Kumbe hii kesi wanajaribu kumwondoa Urio. Halafu Akina Khalidi, Kaaya na Gabriel Muhina wakfutiwa kesi baada ya kumaliza mchezo??Habari Wakuu,
Leo 07/ 02/ 2022 shahidi wa 13 anatarajiwa kuendelea kutoa ushahidi wake kwenye kesi inayomkabili Mbowe na wenzake 3.
Kujua Kesi ilipoishia fungua kiungo hiki: Yaliyojiri kesi inayomkabili Mbowe na wenzake leo Februari 4, 2022. Kesi imeahirishwa. Shahidi wa 13 kuendelea kutoa ushahidi Februari 7, 2022
Updates:
Jaji ameingia
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani Muda huu
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Ikupendeze naitwa Robert Kidando nipo pamoja na
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Ikupendeza naitwa Peter Kibatala nipo Pamoja na
- Wakili Pius Hilla
- Abdallah Chavula
- Jenitreza Kitali
- Nassoro Katuga
- Esther Martin
- Tulimanywa Majige
- Ignasi Mwinuka
Jaji anaita Washtakiwa Wote wanne na wote wanaitika
- Wakili Nashon Nkungu
- John Mallya
- Dickson Matata
- Seleman Matauka
- Fredrick Kihwelo
WS Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa na Leo tuna shahidi Mmoja ambaye alishaanza Kutoa Ushahidi Wake, Tupo tayari Kuendelea
Kibatala: Nasisi pia Mheshimiwa Jaji tupo tayari Kuendelea
Jaji: Shahidi nakukumbusha kuwa Ijumaa Ulikula Kiapo na, Leo Utaendelea Kuwa Chini ya Kiapo
Shahidi: Sawa Mheshimiwa
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Sasa Inspector Swila, Siku ile Tulikomea Tarehe 27 October 2020 wakati unampatia DC Goodluck Bastola Baada ya hapo Ulifanya Shughuli gani Nyingine
Shahidi: Niliweza Kupokea Taarifa ya Uchunguzi na SilahaTarehe 27 November 2020 Nilipokea kutoka kwa koplo Azizi wa Kitengo Cha Silaha na Milipuko Nilipokea Silaha, Bastola aina ya Luger A5340, Risasi Moja, Maganda Mawili ya Risasi pamoja na Vichwa Viwili Vya Risasi
Wakili wa Serikali: Wakati unapokea Taarifa ya Risasi Moja pamoja na Maganda Mawawili, Ni wapi ilipokea
Shahidi: Katika Kitengo Cha Uchunguzi Wa Silaha na Milipuko
Wakili wa Serikali: Uliwezaje Kujua kama Ndiyo Silaha uliyopeleka
Shahidi: Niliweza Kuangalia Serial Namba ya Silaha, Nikakuta ni A5340 na Silaha aina ya Luger
Wakili wa Serikali: VIpi Kuhusiana na Risasi Zenyenwe zilikuwa na hali gani
Shahidi: Risasi niliyo pokea ilikuwa ni Moja, Ilikuwa haujatumika, Ilikuwa na Alama A3 na Risasi ambazo zimetumika Nilikuta zimepewa alama ya T1 na T2
Wakili wa Serikali: Nani aliweka alama katika Vielelezo hivyo
Shahidi: Mchunguzi Wa Vielelezo hivyo
Wakili wa Serikali: Baada ya Kuwa umepokea Riport na Vielelezo Ulifanya nini.?
Shahidi: Vielelezo nilipeleka Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam na Kwenda Kuvikabidhi
Wakili wa Serikali: Kitu gani hicho ulienda Kukabidhi Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam
Shahidi: Nilienda Kukabidhi Silaha, Bastola aina ya Luger A5340 na Risasi Moja, Maganda Mawili pamoja na Vichwa Vyake
Wakili wa Serikali: Na Report Ulifanyia nini
Shahidi: Report nilihifadhi na Kufungia katika Kabati langu la Chuma
Wakili wa Serikali: Baada ya Tarehe 27 November 2020, Nataka Kukurudisha Kwanza hapo ambapo unasema Ulikabidhi Risasi Moja, Maganda Mawili na Silaha, Je Ulimkabidhi nani
Shahidi: Nilimkabidhi Sarjent Nuru, ambaye Yupo Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam, ni Mtunza Vielelezo Katika ghala la Kutunzia Silaha
Wakili wa Serikali: Kabla ya kwenda Katika Shughuli Nyingine za Upelelezi, Ni wakati gani tena Ukiweza Kushughulika na Vielelezo hivyo
Shahidi: Nili shughulika tena wakati Wa Kutoa Mahakamani Kwa ajili ya Ushahidi, Ambapo Nilimkabidhi koplo Hafidh Kwa ajili ya Kuja Kutoa Ushahidi Mahakamani
Wakili wa Serikali: Turudi tena Katika Upelelezi Baada ya Tarehe 27 November 2020, kitu gani kiliendelea Wakati wa Kesi hiyo
Shahidi: Niliweza Kupokea Taarifa Kutoka kwa Mrajisi wa Silaha Siku ya Tarehe 18 March 2021
Wakili wa Serikali: Hiyo Taarifa Ilikuwa inahusu nini
Shahidi: Ilikuwa inahusu Mmiliki Wa Silaha Yenye Sirial namba A5340 aina ya Luger
Wakili wa Serikali: Na Ripoti hiyo ilisemaje
Shahidi: Report hiyo ilionyesha Kuwa Silaha hiyo, haina Usajili wowote Katika Ofisi Ya Mrajisi Wa Silaha Hapa Nchini
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine kiliendelea baada ya hiyo Tarehe 18 March 2021
Shahidi: Tarehe 30 March 2021 Niliweza Kupokea Taarifa Ya Maabara ya Sayansi, Kutoka Kitengo Cha Uchunguzi Wa Maandishi, Kutoka Kwa koplo Khamis, Wa Kutengo cha Uchunguzi Wa Maandishi. Niliweza Kusoma Ripoti hiyo, Ambapo Ripoti hiyo ilionyesha Kuwa Sampuli Za Maandishi yaliyo chukuliwa Kutoka Kwa Mtuhumiwa Khalfani Bwire Hassan, Ni sawa Sawa na Maandishi Yaliyokuwepo Katika Daftari nililoambatanisha katika Uchunguzi ule
Wakili Wa Serikali: Baada ya Kuwa Umesoma, Ukafanya nini
Shahidi: Niliweza Kuhifadhi katika Jalada langu la Kesi na Kufungia Katika Kabati langu la Chuma
Wakili wa Serikali: Baada ya Tarehe hiyo Kitu gani Kingine Ulifanya Kuhusu Kesi hiyo
Shahidi: Mnamo Tarehe 10 July 2021 Niliweza Kupokea Taarifa ya Simu zile Nane Kutoka Kwenye Maabara ya kisayansi Kitengo Cha Uchunguzi Wa Makosa ya Mtandao
Wakili wa Serikali: Ulipokea Kutoka Kwa nani
Shahidi: Nilipokea Kutoka Kwa Inspector Ndowo wa Kitengo Cha Uchunguzi Wa Makosa ya Ki Mtandao Wa Maabara Ya Kisayansi
Wakili wa Serikali: Baada ya Uchunguzi Wa Taarifa hiyo nini Kilitokea
Shahidi: Alijulishwa DC Goodluck ambaye haikuwepo Dar es Salaam, alinijulisha Kwa Uchunguzi umekamilika, Ndipo nilipoenda Kuchukua Taarifa hiyo
Wakili wa Serikali: Ulimkabidhiwa Kwa Utaratibu Upi
Shahidi: Kwa Kusaini Katika Kitabu cha Kitengo Cha Uchunguzi Wa Makosa ya Mtandao
Wakili wa Serikali: Mwanzono Ulisema Kwamba Ulipeleka simu, Sasa unakabidhiwa Riport, Vipi Kuhusu Zile simu
Shahidi: Pia Nilikabidhiwa Simu Nane ambazo niliziandikia Barua
Wakili wa Serikali: Ulijuaje Kama ndiyo Simu ulizopeleka
Shahidi: Niliweza Kuzikagua Wakati na kabidhiwa Wakili wa Serikali Ulifanyia nini hiyo Riport baada ya Kukabidhiwa
Shahidi: Simu Nane nilipeleka Katika Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam, Nilimkabidhi Coplo Charles ambaye ni Mtunza Vielelezo Katika Chumba Cha Kuhifadhia Vielelezo Katika Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Na Ile Ripoti Ulifanyia nini
Shahidi: Ripoti Ya Uchunguzi Niliweza Kusoma. Na Kuhifadhi katika Jalada la Kesi Kisha Kuweka Katika Kabati langu la Chuma
Wakili wa Serikali: Ripoti hiyo Kwa sababu wewe Ndiye Uliyeomba Uchunguzi, Ni Vitu gani Ukiweza Kupata Kutoka Katika Ripoti hiyo
Shahidi: Katika Report hiyo Niliweza Kugundua Vitu vifuatavyo, Niliweza Kugundua Kuwa palikuwa na Mawasiliano kati ya Shahidi Luteni Denis Urio na Mtuhumiwa Freeman Mbowe ambayo Yalifanyika Katika Mtandao Wa Telegram Pia Kupitia Maelezo Ya Shahidi Luten Denis Urio, aliweza Kusema Kuwa alitumiwa pesa Kutoka Kwa Mtuhumiwa Freeman Mbowe
Ambapo Tarehe 20 July 2020 Namba 0719933386 ambayo ni Ya Mtuhumiwa Freeman Mbowe ilituma Kiasi cha TSh 500,000 Kwenda Kwa namba ya shahidi Luteni Denis Leo Urio ambayo ni 0787 555200.
Pia Tarehe 22 Mwezi huo huo wa July 2020 ilionyesha Kuwa Shahidi Luten Denis Urio Kupitia namba yake ya 0787 555200 ulipokea Kiasi cha TSh 199,000 kutoka Kwenye namba ya Wakala Kama alivyo eleza Luten Denis Urio.
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo Nini Kiliendelea
Shahidi: Tuliendelea Kuandika Taarifa Mbalimbali na Kupitia Ripoti hiyo Niliweza Kujiridhisha kuwa ni kweli Mtuhumiwa Freeman Mbowe aliweza Kutuma hizo Fedha Kwa Luten Denis Urio
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea baada ya hapo
Shahidi: Siku ya Tarehe 27 July 2021 Watuhumiwa Justin Kaaya, Khalid na Gabriel Muhina Walifutiwa Shitaka Lao baada ya Kugundulika hawahusiki na chochote
Wakili wa Serikali: Turudi Baada ya Kupokea Ripoti Ya Uchunguzi Wa Kisayansi Kuhusu Simu, Baada ya Hapo Ulifanya nini
Shahidi: Mnamo Tarehe 18 July 2021 Niliandika Taarifa Kwenda Kwa Afande Mkurugenzi Wa Upelelezi wa Makosa Ya Jinai Nchini, Kuwa Kuna Ushahidi Wa Uhusika wa Mtuhumiwa Freeman Aikael Mbowe, nakuwezesha Kumkamata
Wakili wa Serikali: Mwanzoni Wakati Unatoa Ushahidi Wako Ulizungumzia Kuhusu Kufungua Majalada Mawili, Je ni Jalada lipi ambalo wewe Uliandikia Taarifa
Shahidi: Ni lile Jalada la Kesi tulilo fungulia Polisi, ambalo ni CD/IR /2097 /2020 lenye Chama za Kutaka Kufanya Vitendo Vya Kigaidi
Wakili wa Serikali: Wakati Wa Kufungua Jalada la Kesi hili CD /IR /2097 /2020 Ulisema Kwamba Usiandike Jina la Freeman Mbowe Kwa sababu Kama Ungeandika Jina Taarifa zingeweza Kuvunja, na akasitisha Mpango Wake, Je Ulikuwa Unamaanisha Nini
Shahidi: Nilikuwa namaanisha kuwa angeweza Kusitisha Kumtumia Mtoa Taarifa, angeweza Kutumia Watu wengine ambapo Jeshi la Polisi lisingejua Mahali wala Muda, Kitu ambacho. Lingesababisha Jeshi la Polisi Kushindwa Kuzuia Uhalifu
Wakili wa Serikali: Baada ya Kuandika Taarifa Kwenda Kwa DCI Nini Kiliendelea
Shahidi: Nilipokea Taarifa Kutoka Kwa Afande Ramadhan Kingai Kamishina Msaidizi Wa Polisi alinitaka nitunze Jalada hilo na Kwamba Yeye anafanya Jitihada za Kumkamata Mshitakiwa Freeman Aikael Mbowe
Wakili wa Serikali: Baada ya DCI Kukwambia Hatua ambazo angechukua nini Kilitokea sasa
Shahidi: Mnamo Tarehe 22 July 2021 Nilipokea Karatasi Ya Mtuhumiwa Freeman Aikael Mbowe Kutoka Kwa Afande Jumanne Malangahe Mrakibu Wa Polisi, Kimsingi Nilipokea Maelezo hayo Ikionyesha Mtuhumiwa amekataa Kutoa Maelezo Yake Polisi
Wakili wa Serikali: Kwa Kipindi hicho Ulifahamu huyo Mtuhumiwa Freeman Mbowe amepatikanaje
Shahidi: Nilifahamu Kwamba amekamatwa Mwanza na Kusafirishwa Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Umekuwa Ukizungumza Majina Ya Watu Kadhaa Hapa Mahakamani akiwepo, Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe. Hebu ieleze Mahakama Kama Watu hao wapo hapa Mahakamani
Shahidi: Ndiyo Watu hawa wapo hapa Mahakamani
Wakili wa Serikali: Hebu onyesha sasa
Shahidi: Mtuhumiwa Wa Kwanza, Kutoka Upande Wa Kulia ni Khalfani Bwire Hassan, Wapili kutoka Kulia Kwangu ni Adam Hassan Kasekwa, Watatu Kutoka Kulia Kwangu ni Mohammed Abdilah Ling'wenya na Wanne Kutoka Kulia Kwangu ni Freeman Aikael Mbowe
Wakili wa Serikali: Sasa Mwanzoni Wakati Unatoa Ushahidi Wako Ulizungumzia Kuhusu Khalfani Bwire, Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya Walifikishwa Mahakamani Tarehe 19 August 2020, Mtuhumiwa Freeman Mbowe alifikishwa Mahakamani Tarehe ipi
Shahidi: Mtuhumiwa Freeman Mbowe alifikishwa Mahakamani Tarehe 26 July 2021
Wakili wa Serikali: Ni tofauti gani ipo Kutokana na Kufikishwa Tarehe tofauti na Wale 3
Shahidi: Utofauti unakuja Kutokana na Kusubiri Kwa Taarifa Ya Uchunguzi Wa Makosa ya Mtandao, ambao Kimsingi Nilipokea Tarehe 10 July 2021
Wakili wa Serikali: Sasa na Upelelezi Wa Kesi inayo wakabili, Ni Ushahidi gani ulipata Kwamba Walikula Njama za Kutenda Matendo Ya Ugaidi
Shahidi: Ni Kupitia Maelezo Yao ya Onyo ya Mshtakiwa Wa Pili Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya pamoja na Mshitakiwa Wa kwanza Khalfani Bwire Hassan, Pia Ushahidi Mwingine ambao Unaonyesha walikuwa Njama ni Kupitia Maelezo Ya Shahidi Luten Denis Urio,
Shahidi: Maelezo Ya Askari Walio wa kamata, Askari Walio andika Maelezo Ya Watuhumiwa
Wakili wa Serikali: Kuhusiana na Pesa iloyotumwa, Uliiweza Kubaini nini?
Shahidi: Niliweza Kubaini Fedha hiyo ilitumwa kutoka Kwa Freeman Mbowe Kwenda Kwa Luten Denis Urio, Ambapo Fedha hiyo iliweza Kuwawezesha Watuhumiwa Mshitakiwa Wa Pili na watatu pamoja na Mwingine ambaye hajakamatwa Kuweza Kufika Eneo la Uhalifu ambalo lilikuwa Eneo la Moshi Niliweza Kubaini Kuwa Fedha hiyo ilitumwa iliwezesha Watuhumiwa Kufika Eneo la Utekelezaji Wa Uhalifu
Wakili wa Serikali: Unaposema Kwamba Mshitakiwa Wa Pili, Watatu na Mwingine hajakamatwa, Vipi Mtuhumiwa Wa Kwanza Kuhusiana na Fedha hii
Shahidi: Kuhusu Mshtakiwa Wa kwanza Inaonyesha Pia aliweza Kupokea Pesa kutoka kwa Luten Denis Urio Kwa ajili ya Utekelezaji Wa Vitendo Vya Kigaidi
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Naomba Kukomea hapo Kwenye Examination inchief
Upande wa Utetezi
Wakili Nashon Nkungu: Shahidi Habari za Leo
Shahidi: Njema
Nashon: Shahidi umepona?
Shahidi: Bado
Nashon: Umemeza Dawa zako
Shahidi: Ndiyo
Nashon: nadhani Shahidi unatambua Ukubwa wa hii Kesi
Shahidi: Sahihi
Nashon: Kwamba Ugaidi ni Jambo Serious kwa Nchi na Dunia
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Kutokana na Userious wa Mashitaka, Hata Uchunguzi Wako Ulitakiwa Uwe serious Ku Match na Makosa haya
Shahidi: Sahihi
Nashon: Kupitia Ushahidi Wako uliotoa, Unaweza Kusimama Kifua mbele Kwamba ulitendea Haki Uchunguzi Wa Kesi hii
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Makosa ni Vitu Vinavyotengenezwa na Sheria
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Kuna Sheria ambazo zilikuwa zinawaongoza
Shahidi: Ni sahihi
Shahidi: Tutajie Sheria zipi Mlikuwa Mnazitumia Kuwa Guide
Shahidi: Sheria Mbalimbali
Nashon: Nitajie Sheria Mbili Mlikuwa Mnazitumia
Shahidi: Sheria ya Kuzuia Ugaidi na Sheria ya Mwenendo Wa Makosa ya Jinai
Nashon: Ni nani aliye angalia Sheria akatoa conclusion Kwamba alisema Kwa Story hii, haya ni Makosa ya Ugaidi
Shahidi: Ni Ramadhan Kingai Kamishina Msaidizi Wa Polisi
Nashon: Wewe huku take part katika Kujua haya ni Makosa ya Ugaidi
Shahidi: Hata Mimi Mwenyewe pia nilikuwa najua haya Makosa ni ya Ugaidi
Nashon: Una utaalam wa Kung'amua Kuwa haya ni Makosa ya Ugaidi
Shahidi: Ndiyo
Nashon: Ulisomea wapi
Shahidi: INTERNATIONAL LAW ENFORCEMENT ACADEMY Botswana
Nashon: Kozi gani
Shahidi: FIRST BURST SCENE
Nashon: Kwa hiyo Walimu Wako wakakwambia Kwamba Kozi hiyo ina husika na Ugaidi
Shahidi: Inahusika na Milipuko
Nashon: Shahidi Ulisema Kwamba Mmoja ya Watuhumiwa Katika kesi hii ni Justin Kaaya
Shahidi: Sahihi
Nashon: Uliwahi Kumuandika Kaaya Maelezo Ya Onyo
Shahidi: Hapana
Nashon: Je Unafahamu Kwamba Kaaya alitumiwa pesa na Freeman Mbowe
Shahidi: Ni Kweli
Nashon: Uliwahi Kumuandika Kaaya Maelezo Ya Ushahidi
Shahidi: Sahihi
Nashon: Alikwambia Kwamba aliwahi kutumiwa pesa na Freeman Mbowe
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Ni sahihi Kwamba alitumiwa pesa kama Watuhumiwa Wengine hapa Mbele
Shahidi: Hapana
Nashon: Justine Kaaya, Khalfani Bwire wote Walitumiwa pesa na Freeman Mbowe
Shahidi: Sahihi
Nashon: Wote hawa Wametumiwa pesa na Freeman Mbowe
Shahidi: Sahihi, lakini Malengo ni tofauti
Nashon: Malengo ya pesa ya Khalfani Bwire unayatoa Wapi
Shahidi: Maelezo ya Mtuhumiwa
Nashon: Maelezo ambayo Washtakiwa Wanataka kwamba hawakuyatoa Kwa hiari yao, Bali kwa Mateso ndiyo Ushahidi Wako wa Pekee?
Shahidi: Maelezo ya Washtakiwa Wengine
Nashon: Je Unafahamu Kwamba Kaaya alisema alikuwa anapewa pesa na Freeman Mbowe Kwa ajili ya Kutoa Taarifa Za Sabaya
Shahidi: Lakini alikuwa hafahamu Malengo
Nashon: Je tangu ugundue hakuwa na Nia Mbaya ilikuwa ni Muda gani baada ya Kumkamata
Shahidi: Zaidi ya Miezi 10
Nashon: Ulimkamata lini
Shahidi: Mwezi September 2020
Nashon: Ukaja Kumuachia lini
Shahidi: Mwezi July 2021
Nashon: Baada ya Mwaka mmoja ndiyo Ukajua hakuwa na Melengo Mabaya
Shahidi: Sahihi
Nashon: Ni sahihi Taarifa za Sabaya Freeman Mbowe alizitoa Kwa Kaaya
Shahidi: sahihi
Nashon: Kwamba alilipwa kwa kazi hiyo
Shahidi: sahihi
Nashon: wewe Hukuona Kosa
Shahidi: sahihi
Nashon: Na Kwamba alikuwa anakaa Kikao na Mbowe Kutoa Taarifa hiyo
Shahidi: Sahihi
Nashon: Kwa Kushiriki Kikao hicho Kaaya alikuwa anashiriki Kikao cha Kigaidi
Shahidi: Alikuwa ajui Dhumuni La Kikao, Kwa hiyo ajashiriki Kikao cha Kigaidi
Nashon: Lakini katika Kikao hicho hicho Mbowe alishiriki Kikao cha Ugaidi
Shahidi: Ndiyo
Mahakama: KICHEKO
Nashon: wakati gani ulipokea Bastola
Shahidi: Baada ya Kutoka Maabara
Nashon: Uli label?
Shahidi: Siku Label
Nashon: Lakini Simu za Mshtakiwa Wa kwanza ndiyo Uli Label
Shahidi: Hapana Siku Label
Nashon: Wewe Uli Label Simu za nani
Shahidi: Luten Denis Urio
Nashon: Na uli Label lini
Shahidi: Tarehe 11 na 13 August 2020
Nashon: Je ni sahihi Kwamba Ulichukua Bastola ya A5340 pamoja na Risasi kutoka Kwa Coplo Hafidh
Shahidi: Nilipokea Silaha A5340 aina ya Luger kutoka Kwa Hafidh Ikiwa na Risasi Moja, Maganda Mawili
Nashon: Ulipokea Vielelezo Kutoka kwa koplo Hafidh
Shahidi: Sahihi
Nashon: Naomba Upokeee Simu, Mheshimiwa Jaji ni Kutoka Katika Kielelezo P28
Nashon: hii aina au dizaini la Ku Label unaitolea wapi
Shahidi: Kipo Kwenye Sheria
Nashon: Sheria ambayo unaitumia ni Sheria gani
Shahidi: Ni PGO
Nashon: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kama ulijaza Makabidhiano wakati wa Makabidhiano
Shahidi: Humu sijaandika
Nashon: Unafahamu Kwamba Katika Kielelezo, Lebel ya Kielelezo pale Unapo ambatanisha namba ambayo unaambatanisha inatakiwa uwe namba ya Jalada la Kesi
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Unafahamu Kwamba Unatakiwa pia uwe na Exhibit Serial number
Shahidi: Siyo lazima, Kwa sababu hivi Vielelezo Vilikuwa kwenye Mfuko kwa hiyo Exhibit Serial number inakuwa kwenye Mfuko
Nashon: Hiyo PGO Unayosema Ulitumia inataka uwe na Mahala, namba na Tarehe mnayokabidhiana
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Lakini hapa Hakuna hata Moja
Shahidi: Ndiyo hapo Hakuna
Shahidi: SAMAHANI MHESHIMIWA JAJI NAOMBA NIENDE WASHROOM (CHOONI)....
Shahidi karejea
Nashon: Nipo interested na Shahidi ambaye alikuwa Mtuhumiwa akaachiwa
Nashon: Je ni sahihi Katika Maelezo Uliyo Mwandika Wewe, aliandika Kuwa aliwahi Kuwa Msaidizi Wa Katibu wa CCM Wilaya ya Meru
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Pamoja na Kwamba kapokea Fedha, na Kashiriki Vikao ila akaachiwa
Shahidi: Sahihi
Nashon: nani ni Mwamuzi ambaye aliamua kuwa Pesa hizo siyo za Ugaidi
Shahidi: ni Upelelezi
Nashon: Ni nani hasa
Shahidi: Mchakato Wa Upelelezi
Nashon: Ni sahihi Kwamba Uliwahi kuandila Maelezo Yako Mwezi 6 August 2020
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Ni sahihi Kuwa katika Maelezo yako Uliwahi Kusema Kuwa Mbowe ameshiriki Vikao Vya Kigaidi
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Na Katika Maelezo yako Ulisema Kwa, Kuthibitisha hilo ni Kupitia Maelezo ya Onyo ya Washtakiwa Wenzie
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Ni sahihi Kwamba wewe na Wapelelezi Wenzio hamkuwahi Kushuhudia Mbowe akiwa katika Kikao cha Ugaidi
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Ni sahihi Kwamba Wewe na Wapelelezi Wenzio hamkuwahi Kushuhudia Mbowe akiwa katika Kikao Mbeya au Arusha?
Shahidi: Sahihi
Nashon: Ni sahihi Kwamba pia nyie Kama Wapelelezi wa Kesi hii hamna CCTV Camera
Shahidi: Ni sahihi hatuna
Nashon: Ni sahihi Kwamba wewe na Wapelelezi Wenzio hamna hata Sauti ya Mbowe akipanga Ugaidi
Shahidi: Ni sahihi hatuna
Nashon: Ni sahihi Kwamba Jeshi la Polisi lina Vifaa Vya Kurekodi Sauti
Shahidi: Siwezi Kuzungumzia hilo
Nashon: Lakini Unafahamu Kwamba Simu inaweza Kurekodi Sauti
Shahidi: Ndiyo
Nashon: Na Jeshi la Polisi hamkazwi kutumia Simu Kurekodi Sauti
Shahidi: Ndiyo
Nashon: unajua Kuwa Mahakama Inaruhusu Kutumia Video na Sauti katika Ushahidi
Shahidi: Sifahamu
Nashon: Nikumbushe Cheo Chako huko Polisi
Shahidi: Inspector Wa Polisi
Nashon: Na Inspector Wa Polisi Ujui Kuwa Mahakama Inatumika Video na Sauti Katika Ushahidi
Shahidi: Ndiyo
Nashon: Ndiyo Maana hamkuleta Video wala Sauti Mahakamani Kwa sababu ufahamu Ka Inatumika Mahakamani Kama Ushahidi
Shahidi: Ndiyo
Nashon: Nionyeshe Sasa sehemu ambayo Mahakama itaona Mbowe alikaa Vikao Vya kigaidi
Shahidi: Ilikuwa Kwenye Gari, Ukisoma Maelezo Utaona
Nashon: Naomba Sasa Mahakama Ikupatie hizo Meseji Shahidi: Nimeona Meseji ya Tarehe 22 July 2020 Muda wa Saa 7 na Dakika 49 "Kutakuwa na Safari ya kwenda Hai, Leo Usiku au Asubuhi" Mahakama
Nashon: Naomba Sasa Mahakama Ikupatie hizo Meseji
Shahidi: Nimeona Meseji ya Tarehe 22 July 2020 Muda wa Saa 7 na Dakika 49 "Kutakuwa na Safari ya kwenda Hai, Leo Usiku au Asubuhi"
Mahakama: Kicheko
Shahidi: hii Inaelezea Sasa Kwamba Kutakuwa Kuna Kikao
Nashon: Katika hiyo Meseji wataje Wanaokutana
Shahidi: Mtuhumiwa Wa Kwanza, Wa pili, Watatu na Wanne
Nashon: Kwa hiyo akisoma hiyo Meseji ataona Kwamba Kuna Kikao cha Ugaidi
Shahidi: Ushahidi ni Kuunganisha Dot
Nashon: Kwa hiyo Nikisoma Meseji ipi nitaona nani na nani wametajwa, Saa ngapi na Wapi
Shahidi: Kwenye Meseji Hauwezi Kuona, ila Kwa Kuunganisha Dot
Mahakama: Kicheko
Nashon: Tutoke hapo umesha Sema hatutoona. Meseji Twende Kwingine
Nashon: Ni kweli Kwamba Mlikuwa na Msiri wenu Denis Urio
Shahidi: Ndiyo
Nashon: Baada ya Kuona hiyo Meseji Kwamba wanaenda Hai, nyie Hamku fuatilia
Shahidi: Hatukufutilia
Nashon: Mnafahamu Kuwa Aishi Hotel Ina CCTV Camera
Shahidi: Sifahamu
Nashon: Na hufahamu kwa sababu hujawahi Kufika Aishi Hotel
Shahidi: Kimya
Nashon: Sasa Ulifanya Juhudi zozote za Kwenda Pale Aishi Hotel kama Mpelelezi ambaye Yupo serious, labda Kuandaa Warranty, CCTV CAMERA Kuangalia List ya Wageni
Shahidi: Sikuwahi Kufanya hivyo
Nashon: Kwa ujasiri kabisa Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa Uliwezaje Kuwaleta Watuhumiwa Mahakamani Kwamba Wamekutana sehemu fulani ambayo wewe na Polisi Wengine hamjawahi Kufika
Shahidi: Mimi nilikuwa sehemu ya Upelelezi tu, Kuna wengine ambao walikuwa Arusha na Kilimanjaro
Nashon: Kwa hiyo Wewe Kwa sababu upo Dar es Salaam hukuona Sababu
Shahidi: Hapakuwa na Ulazima
Nashon: Sasa Pale Aishi Walifanya Nje au Ndani
Shahidi: Nje Kwenye Garden
Nashon: Garden ya upande upi
Shahidi: Sifahamu Sijawahi Kufika
Nashon: Katika Ushahidi Wako Nimekusikia Mahala Kwamba Unasema Ulikuwa unapokea Vielelezo na Kuvitunza, Je Hapa Mahakamani umewahi Kusema Kuwa Uliwahi Kuwa Forensic Beaural
Shahidi: Sijawahi Kusema
Nashon: Wewe Ulikaa na Vielelezo Vipi ambavyo Uliviandaa Kwa ajili ya Ushahidi
Shahidi: Simu za Urio Nashon Simu za Urio tu?
Shahidi: Simu zote Nane
Nashon: za Kwanza
Shahidi: Nilipokea Tarehe 07 August 2020 Mpaka Tarehe 13 August 2020
Nashon: tukumbushe nani alivileta Mahakamani
Shahidi: Hivyo Vielelezo Nilimpa Inspector Ndowo
Nashon: Lini
Shahidi: Sikumbuki
Nashon: Kwa sababu hamkuandikishana
Shahidi: Tuliandikishana
Nashon: Lakini Tukiangalia katika PF 145 Hatuoni sehemu Mliyo kabidhiana
Shahidi: Ni sahihi Hakuna
Nashon: Ulikuwa unafahamu kuwa Sheria inataka uonyeshe Katika PF 145
Shahidi: Nilikuwa nafahamu
Nashon: ila Ukaamua Kupuuza Sheria
Shahidi: Hapana
Nashon: Ni sahihi Uliondoka HQ August 2021
Shahidi: sahihi
Nashon: Ni sahihi Kwamba hujaeleza Mahakama Baada ya Kuondoka Ofisini Kwako Vielelezo ulimuachia nani
Shahidi: Usipotoshe Mahakama, Nilisema Kwamba Vielelezo Vyote nilikuwa nimepeleka Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam
Nashon: Unakumbuka Muda ambao Ulikaa na Vielelezo, Ambapo Vilienda Polisi Kati Dar es Salaam na kukaa navyo katika Kabati la Chuma
Shahidi: Kwa nani? Kwa Tarehe ipi?
Nashon: Je ni sahihi Kwamba Ulichukua Vielelezo Kutoka Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam Yes or No Shahidi Yes
Nashon: Kwanini Sasa unapoteza Muda Wa Mahakama
Nashon: Baada ya Uchunguzi Ulikaa navyo au ulipitiliza Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam
Shahidi: Nilipeleka Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam
Nashon: Kwa hiyo ni sahihi Kwamba Ulikuwa Umekaa na Vielelezo Katika Kabati lako wakati wewe siyo Mtunza Vielelezo
Shahidi: Nilikaa navyo Kwa ajili ya Kuviandikia Barua, Sababu ya Upelelezi
Nashon: Ilikuwa inashindikana Kwa wewe Kuandika Barua Vielelezo Vikiwa Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam
Shahidi: Ilikuwa Haiwezekani
Nashon: Unafahamu Kwamba OC Forensic Beaural ndiye anaye husika Katika Kuandaa na Kutunza Vielelezo Kabla ya Kwenda Kufanyiwa Uchunguzi
Shahidi: OC wa Forensic Beaural anapelekewa na Mpelelezi
Nashon: Je Unafahamu Kwamba OC Forensic Beaural ndiye anaye husika Katika Kutunza, Kuandaa na Kupeleka kwa Expert Examination
Jaji: sijui Mimi Ndiyo sielewi, Naomba Wakili unisaidie
Wakili Kihwelo: Swali lake linahusu Custodian wa Kutunza kabla ya kwenda Kwa Expert Examination
Shahidi: Sifahamu
Nashon: Katika Ushahidi Wako Kuna sehemu Kwamba Ulisema DCI alikwambia pamoja na OC Forensic Beaural ndiyo Mtunza Kielelezo, lakini wewe Kaa navyo
Shahidi: Sikueleza hayo
Nashon: Kwakuwa Umeibuka Mjadala hapo, Na Kwakuwa Mheshimiwa Jaji Shahidi alisema anaifahamu PGO naomba ni Muonyeshe Shahidi PGO hii ambayo alikuwa anaitumia Wakati wa Kufanya Kazi, PGO ya 8 Paragraph ya 9
Jaji: Rudia na uongeze Sauti
Nashon: Soma Kipengele (e)
Jaji: Samahani, Hapa OC anahusika baada ya OC kuwa ameletewa Vielelezo Hapa Sheria inasema Kwamba OC Forensic Beaural, Ndani ya Forensic baada ya Kuvipokea Nataka sasa Kufahamu Premise ya swali lako naandikaje, Inawezekana Unahoja ila namna ya ulivyoliweka ndiyo Unanichanganya
Nashon: labda Kwako Mheshimiwa Jaji, lakini najua siyo sawasawa.
Wakili John Malya: Mheshimiwa Jaji Kwa Kuokoa Muda, wakili aende Kwenye eneo lingine baadae ndiyo arudi kuunganisha hapo
Jaji: Sawa
Wakili wa Serikali Robert Kidando Mheshimiwa Jaji hata sisi tunapata tabu sababu Shahidi Alisha Sema siyo Utaratibu, nilifikiri Kuanzia pale ndiyo tuelezwe Jaji Ndiyo Maana wanasema Watarudi Baadae
Nashon: Shahidi Ni sahihi Kwamba Wewe ndiyo ulimuandika Maelezo Luten Denis Urio
Shahidi: Sahihi
Nashon: Je Hukuona Kosa pale Ambapo Luteni Denis Urio aliposema Kwamba "Mlimkubalia kwa kwenda Kutafuta Watu wa Kufanya Vitendo Vya Kigaidi" alikuwa anatenda Kosa
Nashon: Shahidi Soma yote ndiyo Utaona siyo Kosa
Wakili Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji naomba hapa Kuweka Sawa, Shahidi anaitwa kwa Sheria tofauti na Kifungu tofauti, Sasa anapoelekea Wakili akatazwe, shahidi awezi Kuwa mtuhumiwa
Wakili Nashon Nkungu: Mheshimiwa Jaji kumsitiri Kaka Yangu Abdallah Chavula PGO 236 Paragraph 08 ambapo inasema During police officers during taking statement.................
Wakili Wa Serikali Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji Nafikiri aendelee
Nashon: Kwa Ufahamu Wako Kumtafutia Mhalifu Wahalifu Wa Kwenda Kutimiza Uhalifu Siyo Kosa
Shahidi: Inategemea
Nashon: Huyu Luteni Denis Urio alikuwa ni Askari Polisi
Shahidi: Hakuwa Askari Polisi
Nashon: Je huyu Luteni Denis Urio Mlimpa Ulinzi Wa Kisheria
Shahidi: Siyo Mimi niliye pokea Taarifa zake, Mara ya Kwanza alitoa Taarifa Kwa DCI
Nashon: Kwani huyu Luteni Denis Urio alikuwa na Taaluma ya Upelelezi
Shahidi: Siyo Mimi niliye pokea Taarifa
Nashon: Kwani Luten Denis Urio Mlimfundisha Kuhusu Kufanyia Watu Upelelezi
Shahidi: Mimi Sikuwahi Kumuona Luten Denis Urio kabla
Nashon: Umesikiliza Ushahidi Wa Luten Denis Urio
Shahidi: Wapi
Nashon: alipokuwa hapa Mahakamani
Shahidi: Sikuwepo Mahakamani
Nashon: Sawa, Ngoja ni kwambie sasa, Urio Mada aliwatafuta Watuhumiwa lakini hawakuwa wanajua Kuwa wanaenda Kufanya Ugaidi
Nashon: Je Muda gani sasa Khalfani Bwire alipata Guilty Mind
Shahidi: anafahamu Mwenyewe
Nashon: Je ni muda gani Adam Kasekwa alipata Guilty Mind
Shahidi: anajua yeye Mwenyewe
Nashon: Je ni Muda gani Mohammed Ling'wenya alipata Guilty Mind
Shahidi: Sifahamu
Nashon: Katika Ushahidi Wako Ulisema Uliitwa Tarehe 14 July 2020 kwa Mkurugenzi, Je ni sahihi
Shahidi: Siyo Sahihi
Nashon: Wacha nisome... Wakili anasoma
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Kwa hiyo Tarehe 14 July 2020 Taarifa zimekuja tayari Kuna Kundi
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Unafahamu Kwamba Pesa zimeanza kutumwa Tarehe 20 July 2020
Shahidi: Ndiyo
Nashon: Je hilo Kundi lililkuwepo Kabla halijakutana Tarehe 20 July 2020
Shahidi: Lilikuwepo Kabla
Nashon: Je Unafahamu Kwamba Kundi Lilianza kutengenezwa na Luteni Denis Urio Tarehe 20
Shahidi: Kundi Lilikwepo Mara baada ya Luteni Denis Urio Kukutana NA Freeman Mbowe
Nashon: Kwani hilo Kundi ni hili au Kundi lingine
Shahidi: Ni hili
Nashon: Kwa hiyo Wewe na Luteni Denis Urio Mahakama iangalie nani anasema Kweli
Shahidi: Mahakama ndiyo itajua
Nashon: Shahidi Ni sahihi Ulisema Kwamba Hamkuandikisha Jina la Freeman Mbowe Kwa sababu Taarifa zingevuja
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Kwa hiyo Kuna Askari siyo Waaminifu
Shahidi: Tulihofia Kwamba Kile Kitabu kinasomwa na kubadilishana Taarifa Kwa Polisi
Nashon: Kwani wewe Unafahamu sheria yoyote inayoruhusu Kufungua Kwa Jalada bila Kujaza Jina
Shahidi: Hakuna
Nashon: Lakini Unafahamu Sheria ambayo Inaelekeza Majina yajazwe
Shahidi: Nafahamu
Nashon: Shahidi Wakati Unaenda Kule Coco beach, Kumtafuta Khalfani Bwire, Hukuona haja ya Kuwa chukua Watuhumiwa Wenzake Kwenda pamoja Kumtafuta Khalfani Bwire Kwa sababu wangemtambua hata Kama kawapa Mgongo
Shahidi: Hapakuwa na haja hiyo
Nashon: Shahidi, Ulisema Kuna Kidaftari
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: Ulisema Kile Kidaftari Kina Michoro Ya Ramani
Shahidi: Sahihi
Nashon: Kwani wewe Unataaluma Ya Ramani
Shahidi: Hapana, ila naweza Kusoma Ramani
Nashon: Kwani Nikochora Duara Utajua ni Kisima
Shahidi: Hapana
Shahidi: waliandika Majina ya Barabara, na Mishale ya Kuingia na Kutoka
Nashon: Kwani Walitaja Mikoa
Shahidi: Hapana
Nashon: GBP na Bigbon
Shahidi: sahihi
Nashon: Kilicho Kufanya Ujue ni Kariakoo na Morocco uliyokwenda ni ipi
Shahidi: Sababu palikuwa na Majina ya Barabara
Nashon: Ulisema Kwamba Khalfani Bwire alikataa Sampuli ya Maandishi
Shahidi: Ndiyo
Nashon: Unafahamu Kwamba Unapokuwa unuhoji Mtuhumiwa Kuna Haki zake ikiwemo Kuandika Maelezo Ya Onyo
Shahidi: Nafahamu
Nashon: Maelezo ya Kukataa hapa Mahakamani yapo Wapi
Shahidi: Hakuna
Nashon: Kwani Hakuna Majina ya Barabara yanayo Fanana, Kama Morocco zipo mbili Kinondoni
Shahidi: Nafahamu zipo Mbili
Nashon: Hicho Kidaftari Kipo hapa Mahakamani
Shahidi: Hapana
Nashon: Unasema Ulikuwa Unawatoa Watuhumiwa Mahabusu Kuwachukua sampuli Je huo Muda Ulifanyika Kisheria
Shahidi: Ndiyo
Nashon: Umeleta Detention Register ambayo Inaonyesha Walitoka Saa ngapi na Kurudi Saa ngapi
Shahidi: Hapana
Nashon: Nikikataa kuwa Hukuwa toa Kisheria unaushahidi gani
Shahidi: Maelezo yangu
Nashon: Mheshimiwa Jaji naomba Kuishia hapa Kwa Shahidi huyu
Wakil John Mallya: Mheshimiwa Jaji Nina Maswali Kadhaa, Ila naona Muda wa Health Break Umefika, Naomba tuairishe Kwa sasa
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Kwa Dakika 45
Jaji: naahirisha mpaka saa 7 na Dakika 45
Jaji anatoka 07:30
*************************
Jaji amerejea 08:30
Kesi inatajwa
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa Quorum ipo Kama awali tupo tayari Kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji na sisi tupo kama awali tupo tayari Kuendelea
Jaji: Malya karibu
John Malya: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo
Malya: ile namba ya Kesi CD /IR /2097/2020 Ipo sahihi
Shahidi: Sahihi
Malya: ina Maana yoyote hapa
Shahidi: Inafanya Reference Kwenye kesi ambayo ipo Mahakamani
Malya: Je hiyo namba imepangwa Kwa Mtiririko wa Kesi au Hapana
Shahidi: Ni Mtiririko Wa Kesi zilizopo
Malya: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba 39
Malya: by The way Mhe Kielelezo kimeandikwa Namba 29 nafikiri ni Makosa ya Karani wa Mahakama, Ilitakiwa Kuwa Kielelezo namba 39
Malya: Shahidi namba hii Ndiyo tunayoiona hapa
Shahidi: Sahihi
Malya: Kwa hiyo Hakuna namba Nyingine ambayo Inafanana na hii namba hapa Mahakamani
Shahidi: Sahihi
Malya: na hizi feature zote ni za Muhimu Katika Kuandika namba ya Kesi katika hili faili
Malya: Naomba Mheshimiwa Kielelezo namba P 37
Malya: Tazama katika Karatasi hii, Je ni sahihi Hakuna Mkwaju.?
Shahidi: Ni sahihi, Hakuna Mkwaju katika Kielelezo namba 37
Jaji: huo Mkwaju unamiss wapi
Malya ANAMUELEKEZA
Malya: Wakati Mnakabidhiana Simu na Denis Urio Ulikuwa wapi
Shahidi: Ofisi Ndogo ya Mkurugenzi wa Upelelezi Makosa Ya Jinai
Malya: Ni sahihi Kwamba Ofisi ile ndiyo Ofisi Kubwa ya Upelelezi Kuliko zote kwa Dar es Salaam
Shahidi: Ni sahihi
Malya: Je Ofisi Ya DCI Dar es Salaam ina uhaba wa Vifaa.?
Shahidi: Inategemea
Malya: Wakati Wa Shauri Kubwa kama la Kesi ya Ugaidi, Utakubali Kuvunja Sheria au utasubiri Vifaa
Shahidi: Nitasubiri Vifaaa
Malya: Sasa hii Fomu hapa iliyojazwa hivi, Ni Just for Cosmetics au inatakiwa Kujazwa kama. Inavyotakiwa
Shahidi: Inatakiwa inajazwe Kama inavyotakiwa
Malya: hizo features zilitakiwa Zijazwe au zisijazwe
Shahidi: Zilitakiwa zijazwe
Malya: Ni sahihi hizo fomu Mlitakiwa Makabidhiane Askari Polisi Kwa Askari Polisi
Shahidi: Ni sahihi
Malya: Sasa wewe ulikabidhiana kwa fomu hiyo na Askari
Shahidi: Hapana
Malya: Je Denis Urio alikuwa ni Askari Polisi.?
Shahidi: Hapana, Kwa sababu yeye ni shahidi
Malya: Mwambie Mhe Jaji akisoma wapi atajua yeye ni Shahidi
Shahidi: Hapa haionyeshi
Malya: fomu yenyewe inajieleza Kuwa anayekabidhi, Jina na Sahihi anaye kabidhi
Shahidi: Mtu anayekabidhi,Hakuna Jina
Malya: Mhe Jaji naomba nipatiwe Kielelezo D4 Maelezo Ya Bwana Denis Urio
Malya: Shahidi tumeukizana Habari ya Jina, Kujiridhisha kama. Kweli huyo Mtu alikuwa ni Urio, Je katika Signature Ya Denis Urio Kuna features zipi ambazo zinaonyesha
Shahidi: anaye weza Kuitambua hii ni Mtaalamu Wa Maandishi
Malya: Kwahiyo Hauwezi Kuitambua
Shahidi: anayeweza Kuitambua hii ni Luteni Denis Urio Malya: Sijauliza kama Unaitambua au huitambui Shahidi: Kuna Mkorogo tu, anaye weza Kuitambua hii ni Mtaalamu Wa Maandishi
Malya: Sasa hapa pia Nina Maelezo Ya Denis Urio, Yana Signature pia, Je Kwa Macho yako Zinafanana au hazifanani Shahidi zinafanana
Malya: Sawa Nenda pale Kwa Ruhusa Ya Mheshimiwa Jaji, Muonyeshe zinavyofanana
Malya: Mheshimiwa Jaji naomba nipatiwe Kielelezo P 30
Mallya: Je Shahidi Katika Simu ya Bwire wewe ndiye uliye andika Exhibit Label
Shahidi: Nilimjibu siyo Mimi
Malya: Maana ya Kuhamisha Faili Maana yake ni nini
Shahidi: Namba ya Faili inabakia Vile vile
Malya: Je Unasema Kwamba Shughuli zinafanyikia wapi
Shahidi: Inategemea
Malya: Ulielezea Kwa Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Hapana
Malya: Bwire alikamatwa wapi
Shahidi: Chang'ombe
Malya: Unajua aliyejaza simu za Bwire alijaza wapi
Shahidi: Sijui
Malya: Wakati Wa Kingai na Goodluck wamemkamata Bwire wewe Ulikuwa Central.?
Shahidi: Sahihi
Malya: Hii Simu ambayo nimeshika ni ya Bure, Je ilijaziwa wapi
Shahidi: Sijui
Malya: Lakini Kingai na Goodluck Walikukuta Central
Shahidi: Sahihi
Malya: msomee Mheshimiwa Jaji Sehemu Iliyo andikwa Station
Shahidi: Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam
Malya: na Simu ya Urio Ulichukua wapi
Shahidi: Ofisi ya DCI
Malya: Shahidi Nakuonyesha Kielelezo P28, Simu ya Urio imeandikwa wapi
Shahidi: Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam
Malya: Kielelezo P 29 Msomee Mheshimiwa Jaji Sehemu ya Station
Shahidi: Polisi Kati Dar es Salaam
Malya: Shahidi Tarehe 11 August 2020 ndiyo Urio alikuja Ofisini Kwako, akakuachia Simu Moja
Shahidi: Sahihi
Malya: Wewe ni Mpelelezi Wa aina gani, Anaye Jipanga au Kukurupuka
Shahidi: anayeJipanga
Malya: Kama amayejipanga, Urio alipokwambia Kesho anakuja, Ulikuwa umejipanga au Hukuwa umepanga
Shahidi: za Makabidhiano nilikuwa nazo ila PF 145 sikuwa nazo
Malya: Kwa hiyo Ulijipanga kuwa na fomu za Makabidhiano ila za PF 145 Hukuwa nazo
Shahidi: Ndiyo Nilivyo Eleza
Malya: haya Shahidi Muonyeshe Mheshimiwa Jaji Sehemu ya Station Imeandikwaje
Shahidi: Polisi Kati Dar es Salaam
Malya: Shahidi Umeeleza wewe Ulikuwa Mjumbe wa Kikosi X, Je Wajumbe wa Kikosi X Wanafamika na Jamii?
Shahidi: Wanafahamika
Malya: Jumanne alikuwa Katika Kitengo hicho
Shahidi: Hapana
Malya: Kingai
Shahidi: Hapana
Malya: Goodluck
Shahidi: Hapana
Malya: Mahita
Shahidi: Hapana
Malya: Mwenzako wa Kitengo X alikuwa nani
Shahidi: Afande MSANGI
Malya: Mwingine nani
Shahidi: Ni huyo tu
Malya: Kumtukana Rais Mtandaoni ni Kuhatarisha Usalama wa Nchi
Shahidi: Hapana
Malya: Ugaidi ni Kuhatarisha Usalama wa Nchi
Shahidi: Ndiyo
Malya: Kwa sasa upo Ofisi ya RCO Temeke
Malya: Ni sahihi Kwa Mlalamikaji kuteua Mpelelezi Wangu
Shahidi: Hapana
Malya: katika kesi hii Mlalamikaji ni nani
Shahidi: Afande DCI
Malya: wewe alikuteua nani
Shahidi: Afande DCI
Malya: Kwa hiyo sisi haturuhusiwi Kuchagua Mpelelezi ila Kwa DCI analalamika na kuteua Wapelelezi
Shahidi: Kwa hili Mazingira ni tofauti
Malya: Ulimweleza Mheshimiwa Jaji Hayo Mazingira tofauti
Malya: Nilisikia Umeandika Barua Kwa DCI wakati huo Wambura Tarehe 18 July 2021
Shahidi: Ni sahihi
Malya: Wakati Unatoa Riport Kwa DCI ulikuwa unamdangamya au Ulikuwa serious
Shahidi: Nilikuwa Nipo Serious
Malya: Wakati Unaandika Ripoti kwa DCI Watuhumiwa Wengine Walikuwa tayari Upelelezi Wao tayari au bado
Shahidi: Ilikuwa tayari Katika Ripoti hiyohiyo
Malya: Wakati Unaandika Ripoti hiyo ya Kutaka Sasa Mbowe akamatwe ulikuwa na Ushahidi au Ulikuwa unataka Mbowe akae ndani Kidogo
Shahidi: Nilikuwa na Ushahidi Wa Kutosha
Malya: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo D1
Malya: Tarehe 18 July 2021 umemuandikia DCI una ushahidi Wa Kutosha
Shahidi: Ndiyo
Malya: Ni sahihi Kwamba Maelezo Ya Justine Kaaya Uliyachukua Tarehe 30 July 2021 Kuhusu Ugaidi wa Mbowe Wakati huo Umeshamkamata Mbowe tayari
Shahidi: Ndiyo lakini, Huo ni Ushahidi Wa ziada
Malya: Una taarifa Mwaka huu Kuna Masoko yameungua
Shahidi: Ndiyo
Malya: na Moshi na Kwingine Kote Masoko yameungua
Shahidi: Ndiyo
Malya: Masoko hayo yameungua Wakati hawa wapo ndani, Mnasema Kwamba Walipanga Kuchoma,masoko, Je nikisema Yanaungua Sababu ya laana ya Kumsingizia Mbowe nitakuwa Nakosea
Shahidi: Ni Uongo, hilo ni Kosa Moja, lakini Wanashitakiwa na Makosa ya Kukata Miti Barabarani, Kupanga Njama za Ugaidi, Kutaka Kudhuru Viongozi
Malya: Wakati Unaandika Taarifa ya Kwenda Maabara Ya Kisayansi, Simu ya Kaaya na wenzake ulikuwa nazo
Shahidi: Ndiyo
Malya: Uliambatanisha katika Maombi ya Uchunguzi?
Shahidi: Hapana Walikamatwa baada ya Kuwapeleka hawa Mahakamani, Nilipeleka Simu za Watu wa tatu tofauti
Malya: Wakati Wa Ushahidi Wako Ulizungumzia hilo
Malya: katika Maelezo Ya Kaaya, Kaaya anasema alikuwa anapigiwa Simu na Mbowe
Shahidi: Sahihi
Malya: Je finding za Kaaya zipo hapa Mahakamani
Shahidi: Hapana
Malya: Ushahidi Wa Utaalamu Wa Uchaguzi wa Simu ya Kaaya Mnayo Jeshi la Polisi
Shahidi: Taarifa zimeanza Kufanya Tarehe 10 August 2020
Malya: Kwa hiyo Mbowe na Kaaya waliwasiliana baada ya hawa Mabwana Kukamatwa
Shahidi: Hakuendelea Kuwasiliana naye
Malya: Conlusion Naiachia Mahakama
Malya: Kuna Simu Ulipewa na IMEI namba yake Ilikuwa Imefutika
Shahidi: sahihi
Malya: Ulipewa Katika hali gani
Shahidi: Ikiwa Imezimwa na Ukiwasha inakuwa katika Flight Mode
Malya: Simu ya nani hiyo
Shahidi: Mohamed Abdilah Ling'wenya
Malya: Wakati Unakabidhwa Ulikuwa wapi
Shahidi: Nilikabidhiwa Nikiwa Katika Kituo Cha Polisi Kati Dar es Salaam
Malya: Umepewa su Ukaambiwa IMEI namba zake zimefutika, Wakati Unapewa simu ulikuwa wapi
Shahidi: Nilikuwa Ofisi Ndogo ya DCI
Malya: Ulikuwa na nani aliye shuhudia
Shahidi: DC Goodluck
Malya: Mohammed Ling'wenya alikwepo
Shahidi: Hakuwepo
Malya: Anita Mtaro
Shahidi: Hakuwepo
Malya: Esther Nduguuru
Shahidi: Hakuwepo
Malya: na Ukasema Ukabonyeza namba fulani fulani Ukapata Taarifa Uliyokuwa unatafuta katika Ile simu
Shahidi: Ni sahihi
Malya: turudi tena Pale Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam
Mallya: Ni sahihi Ulisema Kwamba siku ya Tarehe 07 August 2020 ulipigiwa Simu Kuwa Uje Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam
Shahidi: Ni sahihi
Malya: Ni sahihi Ulikabidhiwa Simu
Shahidi: Ni sahihi
Malya: Baada ya hapo Mlitoka Kwenda Sinza na Coco beach
Shahidi: Ni sahihi
Malya: Mpaka hapo Hukusema zile simu Ulihifadhi wapi
Shahidi: nilirudisha
Malya: Uliyasema hayo Wakati anakuongoza Kaka Yangu Kidando
Shahidi: Hapana
Malya: Vifaa Simu na Computer, Vilivyokamatwa Kuhusu Kesi hii Vilikuwa Vinakuja kwako
Shahidi: Siyo Sahihi
Malya: Unafahamu Kwamba Computer, Rooter za Watoto na Mke wake Vilikamatwa
Shahidi: Ni nacho fahamu Mimi, Mtuhumiwa alikamatwa na Simu na Laptop
Malya: Simu Ngapi
Shahidi: Si zaidi ya Moja
Malya: Aina gani ya Simu
Shahidi: Sikumbuki
Malya: Computer
Shahidi: Zaidi ya Moja
Malya: angalau zilikuwa Mbili
Shahidi: Sikumbuki
Malya: Vitu hivi ulipeleka wewe Maabara Ya Uchunguzi
Shahidi: Ndiyo
Malya: Wakati Wakili wa Serikali Robert Kidando anakuongoza ulitoa Ushahidi huo wa Kupeleka Vifaa hivyo
Shahidi: Hapana Sikusema
Malya: Uchunguzi huo unasemaje
Shahidi: Leo Ndiyo nimejulishwa kuwa Matokeo ya Uchunguzi yamekamilika
Malya: Kwa hiyo Leo Ndiyo Upelelezi Wa Kesi Ya Mbowe Umekamilika
Shahidi: Sahihi
Malya: Kuna tuhuma hapa, Line za Simu za Denis Urio hazifahamiki zilipo, Je Umepeleka Wapi
Shahidi: Zipo Katika Simu zake
Malya: Denis Urio alikuja hapa akawasha Simu zake akasema hazioni line zake, Kwa hiyo Jaji atapima Maelezo Yako wewe na Denis Urio
Malya: Ni sahihi Kwamba Madawa ya Kulevya yanaongeza hali ya uhalifu
Shahidi: Ni sahibi
Malya: Je Mbowe anaweza Kuwapa hawa Vijana Madawa ya Kulevya ili Wakafanye Uhalifu
Shahidi: Inategemea
Malya: Shahidi Je Tuhuma Za Ugaidi na Madawa ya Kulevya Yanaunganika.?
Shahidi: Inategemea
Malya: Ni sahihi Kwamba Kukuta kwa Madawa ya Kulevya Kungeweza Kuongeza Hali ya wao Kutenda Ugaidi Sasa
Shahidi: Madawa ya Kulevya hayahusiani na Ugaidi, Kwa sababu Ugaidi ni Kesi Nyingine na Madawa ni Kesi Nyingine
Malya: Kesi ya Madawa ipo wapi
Shahidi: Ilifunguliwa Moshi
Malya: Inaanza lini,kmi Wakili wake Adamoo ni jiandae
Shahidi: Siwezi Kufahamu
Malya: Wakati DC Goodluck anakukabidhi Vielelezo alikwambia anatoka wapi
Shahidi: alisema Anatoka Moshi
Malya: Kwamba alienda nazo Kwa Mama Mtilie Kunywa Supu na Kupiga Mswaki Hakukwambia
Shahidi: Hakuniambia
Malya: hivi Malalamiko kuja Kitengo X yalikuwa Ofisi za DCI ila wewe Ukaenda Kufungua Kesi Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam
Shahidi: Malalamiko yalianzia Kwa DCI
Malya: nani alisema Ukafungue Kesi Kituo Cha Polisi Kati Dar es Salaam
Shahidi: Ni Kingai
Malya: alikwambia kwanini hakukwambia Ukafungue Kituo cha Temeke au Oysterbay
Shahidi: Hakuniambia
Malya: Je angekwambia Ukafungue Oysterbay Ingekuwa Tofauti?
Shahidi: Kwa Nature ya Kesi Yenyewe Isingewezekana, Kwa sababu Kuna Mikoa inahusika
Malya: Kwa nini, Hamku Fungua Moshi, Kilimanjaro
Shahidi: Kwa Nature ya Offense Yenyewe
Malya: Je Kitengo X Kinaweza kutoa Amri kwa Polisi Wa Mkoa wa fulani Wamkamate Mtu fulani
Shahidi: Inawezekana
Malya: Tarehe 14 July 2020 Kidando alitoa Wapi hii Tarehe
Wakili Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Mimi nilikuwa nuongoza Shahidi, Sasa sijui wakili ana Lengo gani
Malya: Sawa Nitarudia Swali, Je Tarehe 14 July 2020 aliyokuwa anakuuliza alitoa wapi
Shahidi: Alitoa Kwangu
Malya: Maelezo Yako ninayo hapa, Hakuna Sehemu Umeandika Kuhusu Tarehe 14 July 2020
Shahidi: Ni sahihi Hakuna Tarehe 14 July 2020
Malya: huyu Mtu alitoa Wapi sasa hii Tarehe 14 July 2020
Shahidi: Mimi Ndiyo nimetoa wakati wa Kukumbushia Maelezo Yake
Malya: wewe Ulimweleza Mheshimiwa Jaji, kuwa Ulitoa wapi hizo Memory
Shahidi: Sikumueleza
Malya: Unasema Tarehe 07 August 2020 Kingai alikupigia Simu Kwamba Wale Watu weshapatikana
Shahidi: Ni sahihi
Malya: Maelezo Ya Kingai umeshawahi Kuyaona
Shahidi: Ndiyo Malya: Sasa....... Sauti ya Shahidi inamkatisha
Shahidi: MHESHIMIWA JAJI NAOMBA NIENDE WASHROOM (CHOONI)
Shahidi Karejea Malya: Je Shahidi Unajua Kuwa Kingai alipopata Taarifa
Shahidi: Nilikuwa najua
Malya: na Unaamini Kuwa alikuwa hadanganyi na Hamuonei Mbowe.. Simu ya nani ilikuwa Ina Coordinate
Shahidi: Simu ya Mbowe
Malya: kwenda Kwa nani
Shahidi: Kwa Luten Denis Urio
Malya: wale ambao Sasa Tarehe 14 mnaosema Kuwa Wale Watu wamepatikana, Je Hapa Mahakamani Wapo
Shahidi: Hawapo, Siku ambayo Luteni Denis Urio alikutana na Freeman Mbowe, Ndiyo Ulisoma Mbowe anasema Kwamba mimi na Chama Changu Chadema Kimedhamiria Kuchukua Nchi
Malya: kwa hiyo Kundi lake mlilofungulia Kesi ni Chama Chake
Shahidi: Sijui sasa Kama Chama Chake
Malya: Kwa hiyo hao anaosema Chama Changu wewe huwajui
Shahidi: Siwajui
Malya: Unafahamu Kwamba 2020 Ulikuwa Mwaka Wa Uchaguzi
Shahidi: Nafahamu
Malya: Unafahamu Kwamba Mbowe na Wenzake Walikuwa wanagombea nafasi Mbali mbali
Shahidi: Nafahamu
Malya: Je unafahamu Kwamba Vyama Vya siasa Vimeundwa Kwa Dhumuni la Kuchukua Dola
Shahidi: Ni sahihi kama utafuata Sheria
Malya: Ni sahihi Kwamba Vyama Vingine Vimeundwa kwa Lengo la kushiriki Uchaguzi la Kuchukua Dola
Shahidi: Lengo Kubwa la Chama ni Kuchukua Dola
Malya: Unafahamu Kwamba Mwenyekiti Freeman Mbowe ni Kiongozi wa Chama gani
Shahidi: CHADEMA
Malya: Chama Cha Mheshimiwa Mbowe Mwaka 2020 kilishiriki Uchaguzi au hakikushiriki
Shahidi: Kilishiriki
Malya: Wewe Kama Mpelelezi Uliwahi Kumuhoji Lengai Ole Sabaya
Shahidi: Sijawahi
Malya: Je Kama Hiyo Mipango Ingetimia angedhurika
Shahidi: Ndiyo
Shahidi: Malya hata Kingai Mwenyewe hajawahi Kumuhoji Sabaya
Shahidi: Hajawahi
Malya: hujawahi Kusikia Kauli ya Afande Siro Kwamba Kesi ya Kupigwa Risasi Tundu Lissu wanashindwa Kufanya Upelelezi Kwa sababu Wameshindwa Kumuhoji Lissu
Shahidi: Sijawahi Kusikia
Malya: haya Sabaya sasa ambaye ni Victim, hajawahi Kuhojiwa lakini Upelelezi Wake Umekamilika, Je hii siyo Double Standard?
Shahidi: Sabaya bado Siyo Victim
Malya: Kuna Mtu kapiga Risasi Upelelezi wake haujakamilika, lakini Kunatu hata hajaguswa na Upelelezi Umekamilika
Shahidi: Siwezi Kuzungumzia Suala ambalo sijapeleleza
Malya: Lengo la Kwenda Tigo na Airtel ilikuwa Kuleta Mahakamani kama ni kweli.?
Shahidi: Ni sahihi
Malya: Sasa Kilichokushinda Kuandika Barua Kwenda EWURA Kuthibitisha Kwamba kweli Kuna Kituo cha Mafuta oe Morocco
Shahidi: Sikuona haja hiyo
Malya: Je ulithibitisha Vipi Kama Kituo kama Kinauza Mafuta kweli, ulinunua hata Mafuta ya TSh 5000?
Shahidi: Hapana
Malya: haya Ulienda Kuthibitisha Masoko Katika Vyama Vya Ushirika kwa Kuandika Barua
Shahidi: Sikuona haja hiyo
Malya: Mimi nikibisha Kwamba Hakuna hayo Masoko sasa, Utathibitisha kwa Lipi
Shahidi: Kwa Ushahidi Wangu
Malya: Shahidi Mnataka Kujenga Picha Kwamba Mlifahamu Mbowe alitaka Kutenda Ugaidi na Nyie Mkamuwezesha Kufikia Lengo lake
Shahidi: Si Kweli
Malya: Kufanya Kikao cha Ugaidi ni Kosa au siyo Kosa?
Shahidi: Kosa
Malya: Kama Kukaa Kikao cha Ugaidi ni Kosa, Je hao waliokaa Kikao cha Ugaidi Walitoka wapi
Shahidi: Sifahamu
Malya: hao Watu ambao Mbowe anashitakiwa Kufanya nao Kikao cha, Mbowe aliwapata wapi
Shahidi: alitafutiwa kwa Lengo la Kuku Sanya Taarifa
Malya: Kwa hiyo Wakati Wanafanya Kikao Walikuwa wanafanya Ugaidi au Wanakusanya Taarifa
Shahidi: Walikuwa wameshashawishiwa
Malya: Kwani Kikao cha Ugaidi Walikuwa wamekaa Wapi na wakina nani
Shahidi: Washtakiwa wanne katika Hotel ya Aishi
Malya: Kwani Tarehe ngapi Walikuwa wamebadirika Kuwa Magaidi
Shahidi: Tarehe 25 July 2020
Malya: Swali langu Tarehe 20 July 2020 wakati wanatumiwa pesa Walikuwa Magaidi au siyo Magaidi
Shahidi: Hawakuwa Magaidi
Malya: Kama Mbowe Tarehe 20 July 2020 Mbowe anatuma Pesa Kwa Wale Watu zilikuwa Safi au Chafu
Shahidi: Ilikuwa Chafu kwa sababu Mbowe alikuwa anajua Lengo
Malya: na Muamala Wa Tarehe 22 July 2020 zile pesa ambazo Walitumiwa Siku hiyo na zenyewe Safi au Chafu
Shahidi: Pesa chafu
Malya: Tarehe 25 July 2020 Kama Wangekataa zile pesa Wangekuwa na Hatia
Shahidi: Wasingekuwa na Hatia
Malya: Mbowe Katika hicho Kikao cha Watu Wanne angekuwa amekaa Kikao cha Ugaidi au Siyo
Shahidi: Angekuwa amekaa Kikao cha Ugaidi
Malya: Je Shahidi Kama Upo Ofisini Kwako akasema anataka Kwenda Kuiba Benki, utakuwa na Wajibu wa Kuzuia au Utamuacha
Shahidi: Hilo haliwezekani, Mhalifu akupe Taarifa
Malya: Je nikija Kwako Kwamba nataka Kuiba Benki, Je utanizuia au Utaniacha
Shahidi: Nitakuzuia
Malya: Sasa DCI kapata Taarifa Kutoka kwa Luten Denis Urio (Msiri wake) kwamba Mbowe anataka Kufanya Uhalifu Wa Kigaidi, Je alikuwa ana wajibu wa Kuzuia au lah?
Shahidi: Ndiyo Maana alizuia
Malya: Vipi Kikao Kilifanyika au hakikufanyika.?
Shahidi: Kilifanyika
Malya: Sasa Luteni Denis Urio anasema alimpatia DCI Taarifa Kwamba Mbowe anatafuta Watu akae nao Kikao cha Kigaidi, lakini DCI Haku fanya lolote Kikao Kika fanyika, DCI katika hili hakuwajibika
Shahidi: Si Kweli
Malya: Unafahamu Kwamba Kuna Njia ya Kuweka Mamluki ambao Mtu anakuwa nao akizani ni wenzake halafu Kumbe wanatoa Taarifa
Shahidi: Nafahamu
Malya: Je Katika Ushahidi Wako Ulizungumzia Kuhusu Kuweka Mamluki au Kutokuweka
Shahidi: Sikueleza
Malya: Unasema Kwamba Mbowe alikaa Vikao Kuanzia May Mpaka July Kula Njama za Kutenda Ugaidi
Shahidi: Sahihi
Malya: Kuna sehemu Umetaja Vikao Vilifanyika wapi
Shahidi: Hapana
Malya: Wewe ndiye ulikuwa Mpelelezi Katika hili Shauri, Je wewe Uliwahi Kumwambia Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Kuna watu Wemeshafungwa katika Shauri hili
Shahidi: Sijawahi Kumwambia, Na Ndiyo nasikia Leo
Malya; Je Shahidi Unafahamu Kwamba Wakati Mheshimiwa Mbowe anakamatwa alikuwa Mwanza Katika Kongamano la Katika
Shahidi: Sifahamu
Malya: Kuna tuhuma dhidi yako Kwamba Ulipokuwa Tazara Ulishiriki Kumpiga, Kwa Kusema Mshusheni Chini tumshughulikie
Shahidi: Si Kweli, Mtuhumiwa Ni kutana naye Chang'ombe Polisi
Malya: Kwani Kituo cha Polisi Chang'ombe ni Cha Ghorofa
Shahidi: Hapana
Malya: Kwanini Sasa Useme Mshusheni Chini tumshughulikie
Shahidi: Si Kweli
Malya: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba P 36
Malya: Unaulizwa Maswali na Wakili Msomi Nashon Nkungu Ulifanya Reference katika hii
Shahidi: Ndiyo
Malya: soma tena
Shahidi: Watakuwa tena na Safari ya kwenda Moshi Leo au Kesho Asubuhi
Malya: Kuna Meseji Yoyote inasema Kwamba Wamefika Hai
Shahidi: Hakuna
Malya: Mheshimiwa Jaji naomba nipatiwe Kielelezo P 15, 16, na 17
Malya: Ni Kuuliza Swali Mwanzo Kwamba wewe ni Mpelelezi Unaye Jipanga au Kukurupuka, Ukasema Unajipanga, Ni sahihi Kwamba Uliomba Taarifa za Namba 3
Shahidi: Ni sahihi
Malya: Ni sahihi Wakati Airtel wanajibu Walijibu namba 2
Shahidi: Ni sahihi
Malya: namba ipi Taarifa zake Zina Miss
Shahidi: Ni Namba 0782 237913
Malya: unataka Nikuulize Miamala ya Denis Urio, Wacha Nikuulize Shahidi
Mallya: Mheshimiwa Jaji namuuliza Extraction Ya Denis Urio, Kielelezo namba P 20, Mhamala Kutoka Kwa Wakala
Malya: Muamala Wa Tarehe 22 July 2020, TSh 199,000 imeingia
Shahidi: Ni sahihi Kuwa Mhamala Wa TSh 199,000 umeingia Kwenye namba ya Simu ya Luten Denis Urio
Malya: Unafahamu hii namba ya Chini Mhamala Wa TSh 7000 alipewa nani Kwenda namba 0787000027
Shahidi: Sifahamu
Malya: Shahidi Ulisema Kwamba Ulimruhusu Shahidi Kwa Sababu Hata Ulitoa line ya Simu Mawasiliano Yatabakia Kwenye Simu
Shahidi: Ndiyo
Malya: Unafahamu au Ulikuwa unajiongeza
Shahidi: Nilikuwa nafahamu
Malya: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo P 22 Mpaka Kielelezo namba P 27 nimpatie Mtaalamu Wa Telegram
Malya: Nakuonyesha Kielelezo namba P 26, Kielelezo ameleta Bwana Ndowo
Shahidi: Nilicho kuwa nasema Mimi, Kwamba hata Ukitoa line Kwenye Simu bado Extraction Riport ya Simu na Simu Taarifa zitafanana
Malya: haya Namba ya Bwana Denis Urio katika Ripoti ya Bwana Ndowo Hebu itaje Sasa
Shahidi: 1130138344
Malya: Ulitoa Explanation Wakati Unaongozwa na Wakili Msomi Kidando, Kuhusu hii Variation iliyopo katika Simu na Extraction Riport
Shahidi: Sikutoa
Malya: Wewe na Goodluck Ndiyo Mlibadilishana Vielelezo, Je ulitoa Maelezo Kuhusu Mvunjiko vunjiko wa Simu pembeni Katika Kielelezo namba 27 na 35
Shahidi: Sikueleza
Malya: Ulihifadhi hizi Simu, Kuna simu iliwashwa Ilikuwa na Chaji na Zingine Hazikuwaka, Je Unaweza Kueleza Kwanini Simu Moja tu ya Denis Urio iliweza Kuwaka Hapa Mahakamani
Shahidi: Siwezi Kujua, mimi Nilikabidhi Siku Nyingi
Malya: Wewe lakini unatabia za Kuchungukia Simu za Watu, Unakumbuka ulichungulia Simu ya Ling'wenya
Shahidi: Siyo Kuchungulia, Bali niliangalia IMEI namba
Malya: Ni sahihi Kwamba hii namba ya Jalada la Kesi, Inawashtakiwa zaidi ya Hawa wanne
Shahidi: Ndiyo
Malya: Je Katika Wingi huo naweza Kutaja Kitu cha Mtu bila Kufafanua
Shahidi: kama Kuna Jina au Namba unaweza Kujua
Malya: Sasa Katika Maelezo Yako Kuna sehemu Unasema Pia Uchunguzi Wa Cyber Unaonyesha Waziwazi na Jinsi Mtuhumiwa Freeman Mbowe aliwaelekeza Wenzake Jinsi ya Kutekeleza Mipango yake
Shahidi: Ni sahihi
Malya: Sasa Umeonyesha Mahakamani Wakati Wa Ushahidi Wako Kuwa hapa Ndiyo alikuwa anawaelekeza Watuhumiwa Cha Kufanya
Shahidi: Ndiyo nimeonyesha
Malya: Ulipata Kujua Sasa Wakala aliyetuma Pesa ni Yupo wapi
Shahidi: Hapana
Malya: Umeeleza ni Wakala wa Mtandao gani
Shahidi: Kama Nilivyo Jibu awali, Sikueleza
Malya: Kuhusiana na Taarifa ya Ballistic, Ni kweli Wewe Ndiye uliyempa Ruhusa koplo Hafidh Kuharibu zile Risasi
Shahidi: Hakuziharibu alizichunguza
Malya: Ulipompelekea Wewe koplo Hafidh zile Risasi, zilikuwa ngapi
Shahidi: Zilikuwa Tatu
Malya: zilikuwa na Hali gani
Shahidi: Zilikuwa Moja ni Nzima na Mbili zilikuwa zimetumika
Malya: hizi Mbili ambazo ulipeleka zilikuwa Sawa na Wakati unazipeleka?
Shahidi: Zilikuwa katika Hali ya Kutumika
Wakili John Malya: Mheshimiwa Jaji Sina Swali la zaidi. Naomba Kurudisha Vielelezo
Wakili Fredrick Kihwelo: Mheshimiwa Jaji Tumebakia na Dakika 5 sababu ya Muda tunaomba airisho Kwa sababu hizo Dakika hazitoshi
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Hakuna Pingamizi
Jaji:Kufuatia Maombi yaliyoletwa na Wakili Wa Mshtakiwa Wa tatu, Juu ya Muda, Na-airisha Shauri Mpaka Kesho Saa 3 Asubuhi. Shahidi Naomba Kesho Tarehe 08 urudi Kutoa Ushahidi wako. Washtakiwa wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Kesho Asubuhi Saa 3 Asubuhi.