Yaliyojiri Uwanja wa Amani, katika Kilele cha Sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar 12 Jan, 2016

Kibo10

JF-Expert Member
Aug 20, 2013
11,277
8,836
zanzibar.jpg



WAZANZIBARI leo wanasherehekea miaka 52 ya Mapinduzi ya Januari 12 mwaka 1964, ambayo yaling’oa utawala wa Sultani kutoka Oman na kuwezesha wazalendo wengi kushika hatamu ya kuongoza nchi.

Katika kilele cha sherehe hizi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein atahutubia taifa katika uwanja wa Amaan.

Matukio mengine makubwa yaliyofanyika katika uwanja huu ni Rais Shein kukagua gwaride la heshima la vikosi ya ulinzi na usalama, vikiongozwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Amepokea maandamano ya wananchi wa mikoa mitano ya Unguja.

Rais John Magufuli, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu na Viongozi wastaafu, Mzee Mwinyi, Benjamin Mkapa Aman Karume na Wengine Wengi wa Kitaifa, wamewasili uwanja wa Amani katika sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi ya Z'bar.

Vilevile Mkuu wa Majeshi Mwamnyange amehudhulia. Viongozi wengi wa Kitaifa wamehudhulia.

Maalim Seif Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar amekwepa Sherehe hizi.

Hizi sherehe za mapinduzi leo zimepoa. Hii inadhiirisha tatizo kubwa la mkwamo wa kisiasa lilipo Zanzibar, Si kama miaka ya nyuma.
=========

Shein: Kwa upande wa Zanzibar, kama sote tunavyofahamu, tume ya uchaguzi ilifuta uchaguzi wa Zanzibar tarehe 28 October mwaka jana baada ya kubainika kutokea kasoro kadhaa kama zilivyoelezwa na tume ya uchaguzi ya Zanzibar. Kadhalika uamuzi huo wa tume ulitangazwa katika gazeti rasmi la serikali tarehe 6 November mwaka 2015 kwamba tume ya uchaguzi ya Zanzibar imeyafuta matokeo yote ya uchaguzi mkuu wa Zanzibar na kwamba uamuzi wa tume kutangaza tarehe nyingine ya kurudia uchaguzi mkuu wa Zanzibar utatangazwa baadae.

Nawaomba wananchi waendelee kuishi kwa amani na waendelee kupendana huku tukisubiri tume ya uchaguzi ya Zanzibar itangaze tarehe nyingine ya kurudia uchaguzi wa Zanzibar. Kwa hio uchaguzi kwa mujibu wa katiba na sheria ya Zanzibar ya uchaguzi utarudiwa.


Kwa Hotuba kamili, Soma hapa chini.

HOTUBA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI, MHE. DK. ALI MOHAMED SHEIN, KATIKA MAADHIMISHO YA SHEREHE ZA MIAKA 52 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR, AMAAN STADIUM TAREHE 12 JANUARI, 2016.
 
Sherehe zimeanza wageni wengi wameshaingia uwanjani anayeingia sasa uwanjani ni mke wa rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Mama Mwanamwema Shein.
Mh. Mzakam wa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania sasa ndiyo anaingia uwanjani. Mlango wa gari yake ulisumbua kidogo.
Ukweli ni kwamba uwanjani watu ni wachache watoto wa alaiki ndiyo wengi zaidi uwanjani hapa.
Mh. Rais John Pombe Magufuli ameshaingia hapa uwanjani na anayesubiriwa sasa ni Rais wa Zanzibar Mh. Ally Mohamed Shein.
 
Last edited:
Wananchi wa Zanzibar hawawezi kufurahia hizo sherehe kwa ss, Nchi yao ni kama jahazi lililo kwenye mawimbi mazito kwa ss, hawajui pa kushika, hawaelewi hatima ya Nchi yao......hiyo furaha itatoka wapi?
Binafsi naiombea Zanziba kikombe cha Burundi kiwaepuke maana huu ukimya wao napata wasiwasi wa mshindo mkuu.
 
Inabidi ucheki ili ushuhudie mwenyewe...............Shein anazungushwa kwenye ki gari uwanjani amenunaaaaaaa
Mkuu nafsi inamsuta,mimi siwezi kuyaangalia ni heri nikatumia siku hii ya leo kuhamasisha wana mageuzi wenzangu tukaenda kufanya usafi kwenye ofice zetu za wilaya na mikoa
 
Hizi sherehe za mapinduzi leo zimepoa sana.Istoshe uwanja ni mweupe haijawahi tokea.
Watu ni wapweke,Wamejawa na mawazo.Hii inadhiirisha tatizo kubwa la mkwamo wa kisiasa lilipo Zanzibar.Wananchi wengi ni kama wamesusa,Si kama miaka ya nyuma.Watu walikuwa na raha shamra shamra kubwa na viongozi walikuwa na nyuso za furaha.Lipo tatizo
Nami muda huu naangalia matangazo hayo ambayo yanatangazwa moja kwa moja kupitia vituo mbalimbali vya luninga.
Ni kweli kabisa ulichokisema uwanja huo haujajazwa na wananchi wa kawaida, badala yake more than 90% ya waliohudhuria ukiacha viongozi wa kitaifa wa CCM, waliohudhuria kwa wingi ni wanajeshi wa JWTZ na wanausalama na idadi ndogo ya wanaUVCCM na mashabiki wachache wa chama cha magamba.
Kama alivyoeleza Maalim Seif jana kuwa chama chake kimesusia sherehe hizo na imethibitika uwanjani hapo kuwa hakuna kiongozi yeyote wa CUF wala vyama vinavyounda Ukawa aliyehudhuria sherehe hizo.
 
Kumbe Zanzibar wana mkuu wa majeshi wao!!? Nimesikia wakati nikifuatilia sherehe za Mapinduzi kupitia Azam tv. Wadau hili ni kweli au Nimepotoshwa?
Kama hili ni kweli basi tumekwisha.
 
Wananchi wa Zanzibar hawawezi kufurahia hizo sherehe kwa ss, Nchi yao ni kama jahazi lililo kwenye mawimbi mazito kwa ss, hawajui pa kushika, hawaelewi hatima ya Nchi yao......hiyo furaha itatoka wapi?
Binafsi naiombea Zanziba kikombe cha Burundi kiwaepuke maana huu ukimya wao napata wasiwasi wa mshindo mkuu.
Kweli nafurahi sana ujumbe huu aupate Lizaboni
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom