Uchaguzi 2020 Yaliyojiri kwenye kampeni za Mgombea Urais wa CHADEMA, Tundu Lissu Mikoa ya Kagera na Geita

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,517
217,784
Wakuu natanguliza salamu na baada ya salamu naingia moja kwa moja kwenye mada, kama mnavyojua Kampeni zinaendelea na leo tena Mh Lissu ambaye anapewa asilimia kubwa kutwaa urais wa nchi atakuwa kwenye mikoa ya Kagera na Geita, katika kanda hii kunatarajiwa kupigwa mkutano maalum wa kipekee kwenye jimbo la Chato.

Endelea kubaki hapahapa JF kwa taarifa za uhakika.

Mgombea Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Tundu Lissu ataendelea na  ( 640 X 640 ).jpg

========

UPDATES:

Picha mbalimbali za Mkutano wa Kampeni wa Mgombea Urais wa Chadema, Mhe. Tundu Lissu mapema asubuhi leo, Septemba 21 katika eneo la Nyakanazi, Kata ya Lusahunga, Wilaya ya Biharamulo, mkoani Kagera.

Akiwa hapo Mhe. Lissu amewanadi Mgombea Ubunge wa Chadema (mwenye kofia na rungu mkononi), Mbelwa Petro na Mgombea Udiwani Kata ya Lusahunga, Damasi Buyago.

Mhe. Tundu Lissu hapo, amesema;

Wananchi Nyakanazi Ahsante kwakutupokea Vizuri natumelala hapa Nawashukuru sana.

Kwenye Uchaguzi mkuu huu Tunahitaji kufanya Mabadiliko makubwa sana, na moja ni manyanyaso yenu wananchi kuuziwa Vitambulisho vya Wajasiriamali. Kwanini muuziwe vitambulisho, nchi hii Vitambulisho vinatolewa bure lakini serikali ya CCM inauza vitambulisho kwa wananchi wake, na hawatoi hata receipts za EFD. Nasema kuwa tunaliwa na hawa MaCCM. Sasa haya yote mwisho ni tarehe 28 Mwezi wakumi 2020.

Hapa Nyakanazi Wengine niwakulima wanahangaika wenyenyewe kipindi cha kulima na kupalilia Ila ukivuna tu.. Wanaweza mageti kila unapopita.

Sasa Uchaguzi Mkuu Huu twendeni tukachague wagombea wa Chadema Ili tuondoe Huu Udhalimu.

Chagueni Mbunge Wangu Wa Jimbo La Biharamulo "Mbelwa Petro" nanisikia mnamuita asiyempenda kaja, na diwani Bwana Damasi Buyago wachagueni Tufanye Mabadiliko. Nakwenye Kura Ya Urais Uamuzi ni Wenu Kati Ya Tundu Lissu au Jiwe... Sasa watu wa Nyakanazi naombeni kura zenu mnipe dhamana Yakuongoza.

Ahsanteni watu wa Nyakanazi.

1600676185389.png
1600676028658.png
1600676115816.png
1600676060419.png
1600676160670.png

1600675950856.png
1600675963953.png
1600675985802.png
1600676001797.png

NGARA; Picha zikionesha matukio mbalimbali kwenye Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema, Mhe. Tundu Lissu katika Uwanja wa Kokoto, Ngara mjini. Tundu Lissu pia alimpatia pole Mgombea Udiwani Kata ya Ngara mjini kwa tiketi ya Chadema, Bi. Herieth Gwaje, aliyefiwa na Baba yake mzazi, Mzee Malingumu, usiku wa kuamkia leo.
1600704404888.png
1600704542915.png

1600704306398.png

1600704199144.png

1600704354636.png
1600704376660.png
1600704427344.png
1600704439777.png
1600704452442.png
1600704468144.png
1600704495604.png
1600704512484.png

Picha; Wananchi wakifuatilia Mkutano wa Kampeni wa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema, Mhe. Tundu Lissu, baada ya kumsimamisha katika eneo la Nyakahura, Biharamulo (mizani) akiwa njiani kuelekea Ngara.
1600704591758.png
1600704603577.png

Tundu Lissu hapa chini kwenye Video Akisalimiana na Wananchi wa Nyakanazi Biharamlo baada ya Kuamka, alilala Nyakanazi, Video ya Pili ni akiwasili Ngara Kagera​

 
Ukweli watanzania wamechoka CCM. Ili ukubwliane na maneno yangu subiri TL akiwa mkoa wa Geita alilizaliwa JPM utaona atakavyoungwa mkono.
Mkuu sanduku la kura ndio huamua yote, wanaomlalamikia JPM wapo lakini wanafahamika kwa makundi.
Lowasa aliungwa mkono kuliko Mrema, kuliko Tundu Lissu leo.
 
Wakuu natanguliza salamu , na baada ya salamu naingia moja kwa moja kwenye mada , kama mnavyojua Kampeni zinaendelea na leo tena Mh Lissu ambaye anapewa asilimia kubwa kutwaa urais wa nchi atakuwa kwenye mikoa ya Kagera na Geita .

Endelea kubaki hapahapa JF kwa taarifa za uhakika .

View attachment 1575824
Mh Rais mtarajiwa, mkoa wa Geita tunaomba utembelee mji wa katoro na buseresere hatuna huduma ya maji Safi nasalama tangu mwaka 1961, hatuna barabara za lami kwenye mji huo vumbi Lila mahali. Pia karibu utembelee vijiji vya Nyamikoma, Kamwanga na lwenge vipo geita vijijini hakuna nishati ya umeme,hakuna maji, hakuna hata barabara ya magari ya kuvitembelea.

Maeneo yote haya Kuna uchumi mkubwa wa madini ya dhahabu Ila Hali ya umaskini ni mkubwa Sana. Pia ukiwa geita tutembelee wilaya ya chato Kijiji Cha majengo ambalo ni Kijiji cha nyumbani kwa Rais magufuli hakuna maji Safi na salama wananchi wanachota maji ya matumizi ndani ya ziwa Victoria
 
Wakuu natanguliza salamu , na baada ya salamu naingia moja kwa moja kwenye mada , kama mnavyojua Kampeni zinaendelea na leo tena Mh Lissu ambaye anapewa asilimia kubwa kutwaa urais wa nchi atakuwa kwenye mikoa ya Kagera na Geita .

Endelea kubaki hapahapa JF kwa taarifa za uhakika .

View attachment 1575824
TL tembelea wilaya ya Bukombe, mbongwe, nyangwale, Chato, Geita vijijini na Jimbo la busanda ukiwa mkoa wa Geita. Hali ya barabara, umeme, maji Safi na salama hakuna. Pia tembelea Nyarugusu, Rwamgasa, na Kakola
 
Kwani ninyi ccm mna hati miliki ya wapiga kura wa nchi hii....kama ulikuwa hujua fahamu leo kuwa Lissu ndiye Rais wako ajaye
kama ulikuwa huijui Tanzania vizuri kwa Huba na Mahaba yako utaifahamu vizuri mwaka huu, na utashangaa.
 
Back
Top Bottom