Yaliyosemwa Leo Bungeni Na Waziri Wa Mambo ya Nje Na Ushirikiano Wa Kimataifa Mh. Benard Membe!!

chakii

JF-Expert Member
Sep 15, 2013
19,666
22,674
Habari wakuu,.

Ni katika kikao cha bunge leo Mjini Dodoma Mh. Membe akijibu maswali ya wabunge,.

Akijibu swali kuhusiana na safari za Mh. Rais Jakaya Kikwete,.

''Kasema Rais anapata Safari za Nje mara kwa mara ni kwa sababu anatambulika kimataifa hivyo hawezi kukaa ndani ya nchi bila kusafiri na ikitokea hivyo basi Mh. Rais atakuwa anaumwa hivyo siyo Jambo la kawaida kukaa ndani ya nchi kwa muda mrefu bila kusafiri''

My Take, Kuna Ukweli wowote kuhusiana na maelezo ya Mh, Membe?

Je majibu yake yana mashiko?

Nawasilisha,..
 
anaenda kukutana na vimada wake huko kwenye hotel za 5 star na kuomba msaada wa bilioni 20 huku hapa nchini kuna ufisadi wa zaidi ya bilioni 500
 
Ni kauli za kipuuzi tu.Kuna Rais aliyejulikana zaidi kimataifa kumshinda Nyererere? Kwani hicho anachoomba hawezi kusimamia uchumi akakipata?
 
ingekuwa Marais wataumwa endapo hawatasafiri nje ya nchi zao mara kwa mara, basi Mhe. Mugabe angekuwa hoi bin taabani up to now, because he's well known kuliko hata our President JK.
 
ingekuwa Marais wataumwa endapo hawatasafiri nje ya nchi zao mara kwa mara, basi Mhe. Mugabe angekuwa hoi bin taabani up to now, because he's well known kuliko hata our President JK.

labda nikueleweshe mkuu,

kasema Rais hatosafiri labda awe mgonjwa ndiyo atakaa nchini kwa muda bila kusafiri ila kama afya ni njema safari ni lazima maana anatambulika kimataifa!!
 
Habari wakuu,.

Ni katika kikao cha bunge leo Mjini Dodoma Mh. Membe akijibu maswali ya wabunge,.

Akijibu swali kuhusiana na safari za Mh. Rais Jakaya Kikwete,.

''Kasema Rais anapata Safari za Nje mara kwa mara ni kwa sababu anatambulika kimataifa hivyo hawezi kukaa ndani ya nchi bila kusafiri na ikitokea hivyo basi Mh. Rais atakuwa anaumwa hivyo siyo Jambo la kawaida kukaa ndani ya nchi kwa muda mrefu bila kusafiri''

My Take, Kuna Ukweli wowote kuhusiana na maelezo ya Mh, Membe?

Je majibu yake yana mashiko?

Nawasilisha,..


Kwang mm hainiingii akili...
Misafara mikubwa na garama anazotumia kusafiri zingetosha kabisa kuleta maendeleo but viongoz wetu wamekua ma vasco dagama....Sijui wanataka wavumbue nn?? Au n Ile mtu aje ahadisie wajukuu zake kua alienda nchi zote.....
 
labda nikueleweshe mkuu,

kasema Rais hatosafiri labda awe mgonjwa ndiyo atakaa nchini kwa muda bila kusafiri ila kama afya ni njema safari ni lazima maana anatambulika kimataifa!!

alaah.. he still makes no sense, wapo Marais ambao ni maarufu zaidi yake lakini wanatulia katika nchi zao, wakitoka ni kwa sababu maalum.. na hawakai ndani ya nchi zao kwa kuwa ni wagonjwa bali wanajua umuhimu wa kuwa karibu na wananchi wao.
 
Habari wakuu,.

Ni katika kikao cha bunge leo Mjini Dodoma Mh. Membe akijibu maswali ya wabunge,.

Akijibu swali kuhusiana na safari za Mh. Rais Jakaya Kikwete,.

''Kasema Rais anapata Safari za Nje mara kwa mara ni kwa sababu anatambulika kimataifa hivyo hawezi kukaa ndani ya nchi bila kusafiri na ikitokea hivyo basi Mh. Rais atakuwa anaumwa hivyo siyo Jambo la kawaida kukaa ndani ya nchi kwa muda mrefu bila kusafiri''

My Take, Kuna Ukweli wowote kuhusiana na maelezo ya Mh, Membe?

Je majibu yake yana mashiko?

Nawasilisha,..
l
Mawaziri mizigo
 
Ni kauli za kipuuzi tu.Kuna Rais aliyejulikana zaidi kimataifa kumshinda Nyererere? Kwani hicho anachoomba hawezi kusimamia uchumi akakipata?

Huyo ndio waziri wa mambo ya nje. Waziri anayeweza kutamka bila woga kuunga mkono maneno kama yale ya Mbunge Kessy na kesho akataka Jumuia ya Africa mashariki iendelee naushirikiano kama zamani.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Jaman naomba niwe mshamba hivi anavosafiri rais hizo allowances inalipwa na nchi anakoenda au ni hixi kodi ya kwangu mtanganyika wa huku manyara na mzenj?
 
Jaman naomba niwe mshamba hivi anavosafiri rais hizo allowances inalipwa na nchi anakoenda au ni hixi kodi ya kwangu mtanganyika wa huku manyara na mzenj?

kodi yako unayokatwa ndiyo inayogharamia hizo safari mkuu,.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom