Yametimia - Serikali legelege sasa ni maradhi ya degedege

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,886
6,883
Kashfa kubwa ya kuibuliwa kwa rushwa bungeni inayomhusu Katibu Mkuu wa Serikali Jairo, pamoja na wabunge wa CCM kuifichua na kumtaka aachie ngazi jambo ambalo limesababisha hata makadirio ya wizara hiyo kutokukubaliwa na kuwekwa kwapani na serikali hadi baada ya wiki tatu ili ifanyiwe marekebisho, ni jambo ambalo litaigharibu serikali baadaye na Chama Cha CCM.

Pamoja na Waziri Mkuu kuguswa sana na jambo hilo na kumweleza Rais juu ya matukio yaliyoko sasa Dodoma, kauli ya Rais kwamba jambo hilo lisubiri yeye hadi atakapomaliza ziara yake ndipo aje aone afanye nini si kauli yenye uzito stahiki kwa kiongozi wa nchi kwa kiwango cha jambo lililopo.

Kikwete kwake umuhimu ni safari zake lakini matatizo ya taifa ni jambo la ziada ambalo halina usito stahiki. Je hii ni dharau kwa wananchi waliomchagua au ni serikali kupata ugonjwa wa degedege?

Kwa hali ilivyo namwunga mkono Mbunge wa Nzega Dr. Kingwangala kwamba serikali hii ni legelege.
 
Kashfa kubwa ya kuibuliwa kwa rushwa bungeni inayomhusu Katibu Mkuu wa Serikali Jairo, pamoja na wabunge wa CCM kuifichua na kumtaka aachie ngazi jambo ambalo limesababisha hata makadirio ya wizara hiyo kutokukubaliwa na kuwekwa kwapani na serikali hadi baada ya wiki tatu ili ifanyiwe marekebisho, ni jambo ambalo litaigharibu serikali baadaye na Chama Cha CCM.

Pamoja na Waziri Mkuu kuguswa sana na jambo hilo na kumweleza Rais juu ya matukio yaliyoko sasa Dodoma, kauli ya Rais kwamba jambo hilo lisubiri yeye hadi atakapomaliza ziara yake ndipo aje aone afanye nini si kauli yenye uzito stahiki kwa kiongozi wa nchi kwa kiwango cha jambo lililopo.

Kikwete kwake umuhimu ni safari zake lakini matatizo ya taifa ni jambo la ziada ambalo halina usito stahiki. Je hii ni dharau kwa wananchi waliomchagua au ni serikali kupata ugonjwa wa degedege?

Kwa hali ilivyo namwunga mkono Mbunge wa Nzega Dr. Kingwangala kwamba serikali hii ni legelege.

Utata upo kwenye hiyo red. Hii si dharau bali ni adhabu kwa wananchi ambao hawakumchagua maana matokeo ya uchaguzi yalichakachuliwa ...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom