Yaliyosemwa kampeni za CCM kumnadi mgombea ubunge (CCM) Kinondoni mhe. Mtulia kata ya Mwananyamala tar. 15 Feb, 2018

JINOME

JF-Expert Member
May 29, 2017
958
1,424
*

"Nawaomba sana mumpigie kura za ndiyo Mtulia kwa sababu anaweza na ni Mtu sahihi anayewafaa Vijana na Wana Kinondoni wote." - Tabia Mwita, Makamu Mwenyekiti UVCCM Taifa

"Mtulia ni Mtu sahihi kwa maendeleo ya wana Kinondoni." - Tabia Mwita, Makamu Mwenyekiti UVCCM Taifa

"Mtulia anatokana na chama kilichopo madarakani na chenye Serikali. Atawaletea maendeleo, anafaa mpe kura yako ya ndiyo" - Muslim Hassanali

"Mgombea wa Chadema ni miongoni mwa wapiga kura wenu? Atakuwaje Chaguo la wana Kinondoni" - David Kafulila

"Sina mashaka na uwezo wa Mtulia kwa sababu amepikwa vyema, mwaka 2008 alipelekwa Marekani kwenda kupikwa kuwa kiongozi. Ninajua ana uwezo wa kiuongozi" - David Kafulila

"Kama kigezo cha kuchagua chama bora, Chama Cha Mapinduzi ni chama cha kwanza Afrika na cha pili kwa ubora Duniani. Chagueni Chama bora cha CCM" - David Kafulila

"Mtulia amekuwa Mbunge kwa miaka 2, ukimchagua hatakuwa mgeni kiutendaji Bungeni" - David Kafulila

"Mtulia anavyogombea shida yake si mshahara wala posho kwa sababu alikubali kuviacha kwa kujiuzulu. Mtulia ana kiu ya kuwaletea maendeleo wana Kinondoni" - Mhe. Livingstone Lusinde, MB (Mtera)

"Kama ni usaliti, Mtulia hajakusaliti bali ameisaliti familia yake kwani kwa miezi zaidi ya mitatu hapokei mshahara." - Mhe. Livingstone Lusinde, MB (Mtera)

"Ukimchagua Mtulia Serikali itajitahidi kuleta maendeleo Kinondoni ili uchaguzi wa mwaka 2019 na wa mwaka 2020 CCM iweze kushinda kwa kishindo." - Mhe. Livingstone Lusinde, MB (Mtera)

"Wakati Wabunge wa upinzani wakitoka nje, Mtulia ni Mbunge pekee wa upinzani aliyebaki Bungeni kupitisha Bajeti ya nchi. Mtulia anawafaa wana Kinondoni" - Mhe. Suleiman Jaffo, MB (Kisarawe)

"Nyie ni mashahidi namna Mtulia anavyoshirikiana nanyi kukabiliana na mafuriko" - Mhe. Suleiman Jaffo, MB (Kisarawe)

"Mtulia anajua magumu aliyokutana nayo akiwa Mbunge upinzani, ameamua kubadili gia angani na kupanda basi linaloelekea kwenye maendeleo." - Ridhiwani Kikwete, MB (Chalinze)

"Mawaziri, Wabunge, na viongozi wa Serikali waliokuja hapa ni dalili ya ushirikiano tosha atakaoupata Mtulia kuwaletea maendeleo wana Kinondoni. Mchagueni Mtulia" - Dk. Tulia Ackson, NS

"Nimekuwa Mbunge kwa miaka miwili, kuwa Mbunge upinzani ni kazi ngumu sana." - Mtulia

"Namwomba sana Waziri Jaffo atusaidie kutupatia pesa za kusaidia ujenzi wa soko la Mwananyamala" - Mtulia

"Tunaomba Serikali sikivu isamehe deni la Marehemu. Nichagueni nikasimamie hilo" - Mtulia

"Nichagueni nikasimamie Vijana na akina Mama wanapata mikopo ya asilimia 10 toka Manispaa" - Mtulia

"Nichagueni nikaungane na timu kubwa ya Serikali iliyopo madarakani kuwaletea maendeleo" - Mtulia

"Nawaombeni sana Ndugu zangu nyoote mniombee kura na Jumamosi Februari 17 mjitokeze kwa wingi, mapema vituoni mnipigie kura za ndiyo" - Mtulia
 
Back
Top Bottom