Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake 3: Shahidi wa 13, Tumaini Swila ashindwa kufika mahakamani. Kesi imeahirishwa hadi Februari 14, 2022

Huyo shahidi atakuwa ni slow learner ndio maana anapata shida sana kukariri hadi anaugua kwa sababu mind becomes too obsessed.

The government called the music 🎶 let her play to its tunes now.
 
Habari Wakuu,

Leo 10/ 02/ 2022 shahidi wa 13 anatarajiwa kuendelea kutoa ushahidi wake kwenye kesi inayomkabili Mbowe na wenzake 3. Shahidi Tumaini Swila jana Februari 9, 2022 aliomba ahirisho kwakuwa alikuwa hajisikii vizuri.

Kujua Kesi ilipoishia fungua kiungo hiki: Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Swila aomba ahirisho kuwa hajisikii vizuri; kuendelea na ushahidi 10/02/2022

Baki nami.

Updates:

Jaji ameingia Mahakamani Muda huu

Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa

Wakili wa Serikali, Nasorro Katuga: Mheshimiwa Jaji naomba Kuwatambulisha Mawakili
  • Pius Hilla
  • Esther Martin
  • Jenitreza Kitali

Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kuwatambulisha Mawakili
  • Jeremiah Mtobesya
  • Fredrick Kihwelo
  • Sisty Aloyce
  • Iddi Msawanga
  • Michael Mwangasa
  • Edward Heche
  • Gaston Garubindi
  • Hadija Aron
Wakili wa Serikali Nasorro Katuga: Mheshimiwa Jaji Shahidi ameshauriwa na Daktari Kupumzika na sisi hatuwezi Kwenda Kinyume na Ushauri wa Daktari Pia tungeweza Kutafuta Shahidi Mwingine wa Kuendelea naye ila Kwa Muda wa Jana na leo isingetosha Kutafuta Shahidi Mwingine

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba tuhairishe Kesi Mpaka Jumatatu, Kama atakuwa bado hajapona tunaweza Kutafuta Shahidi Mwingine Pia Mheshimiwa Jaji Kwa kutii Agizo la Mahakama Shahidi ameweza Kumtumia Ndugu yake aweze Kuja na Cheti cha Hospitali, lakini Original yake anaweza Kuja nayo yeye Mwenyewe pale atakapo pona

Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba kama Dakika Moja na sisi tuweze Kuangalia Cheti cha Hospitali.

Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Tumesikia Hoja ya Ndugu yangu Nassoro Katuga Nikianza na Hoja yenyewe ya Nyaraka Kutoka Hospitali, Nakumbuka Wakati natoa Hoja Jana, Tuliomba Shahidi atuletee Karatasi Kutoka Hospitali ya Serikali ambapo pia nafahamu Kwamba Askari Polisi anapopatwa na Ugonjwa anatakiwa kwenda huko, Nyaraka Walio leta Wenzetu Inatoka TMJ Super Polyclinic hii siyo Hospitali Ya Serikali Nyaraka hii inazidi Kuweka Wasiwasi zaidi Kwa Nini Mtu aende Kwenye Hospitali ambayo Haifahamiki

Nafikiri Jana tulikubaliana kuwa aje na Uthibitisho kutoka Hospitali ya Serikali Naomba Mahakama Ione kuwa sababu haina Logic wala hazipo Kama Mahakama itaona tofauti Basi Wenzetu Wasisitizwe

Kwa Mujibu Sheria Kesi katika Mahakama hii inatakiwa iishe ndani ya Miezi 9 Tukienda Kwa Mwenendo huu tutalazimika Kuomba Muda wa Nyongeza Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji

Jaji: Hoja ya Kuhusu airisho Sijaona kama Umezungumzia Kuhusu Muda wa airisho

Kibatala: Mheshimiwa Jaji Jumatatu ni Mbali sana, Kwa Vyovyote itakayokuwa, Sasa ni saa Nne, Mpka Kesho Saa Nne ni Zaidi ya Masaa 24 Wana akiba ya Mashahidi 11 zaidi. Basi tutafute kati hao Mashahidi 11 angalau tuairishe Kwa Leo tuweze Kuja Kuendelea Kesho

Wakili wa Serikali Nasorro Katuga: Mheshimiwa Jaji Tumesikia Hoja ya Wenzetu Kutoka kwa Wakili Peter Kibatala Wenzetu Wanasema Kwamba Shaeria na Tangazo la Serikali namba 259 inataka Kumaliza shauri hili ndani ya Miezi 9 tunalifahamu na tumelichukua

Suala la tukishindwa Kuleta Shahidi huyu, tulete shahidi Mwingine nalo tumelichukua Suala la Shahidi Kuleta Cheti cha Hospitali ya Serikali, Shahidi Tulikuwa tunaona hapa tangu Mwanzo Kila Muda alikuwa anaomba Kwenda Msalani Huko Ndipo alipo kuwa anatibiwa kupitia Daktari Wake

Kupata tiba kutoka kwa Daktari Wake ni Nusu ya tiba, Kuhusu Wasiwasi Wa hapo anapotibiwa wanaweza Kwenda Kuuliza na Kuonana na Daktari Wake. Tunasisitiza Sisi Ka Maafisa wa Mahakama hatufurahishwi na airisho Lolote Pasipo Sababu.

Kuhusu Kuairisha Mpaka Kesho na Sitakukubali Kwamba tuje Kesho halafu tukaja na Hadithi ya Kukosa Shahidi. Ndiyo Maana tukaomba tuahirishe Mpaka Jumatatu ili kama Shahidi hata Kama anatakiwa Kusafiri atakuwa amefika

Sisi tunaona Kuwa ni Busara Kuairisha Mpaka Kesho halafu tukaja na story, Mahakama Yako itachoka Kutusikiliza. Sisi tunaomba tupewe airisho Mpaka Jumatatu. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.

Mahakama ipo kimya kusubiri uamuzi mdogo wa Mheshimiwa Jaji (10:15 AM)

Bado Mahakama ipo kimya (10:27 AM)

Jaji: nimesikia Hoja zilizotolewa na pande zote mbili Kama ambavyo Imetolewa na Upande Wa Mashtaka Mahakama hii imekuwa na Spirit ya Kutaka Shauri liishe kwa Haraka nimekuwa nikisisitiza Mawakili wa pande zote Mbili kuzingatia Spirit hii

Ila jana Wakati Shahidi anatoa Ushahidi wake, Shahidi Aliomba Kusitisha Kutoa Ushahidi Na Kwenda Kupata Matibabu Maombi hayo Kwa kuwa yalikuwa ya Msingi, Mahakama Ilielekeza Kuwa Shahidi atakapo rudi Mahakamani Hapa atalazimika kululetea Uthibitisho

Mahakama Haikusema Uthibitisho huo lazima utoke Hospitali ya Serikali, Kwa sababu suala la Matibabu ni la Mtu Binafsi Mahakama ilisita Kutoa Maelekezo hayo Ingekuwa inaingilia Mambo Mengine

Nyaraka iliyokuja hapa Shahidi amepata Uthibitisho Kuanzia Tarehe 9 Mpaka 11 February

Kwa Maana hiyo Shahidi Kwa Kesho Hawezi Kuwepo Upande wa Mashtaka Wanasema Kwamba hawawezi Kuomba airisho Mpaka Kesho Sababu wanaogopa Kuja Kesho bila Shahidi.

Kwa sababu hiyo ni Busara Ya Mahakama Inaona ni Vizuri Kuairisha Mpaka Siku ambayo Shahidi ataweza Kuja Mahakamani

Kwa sababu Hiyo naairisha Mpaka Jumatatu na Kuelekea Upande wa Mashtaka Kuhakikisha Kuwa Jumatatu wanakuja na Shahidi hata Kama yule atakuwa bado hajapona Waje na Mwingine

Kwa Maana hiyo na airisha Shauri Mpaka Jumatatu Saa 3 Asubuhi na Washtakiwa Wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Siku hiyo

Jaji anatoka
Tuwape muda waendelee kujipanga. Ila siku nyingine waweke mashahidi wenye afya zinazoeleweka. Lakini wajue kuwa wajipange wajipangavyo ila wakifika kizimbani, Fimbo tunawachapa. Mpaka wakumbuke kusahau kua Tanzania siyo nchi ya wachache
 
Kwa Maana hiyo na airisha Shauri Mpaka Jumatatu Saa 3 Asubuhi na Washtakiwa Wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Siku hiyo
Tusubiri Jumatatu kama mgonjwa atakua amepona aendelee na dodoso, kama hajapona, aanze shahidi mwingine. Kesi imefika patamu.
 
Swali zuri? Yaliyopokelewa na mahakama yatabaki kwenye taarifa za mahakama na yatatumia kama yalivyo dhidi au kwa manufaa ya pande zote

Na ikatokea shahidi huyu hali yake ya kiafya "ikathibitika na Daktari wa TMJ" kwamba hawezi kuendelea na ushahidi na anahitaji matibabu zaidi kwenye hospitali za rufaa (ambalo "technically" naliona linakuja). Tutaendelea kusubiri ushahidi wa huyu Swila hadi afya yake iimarike kwa huo muda?, wakati tunaendelea na mashahidi wengine kati ya hao 24?
 
Swilla ndo imetoka hiyo harudi ng'oo cross siyo mchezo jamani nilipigwa moja 2019 nilikuwa nawaza siku 5 mfululizo nashukuru Mh Hakimu alinielewa akatoa pumziko nikaenda kunolewa na wakili wangu nikarudi upya nilimwanga mtu nyaaa Ila kwa mbinde Sana jamaa akalipa faini akawa huru
 
Wataalamu wa kuanzisha Nyuzi anzisheni uzi wa kumpongeza Jaji kajitahidi sana kuanzia alipoanza Denis Urio ,kaenda bila upendeleo .
Uko sahihi kabisa. Jaji ameshaona picha nzima ya hii kesi baada ya shahidi wa muhimu kabisa, Luteni Denis Leo Urio. Huyu ndiye amebeba maamuzi ya hii kesi.
 
Boaz ambaye ndiye alitakiwa kuwa shahidi wa kwanza kaingia mtini ..... badala yake kaweka mrorongo wa watu wa chini yake. Tangu lini mashahidi wote wanatoka ofisi moja tena kwa maelekezo ya Boss wao .... Only in Tanzania.

Ila sitashangaa kabla ya hii kesi kuisha kuna shahidi wataondoka naye, I mean watamalizana naye ......!!!
Kumalizana naye, una maana "kumpoteza"? Swila anaumwa, tumuombee apone aje aendelee na ushahidi wake.
 
Mheshimiwa jaji, kwa niaba yangu na familia yangu, tunapenda kukujulisha kuwa tunafuatilia mwendo wa kesi hii kwa tuo. Aidha kwa mwenendo wa kesi hii mpaka Sasa hatuoni haki ikitendeka maana mawakili wa serikali wamekuwa na visingizio vingi kwa lengo la kuchelewesha kesi na kwa bahati mbaya mahakama yako imekuwa ikibariki mchezo wao. Vyovyote itakavyokuwa, tunaamini haki haijaonekana kutendeka na haitatendeka. Naomba kutoa hoja.
 
Ukiwa shahidi kwa suala unalolijua kikamilifu. Huwezi kupata wasiwasi.

Kwanza hata ukiandaliwa na wakili ni dakika 20 ikizidi nusu saa.

Ila ushahidi wa kitu cha kutengeneza. Aisee ni ushahidi mgumu sana. Ukiandaliwa na wakili inabidi hata siku mbili ukae na manotebook.. Kalamu.. Ukariri.. Yaani ni shida tupu.

Ndio maana mawakili wa Serikali hawawezi kukubali eti kesho tuu walete shahidi mwengine, ni kazi kubwa sana kuwaandaa na muda ni mfupi.

Kwahiyo wanakimbilia Jumatatu
Hata hiyo jumatatu lazima atepete kizimbani plus guilty mind inamsumbua.
 
Ushahidi mkuu mbona uko tayari kwenye committal bundle na hakimu alishaona unaweza kutia mtu hatiani?
Mkuu, kwa hiyo huku mahakama kuu kinachofanyika hakina maana yoyote? Siku ukisikia Mbowe amehukumiwa kifungo jela, hutalala kwa furaha. Hawa kina Ndowo, Urio, Swila etc, wanaotoa ushahidi usiokufurahisha wanakuudhi sana.

Ni kipi kinakufanya umchukie kiasi hicho Freeman Mbowe?
 
Ule utopolo wake hauwezi kupokelewa popote.


Tumia kichwa chako vizuri na sio kuongeza uzito juu ya mebega yako
Huyu comte anapenda iwe hivyo. Angependa hawa mashahidi wa jamhuri wasiwe wanafanyiwa cross examination, ili wakileta uongo wao uchukuliwe hivyo ulivyo. Huyu jamaa anapata shida sana na hali ya hii kesi inavyoenda kwa sasa. Tukipata majaji wenye roho kama hizi za comte ni hatari sana.

Huyu jamaa nimemfuatilia kwenye nyuzi za hii kesi, anaonekana ni mtu mwenye chuki sana na Freeman Mbowe.

Siku hii kesi ikifutwa, ataugua huyu.
 
Maswali ya kijinga yamesababisha afande nyoka kulazwa.

Taarifa za ndani zinadai kagoma kabsa kuja, na hata jumatatu kawaambia yeye hawezi.
Waende waliomtuma wakapambane na Kibatala.
Safi sana. Kama mbwai na iwe mbwai. Walimtuma afungue jalada la kesi isiyokuwepo, halafu sasa yeye anateseka na maswali huku wao wamerelax. Na mbaya zaidi hii kesi inaweza kumharibia kazi yeye Swila kuliko huyo Kingai.

comte
 
Maswali ya kijinga yamesababisha afande nyoka kulazwa.

Taarifa za ndani zinadai kagoma kabsa kuja, na hata jumatatu kawaambia yeye hawezi.
Waende waliomtuma wakapambane na Kibatala.
Mkuu ongeza nyama hapo kwenye "kagoma kabisa"
 
Back
Top Bottom