Yanayotokea awamu hii ya tano, kuna watu hatutawasamehe

KISHADA

JF-Expert Member
Oct 18, 2012
2,224
3,290
Malalamiko yamezidi sasa katika kila kona na nyanja mbali mbali za maisha. Kuanzia wafanyakazi serikalini, wafanyabiashara wakubwa na wadogo, wakulima, wavuvi, wasomi, wanafunzi na walimu, wanaume na wanawake na mifano ya hio.

Lakini kwanini yote haya?. Je, imekuja hali hii kwa bahati mbaya? kwangu mimi HAPANA.

Ndio hapana, kwa sababu hakukuwa na maandalizi juu ya Taasisi ya Uraisi huu ndio ukweli.

Wengine wanaiita ajali, wengine wataita kukosa weledi, wengine wanaita hulka ilimradi yote hayo yanarudi kwenye neno KUKOSA MAANDALIZI.

Kuna watu hatutawasamehe kwa haya.

- Wale walioshiriki kutumia nyadhifa zao kuchochea kuvurugwa taratibu za kumpata mgombea aliyeandaliwa kwa kujali mirengo yao na visasi- hatutawasamehe wote.

- Wale wote waliotumika kufanikisha mpango huo wa kumpata Mteule asiyeandaliwa.

- Wale wote waliodiriki kutumia rasilimali mbali mbali ili kufanikisha mpango uliokosa maandalizi.

- Wale wote waliotumika kushawishi na kuwaaminisha watanzania kuwa kibaya kitakuwa kizuri wakati wanajuwa hakuna maandalizi yaliyofanywa.

- Wale wote waliotumika kwa kufanya upendeleo wowote ilimradi mteule asiye maandalizi aweze kupita kwa urahisi siku ya uchaguzi kama wapo.

- Waandamizi wote na wazoefu wa mfumo(system) ambao walinyamaza hata pale taasisi iliyotwaa ushindi , ilivuruga taratibu kwa uwazi wakati wa kumpata mteule wao.

- Waandishi wote waliotumika na kuacha uweledi wa kazi zao ili kupotosha ukweli ilimradi mtu aliyekosa maandalizi ashinde.

Hayo ni maoni yangu, naamini watanzania wengi leo hii wanajuwa ukweli wa hili. Awamu ya tano ilikosa maandalizi kutoka awali na hiki kinachoendelea leo ndio natija yake.

Tujifunze lakini tusirudie makosa, hata hivyo waliotukosea watuombe radhi au hatutawasamehe.

Kishada
 
Nchi zinazoandaa urithi wa uongozi ni za Kifalme na Kisultani tu.

Mshauri mbunge wako apeleke muswada huo ili ukikubalika pawe na Mfalme au Sultani na maandalizi ya mrithi wa Ufalme au Usultani.

Bila hivyo hilo ulitakalo haliwezekani, tutabaki kuchaguwa tumtakae kila baada ya miaka 5.

Ataecheza karata zake vizuri ndiyo yeye huyo.
 
Nchi zinazoandaa urithi wa uongozi ni za Kifalme na Kisultani tu.

Mshauri mbunge wako apeleke muswada huo ili ukikubalika pawe na Mfalme au Sultani na maandalizi ya mrithi wa Ufalme au Usultani.

Bila hivyo hilo ulitakalo haliwezekani, tutabaki kuchaguwa tumtakae kila baada ya miaka 5.

Ataecheza karata zake vizuri ndiyo yeye huyo.
Tumeipenda wenyewe acha Waisome namba ahaa ahaa watu walijua wimbo unamuhusu Lowasa na Mbowe ambao walijijenga kiuchumi kitambo,Namba zinasomeka kwa wategemea biashara za ndani na wafanyakazi tehe tehe
 
Nchi zinazoandaa urithi wa uongozi ni za Kifalme na Kisultani tu.

Mshauri mbunge wako apeleke muswada huo ili ukikubalika pawe na Mfalme au Sultani na maandalizi ya mrithi wa Ufalme au Usultani.

Bila hivyo hilo ulitakalo haliwezekani, tutabaki kuchaguwa tumtakae kila baada ya miaka 5.

Ataecheza karata zake vizuri ndiyo yeye huyo.

Assalam aleikum dada

Hapana, naamini unajuwa kuwa hata taasisi za kivyama zina utaratibu wake ndio maana kukawa na kitengo cha itikadi. hili unalijuwa.

Kuelekea 2015. CCM kama taasisi ilikumbwa na harika ya kumpata mgombea. Huo ndio ukweli. Kuanzia hapo kila kitu kiliharibika na leo hii tunaona madhara ya gharika.

Naamini CCM kama chama kizoefu kina utaratibu wake wa kuwaandaa wateule hasa taasisi ya Uraisi. Lakini ni kweli hapa walibugi step.

Sikushangaa baadhi ya wazoefu kunyamaza kimya.
 
Malalamiko yamezidi sasa katika kila kona na nyanja mbali mbali za maisha. Kuanzia wafanyakazi serikalini, wafanyabiashara wakubwa na wadogo, wakulima, wavuvi, wasomi, wanafunzi na walimu, wanaume na wanawake na mifano ya hio.

Lakini kwanini yote haya?. Je, imekuja hali hii kwa bahati mbaya? kwangu mimi HAPANA.

Ndio hapana, kwa sababu hakukuwa na maandalizi juu ya Taasisi ya Uraisi huu ndio ukweli.

Wengine wanaiita ajali, wengine wataita kukosa weledi, wengine wanaita hulka ilimradi yote hayo yanarudi kwenye neno KUKOSA MAANDALIZI.

Kuna watu hatutawasamehe kwa haya.

- Wale walioshiriki kutumia nyadhifa zao kuchochea kuvurugwa taratibu za kumpata mgombea aliyeandaliwa kwa kujali mirengo yao na visasi- hatutawasamehe wote.

- Wale wote waliotumika kufanikisha mpango huo wa kumpata Mteule asiyeandaliwa.

- Wale wote waliodiriki kutumia rasilimali mbali mbali ili kufanikisha mpango uliokosa maandalizi.

- Wale wote waliotumika kushawishi na kuwaaminisha watanzania kuwa kibaya kitakuwa kizuri wakati wanajuwa hakuna maandalizi yaliyofanywa.

- Wale wote waliotumika kwa kufanya upendeleo wowote ilimradi mteule asiye maandalizi aweze kupita kwa urahisi siku ya uchaguzi kama wapo.

- Waandamizi wote na wazoefu wa mfumo(system) ambao walinyamaza hata pale taasisi iliyotwaa ushindi , ilivuruga taratibu kwa uwazi wakati wa kumpata mteule wao.

- Waandishi wote waliotumika na kuacha uweledi wa kazi zao ili kupotosha ukweli ilimradi mtu aliyekosa maandalizi ashinde.

Hayo ni maoni yangu, naamini watanzania wengi leo hii wanajuwa ukweli wa hili. Awamu ya tano ilikosa maandalizi kutoka awali na hiki kinachoendelea leo ndio natija yake.

Tujifunze lakini tusirudie makosa, hata hivyo waliotukosea watuombe radhi au hatutawasamehe.

Kishada
Umeeleweka vizuri sana. HAWATASAMEHEWA KATU. HATA MASHEHE NA MAASKOFU WAJE NA MAPAMBIO YAO NA KASWIDA, HATUTAWASAMEHE
 
Nchi zinazoandaa urithi wa uongozi ni za Kifalme na Kisultani tu.

Mshauri mbunge wako apeleke muswada huo ili ukikubalika pawe na Mfalme au Sultani na maandalizi ya mrithi wa Ufalme au Usultani.

Bila hivyo hilo ulitakalo haliwezekani, tutabaki kuchaguwa tumtakae kila baada ya miaka 5.

Ataecheza karata zake vizuri ndiyo yeye huyo.
CCM ina tofauti gani na utawala wa Kisultan au Kifalme!?

Nchi zenye mfumo kama ya CCM, China au Cuba kiongozi haibuki tu bali anaandaliwa. Kwa kweli CCM wangeitendea haki nchi hii kama angechagua viongozi walioandaliwa.
 
Hapa tatizo si mtu aliyechaguliwa. Kwa namna nchi ilivyokuwa ikiendeshwa kwa miaka zaidi ya 50 na matokeo ndio haya tunayaona. Vyovyote vile ilikuwa lazima tukwame.
Kilichopo mbele yetu ni viongozi tu kutokusema wazi kwamba tumekwama na tujipange. Tulikwama siku nyingi na tukaweza kuishi kwa kuunga-unga. Haiwezekani tena.
Huu mfumo una machungu yake tatizo tu hayawafikii waliotufikisha hapa- they are not normally distributed. Wenyewe huitwa makaburi yaliyozeeka ambayo hayafukuliki.
 
CCM ina tofauti gani na utawala wa Kisultan au Kifalme!?

Nchi zenye mfumo kama ya CCM, China au Cuba kiongozi haibuki tu bali anaandaliwa. Kwa kweli CCM wangeitendea haki nchi hii kama angechagua viongozi walioandaliwa.


Hoja yako inajipinga, jisome vizuri, mara unataka kutuaminisha CCM haina tofauti na Usultani, mara unataka kutuaminisha kuwa CCM haijaandaa kiongozi. Unaonesha hata unachokiongea hauelewi ni nini.

Nyerere alirithiwa na mwanawe au nduguye?
 
Mi nadhani kitengo cha itikadi kilikuwa sahihi kwa mujibu wa hali ya chama ilivyokuwa wakafanya yale waliyoyafanya so mi nadhani katika kuisoma namba tunaisoma sisi lakini walioandika namba hiyo hata haiwagusi
 
Hapa tatizo si mtu aliyechaguliwa. Kwa namna nchi ilivyokuwa ikiendeshwa kwa miaka zaidi ya 50 na matokeo ndio haya tunayaona. Vyovyote vile ilikuwa lazima tukwame.
Kilichopo mbele yetu ni viongozi tu kutokusema wazi kwamba tumekwama na tujipange. Tulikwama siku nyingi na tukaweza kuishi kwa kuunga-unga. Haiwezekani tena.
Huu mfumo una machungu yake tatizo tu hayawafikii waliotufikisha hapa- they are not normally distributed. Wenyewe huitwa makaburi yaliyozeeka ambayo hayafukuliki.

Naam.

Kuhusu kukwama kwa mfumo hapa mimi siongei sana , maana hili lilipigiwa kelele mpaka na Tume ya warioba waliliona lakini ni hao hao CCM walipinga.

Kilichopo juu ya hiyo hoja ya walau KUUNGAUNGA basi mara hii mafundi walipotea hawakufanya maandalizi.
 
Tatizo Dada Faidha anajibu kwa hisia za kichama kuliko utaifa.Hivi leo ccm ilimwambia Mwijage adanganye umma? Tulifurahi sana kugunduliwa gas,tukayaona maisha yetu yakirahisishwa hasa kwa matumizi ya gas yenyewe na umeme wa bei nafuu.Tukaiona Tanzania yenye umeme wa kutosha na bidhaa kuuzwa kwa bei rahisi.Tukasema sasa hata Mtz wa chini kabisa hata nyeshewa mvua kwa kukosa nyumba hata bati 16.Je ni kweli ccm ndiyo imefanya haya yote yashindikane? Tunatakiwa kutafuta njia yakujikwamua hapa tulipo kuliko kupashana humu JF.Tufanye mijadala kwa hisia za Utaifa na si Uchama.
 
Malalamiko yamezidi sasa katika kila kona na nyanja mbali mbali za maisha. Kuanzia wafanyakazi serikalini, wafanyabiashara wakubwa na wadogo, wakulima, wavuvi, wasomi, wanafunzi na walimu, wanaume na wanawake na mifano ya hio.

Lakini kwanini yote haya?. Je, imekuja hali hii kwa bahati mbaya? kwangu mimi HAPANA.

Ndio hapana, kwa sababu hakukuwa na maandalizi juu ya Taasisi ya Uraisi huu ndio ukweli.

Wengine wanaiita ajali, wengine wataita kukosa weledi, wengine wanaita hulka ilimradi yote hayo yanarudi kwenye neno KUKOSA MAANDALIZI.

Kuna watu hatutawasamehe kwa haya.

- Wale walioshiriki kutumia nyadhifa zao kuchochea kuvurugwa taratibu za kumpata mgombea aliyeandaliwa kwa kujali mirengo yao na visasi- hatutawasamehe wote.

- Wale wote waliotumika kufanikisha mpango huo wa kumpata Mteule asiyeandaliwa.

- Wale wote waliodiriki kutumia rasilimali mbali mbali ili kufanikisha mpango uliokosa maandalizi.

- Wale wote waliotumika kushawishi na kuwaaminisha watanzania kuwa kibaya kitakuwa kizuri wakati wanajuwa hakuna maandalizi yaliyofanywa.

- Wale wote waliotumika kwa kufanya upendeleo wowote ilimradi mteule asiye maandalizi aweze kupita kwa urahisi siku ya uchaguzi kama wapo.

- Waandamizi wote na wazoefu wa mfumo(system) ambao walinyamaza hata pale taasisi iliyotwaa ushindi , ilivuruga taratibu kwa uwazi wakati wa kumpata mteule wao.

- Waandishi wote waliotumika na kuacha uweledi wa kazi zao ili kupotosha ukweli ilimradi mtu aliyekosa maandalizi ashinde.

Hayo ni maoni yangu, naamini watanzania wengi leo hii wanajuwa ukweli wa hili. Awamu ya tano ilikosa maandalizi kutoka awali na hiki kinachoendelea leo ndio natija yake.

Tujifunze lakini tusirudie makosa, hata hivyo waliotukosea watuombe radhi au hatutawasamehe.

Kishada
Huruka ya mtu ndio tatizo mkuu
 
Naam.

Kuhusu kukwama kwa mfumo hapa mimi siongei sana , maana hili lilipigiwa kelele mpaka na Tume ya warioba waliliona lakini ni hao hao CCM walipinga.

Kilichopo juu ya hiyo hoja ya walau KUUNGAUNGA basi mara hii mafundi walipotea hawakufanya maandalizi.
Bado ninasisitiza, style tuliozoea imezeeka. Ni lazima itafutwe mpya. Tungekwama wote na mabepari wetu. Angalia mabenki yao, wanajikopesha mabilioni tunalipa kwa deposits za serikali. Wao lakini wana nafuu, sie tuliyenyoka muda wote ndio tunasaga meno.
 
Hapa tatizo si mtu aliyechaguliwa. Kwa namna nchi ilivyokuwa ikiendeshwa kwa miaka zaidi ya 50 na matokeo ndio haya tunayaona. Vyovyote vile ilikuwa lazima tukwame.
Kilichopo mbele yetu ni viongozi tu kutokusema wazi kwamba tumekwama na tujipange. Tulikwama siku nyingi na tukaweza kuishi kwa kuunga-unga. Haiwezekani tena.
Huu mfumo una machungu yake tatizo tu hayawafikii waliotufikisha hapa- they are not normally distributed. Wenyewe huitwa makaburi yaliyozeeka ambayo hayafukuliki.

How do you think they are distributed; binomial, Poisson, hypergeometrical, degenerative, beta-binomial or?
 
haitasaidia kitu bwana, 2shaingizwa mkenge. ccm n ile ile na watz n wale 2020 utaona watz watavyoidad ccm kwa pambio
 
Aliyetoa jina la mgombea mfukoni na aliyekuwa anatangaza matokeo kadri yalivyokuwa yanamfikia wana DHIMA na mustakabali wa uchumi, utengemano wa taifa, na umoja wa watanzania.

"Hashim Rungwe Spunda amepata kura....... sawa na asilimia sifuri nukta sifuri moja!!!"
 

Similar Discussions

18 Reactions
Reply
Back
Top Bottom