Yamoto bend wafunguka kuhusu ugomvi wao na Fella na sababu za ukimya wao

Nucky Thompson

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
1,817
4,058

Baada ya tetesi za kutokuwa na maelewano mazuri ndani ya kundi la Yamoto Band kwa muda yaliyosababisha kutoachia kazi mpya, mmoja ya wasanii wanaounda kundi hilo Enock Bella amefunguka na kudai kwa sasa mambo yapo sawa.
Akiongea na kipindi cha E News cha EATV, Enock amesema japo kulikuwa na kutoelewana kati ya uongozi unaowasimamia na wao wasanii lakini kwa sasa wapo sawa na amemtaja Said Fella ndio mwenye uwezo wa kuwapoteza kwenye ramani ya muziki kwa kuwa yeye ndio aliyewatoa.

“Unajua hapo awali kidogo ni kweli tulikuwa na mvurugano kidogo kati ya wasanii na uongozi lakini sasa hivi hakuna tofauti yoyote ile na kila kitu kipo sawa kabisa, na upendo uleule na siyo kuvurugana,” amesema Enock.

wasanii walikuwa hawataki au kugombana kabisa, kwa sababu Mkubwa yeye ndiye aliyetuleta na yeye ndiye atakayetupoteza. Saidi Fella ni mzee wetu hivyo huwezi kusikia hata siku moja kuwa Yamoto Band wamegombana na Fella,” ameongeza.
 
Fella kishaanza kuvuna shamba lake.

Kama madogo hawakuanika juani basi washautwanga mbichi kama wanabisha wamuulize Nature kilichomkuta.
 
Habari za EATV na EA Radio habari zao mara nyingi ni zile zenye ujumbe m'baya kwa wasanii wote walio na "mafungamano" ya moja kwa moja au kwa namna nyingine na "TIMU YA MAFANIKIO" lakini hata siku moja utosikia habari mbaya inayomuhusu "balozi wa tembo" (UTAYAONA HAYO KAMA UKO VIZURI KICHWANI,ILA KAMA BURE KICHWANI UWEZI KUONA)
 
ukigombana na tale na fela ....tafuta shamba ukalime lakin sio kuimba
 
Habari za EATV na EA Radio habari zao mara nyingi ni zile zenye ujumbe m'baya kwa wasanii wote walio na "mafungamano" ya moja kwa moja au kwa namna nyingine na "TIMU YA MAFANIKIO" lakini hata siku moja utosikia habari mbaya inayomuhusu "balozi wa tembo" (UTAYAONA HAYO KAMA UKO VIZURI KICHWANI,ILA KAMA BURE KICHWANI UWEZI KUONA)
Wasafi wametuharibia vijana kwa kweli.
 
Wakati wao umepita, hata wakirudi wala wasitegemee kuwa wale, sasa mkubwa anapromote bendi yake ya taarab, kama walimzingua kwalipopata umaarufu wamejimaliza.
 
Baada ya uchaguzi tu madogo chali yaani ht nyimbo zao nilizokuwa nazipenda ss hivi nikisikia zinaniumiza kichwa. Na bado wengine.
 
Habari za EATV na EA Radio habari zao mara nyingi ni zile zenye ujumbe m'baya kwa wasanii wote walio na "mafungamano" ya moja kwa moja au kwa namna nyingine na "TIMU YA MAFANIKIO" lakini hata siku moja utosikia habari mbaya inayomuhusu "balozi wa tembo" (UTAYAONA HAYO KAMA UKO VIZURI KICHWANI,ILA KAMA BURE KICHWANI UWEZI KUONA)
Sio bure,wewe na mabosi wako mna matatizo na EA RADIO/EATV.Hiki kinacho onyeshwa hapo ni maneno ya kutungwa au dogo mwenyewe anaongea? Ni nani asiyejua kuwa Fella amekuwa anawanyonya madogo? Acheni kupeleka ngoma zenu kwao na msusie interviews, sio kueneza propaganda za kitoto mitandaoni.Watu wamepitia blood,sweat and tears kujenga hizo brands halafu nyie mnakesha mitandaoni kujaribu ku tarnish image yao katika jamii.Hii haikubaliki, akirushiwa jiwe Diamond mbio utakuja kutukana hapa.Waacheni wafanye yao na nyie fanyeni yenu kwa style zenu.
 
ukigombana na tale na fela ....tafuta shamba ukalime lakin sio kuimba
Umemsahau na Ruge mkuu.Huu ni upuuzi,kwa jinsi teknolojia alivyokuwa sielewi kwanini wasanii bado wanaendelea kuwa nyenyekea hao.Ukizingatia pia radio sio moja inchi hii.
 
Wakati wao umepita, hata wakirudi wala wasitegemee kuwa wale, sasa mkubwa anapromote bendi yake ya taarab, kama walimzingua kwalipopata umaarufu wamejimaliza.
Kama vipaji wanavyo, sioni kikwazo cha wao kufanikiwa.Wewe una uhakika gani ni wao ndio walio mzingua na sio yeye? Tuache kuhukumu pasipo kuwasikiliza.Mfano iwe tatizo lilikuja kwenye maslafi, hawa madogo unadhani wao hawana kiu ya mafanikio? hawana haki ya kuhoji mfano wakiona hela zinaingia lakini maslafi yao hayaeleweki ukilinganisha na kinacho patikana?
 
Kama vipaji wanavyo, sioni kikwazo cha wao kufanikiwa.Wewe una uhakika gani ni wao ndio walio mzingua na sio yeye? Tuache kuhukumu pasipo kuwasikiliza.Mfano iwe tatizo lilikuja kwenye maslafi, hawa madogo unadhani wao hawana kiu ya mafanikio? hawana haki ya kuhoji mfano wakiona hela zinaingia lakini maslafi yao hayaeleweki ukilinganisha na kinacho patikana?
Mkuu acha povu nimesema KAMA, sijahukumu na uje hata wakiwa na vipaji kwa nini wasisimame wenyewe bado wanamuhitaji Fela? Hapo ujue kila jambo kuna kutegemeana.
 
Mkuu acha povu nimesema KAMA, sijahukumu na uje hata wakiwa na vipaji kwa nini wasisimame wenyewe bado wanamuhitaji Fela? Hapo ujue kila jambo kuna kutegemeana.
Hapo mwisho umemalizia vizuri,kila jambo kuna kutegemeana, ila kuna jambo unalisahau, kila mmoja amuheshimu mwenzie kwa mchango wake.Isionekane kwamba siku zote mmoja ndio anayefanikiwa na mwingine kunyonywa.
 
Back
Top Bottom