Yaliyojiri wakati wa mkutano wa Rais Magufuli na Rais Felix Tshisekedi

Mathayo Fungo

JF-Expert Member
Nov 13, 2018
319
510
YALIYOJIRI LEO JUNI 14, 2019 WAKATI WA MKUTANO WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, DKT. JOHN POMBE MAGUFULI NA RAIS WA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA CONGO, MHE. FELIX TSHISEKEDI

Aliyoyazungumza Rais Felix Tshisekedi


#Sababu ya ziara hii ni kwa ajili ya kukuza mahusiano baina ya nchi zetu hivyo tumejadili na kukubaliana masuala ambayo yataelekezwa katika kukuza mahusiano haya.​

#Tumekubaliana kuwa hatuwezi kufanya jitihada zozote bila kuwa na amani itakayosaidia watu wa nchi hizi mbili ili waweze kunufaika.

#Tumekubaliana pia kuna umuhimu wa kukuza fursa za kiuchumi ili kukuza uchumi wetu, tumegundua kuwa biashara kati yetu ni ndogo hivyo lazima Tume ya Pamoja lazima ikae kwa haraka ili kuchambua sababu zinazosababisha hali hiyo.​

#Tumekubaliana pia katika ujenzi wa miundombinu pamoja na kushughulikia changamoto ya vizuizi vya kibiashara.

#Nashukuru kwa mualiko katika mkutano wa SADC na niko tayari kuja katika mkutano huo.​

Aliyoyaongea Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

#Ziara hii inatoa fursa kwa nchi zetu mbili kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano hasa kwenye masuala ya kiuchumi kwani licha ya uhusiano wa muda mrefu ushirikiano wetu wa kiuchumi sio mkubwa sana.​

#Tumekubaliana kuwa Rais wa DRC aimarishe Bandari upande wa DRC ili tusiwe na matatizo wakati wa kusafirisha bidhaa.

#Tumezungumza pia juu ya ujenzi wa barabara mbalimbali nchini pamoja na suala la usafiri wa anga ili kwa kupitia mashirika haya mawili ya ndege, Air Tanzania iweze kwenda kwenye baadhi ya miji ya DRC.​

#Naomba ukashughulikie shida za watu wa DRC kwa ajili ya kuikomboa nchi hiyo kwa sababu nchi hiyo haikutakiwa uchumi wake kukua kwa asilimia nne (4%).

#Kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wetu, tumeamua kuifufua Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kwani haijakutana tangu mwaka 2002.​

#Tumekubaliana Mamlaka zetu husika na Wafanyabiashara kufanya vikao vya ujirani mwema kwa ajili ya maendeleo yetu.

#Tumebadilishana mawazo kuhusu masuala ya kimataifa kwani ni vizuri kutetea maslahi ya Ukanda wetu pamoja na Bara letu kiujumla.​

drc.JPG
 
Tukiungana na wacongo kiukweli kabisa na kushirikiana, mataifa yetu mawili yatapiga hatua kubwa na wananchi wake kunufaika sana!🙏🏾 Kwanza kuna wanaodhani tumechelewa kidogo...

Ni wakati wa kuichukuwa Congo sasa, halafu mtaona jinsi mabeberu watajileta. Maana mcongo anatusikiliza. Lakini pia beberu ndo mnufaika mkuu kule Congo, hataki kuwepo na amani!

Tena tuungane nao tuwe kitu kimoja ikiwezekana, wengine watafuatia. Pale Congo, makampuni ya mabeberu ndiyo yanayochota rasilimali kama shamba la bibi. Yenyewe yana vikosi vya majangiri huko porini wanavyovifadhili! Hadi Kagame naye! Na ndiyo maana mabeberu na Rwanda, Rwanda na wao!
 
Uses of Tantalum. Tantalum is used in the electronics industry for capacitors and high power resistors. It is also used to make alloys to increase strength, ductility and corrosion resistance. The metal is used in dental and surgical instruments and implants, as it causes no immune response.

There are billions of cellphones in the world, and all of these gadgets work because of a conflict mineral known as coltan. ... Tantalum capacitors are a vital part of many electronic devices, particularly mobile phones, laptops and pagers.
 
Hivi kwanini wkt wa mobutu sijawahi kumuona mobutu akitia mguu hapa kwetu au marais kwenda congo, je tulikuwa na bifu nao au ilikuwaje mnaofatilia historia?
 
Coltan (short for columbite–tantalites and known industrially as tantalite) is a dull black metallic ore, from which the elements niobium and tantalum are extracted. The niobium-dominant mineral in coltan is columbite (after niobium's original American name columbium), and the tantalum-dominant mineral is tantalite.

Tantalum from coltan is used to manufacture batteries for electric cars and, in tantalum capacitors, it is used in electronic products.

Coltan mining has helped to finance serious conflict in the Democratic Republic of Congo, for example the Ituri conflict and the Second Congo War.
 
Hivi kwanini wkt wa mobutu sijawahi kumuona mobutu akitia mguu hapa kwetu au marais kwenda congo, je tulikuwa na bifu nao au ilikuwaje mnaofatilia historia?
Mobutu ni wazungu walikuwa wanamtumia na yeye pesa mabilioni ya usd aliweka marekani na Europe! Hata alivyoondoka madarakani, wali freeze assets zake zote na sidhani kama wacongo wamesharudishiwa! Ilikuwa ni billions of dollars!

Na hata za Gaddafi si wanazo pia? Watahakikisha hakuna Amani tena pale kwasababu huwa hawataki kurudisha hizo assets. Zinabaki kwao! Bush mkubwa alizuia za Mobutu. Na za Gaddafi zimezuiwa pia. Africans should wake up.
 
Lakini ni lazima tuwe na mazingira ya kutuwezesha kuwa na uhitaji wa hizo malighafi. Hatuwezi kuzihitaji kama hatuna viwanda vya ukweli. Na hatuwezi kuwa na viwanda vya ukweli bila umeme wa uhakika.

That’s the way I see it...
 
Duh...kwaiyo jamaa alikuwa anaiishi Ulaya ndani ya Afrika.
Mobutu ni wazungu walikuwa wanamtumia na yeye pesa mabilioni ya usd aliweka marekani na Europe! Hata alivyoondoka madarakani, wali freeze assets zake zote na sidhani kama wacongo wamesharudishiwa! Ilikuwa ni billions of dollars!

Na hata za Gaddafi si wanazo pia? Watahakikisha hakuna Amani tena pale kwasababu huwa hawataki kurudisha hizo assets. Zinabaki kwao! Bush mkubwa alizuia za Mobutu. Na za Gaddafi zimezuiwa pia. Africans should wake up.
 
Back
Top Bottom