Mabibi na mabwana ni ukweli usiofichika kuwa wengi wa walio wazalendo, wanayo furaha kubwa kumpata mama Samia kama Rais wetu wa JMT kwa sasa.
Katika kumtia shime mama yetu kazi inapoendelea si haba kuyapitia yale ambayo haswa, yanayotukosha nyoyo za zetu kutokana na utendaji wake:
1. Corona na ripoti ya tume: hili linabeba maisha yetu. Mapendekezo ya tume ya wataalamu yamekwisha tolewa na yako mikononi mwake.
2. Kutambua rasmi kuwa tumekuwa tukibambikiziwa kesi na taasisi za serikali. Tayari kesha wanyooshea vidole stahiki: takukuru, TRA, polisi wakiwamo wale wakubrashi viatu, nk.
3. Ripoti za CAG BOT na TPA: Mama machale yameshamcheza (tumekuwa tukipima) amemhitaji CAG awe muwazi zaidi kwenye ripoti zake, wala asimung'unye maneno. Dalili za wazi kuwa mama hana urafiki na majizi hata kama anakaa nayo meza moja kwa sasa. Tulipo tuko mkao wa kula tukimsubiria CAG Kichere kuunguruma.
4. Viongozi washukiwa wakubwa wa ukiukaji haki za watu, habari wanayo. Tayari DC Ole yuko benchi kwa uchunguzi. Huyo ni aliye hadharani. Ole kama Papa waliokuwa wakivuma baharini kweli kweli, yafahamika hakuwa peke yake!
5. Mama kasema hataki dhuluma za namna yoyote. Mama ni mcha Mungu hataki kuchonganishwa na Mola wake. Mungu atupe nini sisi?
6. Mama amekuwa muwazi kueleza hali yetu ilivyo. Nini hakiwezekani na nini kinawezekana sasa, amefafanua kwa kila mtu anayetaka kuelewa. Mama anatambua haki za watu kupandishwa mishahara, kupata ajira, nk. Tayari kuna ajira mpya kwenye hatua za utekelezaji.
Waungwana karibuni nanyi kutupia vya kwenu katika kutambua jitihada za Mama yetu Rais wetu wa JMT, kazi inapoendelea.
Nani kama Mama?
Katika kumtia shime mama yetu kazi inapoendelea si haba kuyapitia yale ambayo haswa, yanayotukosha nyoyo za zetu kutokana na utendaji wake:
1. Corona na ripoti ya tume: hili linabeba maisha yetu. Mapendekezo ya tume ya wataalamu yamekwisha tolewa na yako mikononi mwake.
2. Kutambua rasmi kuwa tumekuwa tukibambikiziwa kesi na taasisi za serikali. Tayari kesha wanyooshea vidole stahiki: takukuru, TRA, polisi wakiwamo wale wakubrashi viatu, nk.
3. Ripoti za CAG BOT na TPA: Mama machale yameshamcheza (tumekuwa tukipima) amemhitaji CAG awe muwazi zaidi kwenye ripoti zake, wala asimung'unye maneno. Dalili za wazi kuwa mama hana urafiki na majizi hata kama anakaa nayo meza moja kwa sasa. Tulipo tuko mkao wa kula tukimsubiria CAG Kichere kuunguruma.
4. Viongozi washukiwa wakubwa wa ukiukaji haki za watu, habari wanayo. Tayari DC Ole yuko benchi kwa uchunguzi. Huyo ni aliye hadharani. Ole kama Papa waliokuwa wakivuma baharini kweli kweli, yafahamika hakuwa peke yake!
5. Mama kasema hataki dhuluma za namna yoyote. Mama ni mcha Mungu hataki kuchonganishwa na Mola wake. Mungu atupe nini sisi?
6. Mama amekuwa muwazi kueleza hali yetu ilivyo. Nini hakiwezekani na nini kinawezekana sasa, amefafanua kwa kila mtu anayetaka kuelewa. Mama anatambua haki za watu kupandishwa mishahara, kupata ajira, nk. Tayari kuna ajira mpya kwenye hatua za utekelezaji.
Waungwana karibuni nanyi kutupia vya kwenu katika kutambua jitihada za Mama yetu Rais wetu wa JMT, kazi inapoendelea.
Nani kama Mama?