Yanga dhidi ya Simba, ukweli lazima usemwe

marcoveratti

JF-Expert Member
Sep 21, 2017
915
1,580
Hemed Suya.

Kwanza nianze kwa kuwasalimu, na kuwatakia Eid l-Adh-ha Mubaarak jamii yote ya wapenda soka.

Jion hii nalazimika kushika kalamu kuandika baada ya kumaliza mialiko ya nyama kutoka sehemu mbali mbali na sasa nikiwa nimeshiba vyema naukumbuka mjadala unaoendelea mitandanoni kumhusu Dismas Ten nami nalazimika kuweka machache sana kumhusu.

1. Ten analaumiwa kwa kushindwa kuwahamasisha wanayanga kwenda uwanjan kushangilia mechi yao dhid ya Township Rollers, Ten analaumiwa eti hafanyi kama Manara kuhamasisha watu kujaa uwanjani! Katika hili wanamuonea Ten si kweli.

2. Sio kweli kwamba Haji Manara ndio chachu ya mashabiki wa Simba kujaa uwanjani, hapa nitauliza swali dogo sana, hv Haji kaanza kazi Simba msimu uliopita? Kama kaanza kazi Simba siku nyingi kwa nn watu walikuwa hawajai huko nyuma mpaka msimu uliopita?

Swali lingine, Simba wakati wanafunagwa goli 5 na Al Ahly Manara aligombana na mashabiki wa Simba kias ambacho Haji hakuhusika kabisa ku promote game ya marudiano.

Na ile game bado Simba walijaza sana uwanja, kama kweli Simba huwa wanajaza kwa sabb ya Haji mbona uwanja ulijaa licha ya Haji kutoi promote hyo game?

3. Hapa utagundua sio kweli kinachofanya Simba wajae uwanjani ni Haji. Licha ya yy mwenyewe Haji kujisifu kwa hiki lkn sio kweli kwamba anastahiki sifa hizi kwa sababu Haji alianza kazi tangu 2014 lakini Simba haina miaka miwili kuanza kujaza uwanja, pia game ya Ahly hakupiga promo na bado uwanja ulitapika. Hapa kipo kitu cha ziada kinachofanya Simba waende uwanjan na ni kikubwa kuliko kelele za Haji. Ni nn hiko?

4. Ni matokeo bora na mpira mzuri unaoonyeshwa na team ya Simba ambayo ni matokeo ya awali ya uwekezaji ndani ya klabu hii. Mashabiki wana hamasa na hamu ya kuiona team yao na wakienda uwanjani wanakutana na team kweli yenye kucheza mpira mzuri na kuwapa matokeo. Kitu kinachowaongezea hamasa.

5. Kwa Yanga week ya Mwananchi ilikuwa na hamasa kubwa sana sana kias kilichopelekea mashabiki wengi sana uwanjan kuwah kutokea.

Lakini walichokiona kiuchezaji kuhusu team yao bado sio kwa kiwango kikubwa walichokitarajia hasa baada ya kuwa na iman mwaka huu wana team bora sana. Kiwango walichokiona hakikutosha kuwahamasisha wajae uwanjan ten kwenye mechi ya klabu Bingwa dhid ya Township Rollers.

6. Lazima yanga wakubali fact kwamba kwa sasa Simba wamewazid kwa hatua kubwa sana hasa kwenye branding ya team yao. Ni kweli kwamba yanga ni wa pili baada ya Simba, ni ukweli kwamba Unapoitaja Simba basi mwenzake unayeweza kumtaja lazima awe yanga, Ila kiuhalisia kuna gap kubwa sana kwa sasa baina ya Simba na Yanga
Simba wamefanikiwa kwenye Branding, na Brand yao inaendelea kukua kwa kasi siku baad ya siku. Yanga bado wako nyuma sana, ni Hii brand ya Simba inayowahamasisha mashabiki wao kujaa uwanjan. Anachokifanya Haji ni kitu kidogo kama Sugar coating au Sugar icing kwenye cake iliyo tayari.

7. Kwa hiki kinachoendelea leo Pale yanga ni kumuonea tu Dismas Ten, wala sio kosa lake hata afanye kama Haji wala yanga hawatojaa, na ukitaka kuamini Ten wa swap nafas yake na Haji uone kama Ten hatajaza watu Simba na Haji akashindwa kujaza kule kwa yanga. Ni lazima yanga watafte mwekezaji atayeweka hela ya kutosha kwenye team yao, akasaidia kukuza zaid brand ya klabu yao na kazi ya kujaza uwanja itakuwa kama kumsukuma mlevi tu.
 
Mnyonge mnyongeni, Haji anachangia sehemu kubwa ya munkari kwa timu na mashabiki
Matokeo ya uwanjani ndio yanayo wapeleka mashabiki uwanjani na ndio yanayo wakimbiza mashabiki uwanjani. Haji Manara wala Dismas ten awana uwezo wowote wa kuwahamasisha mashabiki ambao hawana uhakika na matokeo ya uwanjani. Yanga ndio timu yenye mashabik wengi katika ukanda uu wa Afrika mashariki na kati ila matokeo ya uwanjani ndio yanawafanya mashabik kutofika viwanjani. Kama yanga itarudisha ubabewake uwanjani uwanja utakua hautoshi.
 
Matokeo ya uwanjani ndio yanayo wapeleka mashabiki uwanjani na ndio yanayo wakimbiza mashabiki uwanjani. Haji Manara wala Dismas ten awana uwezo wowote wa kuwahamasisha mashabiki ambao hawana uhakika na matokeo ya uwanjani. Yanga ndio timu yenye mashabik wengi katika ukanda uu wa Afrika mashariki na kati ila matokeo ya uwanjani ndio yanawafanya mashabik kutofika viwanjani. Kama yanga itarudisha ubabewake uwanjani uwanja utakua hautoshi.
Hapo kwenye idadi kubwa ya washabiki, umetumia akili ya zamani. Kung'uta vumbi lililojaa kwenye ubongo wako kwanza, halafu uandike upya!
 
Mm kila siku huwa nasema km kweli haji mhamasishaji mbona alishindwa kuhamasisha watu kujaa uwanjani tangu 2014 hko? Watu wameanza kujaa Simba hii ya mo uwekezaji mzuri mpira mzuri lazma watu wajae uwanjani tusilete sifa za kijinga kwa hyo mropokaji mashabiki wanapenda matokeo!
 
Mm kila siku huwa nasema km kweli haji mhamasishaji mbona alishindwa kuhamasisha watu kujaa uwanjani tangu 2014 hko? Watu wameanza kujaa Simba hii ya mo uwekezaji mzuri mpira mzuri lazma watu wajae uwanjani tusilete sifa za kijinga kwa hyo mropokaji mashabiki wanapenda matokeo!
simba ganiinayocheza mpira mzuri!?
 
Mnyonge mnyongeni, Haji anachangia sehemu kubwa ya munkari kwa timu na mashabiki
Hilo ni kweli kabisa na sababu zake ni rahisi tu.

Timu inafanya vizuri na mashabiki wengi wa timu zetu ni level ya Haji kwenye uelewa, mtazamo na vitu kama hivyo.

Tusisahau wakati ule Yanga inafanya vizuri kuliko Simba, hakuna aliyesema mashabiki wa Yanga wanaoenda mpirani ni wachache. Wa Simba walikuwa wachache nyakati zile.

Timu ikifanya vizuri, mashabiki watakuja tu.
 
Hiyo ya uwingi wa mashabiki umechemka sana bro
Matokeo ya uwanjani ndio yanayo wapeleka mashabiki uwanjani na ndio yanayo wakimbiza mashabiki uwanjani. Haji Manara wala Dismas ten awana uwezo wowote wa kuwahamasisha mashabiki ambao hawana uhakika na matokeo ya uwanjani. Yanga ndio timu yenye mashabik wengi katika ukanda uu wa Afrika mashariki na kati ila matokeo ya uwanjani ndio yanawafanya mashabik kutofika viwanjani. Kama yanga itarudisha ubabewake uwanjani uwanja utakua hautoshi.

!! Zamani miaka ya 90 yawezekana ukawa sahihi lakini sio kwa miaka hii
 
Hemed Suya.

Kwanza nianze kwa kuwasalimu, na kuwatakia Eid l-Adh-ha Mubaarak jamii yote ya wapenda soka.

Jion hii nalazimika kushika kalamu kuandika baada ya kumaliza mialiko ya nyama kutoka sehemu mbali mbali na sasa nikiwa nimeshiba vyema naukumbuka mjadala unaoendelea mitandanoni kumhusu Dismas Ten nami nalazimika kuweka machache sana kumhusu.

1. Ten analaumiwa kwa kushindwa kuwahamasisha wanayanga kwenda uwanjan kushangilia mechi yao dhid ya Township Rollers, Ten analaumiwa eti hafanyi kama Manara kuhamasisha watu kujaa uwanjani! Katika hili wanamuonea Ten si kweli.

2. Sio kweli kwamba Haji Manara ndio chachu ya mashabiki wa Simba kujaa uwanjani, hapa nitauliza swali dogo sana, hv Haji kaanza kazi Simba msimu uliopita? Kama kaanza kazi Simba siku nyingi kwa nn watu walikuwa hawajai huko nyuma mpaka msimu uliopita?

Swali lingine, Simba wakati wanafunagwa goli 5 na Al Ahly Manara aligombana na mashabiki wa Simba kias ambacho Haji hakuhusika kabisa ku promote game ya marudiano.

Na ile game bado Simba walijaza sana uwanja, kama kweli Simba huwa wanajaza kwa sabb ya Haji mbona uwanja ulijaa licha ya Haji kutoi promote hyo game?

3. Hapa utagundua sio kweli kinachofanya Simba wajae uwanjani ni Haji. Licha ya yy mwenyewe Haji kujisifu kwa hiki lkn sio kweli kwamba anastahiki sifa hizi kwa sababu Haji alianza kazi tangu 2014 lakini Simba haina miaka miwili kuanza kujaza uwanja, pia game ya Ahly hakupiga promo na bado uwanja ulitapika. Hapa kipo kitu cha ziada kinachofanya Simba waende uwanjan na ni kikubwa kuliko kelele za Haji. Ni nn hiko?

4. Ni matokeo bora na mpira mzuri unaoonyeshwa na team ya Simba ambayo ni matokeo ya awali ya uwekezaji ndani ya klabu hii. Mashabiki wana hamasa na hamu ya kuiona team yao na wakienda uwanjani wanakutana na team kweli yenye kucheza mpira mzuri na kuwapa matokeo. Kitu kinachowaongezea hamasa.

5. Kwa Yanga week ya Mwananchi ilikuwa na hamasa kubwa sana sana kias kilichopelekea mashabiki wengi sana uwanjan kuwah kutokea.

Lakini walichokiona kiuchezaji kuhusu team yao bado sio kwa kiwango kikubwa walichokitarajia hasa baada ya kuwa na iman mwaka huu wana team bora sana. Kiwango walichokiona hakikutosha kuwahamasisha wajae uwanjan ten kwenye mechi ya klabu Bingwa dhid ya Township Rollers.

6. Lazima yanga wakubali fact kwamba kwa sasa Simba wamewazid kwa hatua kubwa sana hasa kwenye branding ya team yao. Ni kweli kwamba yanga ni wa pili baada ya Simba, ni ukweli kwamba Unapoitaja Simba basi mwenzake unayeweza kumtaja lazima awe yanga, Ila kiuhalisia kuna gap kubwa sana kwa sasa baina ya Simba na Yanga
Simba wamefanikiwa kwenye Branding, na Brand yao inaendelea kukua kwa kasi siku baad ya siku. Yanga bado wako nyuma sana, ni Hii brand ya Simba inayowahamasisha mashabiki wao kujaa uwanjan. Anachokifanya Haji ni kitu kidogo kama Sugar coating au Sugar icing kwenye cake iliyo tayari.

7. Kwa hiki kinachoendelea leo Pale yanga ni kumuonea tu Dismas Ten, wala sio kosa lake hata afanye kama Haji wala yanga hawatojaa, na ukitaka kuamini Ten wa swap nafas yake na Haji uone kama Ten hatajaza watu Simba na Haji akashindwa kujaza kule kwa yanga. Ni lazima yanga watafte mwekezaji atayeweka hela ya kutosha kwenye team yao, akasaidia kukuza zaid brand ya klabu yao na kazi ya kujaza uwanja itakuwa kama kumsukuma mlevi tu.
Haji Manara ana mchango mkubwa sana aisee, umesahau alivyokuwa anapambana mpaka kuja na TV kwenye press, Haji anamchango wake na Hamasa yake, umesahau majina kama Kwasu kwasu fc, gongowazi, mbutembute yametoka kwa haji leo kila mtu anayatumia
 
Mm kila siku huwa nasema km kweli haji mhamasishaji mbona alishindwa kuhamasisha watu kujaa uwanjani tangu 2014 hko? Watu wameanza kujaa Simba hii ya mo uwekezaji mzuri mpira mzuri lazma watu wajae uwanjani tusilete sifa za kijinga kwa hyo mropokaji mashabiki wanapenda matokeo!
Kwanza punguza chuki kwa H.Manara mkuu..
Matokeo ndio huleta watu uwanjani.. Je Yanga na kubeba ubingwa X3 mfululizo bila huruma ya bosi Manji walikuwa hawajai uwanjani.
Ten wanamuonea japo wabongo tumezoea kubustiwa utafikiri hatujui kinachoendelea... Lakini timu kama Yanga wakihitaji promo ya D10 basi watafute mtu mwingine Ten apewe kazi nyingine.
Kweli uwekezaji una hamasa yake lakin hata Haji ana nafasi yake katika hamasa hiyo.
TUNAPENDA KUSUKUMWA KAMA WATOTO NA TUMEZOEA HIVYO.
 
Hemed Suya.

Kwanza nianze kwa kuwasalimu, na kuwatakia Eid l-Adh-ha Mubaarak jamii yote ya wapenda soka.

Jion hii nalazimika kushika kalamu kuandika baada ya kumaliza mialiko ya nyama kutoka sehemu mbali mbali na sasa nikiwa nimeshiba vyema naukumbuka mjadala unaoendelea mitandanoni kumhusu Dismas Ten nami nalazimika kuweka machache sana kumhusu.

1. Ten analaumiwa kwa kushindwa kuwahamasisha wanayanga kwenda uwanjan kushangilia mechi yao dhid ya Township Rollers, Ten analaumiwa eti hafanyi kama Manara kuhamasisha watu kujaa uwanjani! Katika hili wanamuonea Ten si kweli.

2. Sio kweli kwamba Haji Manara ndio chachu ya mashabiki wa Simba kujaa uwanjani, hapa nitauliza swali dogo sana, hv Haji kaanza kazi Simba msimu uliopita? Kama kaanza kazi Simba siku nyingi kwa nn watu walikuwa hawajai huko nyuma mpaka msimu uliopita?

Swali lingine, Simba wakati wanafunagwa goli 5 na Al Ahly Manara aligombana na mashabiki wa Simba kias ambacho Haji hakuhusika kabisa ku promote game ya marudiano.

Na ile game bado Simba walijaza sana uwanja, kama kweli Simba huwa wanajaza kwa sabb ya Haji mbona uwanja ulijaa licha ya Haji kutoi promote hyo game?

3. Hapa utagundua sio kweli kinachofanya Simba wajae uwanjani ni Haji. Licha ya yy mwenyewe Haji kujisifu kwa hiki lkn sio kweli kwamba anastahiki sifa hizi kwa sababu Haji alianza kazi tangu 2014 lakini Simba haina miaka miwili kuanza kujaza uwanja, pia game ya Ahly hakupiga promo na bado uwanja ulitapika. Hapa kipo kitu cha ziada kinachofanya Simba waende uwanjan na ni kikubwa kuliko kelele za Haji. Ni nn hiko?

4. Ni matokeo bora na mpira mzuri unaoonyeshwa na team ya Simba ambayo ni matokeo ya awali ya uwekezaji ndani ya klabu hii. Mashabiki wana hamasa na hamu ya kuiona team yao na wakienda uwanjani wanakutana na team kweli yenye kucheza mpira mzuri na kuwapa matokeo. Kitu kinachowaongezea hamasa.

5. Kwa Yanga week ya Mwananchi ilikuwa na hamasa kubwa sana sana kias kilichopelekea mashabiki wengi sana uwanjan kuwah kutokea.

Lakini walichokiona kiuchezaji kuhusu team yao bado sio kwa kiwango kikubwa walichokitarajia hasa baada ya kuwa na iman mwaka huu wana team bora sana. Kiwango walichokiona hakikutosha kuwahamasisha wajae uwanjan ten kwenye mechi ya klabu Bingwa dhid ya Township Rollers.

6. Lazima yanga wakubali fact kwamba kwa sasa Simba wamewazid kwa hatua kubwa sana hasa kwenye branding ya team yao. Ni kweli kwamba yanga ni wa pili baada ya Simba, ni ukweli kwamba Unapoitaja Simba basi mwenzake unayeweza kumtaja lazima awe yanga, Ila kiuhalisia kuna gap kubwa sana kwa sasa baina ya Simba na Yanga
Simba wamefanikiwa kwenye Branding, na Brand yao inaendelea kukua kwa kasi siku baad ya siku. Yanga bado wako nyuma sana, ni Hii brand ya Simba inayowahamasisha mashabiki wao kujaa uwanjan. Anachokifanya Haji ni kitu kidogo kama Sugar coating au Sugar icing kwenye cake iliyo tayari.

7. Kwa hiki kinachoendelea leo Pale yanga ni kumuonea tu Dismas Ten, wala sio kosa lake hata afanye kama Haji wala yanga hawatojaa, na ukitaka kuamini Ten wa swap nafas yake na Haji uone kama Ten hatajaza watu Simba na Haji akashindwa kujaza kule kwa yanga. Ni lazima yanga watafte mwekezaji atayeweka hela ya kutosha kwenye team yao, akasaidia kukuza zaid brand ya klabu yao na kazi ya kujaza uwanja itakuwa kama kumsukuma mlevi tu.
Huu ndo ukweli ambao baadhi ya fans wa yanga hawautaki.NakumBuka miaka ya nyuma Sikuwa mpenzi Sana wa kutazama soka la bongo, lkn siku hizi kila nikisikia simba ana cheza nina Shauku ya kukaa kitako niwatazame.Yanga wana kazi Kubwa ya Kufanya wawafikie simba
 
Uwezi kubeza mchango wa haji manara kwa Simba kwenye uwamasishaji manara huyu huyu alisema hata ije Barcelona au real Madrid uwanja wa taifa watafungwa kias ambacho mashabiki wa Simba wakaamini amekuwa akaanzisha slogan mbalimbali kukuza brand ya timu pamoja kuwamasisha mashabiki Kama vile This is simba,iga ufe this is next level n.k alafu Leo unambeza kweli?
 
16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom