Yanayojiri muda ktk kuapishwa Raila Odinga na Kalonzo Mwisyoka.

Freed Freed

JF-Expert Member
Jun 27, 2017
6,224
6,467
Habari wadau.

Kutoka Kenya ni kuwa vikosi vya polisi na vifaa vyao vimeamuriwa kuondaka uwanja wa Uhuru park na kupisha kuapishwa kwa Raila na Makamu wake. Hapo Jana na Leo asubuhi vikosi mbalimbali vya usalama vilikuwa vimeuzingira uwanja huo.

Hata hivyo kuondolewa kwa vikosi hivyo huenda ni mtego wa kuwafungulia mashitaka ya uhaini watakaoapishwa. Uwanja umefurika wafuasi wa NASA kutoka kote nchini Kenya.Viongozi wakuu wa NASA wameingia ktk kikao cha dharura kabla ya hafla hii ya kuapishwa na haijulikani kikao kitachukua muda gani.

Kutokana na kikao hiki cha mikakati kuibuka, Rais mtarajiwa na Makamu wake bado hawajafika uwanjani.

MREJESHO: Raila odinga ameshakula kiapo na kujitaja yeye ni kama Rais wa wananchi. Amekula kiapo huku akiahidu Makamu wa Rais ataapishwa baadae na kwamba wananchi watajua nini kimetokea kwa Kalozo hadi kushindwa kufika uwanjani. Vigogo wengine wa NASA pia hawakufika uwanjani na kutokufika kwao nitawaletea baadae.

Nitaleta updates mara kwa Mara.
 
Mbona wakati muafaka umeshapitiliza!! Yaani inatakiwa aapishwe tangu saa 4 asubuhi na sio zaidi ya saa 8 mchana. Imekuwaje??
 
Mbona wakati muafaka umeshapitiliza!! Yaani inatakiwa aapishwe tangu saa 4 asubuhi na sio zaidi ya saa 8 mchana. Imekuwaje??
... and should be in public witness. Hii ni kuepusha cases kama za akina Kibaki na Kivuitu kuapishana ghetto usiku wa manane.
 
... and should be in public witness. Hii ni kuepusha cases kama za akina Kibaki na Kivuitu kuapishana ghetto usiku wa manane.

Au yule judge aliyekuwa kakaa pale na mamvi yake ilikuwa kuwapumbaza mapolisi huku RAO akila kiapo Kisumu
 
Screenshot_2018-01-30-17-10-33-1.png
Screenshot_2018-01-30-17-14-42-1.png
Screenshot_2018-01-30-17-13-52-1.png
Screenshot_2018-01-30-17-12-53-1.png


African politics!!
 
Uhuru anajua kucheza vizuri na wapinzani wake. Siyo kila kitu kinahitaji nguvu.
 
Habari wadau.

Kutoka Kenya ni kuwa vikosi vya polisi na vifaa vyao vimeamuriwa kuondaka uwanja wa Uhuru park na kupisha kuapishwa kwa Raila na Makamu wake. Hapo Jana na Leo asubuhi vikosi mbalimbali vya usalama vilikuwa vimeuzingira uwanja huo.

Hata hivyo kuondolewa kwa vikosi hivyo huenda ni mtego wa kuwafungulia mashitaka ya uhaini watakaoapishwa. Uwanja umefurika wafuasi wa NASA kutoka kote nchini Kenya.Viongozi wakuu wa NASA wameingia ktk kikao cha dharura kabla ya hafla hii ya kuapishwa na haijulikani kikao kitachukua muda gani.

Kutokana na kikao hiki cha mikakati kuibuka, Rais mtarajiwa na Makamu wake bado hawajafika uwanjani.

MREJESHO: Raila odinga ameshakula kiapo na kujitaja yeye ni kama Rais wa wananchi. Amekula kiapo huku akiahidu Makamu wa Rais ataapishwa baadae na kwamba wananchi watajua nini kimetokea kwa Kalozo hadi kushindwa kufika uwanjani. Vigogo wengine wa NASA pia hawakufika uwanjani na kutokufika kwao nitawaletea baadae.

Nitaleta updates mara kwa Mara.


Hii Habari ina tofauti gani na breaking news nyingine kuhusu kuapishina kwa hao Wakenya?
 
Back
Top Bottom