Uchaguzi 2020 Yaliyojiri uzinduzi wa Kampeni za CCM jijini Mwanza - Septemba 7, 2020

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,805
11,965
Leo mgombea wa Urais kupitia chama cha mapinduzi (CCM), Dkt. John Magufuli yupo jijini Mwanza baada ya kuwasili jana ambapo yeye na chama chake wanatarajia kuzindua kampeni zao jijini humo kwenye uwanja wa CCM Kirumba kuomba ridhaa ya wananchi kuendelea kuongoza serikali.

Mwaka 2015, Dkt Magufuli na chama chake walipata ushindi mnono jijini Mwanza na viunga vyake. Je, wapiga kura wataendelea kuwaamini na kuwapa ridhaa? Kuwa nami kukujuza yatakayojiri leo kwenye uzinduzi wa kampeni za chama cha Mapinduzi jijini Mwanza.

=====

Yaliyojiri

Dkt. Magufuli amesema: Tumefanya ukarabati wa Meli 5 na tumejenga Meli mpya kwa gharama ya Bil 152. Tumejenga vivuko vya MV Mwanza na MV Ilemela kwa Bil 2.7

"Nataka Meli zetu za MV Mwanza, MV Victoria na nyingine ziwe zinasafiri hadi Bukoba, Uganda, Musoma na kuja Mwanza"

Tumeanza kujenga Reli ya umeme na ili ikamilike ndiyo maana tumekuja tena kuwaomba kura. Mnaona Ndege kubwa za abiria na mizigo zinaondoka moja kwa moja hadi Ulaya.

"Inawezekana mkachagua wengine tutakuwa tumepoteza mipango ya kuiendeleza Mwanza"

Zamani maeneo ya huku ikiwemo Chato ilikuwa ukitaka kwenda DSM lazima upite Bukoba hadi Uganda, ukazunguke Kenya ndio uende DSM

"Yaani unaenda Makao Makuu ya Nchi yako ila lazima uzungukie Nchi mbili za jirani, haya sasa hayapo. Ukiona vyaelea vimeundwa"

Tunaupanua uwanja huu wa Mwanza, ndege yoyote kutoka nchi yoyote itatua hapa, tuongeze watalii, tukuze uchumi wetu.

Wapo wanaobeza atapigiwa kura na madaraja, watu wanaopita kwenye hayo madaraja, wanaotibiwa kwenye hospitali tulizojenga watanipigia kura Okt. 28.
======

Magufulinew.jpg
Mgombea wa Urais kupitia Tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akimvalisha kofia Msanii wa Bongo Flavor Nasib Abdul Diamond ambaye alikuwa akitumbuiza katika Mkutano ya Kampeni ya Chama cha Mapinduzi CCM uliofanyika leo tarehe 7 Septemba, 2020 jijini Mwanza

photo_2020-09-07_14-05-37.jpg


photo_2020-09-07_14-05-34.jpg


photo_2020-09-07_14-12-07.jpg


photo_2020-09-07_14-05-41.jpg

 
Ndiyo
Mwanza ndipo sehemu pekee ambayo hawapaswi kuiangusha CCM

✓ Barabara nzuri
✓ Wamenunuliwa meli
✓ Daraja la juu
✓ Uwanja wa ndege umepanuliwa vizuri
✓ Biashara za samaki zimeboreshwa siku hizi wanasafirisha kwenda nje ya nchi

Na mengineyo
 
Jana siku nzima barabara ya kutoka Musoma ilikuwa imejaa mpaka Mwanza mjini watu wanamsubiri, katoka Musoma asubuhi kafika Mwanza jioni, poleni sana msiompenda huyu mwamba.

wasafifm_20200907_4.jpg
wasafifm_20200907_5.jpg
wasafifm_20200907_2.jpg
wasafifm_20200907_1.jpg
wasafifm_20200907_3.jpg
wasafifm_20200907_4.jpg
wasafifm_20200907_5.jpg
wasafifm_20200907_2.jpg
wasafifm_20200907_1.jpg
wasafifm_20200907_3.jpg
millardayo_20200907_15.jpg
millardayo_20200907_8.jpg
millardayo_20200907_7.jpg
millardayo_20200907_6.jpg
millardayo_20200907_11.jpg
millardayo_20200907_12.jpg
millardayo_20200907_10.jpg
millardayo_20200907_9.jpg

Na leo hali ya hewa Mwanza ipo mujarabu sana, hakuna jua ni mawingu na ubaridi fulani amazing baada ya kunyesha mvua kubwa juzi, mheshimiwa ajiandae kuhutubia maelfu ya wakazi, mkoa wa Mwanza una idadi ya watu ~3million, roughly hakosi kura 800K, wafanyakazi, wapenda kuajiriwa na wapenda vinono, wapenda mishahara mikubwa bila kuhangaika huku hawazidi 200k ambao wengi wao hawataenda kupiga kura ila wataalam wa mitandaoni, so huku Lissu ategemee kura 80K , Membe 0.5K na Hashimu 2K.....

Tujage
 
Leo mgombea wa Urais kupitia chama cha mapinduzi(CCM), Dkt. John Magufuli yupo jijini Mwanza baada ya kuwasili jana ambapo yeye na chama chake wanatarajia kuzindua kampeni zao jijini humo kwenye uwanja wa CCM Kirumba kuomba ridhaa ya wananchi kuendelea kuongoza serikali...
Walimu na wanafunzi Leo wamepewa T-shirt na posho kwenda kujaza CCM Kirumba!!

Kweli CCM mmeishiwa!
 
Leo mgombea wa Urais kupitia chama cha mapinduzi(CCM), Dkt. John Magufuli yupo jijini Mwanza baada ya kuwasili jana ambapo yeye na chama chake wanatarajia kuzindua kampeni zao jijini humo kwenye uwanja wa CCM Kirumba kuomba ridhaa ya wananchi kuendelea kuongoza serikali.

Mwaka 2015, Dkt Magufuli na chama chake walipata ushindi mnono jijini Mwanza na viunga vyake. Je, wapiga kura wataendelea kuwaamini na kuwapa ridhaa? Kuwa nami kukujuza yatakayojiri leo kwenye uzinduzi wa kampeni za chama cha Mapinduzi jijini Mwanza.
Mkuu, stay tuned Magufuli atapata kura nyingi hatari Mwanza.
 
Watanzania tumeshuhudia maiti za Watanzania wenzetu zikiokotwa kwenye fukwe zikiwa zimefungwa mawe na vyuma na nyingine zikiwa kwenye viroba.

Watanzania, tumeshuhudia wenzetu wakitekwa na kupotezwa, wafanyabiashra wakifilisiwa.

Tumeona ndugu na jamaa zetu wakifunguliwa makesi makubwa na yasiyo na dhamana.

Huyu mtu hatufai kabisa.
 
Back
Top Bottom