Uchaguzi 2020 Yaliyojiri Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM: Majina ya walioteuliwa kuwania nafasi za Ubunge kwenye Majimbo mbalimbali nchini

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,797
11,959


Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM kinakutana leo chini ya Mwenyekiti wake Rais Magufuli. Miongoni mwa agenda ni kupitisha majina ya wagombea wa nafasi za Ubunge na Uwakilishi.

Mkutano utarushwa mubashara na Channel ten, TBC na ITV

Up dates;

Wajumbe wa halmashauri kuu tayari wameanza kuingia ukumbini na wengine wanajadiliana hili na lile kwa bashasha.

Mwenyekiti wa chama Dr Magufuli ameshaingia ukumbini na sasa mwenezi komredi Polepole anaelezea utaratibu.

Na sasa Katibu mkuu Dr Bashiru anazungumzia makusudi ya kikao na kwamba kikao hiki kitafanya uteuzi wa wabunge tu kwa sababu ratiba za NEC na ZEC ni tofauti.

===
1597910366707.png

Hotuba ya mwenyekiti wa CCM( - Dkt. John Pombe Magufuli)

Ameanza kwa kutoa salamu kwa wajumbe wote na viongozi mbalimbali wa chama cha Mapinduzi.

Anapenda kuwakaribisha na kuwashukuru kwa kuhudhuria mkuano mkuu na pia anawashukuru wajumbe wa NEC kwa kumpigia kura. "Napenda niwashukuru sana wajumbe wa NEC kwanza kwa jinsi mlivyonipigia kura nyingi, mlikuwa wajumbe hamkuniangusha wajumbe". Mlipokwenda kwenye maeneo yenu mlishiriki kwa upendo mkubwa sana kunitafutia wadhamini na wadhamini walipatika zaidi ya milioni moja point moja.

Nilipotuma wawakilishi kwa ajili ya kwenda kunitafutia wadhamini ili kutimiza masharti ya NEC mlikwenda na nimepata udhamini kwa mikoa mingi sana ya Tanzania bara na Zanzibar nasema hongereni sana na asanteni sana.

Wajumbe wa mkutanao na kikao hiki muhimu natambua kuwa wengine mmesafiri usiku na umbai mrefu ili kuwahi mkutano huu muhimu nasema hongereni sana hii inaonesha mnatambua umuhimu na manakipenda chama chetu.

Mkutano huu una ajenda moja kubwa kufanya uteuzi wa wagombea wa ubunge na uwakilishi kupitia tiketi ya chama cha Mapinduzi. Zoezi la uteuzi ndani ya chama lilianza takribani mwezi mmoja umepita na wajumbe walipiga kura na baada ya kujadiliwa na kamati mbalimbali pia wamefika kwenye mkutano huu ili pia wajadiliwe.

Napenda kuwapongeza wanachama waliojitokeza kugombea nafasi mbalimbali na walijitokeza wengi sana na hiyo ni kwa kuwa wanakipenda sana hivyo nasema hongereni sana.

Wana CCM 10367 walichukua fomu za ubunge wa majimbo na viti maalum na waliojitokeza kuwania ubunge baraza la uwakilishi ni 786 na waliojitokeza kuwania udiwani katika kata wodi na viti maalumu walikuwa 33094 kwa hiyo mytaona waliojitokeza kuwania nafasi mbalimbali walifika 44461 haya ni mafanikio makubwa kwa chama chetu na nafasi hizi ziliomba na watu wa kaliba na tofauti tofauti.

Katika kipindi cha miaka mitano nimekuwa nikiwaona mitembelea miradi mbalimbali na mkikemea kwa waliozembea na kutoa maelekezo mbalimabali na miradi mingi imekamilika na haya ndio matunda ya ufanyaji kazi wenu na ndio maana watu wengi wamejitokeza kuomba nafasi mbalimbali.

Juzi na jana majina ya wagombea yalijadiliwa kwenye vikao katika ngazi ya kamati ya usalama na maadili na kisha kamati kuu kwa ajli ya uchambuzi wa kina na uchambuzi wa kina kweli kweli tulitumia taarifa tulizozipata kupitia vyanzo mbalimbali na kwa yule atakayepata ufafanuzi basi atapatiwa maana nilisoma majina yote kwa kina na hatutakuwa tumempendelea mtu au kumuonea mtu .

Ilitulazimu kutumia taarifa nyingi ili atakaechaguliwa awe na uwezo wa kuipeperusha bendera na awe na uwez wa kungoza nchi yetu na hiyo ni kutokana na unyeti wa nafasi wanayogombea kwa kuwa ndiyo wawakilishi wa wananchi maana ndimo atakapopatikana waziri mkuu na viongozi wengine hivyo ilibidi tuchague mwenye sifa ya kuwa kiongozi.

Ikiwemo kupata viongozi wenye uwezo wa kuongoza, wazalendo, wenye kujitoa kwenye chama wanaofahamu mahitaji ya wananchi wanaokubalika na wananchi na na wenye utayari wa kuwatumikia wananchi na watanzania wote.

Baada ya kufanyika kwa mchakato kwenye ngazi mbalimbali halmashauri kuu ndio imepewa mamlaka ya mwisho kufanya uteuzi wa wagombea kwa mujibu wa kifungu namba 102 ibara ndogo ya 12 g ya katiba ya CCM ya 1977 na toleo la mwaka 2017.



--- UPDATES---

Baada ya kikao cha halmashauri kuu kuketi asubuhi, Katibu mkuu mwenezi wa CCM anaongelea yaliyojiri kwenye kikao hicho mpaka kupata majina ya watu wanaowania ubunge kwa tiketi ya chama hicho kwenye majimbo mbalimbali nchini pia wabunge wa Viti Maalum
=======

Polepole: Vikao vyote cha jana na leo vilikuwa chini ya mwenyekiti wa CCM. Kikao cha halmashauri kuu kilikuwa na lengo moja na limekamilika. Lengo lilikuwa kufanya uteuzi wa mwisho kwa wagombea wa majimbo na viti maalum. Napenda kuleta taarifa hiyo kwenu kwa maana hawa walioteuliwa leo kwa majimbo na viti maalum.

Walijitokeza 10,367 nafasi za majimbo 264, chama chetu kimeandika rekodi na historia ya kukubalika. Upande wa uwakilishi leo haukufanyika uteuzi kwa sababu ya muingiliano wa ratiba ya NEC. Wagombea 33,094 waliomba kukiwakilisha chama cha mapinduzi kwenye udiwani ilhali nafasi zipo kama elfu nne na kitu na kufanya jumla ya watu 43,461 waliiomba kukiwakilisha chama cha mapinduzi kwenye nafasi mbalimbali.

Wajumbe wa halmashauri kuu wametimiza wajibu wao na kikao kimeeleza wajibu wao wa kusimamia serikali mpaka tumefika hapa, uamuzi walioufanya leo umezingatia watu wabobevu kusimamia maslahi ya watu wetu watakaofanya kazi sambamba na serikali ya chama cha Mapinduzi ambayo tunaenda kuiombea kura.

Kwa kauli moja wajumbe wamefanya uteuzi baada ya kupokea majina kwa watakaokuwa wagombea wa CCM kwa nafasi ya ubunge. Vilikuwepo vingezo na sifa ambazo tumezitumia ikiwemo wanaCCM wanaojitoa kwa chama, tumetafuta yule ambae atatuleta pamoja, wenye mahusiano mazuri na wananchi na wanakubalika na jamii.

Watu ambao wameteuliwa leo wanatakiwa wanatakiwa wafanye maandalizi ya msingi.

Kwenye majimbo wanaCCM ni nidhamu tuendelee kuwa watulivu, wagombea ni wengi hatuwezi kupata wote lakini nawahakikishia kwamba, chama chetu ni kikubwa na fursa zake ni nyingi tuendelee kuwa wanyenyekevu na watulivu, chama kina taarifa zenu.


Majina yaliyoteuliwa na Halmashauri kuu ya Taifa kugombea ubunge wa majimbo na ubunge wa viti maalum

ARUSHA
Arusha mijini- Mrisho Mashaka Gambo

Arumeru Magharibi- Noah Lebrus Molel

Arumeru Mashariki- John Palangyo

Karatu- Daniel Tlemai

Longido- Stephen Kirusya

Monduli- Fred Lowassa

Ngorongoro- Ole Nasha

DAR
Ubungo- Prof Kitila Kitila

Kibamba- Issa Jumanne Mtemvu

Kinondoni- Abass Tarimba

Kawe- Askofu Josephat Gwajima

Kigamboni- Dr. Faustine Ndugulile

Ilala- Mussa Zungu

Segerea- Bonna Kamoli

Ukonga- Jerry Slaa

Temeke- Doroth Kilave

Mbagala- Abdallah Chaurembo

DODOMA
Bahi- Keneth Nolo

Chamwino- Deo Dejembi

Mvumi- Livingstone Lusinde

Chemba- Mohammed Moni

Dodoma Mjini- Anthony Mavunde

Kongwa- Job Ndugai

Kondoa mji- Ally Juma Makoa

Kondoa Vijijini- Dr. Ashatu Kijaji

Kibakwe- George Simbachawene

Mpwapwa- George Nataly Malima

GEITA
Busanda- Tumaini Magesa

Geita Mjini- Consatantine Kanyasu

Geita vijijini- Joseph Kasheku(Musukuma)

Bukombe- Dotto Bisheko

Chato- Medard Kalemani

Mbogwe- Nicodemas Maganga

Nyang'alwe- Hussein Amar

IRINGA
Iringa Mjini- Jesca Msavatambangu

Kalenga- Jackson Kiswaga

Isimani- William Lukuvi

Kilolo- Lazaro Nyamoga

Mafinga mji- Cosato Chumi

Mufindi Kaskazini- Exaud Kigahe

Mufindi Kusini- David Kihenzile

KAGERA
Bukoba mjini- Stephen Byabato

Bukoba vijijini- Jackson Rweikiza

Nkenge- Frolent Kyombo

Karagwe- Innocent Bashungwa

Kyerwa- Innocent Bilakwate

Ngara- Ndaisaba Luhoro

Bihalamuro- Ezra Chiwelesa

Muleba Kaskazini- Charls Mwijage

Muleba Kusini- Oscar Kikoyo

KATAVI
Mlele- Isack Kamwele

Kavuu- Geophrei Mizengo Pinda

Mpanda Mjini- Sebastian Kapufi

Nsimbo- Anna Lupembe

Mpanda Vijijini- Moshi Kakoso

KIGOMA
Kasuli Mjini- Prof Joyce Ndalichako

Manyovu- Dr. Philip Mpango

Buyungu- Aloyce Kamamba

Muhambwe- Atashasta Nditiye

Kigoma Mjini- Kirumbe Shabani Ng'enda

Kigoma Kaskazini- Asa Nelson Makanika

Kigoma Kusini- Nashon William

Kasulu vijijini- Augustine Hole

KILIMANJARO
Vunjo- Charls Kimei

Siha- Dr. Godwin Mollel

Moshi Vijijini- Prof. Patrick Ndakidemi

Hai- Salasisha Mafue

Same Mashariki- Anne Kilango Malecela

Same Magharibi- Dr. Mathayo David Mathayo

Rombo- Prof. Adolf Mkenda

Moshi Mjini- Priscus Tarimo

Mwanga- Anania Tadayo

LINDI
Kilwa Kaskazini- Ndulane Franscis

Kilwa Kusini- Kasinge Mohammed Ally

Liwale- Zuberi Kuchauka

Lindi Mjini- Hamida Mohammed Abdallah

Mchinga- Salma Kikwete

Mtama- Nape Nnauye

Nachingwea- Amandus Julius Chinguiye

Ruangwa- Kassim Majaliwa

MANYARA
Babati Mijini- Paulina Gekul

Babati vijijini- Daniel Silo

Hanang- Samwel Kadai

Mbulu mji- Isai Paulo

Mbulu vijijini- Flatei Gregory

Kiteto- Edward Kisau

Simanjiro- Christpher Ole Sendeka

MARA
Musoma Mjini- Vedastus Manyinyi

Musoma Vijijini- Prof. Sospeter Muhongo

Bunda Mjini- Robert Chacha Maboto

Bunda Vijijini- Boniface Getere

Mwibara- Charls Kajege

Butiama- Jumanne Sagini

Rorya- Jaffary Wambura Chege

Tarime Mjini- Mwita Michael Kembaki

Tarime Vijijini- Mwita Waitara

Serengeti- Dr. Jeresabi Mkimi

MBEYA
Busekelo- Atupele Mwakibete

Kyela- Ally Jumbe

Lupa- Masache Kasaka

Mbalali- Franscis Mtega

Mbeya Mjini- Dk. Tulia Akson

Mbeya Vijijini- Oran Njeza

Rungwe- Anthony Mwantona

MOROGORO
Mlimba- Godwin Kunambi

Kilombero- Abubakar Asenga

Morogoro mjini- AbdulAziz Abood

Gairo- Ahmed Shabiby

Malinyi- Antipas Mgungusi

Morogoro Kusini- Innocent Kalogeres

Morogoro Mashariki- Hamis Shaaban Taletale

Mvomero- Jonas Vanzilad

Mikumi- Deniss Lazaro Londo

Kilosa- Prof. Palamaganda Kabudi

Ulanga- Salim Hasham

MTWARA
Mtwara Mjini- Mtenga Hassan Selemani

Mtwara Vijijini- Hawa Ghasia

Nanyamba- Abdallah Chikota

Tandahimba- Katani Katani

Newala mjini- George Mkuchika

Newala Vijijini- Maimuna Mtanda

Masasi- Geofrey Mwambe

Lulindi- Issa Mchungahela

Ndanda- Cecil David Mwambe

Nanyumbu- Yahaya Ali Mhata

MWANZA
Ukerewe- Joseph Mkundi

Ilemela- Dkt. Angelina Mabula

Sengerema- Tabasamu Hamis Mwagao

Buchosa- Erick Shigongo James

Nyamagana- Stanslaus Mabula

Misungwi- Alexander Mnyeti

Sumve- Kasalali Emmanuel Mageni

Kwimba- Shanif Mansour

Magu- Bonaventura Kiswaga

NJOMBE
Lupembe- Edwin Sware

Makambako- Deo Sanga

Njombe Mjini- Deodatus Mwanyika

Makete- Festo Sanga

Wanging'ombe- Dk. Festo John Dugange

Ludewa- Kamonga Zakarius

PWANI
Bagamoyo- Muharami Mkenge

Chalinze- Ridhwan Kikwete

Kibiti- Twaha Mpembenue

Kibaha Mjini- Sylvester Koka

Kisarawe- Selemani Jaffo

Mkuranga- Abdallah Ulega

Mafia- Omar Kipanga

Rufiji- Mohammed Mchengelwa

Kibaha Vijijini- Michael Mwakamo

RUKWA
Nkasi Kusini- Vicent Mbogo

Sumbawanga Mjini- Ayeshi Hilal

Kwera- Deus Sangu

Nkasi Kaskazini- Ally Kessy Alimabodi

Kalambo- Josephat Kandege

RUVUMA
Songea Mjini- Dkt. Damas Ndumbaro

Peraminho- Jennister Mhagama

Madaba- Joseph Mhagama

Nyasa- Stella Manyanya

Mbinga Mjini- Jonas Mbunda

Mbinga Vijijini- Benaya Kapinga

Namtumbo- Vita Kawawa

Tunduru Kaskazini- Hassan Kungu

Tunduru Kusini- Daim Mpakate

SHINYANGA
Shinyanga mjini- Patrobas Katambi Paskal

Solwa- Ahmed Salum

Kahama Mji- Jumanne Kishimba

Msalala- Idd Kassim Idd

Ushetu- Elias Kwandikwa

Kishapu- Boniface Butondo

SIMIYU
Bariadi- Andrea Mathew

Busega- Saimon Songe

Itilima- Njalu Daud Silanga

Maswa Magharibi- Mashimba Ndaki

Maswa Mashariki- Nyongo Stanslaus Harun

Meatu- Leah Komanya

Kisesa- Luhaga Mpina

SINGIDA
Singida Mjini- Mussa Sima

Singida Kaskazini- Ramadhan Ihondo

Singida Mashariki- Miraji Jumanne Mtaturu

Singida Magharibi- Elbariki Kingu

Manyoni Mashariki- Dkt Stephen Chaya

Manyoni Magharibi- Yahaya Omar Masare

Iramba Mashariki- Franscis Isack Minga

Iramba Magharibi- Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

SONGWE
Ileje- Geofrey Kasekenya

Mbozi- George Mwenisongole

Vuawa- Japhet Hasunga

Tunduma- David Ernest Silinde

Momba- Kondesta Sichalwe

Songwe- Philipo A. Mulugo

TABORA
Igunga- Nocholaus Ngassa

Manonga- Seif Hamis

Tabora Kaskazini- Athumani Mahige

Igalula- Venant Protas

Tabora Mjini- Emmanuel Mwakasaka

Nzega Mjini- Hussein Bashe

Nzega Vijijini- Hamis Kigwangallah

Bukene- Selemani Jumanne

Kaliua- Aloyce Kwezi

Uliankulu- Rehema Migila

Urambo- Magreth Sitta

Sikonge- Joseph Kakunda

TANGA
Bumbuli- January Makamba

Korogwe Mjini- Alfred Kimea

Korogwe Vijijini- Timotheo Paul Mnzava

Pangani- Jumaa Aweso

Lushoto- Shaban Shekilindi

Handeni Mjini- Kwagila Mhamanilo

Handeni Vijijini- John Salu

Kilindi- Omar Kigua

Tanga Mjini- Ummy Mwalimu

Mlalo- Rashid Shangazi

Muheza- Hamis Mwinjuma(MwanaFA)

Mkinga- Dastan Kitandula


- MWISHO-

Uchaguzi 2020 - Wafahamu baadhi ya Watia nia ya Ubunge wa CCM ambao hawakushinda katika kura za maoni lakini wamepitishwa kugombea katika majimbo yao
 
Mbona nasikia wagombea wa CCM wameshaenda kuchukua fomu za ubunge udiwani na uwakilishi na ofisi ya Tume haitowi fomu ya jimbo moja mara mbili kwa chama kimoja sasa hawa hakuna faida tena.
 
Bila shaka unamaanisha sehemu ya Genge la wachumia Tumbo Bungeni na Wasaliti wa Wananchi kujulikana leo!!
Unamaanisha pia ndio hao hao watakaopitishwa na kuchaguliwa na wananchi, kwako wewe kinachokukela ni kule tu kuwa wachumia tumbo Bungeni.
 
Back
Top Bottom