[h=1]YANAYOJIRI KESI YA LISSU LEO-LISSU AMBANA SHAHIDI..[/h][h=1]Mbunge wa jimbo la Singida mashariki, Mh. Tundu Lissu, ameiomba mahakama kuu inayosikiliza kesi yake ya kupinga matokeo ya uchaguzi kufutilia mbali utaratibu wa kuvua ushahidi. Hayo yamejitokeza leo asubuhi kufuatia shahidi wa 15, Musa Rajabu Mkanga kuanza kuzungumza vitu vipya kabisa ambavyo havipo katika tuhuma za mwanzo walizokuwa wanamtuhumu Tundu Lissu. [/h][h=1]Hata hivyo Wakili wa serikali waserikali Bw. Juma Ramadhani alimuunga mkono na kusisitiza kuwa Mahakama Kuu iwe mahakama ya sheria, isiwe kama Gachacha..................[/h][h=1]Akina mama wajazana mahakamani kusikiliza kesi ya Lissu.[/h][h=1]Kesi ya Tundu Lissu inaendelea na akina mama wengi sana wameingia mahakamani wakitokea Ikungi kuja kumsikiliza, wengi sana mpaka inatia huruma.[/h][h=1]Mojawapo ya mahojiano ya Lissu na Shahidi yapo hivi: TUNDU LISSU ANAMHOJI.[/h][h=1]T/L. Naomba utusaidie kuzungumza, Cleti Kidamwina na pikipiki yake. Ieleze mahakama je Pikipiki ni T799 BJP. Ndo unayosemea?[/h][h=1]NDIYO.[/h][h=1]Umesema pikipiki hii ni mali ya Cleti Kidamwina?[/h][h=1]Namwonaga nayo.[/h][h=1]Wewe ni M/Kiti wa Kijiji. Unafahamu au unafikiri?[/h][h=1]Nafahamu.[/h][h=1]Je ni sawa au si sawa, kuwa pikipiki ni nyekundu na Nyeusi?[/h][h=1]Ni Nyekundu na Nyeusi.[/h][h=1]T/L. Unamfahamu Joshua Gwae kama mchungaji wa kanisa?[/h][h=1]Namfahamu kama Mwanakijiji wangu, ila ana kanisa lililopo Unyamikumbi, na anaishi Unyaghumpi.[/h][h=1]Ndiyo.[/h][h=1]Unamfahamu Juma Said Daa?[/h][h=1]Ndiyo[/h][h=1]Hao wamesema pikipiki ya Cleti Kidamwina ni nyekundu. Wewe unasema ni nyekundu na nyeusi, nani ni mwongo.[/h][h=1]Mwongo simjui, ila nasema ninachojua mimi.[/h][h=1]T/L nikisema huu ushahidi wa Cleti Kidamwina ni wa kutunga, ni uzushi. Nikikwambia Cleti hajawahi kumiliki pikipiki, utasemaje?[/h][h=1]Nitasema aliwahi kuwa nayo[/h][h=1]Jaji, naomba nimwonyeshe hati ya pikipiki T 799 BJP, ambayo anasema ni ya Cleti Kidamwina.[/h][h=1]Pikipiki ni Mali ya Salehe Ally Dude.[/h][h=1]Unakubaliana?[/h][h=1]Sikubali.[/h][h=1]Umesema pikipiki hiyo ni nyekundu na Nyeusi ni kweli au si kweli?[/h][h=1]NDIYO.[/h][h=1]Mbona hati ya usajili inaonyesha ni nyeusi?[/h][h=1]Kwanini umeamua kuidanganya mahakama?[/h][h=1]SIJUI.[/h][h=1]Kwa hiyo ushahidi uliotolewa na mchungaji Joshua, na wa kwako na Daa ni wa uongo?[/h][h=1]Wenzako wamesema pikipiki ilikuwa nyekundu, hati inayonyesha pikipiki ni nyeusi kwanini Mnadanganya........ Sijui.[/h][h=1] [/h][h=1] [/h]