Uchaguzi 2020 Yaliyojiri Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM: Majina ya walioteuliwa kuwania nafasi za Ubunge kwenye Majimbo mbalimbali nchini

Usiamini wanasiasa. Hata Museven na Kagame waliwahi tangaza mara kibao kuwa ni misimu yao mwisho.
Siwaamini 100% Ila Hilo wamelisisitiza mno
Siwezi kuwafananisha na Museven na Kagame Sababu siasa za Tanzania Ni tofauti, hao waliingia madarakani kwa mtutu wa bunduki na katika Historia ya nchi yao hakuna kiongozi aliyeachia madaraka kwa njia za kawaida, Ni kitu Kigeni kwao

Tofauti na Tz ambalo imezoeleka na Magufuli akirefusha Basi ndio atakuwa amevunja mwiko, na kuweka precedence mbaya, na hili linaweza kukigawa chama

Sisemi kuwa Haiwezekani Ila Ni ngumu Sana
 
Kawe Halima hatoboi, kule Ndanda kwa Cecil Chadema kama kuna mtu mwenye ushawishi jimbo wanalichukua mapema tu..

Arusha ngoma nzito.. Lema anapendwa na vijana wa kiume ila Gambo wamama na wasichana wanamkubali sana..
Amini nakwambia, Gwajima Kawe hatoboi. Kawe sio watu wa kumpapalikia mtu. Ni jimbo la wasomi wengi sana na watu wenye uwezo wa kifedha. Gwajima na mascandal yake Kawe hawezi toboa
 
Baada ya kikao cha halmashauri kuu kuketi asubuhi, Katibu mkuu mwenezi wa CCM anaongelea yaliyojiri.
=======

Polepole: Vikao vyote cha jana na leo vilikuwa chini ya mwenyekiti wa CCM. Kikao cha halmashauri kuu kilikuwa na lengo moja na limekamilika. Lengo lilikuwa kufanya uteuzi wa mwisho kwa wagomea wa majombi na viti maalum. Napenda kuleta taarifa hiyo kwenu kwa maana hawa walioteuliwa leo kwa majimbo na viti maalum.

Walijitokeza 10,367 nafasi za majimbo 264, chama chetu kimeandika rekodi na historia ya kukubalika. Upande wa uwakilishi leo haukufanyika uteuzi kwa sababu ya muingiliano wa ratiba ya NEC. Wagombea 33,094 waliomba kukiwakilisha chama cha mapinduzi kwenye udiwani ilhali nafasi zipo kama elfu nne na kitu na kufanya jumla ya watu 43,461 waliiomba kukiwakilisha chama cha mapinduzi kwenye nafasi mbalimbali.

Wajumbe wa halmashauri kuu wametimiza wajibu wao na kikao kimeeleza wajibu wao wa kusimamia serikali mpaka tumefika hapa, uamuzi walioufanya leo umezingatia watu wabobevu kusimamia maslahi ya watu wetu watakaofanya kazi sambamba na serikali ya chama cha Mapinduzi ambayo tunaenda kuiombea kura.

Kwa kauli moja wajumbe wamefanya uteuzi baada ya kupokea majina kwa watakaokuwa wagombea wa CCM kwa nafasi ya ubunge. Vilikuwepo vingezo na sifa ambazo tumezitumia ikiwemo wanaCCM wanaojitoa kwa chama, tumetafuta yule ambae atatuleta pamoja, wenye mahusiano mazuri na wananchi na wanakubalika na jamii.

Watu ambao wameteuliwa leo wanatakiwa wanatakiwa wafanye maandalizi ya msingi.

Kwenye majimbo wanaCCM ni nidhamu tuendelee kuwa watulivu, wagombea ni wengi hatuwezi kupata wote lakini nawahakikishia kwamba, chama chetu ni kikubwa na fursa zake ni nyingi tuendelee kuwa wanyenyekevu na watulivu, chama kina taarifa zenu.

ARUSHA
Arusha mijini- Mrisho Mashaka Gambo

Arumeru Magharibi- Noah Lebrus Molel

Arumeru Mashariki- John Palangyo

Karatu- Daniel Tlemai

Longido- Stephen Kirusya

Monduli- Fred Lowassa

Ngorongoro- Ole Nasha

DAR
Ubungo- Prof Kitila Kitila

Kibamba- Issa Jumanne Mtemvu

Kinondoni- Abass Tarimba

Kawe- Askofu Josephat Gwajima

Kigamboni- Dr. Faustine Ndugulile

Ilala- Mussa Zungu

Segerea- Bonna Kamoli

Ukonga- Jerry Slaa

Temeke- Doroth Kilave

Mbagala- Abdallah Chaurembo

DODOMA
Bahi- Keneth Nolo

Chamwino- Deo Dejembi

Mvumi- Livingstone Lusinde

Chemba- Mohammed Moni

Dodoma Mjini- Anthony Mavunde

Kongwa- Job Ndugai

Kondoa mji- Ally Juma Makoa

Kondoa Vijijini- Dr. Ashatu Kijaji

Kibakwe- George Simbachawene

Mpwapwa- George Nataly Malima

GEITA
Busanda- Tumaini Magesa

Geita Mjini- Consatantine Kanyasu

Geita vijijini- Joseph Kasheku(Musukuma)

Bukombe- Dotto Bisheko

Chato- Medard Kalemani

Mbogwe- Nicodemas Maganga

Nyang'alwe- Hussein Amar

IRINGA
Iringa Mjini- Jesca Msavatambangu

Kalenga- Jackson Kiswaga

Isimani- William Lukuvi

Kilolo- Lazaro Nyamoga

Mafinga mji- Cosato Chumi

Mufindi Kaskazini- Exaud Kigahe

Mufindi Kusini- David Kihenzile

KAGERA
Bukoba mjini- Stephen Byabato

Bukoba vijijini- Jackson Rweikiza

Nkenge- Frolent Kyombo

Karagwe- Innocent Bashungwa

Kyerwa- Innocent Bilakwate

Ngara- Ndaisaba Luhoro

Bihalamuro- Ezra Chiwelesa

Muleba Kaskazini- Charls Mwijage

Muleba Kusini- Oscar Kikoyo

KATAVI
Mlele- Isack Kamwele

Kavuu- Geophrei Mizengo Pinda

Mpanda Mjini- Sebastian Kapufi

Nsimbo- Anna Lupembe

Mpanda Vijijini- Moshi Kakoso

KIGOMA
Kasuli Mjini- Prof Joyce Ndalichako

Manyovu- Dr. Philip Mpango

Buyungu- Aloyce Kamamba

Muhambwe- Atashasta Nditiye

Kigoma Mjini- Kirumbe Shabani Ng'enda

Kigoma Kaskazini- Asa Nelson Makanika

Kigoma Kusini- Nashon William

Kasulu vijijini- Augustine Hole

KILIMANJARO
Vunjo- Charls Kimei

Siha- Dr. Godwin Mollel

Moshi Vijijini- Prof. Patrick Ndakidemi

Hai- Salasisha Mafue

Same Mashariki- Anne Kilango Malecela

Same Magharibi- Dr. Mathayo David Mathayo

Rombo- Prof. Adolf Mkenda

Moshi Mjini- Priscus Tarimo

Mwanga- Anania Tadayo

LINDI
Kilwa Kaskazini- Ndulane Franscis

Kilwa Kusini- Kasinge Mohammed Ally

Liwale- Zuberi Kuchauka

Lindi Mjini- Hamida Mohammed Abdallah

Mchinga- Salma Kikwete

Mtama- Nape Nnauye

Nachingwea- Amandus Julius Chinguiye

Ruangwa- Kassim Majaliwa

MANYARA
Babati Mijini- Paulina Gekul

Babati vijijini- Daniel Silo

Hanang- Samwel Kadai

Mbulu mji- Isai Paulo

Mbulu vijijini- Flatei Gregory

Kiteto- Edward Kisau

Simanjiro- Christpher Ole Sendeka

MARA
Musoma Mjini- Vedastus Manyinyi

Musoma Vijijini- Prof. Sospeter Muhongo

Bunda Mjini- Robert Chacha Maboto

Bunda Vijijini- Boniface Getere

Mwibara- Charls Kajege

Butiama- Jumanne Sagini

Rorya- Jaffary Wambura Chege

Tarime Mjini- Mwita Michael Kembaki

Tarime Vijijini- Mwita Waitara

Serengeti- Dr. Jeresabi Mkimi

MBEYA
Busekelo- Atupele Mwakibete

Kyela- Ally Jumbe

Lupa- Masache Kasaka

Mbalali- Franscis Mtega

Mbeya Mjini- Dk. Tulia Akson

Mbeya Vijijini- Oran Njeza

Rungwe- Anthony Mwantona
Waooooo!!! Wapi mwenye digrii nne?? Wajumbe bwana. Mtu wa darasa la saba ata bishanaje na mwenye digrii nne??
 
Yani hawa watu wajiandae kutafuta kura za mawe tu.
1. David Silinde
2. Pauline Gekul
3. Salvatory Makundi
4. Cecil Mwambe
5. Pateobas Katambi

Save my content!
Wanapita bila shida, katambi anamaliza mchezo mapema pale shy town.Masele alikuwa mzigo sana na mtu wa kujisikia sana
 
Acha udini wewe
Gwajima kuna kipindi aliikashifu iman ya Kislam na ushahidi wa video upo,pili lile pilau lake kule kwenye site za UTAMU alilo lipika na kondoo wake,linatosha kummaliza.

Kwa kifupi historia yake ina mkaanga mwenyewe,ndio maana sometimes kama una plan za kuwa kiongozi kuwa makini na kauli pamoja na matendo yako.

Kwani ipo siku watu wata kuhukumu kwa kauli na matendo yako ya nyuma.


KAWE mbunge ni MDEE,itunze comment hii.
 
Back
Top Bottom