Yaliyojiri kwenye ukaguzi wa Polisi katika Ofisi za JamiiForums na Nyumbani kwa Mkurugenzi, Maxence

JamiiForums

Official JF Response
Nov 9, 2006
6,200
4,984


Leo (Dec 14, 2016) mida ya mchana, polisi kutoka kituo cha Kati, Dar es salaam wakiambatana na Mkurugenzi mtendaji wa Jamii Media, Ndugu Maxence Melo, walifika katika ofisi za Jamii Media kwa ajili ya ukaguzi.

Zoezi hilo limekwenda sambamba na kuwahoji wafanyakazi (Social Media Engagers na Content Quality Controllers) juu ya utendaji wa shughuli zao za kila siku. Baada ya ukaguzi na mahojiano, polisi wameondoka na nyaraka za usajili wa Jamii Media ikiwemo cheti cha mlipa kodi, cheti cha BRELA, leseni ya biashara, n.k.

Pia polisi imewachukua wafanyakazi wawili kwa mahojiano zaidi.

Polisi wameelekea nyumbani kwa Maxence Melo ambako nako wamefanya ukaguzi ndani ya nyumba. Katika zoezi zima la ukaguzi, sehemu zote mbili, Jeshi la Polisi halikuhitaji wala kuchukua kifaa cha mawasiliano ya kimtandao kama router, flash, hard disc, au kompyuta.

Msafara umeelekea Polisi kituo cha kati kukamilisha mahojiano kati ya Mkurugenzi na wafanyakazi wawili waliochukuliwa.

Tunaomba umma utambue kwamba Jamii Media haina servers wala min-server ofisini kwake, nchini Tanzania wala Afrika. Pili, tunaomba watumiaji wa JamiiForums.com wasitiwe wasiwasi juu ya usalama wa taarifa zao. Teknolojia tunayoitumia (encryption) kumsajili mtumiaji wa JamiiForums.com haituwezeshi kumfahamu mtumiaji yeyote labda yeye akubali kwa hiari yake kujiweka wazi mtandaoni.

Imetolewa na Uongozi,
Jamii Media.
 
Sasa wewe ndugu yangu unaogopa nini wakati unatumia jina lako halisi.
Nani atakukamata sasa.
Mie nawakaribisha wanitafute muda wowote niko Mwanza mjini, ni mama ntilie hapa mjini kwa raha zangu. Lakini penye ukweli tutasema maana hata katiba ya changu kwenye madhumuni yake inasema kuwa nitasema kweli daima fitina kwangu ni mwiko
 
Hata wakienda ofisini hakuna watakachofanya, Data za JF zote zipo kwenye datacentre zilizopo nje ya nchi.
Sanasana labda kama wakiomba jamaa wawape password kulogin kwenye server wao wenyewe kitu ambacho JF wana haki ya kugoma, hili swala mwisho wa siku wata-lose tu watake wasitake labda wajitoe akili watumie mabavu.

Naona wameenda ofisini wamekosa kitu imebidi wazidi kumkaba huyu ndugu yetu. Hawa watu wanafanya mchezo sasa, wamegeuza sheria kua mchezo wa mpira.
 
351 Reactions
Reply
Back
Top Bottom