Singida ndio home
JF-Expert Member
- Feb 23, 2012
- 3,192
- 3,353
Baada ya kuvunjika kwa kundi la Yamoto band, kila msanii wa kundi hilo alianza kufanya kazi kivyake.
1. Aslay alianza kutoa nyimbo moja baada ya nyingine kila baada ya muda mchache bampa to bampa na karibia zote zikafanya poa na hadi sasa ana hit na ngoma ya Subalkheri
2. Beka flavour nae akatoa nyimbo zake nzuri tu kama Libebe, Sikinai na sasa katoa Kiben ten.. Kwa ufupi nae anafanya poa tu kwenye game.
3. Maromboso ambae sasa tunamwita mboso alikaa muda mrefu tukajua kapotea mazima ila akapata bahati ya kujiunga label maarufu nchini ya wasafi. Hii label ina nguvu imemfanya nae arudi kwenye level nzuri.
4. Enock Bella ndio bado anatupa sintofahamu juu ya kazi zake za muziki. Licha ya kutoa ngoma kama nitazoea nado hazija-hit na zinachuja fasta.
NINI HATMA YA ENOCK BELLA? JE, AFANYE NINI ARUDI KWA KISHINDO KWENYE GAME?!