Mafwi Munda
JF-Expert Member
- Nov 30, 2017
- 1,750
- 1,599
Nilidhani wote watu kumbe mingine miti.*YALIYOSEMWA NA MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KINONDONI KWA TIKETI YA CCM, NDUGU MAULID SAID MTULIA KWENYE MKUTANO WA KAMPENI KATA YA KIJITONYAMA LEO JUMAMOSI FEBRUARI 3, 2018*
"Mtulia mie nilienda kuvunja kibubu changu nikaenda Mahakamani kuzuia bomoabomoa, Serikali ikanisikia na Watu hawakubomolewa" - Mtulia
"Nimeacha Ubunge ili nijiunge na chama cha ushindi, chama chenye dola, chama kinacholeta maendeleo" - Mtulia
"Chama nilichotoka wakisema nimewasaliti wapo sahihi maana tulikuwa 10 sasa wamebaki 9. Wewe Mwananchi nimekusaliti nini?" - Mtulia
"Sisi Wabunge ni kama Washenga ukitukana Wakwe utampata Mke? Wabunge wa upinzani wanaitukana Serikali, maendeleo watayapata wapi?" - Mtulia
"Hii ni ilani ya CCM ndio inayoendesha nchi. Kazi yangu mkinichagua ni kwenda kutekeleza ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi" - Mtulia
"Nikishinda mje ofisini kwangu Vijana na Wanawake mjiandikishe mkachukue mikopo yenu toka Manispaa" - Mtulia
"Kuna Mtu amekuja kugombea lakini hana familia wala kadi ya kupigia kura, mtampaje dhamana huyu Mtu?" - Mtulia
"Mtu ameshindwa kwa wapiga kura 3600, atawezaje kushinda kwa Watu zaidi ya laki 2" - Mtulia
"Kama wameshindwa kujenga chama jimbo la Kinondoni ukienda kukodi jeshi usitegemee utashinda. Mbunge wa Kinondoni ni Maulid Said Mtulia" - Mtulia
"Mkinichagua nitashirikiana na Serikali ya CCM kuhakikisha kila kata naleta magari mapya ya kuzolea uchafu" - Mtulia
"Kijitonyama mna matatizo ya kubambikiziwa bili za maji, mkinichagua hilo tatizo litakuwa historia" - Mtulia
"Mtanzania yeyote anayekufa kwenye hospitali ya Serikali, Marehemu asidaiwe pesa endapo uwezo wake ni duni" - Mtulia
"Utakitupaje mkono chama kinacholeta maendeleo, kinacho miliki dola?" - Mtulia
"Watu wa Kinondoni mnaona barabara za mwendo kasi, mnaona madaraja, mnaona hospitali nzuri. Yote ni matunda ya kazi za Chama Cha Mapinduzi" - Mtulia
"Nawaombeni sana mnichague Said Maulid Mtulia niwe daraja la kuwaletea maendeleo" - Mtulia