika uamuzi wao waliipiga faini, waliwapa onyo viongozi wa Yanga na kuitaka klabu hiyo iombe radhi, hivyo kimsingi jukumu lao wamelimaliza na kama TFF itaamua vinginevyo ni wao wenyewe
MAJIRA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom