Cybercrime
JF-Expert Member
- Feb 14, 2014
- 3,246
- 1,113
Leo ni siku muhimu kwa maendeleo ya taifa letu hasa kwa uwekezaji huu mkubwa uliozalisha ajira zaidi ya 200.
Miradi kama hii inadhihirisha tunajikomboa kiuchumi. Hoteli hii yenye hadhi ya nyota tano inachochea kukua kwa uchumi, hongera muwekezaji
Umenifurahisha umelipa kodi toka ulipoanza umelipa Bilioni 4 na ushee hongera Bakhresa
Kwa sasa Sekta ya Utalii inachangia asilimia 80 ya fedha za kigeni Zanzibar. Uwepo wa Hoteli hii utaongeza fedha za kigeni
Mmiliki wa hoteli hii ni Mtanzania mwenzetu ndio maana wakati wote nawaambia watanzania sisi sio maskini tukiamua tunaweza. Nampongeza Mzee Bakhresa kwa uwekezaji katika sekta mbalimbali
Naipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuweka mazingira bora kwa uwekezaji. Kwa uwekezaji huu mkubwa uliogharimu Bilioni 65
Mzee Bakhresa hakuzaliwa tajiri amezaliwa maskini amefanya kazi kwa bidii na kuwa mvumilivu mpaka ametajirika. Wawekezaji sio lazima watoke nje wawekezaji wanaweza kutoka ndani na kuleta tija kwa taifa.
Niwaombe viongozi waweke mazingira mazuri ili kuwatengeneza wawekezaji wazawa kwa maendeleo ya taifa
Watanzania na wanasiasa wenzangu msifiche mali zenu hata kama mlizipata kwa kificho wekezeni ili kulijenga taifa
Tutaendelea kulinda usalama wa wawekezaji na Watanzania ili Tanzania ibaki kuwa yenye neema na sehemu nzuri ya kukimbilia
Miradi kama hii inadhihirisha tunajikomboa kiuchumi. Hoteli hii yenye hadhi ya nyota tano inachochea kukua kwa uchumi, hongera muwekezaji
Umenifurahisha umelipa kodi toka ulipoanza umelipa Bilioni 4 na ushee hongera Bakhresa
Kwa sasa Sekta ya Utalii inachangia asilimia 80 ya fedha za kigeni Zanzibar. Uwepo wa Hoteli hii utaongeza fedha za kigeni
Mmiliki wa hoteli hii ni Mtanzania mwenzetu ndio maana wakati wote nawaambia watanzania sisi sio maskini tukiamua tunaweza. Nampongeza Mzee Bakhresa kwa uwekezaji katika sekta mbalimbali
Naipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuweka mazingira bora kwa uwekezaji. Kwa uwekezaji huu mkubwa uliogharimu Bilioni 65
Mzee Bakhresa hakuzaliwa tajiri amezaliwa maskini amefanya kazi kwa bidii na kuwa mvumilivu mpaka ametajirika. Wawekezaji sio lazima watoke nje wawekezaji wanaweza kutoka ndani na kuleta tija kwa taifa.
Niwaombe viongozi waweke mazingira mazuri ili kuwatengeneza wawekezaji wazawa kwa maendeleo ya taifa
Watanzania na wanasiasa wenzangu msifiche mali zenu hata kama mlizipata kwa kificho wekezeni ili kulijenga taifa
Tutaendelea kulinda usalama wa wawekezaji na Watanzania ili Tanzania ibaki kuwa yenye neema na sehemu nzuri ya kukimbilia