Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 116,495
- 215,349
Wakuu natanguliza salamu , kama mjuavyo kampeni za uchaguzi mkuu bado zinaendelea , sasa basi leo tena yule mgombea urais anayeongoza kura za maoni atakuwa Mkoa wa Mwanza kunadi sera za chama chake na kuomba kura za ndio.
Endelea kufuatilia hapahapa JF kwa taarifa za uhakika
========
Mkutano Mheshimiwaa Tundu Lissu Kwenye Viwanja vya Polisi - Misungwi, Mwanza.
Akiongea na watu Misungwi Amezungumzia yafuatayo.
1. Kuenguliwa kwa wagombea
2. Kuvunja Tume ya Uchaguzi
3. Mamlaka kwa wananchi
4. Kujitokeza Kupiga Kura kwa wingi.
5. Uchaguzi Wa huru na haki.
Halmashauri nzima haina mgombea yeyote wa Chadema.
]
Mkutano Mhe. Tundu Lissu Kwenye Viwanja vya Sokoni G'hungumalwa- Kwimba, Mwanza.
Akiongea na watu Hungumalwa Amezungumzia yafuatayo.
1. Kuenguliwa kwa wagombea ( Mgombea Ubunge nawagombea wa Tano wa udiwani.)
2. Kurudisha mamlaka kwa wananchi
3. Mjitokeze Kupiga Kura na Kulinda kura.
4. Kilimo cha Pamba na mazao mengine.
5. Utozwaji ushuru na msururu wa kodi kwa wafanyabiashara.
6. Uchaguzi Wa huru na haki.
7. Nyongeza za mishahara na upandishwaji wa Madaraja kwa watumishi wa umma.
Ahsanteni sana watu wa G'hungumalwa.
Mkutano Mhe. Tundu Lissu Kwenye Viwanja vya Nyambiti Sumve - Mwanza.
Akiongea na watu Sumve amezungumzia haya.
1. Gharama Za Chapa ya Ng'ombe
2. Msururu wa ushuru wa mazao.
3. Malipo kwa wakulima wa Pamba.
4. Barabara ya Nyambiti
5. Uboreshwaji wa huduma za afya na maji.
6. Uchaguzi Wa huru na haki.
Mgombea ubunge wa Jimbo la Sumve Bwana *Sangarali Shija Masanja.* Nadiwani Ni *Bi. Eunice Tabuse.*
Ahsanteni watu wa Sumve.
Mwanza , Nyamagana
Maelfu ya wananchi wa Mwanza kwenye Mkutano wa Kampeni wa Mhe. Tundu Lissu uliofanyika Uwanja wa Shule ya Msingi Mabatini, Nyamagana.
Ameongea na Wananchi wa Nyamagana...
"Ahsanteni Mwanza ahsante Nyamagana.. Imekuwa wiki yakuvunja record, leo record iko Nyamagana.
Leo Naomba mniruhusu nizungumze mambo mawili tu.
Jambo la kwanza nikuhusu wanajeshi wa Tanzania, ninapozungumza Wanajeshi wanajeshi ni Ma jeshi yaliyotajwa kwenye katiba yetu yaani Jeshi la wananchi, jeshi la polisi, jeshi la Magereza, jeshi la akiba (Mgambo) na hawa Usalama wa Taifa ambao hawajatajwa.
Rai yangu kwenu kwa wanajeshi wa Tanzania, nmeona umati huu umati huu, nmeona wananchi wanataka nini, sasa msije mkataka kutumika kuharibu uchaguzi huu. Msije mkageuza silaha kwa wananchi wanaojua wanataka nini. Ukombozi huu wa Tanzania unawahusu na nyinyi askari wetu, Chadema Ikiingia Madarakani itawalipa na kuwaongeza mishahara.
Lapili watu wa Nyamagana nawaomba tarehe 28 tukapige kura ya mafuriko kama haya ya Leo. Tukipiga kura ya mafuriko hawataweza kuiba, tukapige kura tukawatoe hawa wanaotutia umasikini wakudumu. Tukapige kura ili kira mtu nchi hii atendewe haki, sote tupate haki. Tukapige kura ili tusitishe unyanyasaji uliodumu muda mrefu. Kura za mafuriko kama haya zitaamua hatima ya maisha yetu.
Chombezoo.. Anamwambia OCD "Najua afande namalizia kuongea ila haya pia yanahusu ukombozi wenu.."
Ahsanteni sana Nyamagana na Mungu awabariki Sana Nyamagana.