Tuwape muda waendelee kujipanga. Ila siku nyingine waweke mashahidi wenye afya zinazoeleweka. Lakini wajue kuwa wajipange wajipangavyo ila wakifika kizimbani, Fimbo tunawachapa. Mpaka wakumbuke kusahau kua Tanzania siyo nchi ya wachacheHabari Wakuu,
Leo 10/ 02/ 2022 shahidi wa 13 anatarajiwa kuendelea kutoa ushahidi wake kwenye kesi inayomkabili Mbowe na wenzake 3. Shahidi Tumaini Swila jana Februari 9, 2022 aliomba ahirisho kwakuwa alikuwa hajisikii vizuri.
Kujua Kesi ilipoishia fungua kiungo hiki: Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Swila aomba ahirisho kuwa hajisikii vizuri; kuendelea na ushahidi 10/02/2022
Baki nami.
Updates:
Jaji ameingia Mahakamani Muda huu
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa
Wakili wa Serikali, Nasorro Katuga: Mheshimiwa Jaji naomba Kuwatambulisha Mawakili
- Pius Hilla
- Esther Martin
- Jenitreza Kitali
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kuwatambulisha Mawakili
Wakili wa Serikali Nasorro Katuga: Mheshimiwa Jaji Shahidi ameshauriwa na Daktari Kupumzika na sisi hatuwezi Kwenda Kinyume na Ushauri wa Daktari Pia tungeweza Kutafuta Shahidi Mwingine wa Kuendelea naye ila Kwa Muda wa Jana na leo isingetosha Kutafuta Shahidi Mwingine
- Jeremiah Mtobesya
- Fredrick Kihwelo
- Sisty Aloyce
- Iddi Msawanga
- Michael Mwangasa
- Edward Heche
- Gaston Garubindi
- Hadija Aron
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba tuhairishe Kesi Mpaka Jumatatu, Kama atakuwa bado hajapona tunaweza Kutafuta Shahidi Mwingine Pia Mheshimiwa Jaji Kwa kutii Agizo la Mahakama Shahidi ameweza Kumtumia Ndugu yake aweze Kuja na Cheti cha Hospitali, lakini Original yake anaweza Kuja nayo yeye Mwenyewe pale atakapo pona
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba kama Dakika Moja na sisi tuweze Kuangalia Cheti cha Hospitali.
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Tumesikia Hoja ya Ndugu yangu Nassoro Katuga Nikianza na Hoja yenyewe ya Nyaraka Kutoka Hospitali, Nakumbuka Wakati natoa Hoja Jana, Tuliomba Shahidi atuletee Karatasi Kutoka Hospitali ya Serikali ambapo pia nafahamu Kwamba Askari Polisi anapopatwa na Ugonjwa anatakiwa kwenda huko, Nyaraka Walio leta Wenzetu Inatoka TMJ Super Polyclinic hii siyo Hospitali Ya Serikali Nyaraka hii inazidi Kuweka Wasiwasi zaidi Kwa Nini Mtu aende Kwenye Hospitali ambayo Haifahamiki
Nafikiri Jana tulikubaliana kuwa aje na Uthibitisho kutoka Hospitali ya Serikali Naomba Mahakama Ione kuwa sababu haina Logic wala hazipo Kama Mahakama itaona tofauti Basi Wenzetu Wasisitizwe
Kwa Mujibu Sheria Kesi katika Mahakama hii inatakiwa iishe ndani ya Miezi 9 Tukienda Kwa Mwenendo huu tutalazimika Kuomba Muda wa Nyongeza Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji
Jaji: Hoja ya Kuhusu airisho Sijaona kama Umezungumzia Kuhusu Muda wa airisho
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Jumatatu ni Mbali sana, Kwa Vyovyote itakayokuwa, Sasa ni saa Nne, Mpka Kesho Saa Nne ni Zaidi ya Masaa 24 Wana akiba ya Mashahidi 11 zaidi. Basi tutafute kati hao Mashahidi 11 angalau tuairishe Kwa Leo tuweze Kuja Kuendelea Kesho
Wakili wa Serikali Nasorro Katuga: Mheshimiwa Jaji Tumesikia Hoja ya Wenzetu Kutoka kwa Wakili Peter Kibatala Wenzetu Wanasema Kwamba Shaeria na Tangazo la Serikali namba 259 inataka Kumaliza shauri hili ndani ya Miezi 9 tunalifahamu na tumelichukua
Suala la tukishindwa Kuleta Shahidi huyu, tulete shahidi Mwingine nalo tumelichukua Suala la Shahidi Kuleta Cheti cha Hospitali ya Serikali, Shahidi Tulikuwa tunaona hapa tangu Mwanzo Kila Muda alikuwa anaomba Kwenda Msalani Huko Ndipo alipo kuwa anatibiwa kupitia Daktari Wake
Kupata tiba kutoka kwa Daktari Wake ni Nusu ya tiba, Kuhusu Wasiwasi Wa hapo anapotibiwa wanaweza Kwenda Kuuliza na Kuonana na Daktari Wake. Tunasisitiza Sisi Ka Maafisa wa Mahakama hatufurahishwi na airisho Lolote Pasipo Sababu.
Kuhusu Kuairisha Mpaka Kesho na Sitakukubali Kwamba tuje Kesho halafu tukaja na Hadithi ya Kukosa Shahidi. Ndiyo Maana tukaomba tuahirishe Mpaka Jumatatu ili kama Shahidi hata Kama anatakiwa Kusafiri atakuwa amefika
Sisi tunaona Kuwa ni Busara Kuairisha Mpaka Kesho halafu tukaja na story, Mahakama Yako itachoka Kutusikiliza. Sisi tunaomba tupewe airisho Mpaka Jumatatu. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.
Mahakama ipo kimya kusubiri uamuzi mdogo wa Mheshimiwa Jaji (10:15 AM)
Bado Mahakama ipo kimya (10:27 AM)
Jaji: nimesikia Hoja zilizotolewa na pande zote mbili Kama ambavyo Imetolewa na Upande Wa Mashtaka Mahakama hii imekuwa na Spirit ya Kutaka Shauri liishe kwa Haraka nimekuwa nikisisitiza Mawakili wa pande zote Mbili kuzingatia Spirit hii
Ila jana Wakati Shahidi anatoa Ushahidi wake, Shahidi Aliomba Kusitisha Kutoa Ushahidi Na Kwenda Kupata Matibabu Maombi hayo Kwa kuwa yalikuwa ya Msingi, Mahakama Ilielekeza Kuwa Shahidi atakapo rudi Mahakamani Hapa atalazimika kululetea Uthibitisho
Mahakama Haikusema Uthibitisho huo lazima utoke Hospitali ya Serikali, Kwa sababu suala la Matibabu ni la Mtu Binafsi Mahakama ilisita Kutoa Maelekezo hayo Ingekuwa inaingilia Mambo Mengine
Nyaraka iliyokuja hapa Shahidi amepata Uthibitisho Kuanzia Tarehe 9 Mpaka 11 February
Kwa Maana hiyo Shahidi Kwa Kesho Hawezi Kuwepo Upande wa Mashtaka Wanasema Kwamba hawawezi Kuomba airisho Mpaka Kesho Sababu wanaogopa Kuja Kesho bila Shahidi.
Kwa sababu hiyo ni Busara Ya Mahakama Inaona ni Vizuri Kuairisha Mpaka Siku ambayo Shahidi ataweza Kuja Mahakamani
Kwa sababu Hiyo naairisha Mpaka Jumatatu na Kuelekea Upande wa Mashtaka Kuhakikisha Kuwa Jumatatu wanakuja na Shahidi hata Kama yule atakuwa bado hajapona Waje na Mwingine
Kwa Maana hiyo na airisha Shauri Mpaka Jumatatu Saa 3 Asubuhi na Washtakiwa Wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Siku hiyo
Jaji anatoka
Swali zuri? Yaliyopokelewa na mahakama yatabaki kwenye taarifa za mahakama na yatatumia kama yalivyo dhidi au kwa manufaa ya pande zote
Ushahidi mkuu mbona uko tayari kwenye committal bundle na hakimu alishaona unaweza kutia mtu hatiani?
Tusubiri Jumatatu kama mgonjwa atakua amepona aendelee na dodoso, kama hajapona, aanze shahidi mwingine. Kesi imefika patamu.Kwa Maana hiyo na airisha Shauri Mpaka Jumatatu Saa 3 Asubuhi na Washtakiwa Wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Siku hiyo
Na ikatokea shahidi huyu hali yake ya kiafya "ikathibitika na Daktari wa TMJ" kwamba hawezi kuendelea na ushahidi na anahitaji matibabu zaidi kwenye hospitali za rufaa (ambalo "technically" naliona linakuja). Tutaendelea kusubiri ushahidi wa huyu Swila hadi afya yake iimarike kwa huo muda?, wakati tunaendelea na mashahidi wengine kati ya hao 24?Swali zuri? Yaliyopokelewa na mahakama yatabaki kwenye taarifa za mahakama na yatatumia kama yalivyo dhidi au kwa manufaa ya pande zote
Uko sahihi kabisa. Jaji ameshaona picha nzima ya hii kesi baada ya shahidi wa muhimu kabisa, Luteni Denis Leo Urio. Huyu ndiye amebeba maamuzi ya hii kesi.Wataalamu wa kuanzisha Nyuzi anzisheni uzi wa kumpongeza Jaji kajitahidi sana kuanzia alipoanza Denis Urio ,kaenda bila upendeleo .
Kumalizana naye, una maana "kumpoteza"? Swila anaumwa, tumuombee apone aje aendelee na ushahidi wake.Boaz ambaye ndiye alitakiwa kuwa shahidi wa kwanza kaingia mtini ..... badala yake kaweka mrorongo wa watu wa chini yake. Tangu lini mashahidi wote wanatoka ofisi moja tena kwa maelekezo ya Boss wao .... Only in Tanzania.
Ila sitashangaa kabla ya hii kesi kuisha kuna shahidi wataondoka naye, I mean watamalizana naye ......!!!
Ooooh !Kimenuka.Maswali ya kijinga yamesababisha afande nyoka kulazwa.
Taarifa za ndani zinadai kagoma kabsa kuja, na hata jumatatu kawaambia yeye hawezi.
Waende waliomtuma wakapambane na Kibatala.
Hata hiyo jumatatu lazima atepete kizimbani plus guilty mind inamsumbua.Ukiwa shahidi kwa suala unalolijua kikamilifu. Huwezi kupata wasiwasi.
Kwanza hata ukiandaliwa na wakili ni dakika 20 ikizidi nusu saa.
Ila ushahidi wa kitu cha kutengeneza. Aisee ni ushahidi mgumu sana. Ukiandaliwa na wakili inabidi hata siku mbili ukae na manotebook.. Kalamu.. Ukariri.. Yaani ni shida tupu.
Ndio maana mawakili wa Serikali hawawezi kukubali eti kesho tuu walete shahidi mwengine, ni kazi kubwa sana kuwaandaa na muda ni mfupi.
Kwahiyo wanakimbilia Jumatatu
Naitwa Jimbi, wewe ndugu Matereka Jayunga kwanini unatumia jina fake? Kwanini?Naitwa Matereka Jayunga nafatilia kwa umakini mkubwa kutoka bariadi mkoani simiyu
Mkuu, kwa hiyo huku mahakama kuu kinachofanyika hakina maana yoyote? Siku ukisikia Mbowe amehukumiwa kifungo jela, hutalala kwa furaha. Hawa kina Ndowo, Urio, Swila etc, wanaotoa ushahidi usiokufurahisha wanakuudhi sana.Ushahidi mkuu mbona uko tayari kwenye committal bundle na hakimu alishaona unaweza kutia mtu hatiani?
Huyu comte anapenda iwe hivyo. Angependa hawa mashahidi wa jamhuri wasiwe wanafanyiwa cross examination, ili wakileta uongo wao uchukuliwe hivyo ulivyo. Huyu jamaa anapata shida sana na hali ya hii kesi inavyoenda kwa sasa. Tukipata majaji wenye roho kama hizi za comte ni hatari sana.Ule utopolo wake hauwezi kupokelewa popote.
Tumia kichwa chako vizuri na sio kuongeza uzito juu ya mebega yako
Safi sana. Kama mbwai na iwe mbwai. Walimtuma afungue jalada la kesi isiyokuwepo, halafu sasa yeye anateseka na maswali huku wao wamerelax. Na mbaya zaidi hii kesi inaweza kumharibia kazi yeye Swila kuliko huyo Kingai.Maswali ya kijinga yamesababisha afande nyoka kulazwa.
Taarifa za ndani zinadai kagoma kabsa kuja, na hata jumatatu kawaambia yeye hawezi.
Waende waliomtuma wakapambane na Kibatala.
Mkuu ongeza nyama hapo kwenye "kagoma kabisa"Maswali ya kijinga yamesababisha afande nyoka kulazwa.
Taarifa za ndani zinadai kagoma kabsa kuja, na hata jumatatu kawaambia yeye hawezi.
Waende waliomtuma wakapambane na Kibatala.