Bila bila
JF-Expert Member
- Dec 20, 2016
- 21,471
- 37,733
Hujui hata unachosimamia fala wewe. Umejaa ujinga kwa vile mumeo anakula CCM?Unalipwa baada ya kazi wauaji wakubwa nyinyi
Hujui hata unachosimamia fala wewe. Umejaa ujinga kwa vile mumeo anakula CCM?Unalipwa baada ya kazi wauaji wakubwa nyinyi
Mavi yako! Lowasa alimpiga magufuli kwa mbaali mno! Nchi ya mikondoo shukuruni tu!Nchi igawanyike kwa lipi? Alishindwa kuigawa nchi Lowassa 2015 ije kuwa leo? Hakuna takataka yeyote TZ hii anaweza kusababisha nchi igawanyike
Mkuu usitoe ubinadamu kisa hela unayo pata hapo Lumumba.Kumbuka Mungu ni wetu sote ,Magufuli alikuwa anatamani wabaya wake wafe haraka alikufa kifo cha aibu kabla yao.Ameuwa watu wengi sana
Mimi sijaajiri makomandoo waliofukuzwa jeshi ili kulipua vituo vya mafuta bali Mbowe na akikutwa na hatia anyongwe hadi kufaHaya maombi yatakurudia wewe binafsi
Ukiangalia hata ile kesi ndogo ni basi tu wanaona Aibu kuifuta hii kesi, hii kesi ya kubambikia imebuma lakini watamfunga mbowe miaka mitano kumnusuru Samia na Aibu.Na kila kitu hapana, sasa kama hapana haya mashtaka yametokea wapi? Kuna watu wanatia hasira nyie!
Halafu Rais ni nani alimdanganya kuwa watuhumiwa wengine walishashitakiwa? Kwanini hakujipa muda kujiridhisha juu ya kinachoendelea? Kwa sasa anaona kinachoendelea na je kinaendana na maelezo aliyoiambia dunia? Aibu kubwa!
Matokeo yalienda Kama CCM walivyopangaAnd matokeo yakawaje at the end?
Mbona makubaliano ya kazi hayasemwi? Walianza kazi bila mapatano? Ni mataahira?Yaani kina Kasekwa walikubali kufanya Ugaidi (UGAIDI) bila kujua watalipwa kiasi gani? Sijawahi kuona magaidi wapumbavu kama hawa ambao wako tayari kushindia mihogo kwa Dada yao ili wamfurahishe mwajiri waliyefamiana muda mfupi.
Good kama umetambua na KUKUBALIANA na hilo, then tegemea lolote kwenye uamuzi wa mwishoMatokeo yalienda Kama CCM walivyopanga
Shahidi anasema kapona, mbona hakurudishwa kazini?ninachoshangaa kuwa mtu ambaye aliaachishwa kazi kwa kurukwa na akili sasa anakuwaje tena shahidi.an insane person.
Pole sana. Hakuna ajira iliotolewa na Mbowe, ni maelezo yalio tungwa ili kuianzisha hii case. Urio sio polisi, kwenye case hii anapewa kazi ya kurecruet walinzi (magaigi?)Na inaonesha jinsi gani Mbowe siyo makini pia, utaajiri vipi insane person awe mlinzi wako wa karibu?? So mkiti wa chama kikuu cha upinzani alikuwa anaokota okota tu vibaka mtaani ili wamlinde bila kuwafanyia vetting yeyote? Mtu mzembe kama huyu ndiyo anataka apewe hii nchi aongoze? Stupid kabisa...
Ni hulka ya sisi binadamu kujifariji hata mambo yanapokuwa magumu. Ukweli ni kuwa kesi hii ni mbaya kwa Mbowe. Kwa ushahidi huu kuchomoka ni ngumu.Tayari baadhi ya Wadau wa Maendeleo, akiwemo Mwakilishi wa Ubalozi wa Canada wamewasili Mahakamani.
Hadi saa 3:30 asubuhi hii Watuhumiwa walikuwa bado hawajaletwa Mahakamani.
====
Hatimaye Mbowe na wenzake wameletwa Mahakamani
Jaji Joachim Tiganga ameingia Mahakamani
Wakili wa serikali Robert Kidando anatambulisha Jopo lake
1. Robert Kidando
2. Nassoro Katuga
3. Ignas Mwanuka
4. Esther Martin
5. Tulumanywa Majigo
6. Jenitreza Kitali
Wakili Peter Kibatala anatambulisha Jopo Lake
1. Peter kibatala
2. Jeremiah Mtobesya
3. Michael Mwangasa
4. Nashon Nkungu
5. Dickson Matata
6. Alex Massaba
7. Jonathan Mndeme
8. Hadija Aron 9.
Idd Msawanga
Jaji anaomba Kuwaona Washitakiwa wote 1,2,3 na 4
Wanainuka Kwa kutajwa kwa Namba
Wakili wa Serikali anaomba kesi Kuendelea na Shahidi yupo tayari Lakini Kabla ya Kuendelea anaomba kufuatilia kuhusiana mabadiriko yaliyopalekea mpaka Mheshimiwa Jaji Kuja mwingine kwa mujibu ya kifungu cha 299 CPA (Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai).
JAJI: Upande wa utetezi
Peter Kibatala: hatotatumia Haki ya kumuita tena Shahidi kwa kesi Inayoendelea hapa.
Jaji anaandika.
JAJI: wote mnafahamu na mlikwepo siku ya tarehe 20 mwezi huu na Jaji aliyekuwepo alielekeza Jaji Mwingine atakuja kuendelea na Kesi hii, Na Jaji Mwingine Ndiyo Mimi, kwa mujibu wa sheria ya mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20 Kifungu cha 299.
JAJI: Kwamba Upande wa Utetezi Mnahaki ya a Kumuita tena shahidi kwa kuwa Mmesema hamna nia nitawaruhusu Upande wa Jamhuri Kumuita sasa Shahidi wao tuweze Kuendelea. Mawakili wote Wanainuka ishara ya Kukubaliana na Uamuzi wa Jaji na Kupokea Maelekezo ya Mahakama.
Wakili wa Serikali anatoka Kwenda Kumuita Shahidi wa leo.
Mahakama ipo Kimya
ACP KINGAI anaingia na Kupanda Kizimbani.
Robert Kidando Wakili wa Serikali anamtaarifu Jaji Kuwa Shahidi amefika.
JAJI: Majina yako Tafadhali
SHAHIDI: ACP Ramadhan Kingai
JAJI: Unakumbuka Uliwahi Kufika Mahakamani, ukaapishwa kutoa Ushahidi, Mahakama inakukumbusha Upo chini ya Kiapo hicho. SHAHIDI: sawa Mheshimiwa
JAJI: Mtakumbuka Mawakili kuwa Siku ya Tarehe 20 Jaji alipokea Kielelezo, baada ya Kupokelewa Kinatakiwa Kusomwa Mahakamani. Naomba Kuanzia hapo Shahidi akabidhiwe Kielelezo aweze Kusoma Kielelezo.
WAKILI WA SERIKALI: Soma Sasa Kielelezo Kuanzia kurasa ya kwanza.
SHAHIDI: Adama Kasekwa anaishi Chalinze Maelezo ya Onyo Chini kifungu cha Sheria ya Makosa ya Jinai Sura ya 20. MIMI kingai nakuonya wewe Adam Kasekwa
SHAHIDI: Ulazimishwi kusema lolote Pia unaweza Kualika Ndugu, Jamaa au Mwanasheria Kushuhudia utoajo wako Maelezo. Mtuhumiwa akasaini na Mimi nikasaini.
MAJIBU YA ONYO
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo..
MIMI Adam Kasekwa anaonya na Kingai Chini ya Kifungu cha 24 cha Sheria Mwenendo wa Makosa ya Jinai Silazimishwi na yoyote Kutoa Maelezo yangu. Je, Upo tayari Kutoa Maelezo Yako.
Jibu, Ndiyo Nipo tayari.
Shahidi anasoma kielelezo: Maelezo yamechukuliwa Katika Ofisi ya RCO ilala MIMI Adam Kasekwa Nimezaliwa Mkoa wa Mbeya Wilaya ya Ileje... Mwaka 2011 nilijiunga na Recruting Maktopora. Nikachaguliwa Kujiung na Mafunzo Ukomando 92KJ.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Mwaka 2014 niliteukiwa kwenda kituo cha Msangani Kujifunza ulinzi, amani na nikachaguliwa Kwenda DR Congo. Mwaka 2017 nilimaliza Mkataba na kurejea Nilipata malipo na Kumuoa Mke wangu Lilian ambaye naishi naye Mpaka Leo.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Nimepata naye Mtoto Mmoja. Nilirudi nikaa Miezi 6 kazini Nikaugua Ugonjwa wa aKili Nikaachishwa kazi na kulipwa mafao ya Millioni 4 na Laki 6.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Je unamfahamu Luteni Denis? Ndiyo, nilikuwa Mkinga Mawasiliano hayapatikani. Niliporudi nikaambiwa mwenzangu ananitafuta.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Niliporudi nyumbani nilimpigia Simu Mwenzangu Mohammed Ling'wenya Kwamba Kuna kazi ya VIP protection. Akaniambia inabidi twende Morogoro Kumuona Luteni Urio. Tulipoenda akatuambia Kuna kazi ya VIP protection ya kumlinda Freeman Mbowe
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Akatupatia TSh 21,000 nauli ya Kwenda Moshi. Siku hiyo hiyo tulirudi Chalinze na kuanza Safari ya kwenda Moshi Tulipokelewa na Dereva wake anayeitwa Willy Alitupokea na Pick Up Nyeupe yenye maandishi ya M4C.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Tukaenda Mpaka Kwenye Hotel Ya Mheshimiwa Mbowe Huko tulimkuta Khalfani Bwire aliyetutambulisha kwa Mbowe, "Mkuu wale Vijana tuliowaagiza ndiyo hawa hapa." MBOWE akatueleza Kuwa Sabaya anamvuruga sana na anamvuruga wapiga Kura.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Kwamba anawatisha Wapiga kura wake kiasi cha Kuhatarisha Kurudi kwake. Na kwamba, akatuelekeza tumdhuru Kwa Njia yoyote. Akatuelekeza Maeneo yake ya Moshi na Arusha.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Tulipanga kumdhuru kwa Spray Spray ya sumu alitafuta Mohammed Ling'wenya
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Siku inayofuata tulikuwa Mimi na Mohammed na wanachana wawili siwakumbuki Majina Baada ya Kufika Dar es Salaam Tulimfikisha Mheshimiwa Mbowe Nyumbani
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Akatukabidhi TSh Laki 2 kwaaajili ya Kununua Nguo. Kwa sababu Kesho yake tulikuwa tunampokea Mheshimiwa Lissu. Na Siku ya tarehe 27 Julai Mbowe alitutumia Kila moja TSh 78 Elfu ya Nauli Ya Kwenda Moshi.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: SIKU ya Tarehe 01 August Tulienda Moshi Tukamkuta Mbowe akiwa na Khalfani Bwire Akatuelekeza Kuwa tufanye ile kazi yake Haraka Akatuelekeza Maeneo anayokaa Sabaya kama vile Milestone PIA Akatuelekeza Tuje DSM, Kuchoma Vituo Vya Mafuta.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Kwamba yeye anatachochea maandamano ILi Serikali ionekane Imeshindwa Kuandaa Uchaguzi. Tulienda Maeneo ya Boma Ng'ombe Njia ya kuelekea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kumfuatilia.
Siku ya terehe 03 tulienda Maeneo ya RAU madukani kwa ajili ya kubana Matumizi. Kwa sababu Mheshimiwa alituachia Pesa Laki Moja na Nusu kwa ajili ya kukaa, isingetosha. Tulienda Kukaa kwa Dada yake kukaa kwaajili ya Kubana Matumizi.
Swala la Kupanga Ugaidi ni la kweli Na swala la a kukutwa na Silaha ni la kweli Wakati Polisi wananikamata pia walinikuta na Heroine Baada ya kuchukua Vitu hivyo Askari walisaini na Mimi nikasaini na Polisi walichukua Vitu hivyo kwenda Central
Baada ya Maelezo hayo Adam Kasekwa akasaini Na Mimi Kingai nikasaini Baada ya Kuchukua Maelezo hayo Muda ulikuwa ni saaa tatu.
Wakili wa Serikali: ACP Kingai Kutokana na Maelezo uliyoyasoma hapa mahakamani Yeye alikuelza nini Kutokana na Maelezo Uliyoyasoma Mahakamani Shahidi: alikiri kuwa anamfahamu Luteni Urio. Alikiri Kupewa Maelekezo ya kazi kutoka kwa Mheshimiwa Mbowe
Shahidi: Alikiri Pia alipewa Maelekezo ya kazi Kutoka akwa Mbowe Kupitia Kwa Luteni Deni Urio. Alikiri Pia kuwapo Moshi tarehe 24 Mwezi wa 07, 2020
Shahidi: Alikiri Pia kuwapo Moshi na wenzake Mohammed Ling'wenya na Mwenzake aliyemtaja Kwa Jina la Kakobe. Baada ya Ufutailiaji tukamfahamu ni Moses Lijenje. Alikiri Pia kufanya Mkutano yeye na wenzake wanne.
Yeye Mwenyewe, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya, Moses Lijenje (Aliyemtaja Kwa Jina la Kakobe) Khalfani Bwire na Freeman Mbowe
Wakili wa Serikali: kwa Mujibu wa Mkutano huo nini kiliendelea. Shahidi: Mbowe alitoa Maelezo kuwa Sabaya anamfanyia Vurugu, (Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai)
Wakili wa Serikali: kitu gani Kingine alikueleza Shahidi: Mtuhumiwa alikiri Kupewa Pesa 150,000/= kukidhi Mahitaji kipindi watakapokuwa hapo Moshi.
Wakili wa Serikali: tueleze Shahidi kuhusiana na kilichofuata Shahidi: Alikiri Kuwa Siku ya Tarehe 01 Mwezi wa Nane saa 11 Alfajiri kabla ya Safari ya Kuja DAR ES SALAAM Aliwaelekeza wamdhuru Ole Sabaya.
Shahidi: Akawaonyesha Picha ya Ole Sabaya Kupitia Simu yake ya mkononi Aliwapa Maelekezo Kufanya kazi hiyo na Kwamba baada ya hapo atawataka warudi Dar es Salaam. Alipanga kuwapa kazi ya kwenda Kulipua Vituo Vya Mafuta. Alipanga kufanya Vurugu kwenye masoko.
Mtobesya: OBJECTION Naomba Shahidi ajielekeze Kwenye kikichoandikwa kwenye Statement Mambo ya Kituo cha Mafuta na Masoko havijatajwa.
Jaji: Kwahiyo a some?
Mtobesya: ajielekeze kikichoandikwa hata kama ana Rudia Kuelezea, Sheria inasema Statement itajielezea Yenyewe.
JAJI: Upande wa Mashitaka
Wakili wa Serikali: Sahihi Mheshimiwa tutarekebisha.
Wakili wa Serikali: Alikueleza Lengo ilikuwa ni nini
Shahidi: Lengo ni Serikal ionekane imefeli Alikiri Pia kukamatwa na Polisi Siku ya tarehe 05 Mwezi wa 08, 2020 akiwa Rau Madukani.
Alikiri Pia kukamatwa na Pistol aina ya Ruvern ikiwa na Risasi 03.
Shahidi ACP KINGAI: Alikiri kukamatwa na Kete 58 za Madawa aina ya Heroine.
Wakili wa Serikali: baada ya kuwa umeandika Maelezo hayo, yeye ulimpeleka wapi kwa Siku hiyo.
Shahidi ACP KINGAI: ilikuwa Siku ya tarehe 07 Mwezi wa 08, 2020 nilimrudisha Mahabusu.
Wakili wa Serikali: Shughuli gani Nyingine ili endelea baada ya Shughuli hii
Shahidi ACP KINGAI: tuliendelea na Upelelezi ya Kuwatafuta watuhumiwa wengine. Maeneo ya Chang'ombe tulimkamata Khalfani Bwire.
Wakili wa Serikali: Kwa tuhuma Gani
Shahidi ACP KINGAI: Kwa tuhuma hizi hizi za Kula Njama kutenda Matendo ya Ugaidi.
Wakili wa Serikali: nini kiliendelea
Shahidi ACP KINGAI: nikimtaka Khalfani Bwire aandike Maelezo yake
Wakili wa Serikali: elezea Kuhusu Kumkamata kwake
Shahidi ACP KINGAI: baada ya a kuwasiliana na Askari aliyekuwa kwenye Pointi akiwa kwenye gari, tukielekeza Gari iingie Kituo cha polisi Chang'ombe. Tukawa tumeingia pale na Inspector Mahita na ASP Jumamne.
Jaji: ASP nani? Shahidi: Jumanne
Wakili wa Serikali: baada ya Kumkamata Mlimpeleka wapi
Shahidi: tuliekeza Superitendent Lukangira wa hapo hapo Chang'ombe. Hii ni baada ya Mtuhumiwa kutuelekeza hana Makazi hapa Dar es Salaam ni Mkazi wa Ngerengere.
Wakili wa Serikali: Nia ya Kuuliza kwake ni wapi ilikuwa ni ya nini
Shahidi: nia ilikuwa kufanikisha Shughuli za kiupepelezi
Wakili wa Serikali: baada ya Lukagingira kuandika Maelezo yake nini Kilifuata
Shahidi: Tukawa tunaendelea Kufuatilia Makazi yake, Tofauti na Taarifa alivyokuwa ametoa yeye kwakuwa tulijua haiwezekani awe kila Siku anaenda Ngerengere.
Wakili wa Serikali: Wakati Unapata Taarifa ana makazi Wilaya ya Temeke, elezea Sasa Maelezo yalikuwa yanaandikiwa wapi
Shahidi: Maelezo yalikuwa yanachukuliwa Kituo cha Polisi Chang'ombe na Mimi niliweka Bass Central polisi (Ilala).
Wakili wa Serikali: baada ya Kutoa Maelekezo Hatua Kuchukua Maelezo Isimame, nini kilifuata
Shahidi: tulipata Taarifa Mtuhumiwa anakaa Temeke Makangarawe, Tuliungana na Detective John wa Temeke na RCO kwa ajili ya kwenda Kumpekua Makazi yake.
Wakili wa Serikali: Mlienda sehemu ipi haswa huko Mkangarawe
Shahidi: Ule Mtaa Jina Limenitoka
Wakili wa Serikali: Uliwezaje Kuutambua sasa
Shahidi: tukielekezwa na Watu hadi Nyumba alipokuwa amepanga Mtuhumiwa.
Wakili wa Serikali: Elezea sasa hiyo Shughuli ilifanyikaje na Khalfani Bwire alikuwa wapi.
Shahidi: Tuliongozana na Mtuhumiwa, Tukamtafuta Mwenyekiti wa Ule mtaa, Tukamkuta na Mwenye nyumba aliyempangisha Khalfani Bwire na hata Mke wake alikwepo.
Wakili wa Serikali: huyu Mwenyekiti ni wanini?
Shahidi: Ni Mwenyekiti wa Mtaa
Wakili wa Serikali: Nini Kilifuata
Shahidi: Nilimuelekeza ASP Jumanne Kwa Kushirikiana na Detective John Kutoka Ofisi ya RCO Temeke na kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa Mtaa na hata Mke wake.
Wakili wa Serikali: Elezea sasa Katika Upekuzi huo Mlikuta nini?
Shahidi: Vitu mbalimbali vilipatikana kama Uniforms za JWTZ, Masharti ya JWTZ, Tshirt za JWZT, name tags za kwake za JWTZ.
Wakili wa Serikali: baada ya Kupata Uniforms na Vifaa Mbalimbali nini Kilifanyika baada ya Kupata Vitu hivyo.
Shahidi: Viliorodheshwa katika Hati ya Uchukuaji Mali. Wakati wa Upekuzi tulikuta Kidaftari kilichokuwa na Ramani na Majina ya Vituo Vya Mafuta.
Wakili wa Serikali: baada ya kuorodhesha kitu gani kilifanyika
Shahidi: baada ya Kuwa Viliorodheshwa yaliandikwa Majina ya walioshuhudia Upekuzi huo. Pia wakasaini Hati ya Uchukuaji Mali. Mtuhumiwa pia alisaini Hati ya Uchukuaji Mali na aliyepekua alisaini Hati hiyo.
Wakili wa Serikali: Baada ya Kukamilisha Hati ya Uchukuaji Mali, Kitu gani Kiliendelea
Shahidi: Nilikuwa nimeelekeza Mashahidi walioshuhudia waandikwe Maelezo pale pale
Wakili wa Serikali: baada ya Kukamilisha
Shahidi: Tulichukua Vitu tulivyo orodhesha na Mtuhumiwa akarudishwa a kituo Cha Polisi.
Wakili wa Serikali: Kituo gani cha Polisi Shahidi: Chang'ombe
Wakili wa Serikali: Baada ya kumrudisha Kituo cha Polisi Chang'ombe Kitu gani pia Kiliendelea.
Shahidi: Mtuhumiwa tulimkamata na Kidaftari chenye Ramani ya Vituo Vya Mafuta Dar es salaam, Soko la Kilombero Arusha.
Tukachukua Sampuli za Miandiko ya Watuhumiwa wote. Lakini pia tuliendelea na hatua ya kuwatafuta watuhumiwa wengine
Wakili wa Serikali: watuhumiwa gani wengine Mlikuwa mnawatafuta
Shahidi: Watuhumiwa wengine tuliokuwa tunawafutilia ni Mtu alikuwa anaitwa Gabriel, Lijenje, Malima, Khalid na Jamaa Mmoja anaitwa Kaaya.
Wakili wa Serikali: nini hatima ya hao mliokuwa mnawafuatilia
Shahidi: Ukimuondoa Mtu Mmoja anaitwa Malima, Watuhumiwa wote walifikishwa mahakamani.
Wakili wa Serikali: vipi kuhusu moses Lijenje Shahidi: bado hatujafanikiwa Kumpata
Wakili wa Serikali: Hapa Mahakamani kuna Washitakiwa Wanne inakuwa je hao wengine hawapo Mahakamani kama Walifumgukiwa Mashitaka
Shahidi: walifutiwa Mashitaka baada ya Kuonekana Ushahidi hakuwa wakutosha ukilinganisha na wenzao.
Wakili wa Serikali: ACP kingai katika Ushahidi wako tangu Mwanzoni umezungumzia kukamatwa Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Khalfani Bwire Vipi ukamatwaji wake Mshitakiwa wa Nne.
Shahidi: Freeman Mbowe alikamatwa 21 July 2020 akiwa Mwanza
Wakili wa Serikali: Kwa tuhuma gani
Shahidi: Kwa tuhuma hizi hizi
Wakili wa Serikali: Wakati Unatoa Ushahidi wako Ulizungumzia kukamatwa hawa wengine Mwaka 2020 na huyu 2021 elezea Ilikuwa je hapa Mahakamani.
Shahidi: Tulikuwa tunajirishisha haswa uhusika wake. Tulikuwa bado tunaendelea Kufuatilia mawasiliano Na Uchunguzi wa Forensic ambao ulikuwa unahusiana na Shauri hili
Wakili wa Serikali: Sababu ukamataji ulifanyika 21 July Mwaka 2020, ni lini taarifa zilifahamika rasmi.
Shahidi: Zilifahamika Mwanzoni July 2020
Wakili wa Serikali: wakati anakamatwa Upelelezi ulikuwa umefikia Hatua gani
Shahidi: Upelelezi wetu kwa muda huo tunamkamata ulikuwa umekamilika.
Wakili wa Serikali: Upelelezi wa aina gani ulikuwa unaendelea kwa Mshitakiwa nne
Shahidi: Tulifanya Forensic na Divices za Kieletronic tuliokuwa tunafuatilia Kujiridhisha dhidi yake na Tuhuma zilizokuwa zinamkabili.
Wakili wa Serikali: wakati Unatoa Ushahidi wako Mwanzoni ulisema Ulielezea Kuwa Umelekeza kufungua Jalada la Tuhuma za Kigaidi.
Shahidi: Kulingana na Taarifa ambazo tulikuwa tumezipata kwa Luteni Urio na aina Ya Vitendo vilivyokuwa Vimepangwa na Watuhumiwa Ilikuwa ni Kudhuru Viongozi wa Serikali, kufanya Vurugu sehemu zenye watu wengi, Kulipua Vituo Vya Mafuta, Hata Miti kwenye highway kukatwa Kuzuiwa Magari yasipite, Hasa katika Barabara ya Morogoro kwenda Iringa.
Wakili wa Serikali: Ukatafsiri ni Vitendo gani
Shahidi: Vitendo vyenye kuleta hofu kwa Wanachi Kujiona hawapo salama, Ni Vitendo vinavyoleta Tafsiri la Shitaka la Ugaidi
Wakili wa Serikali: ulisema katika Taarifa ya Luteni Urio ulisema walipanga Kuonyesha kuwa Nchi haitawaliki.
Mtobesya: OBJECTION kaka yangu Wakili Msomi ajielekeze Kwenye fact siyo Opinion Maana huyo ni Shahidi wa Fact, He is doing too Much Sasa Maana Mwanzo tulijua ameteleza.
Wakili wa Serikali: Sawa Mheshimiwa Jaji nitaomba nijielekeze sawa Sasa.
Wakili wa serikali: Vitendo hivi vilipangwa Vifanyike wapi
Shahidi: Mwanza, Moshi, Dar es Salaam na Arusha
Wakili wa Serikali: Vilikuwa Vifanyike Lini
Shahidi: Kabla ya Uchaguzi wa Mwaka Jana
Wakili wa Serikali: ni hayo tu Kwa sasa Mheshimiwa Jaji
Jaji: Upande wa utetezi
Mtobesya: Asante Mheshimiwa Jaji nitaomba niendelee kwa Niaba ya Mshitakiwa wa kwanza.
Mtobesya: ni sahihi Shahidi wewe ulikuwa ni sehemu ya waliokuwa wanahusika na upelelezi wa Kesi hii
Shahidi: ni sahihi
Mtobesya: ni sahihi kuwa Baada ya kupokea Maelezo kwa DCI BOAZI mkafungua Jalada
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji ni lini Mlifungua Jalada
Shahidi: Yalikuwa Majalada Mawili la upelelezi na Kesi
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Lilifunguliwa Jalada la Uchunguzi
Mtobesya: Uchunguzi au Upelelezi
Shahidi: yote ni yale yele labda useme unataka Jalada gani
Mtobesya: wewe Ndiye unayetoa Ushahidi
Shahidi: Sawa Mwanzo Lilifumguliwa Jalada la Uchunguzi wa Kula njama. Ilikuwa July Mwaka Jana.
Mtobesya: yote Mawili Mlifungua kwa Pamoja au Tofauti
Shahidi: Kuna Utaratibu wa Kiupelelezi labda kwa sababu ujawa mpelelezi Ndiyo Maana Unahangaika Kuna Jalada la Awali la Uchunguzi lakini unapopata Taarifa unafungua Jalada la Kesi ya kula njama Lilifunguliwa na Mkaguzi wa Polisi Msaidizi anaitwa Swila
MTOBESYA: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kabla hamjawakamata Watuhumiwa Mlikuwa mmekusanya Taarifa zipi kwa wakati huo
Shahidi: Taarifa za kutaka kuwadhuru Viongozi wa Serikali, Kufanya Maandamano ya siyo na Kikomo, Taarifa za Kukata Miti na Kufanya Uporaji Magari yasipite na Kutaka Nchi isitawarike
MTOBESYA: kwa hiyo hizo Taarifa ndiyo zilitengeneza Kosa la Kula Njama
Shahidi: Sahihi
Mtobesya: Mwambie Mheshimiwa Jaji hizo Taarifa Mlizipata kabla au Baada ya Kumchukua Maelezo Mshitakiwa wa Pili
Shahidi: Kabla
MTOBESYA: kabla ya Kesi Ndogo unakumbuka ulisema Urio aliwapatia Taarifa kuwa Vijana wamepatikana, Unakumbuka ulisema tarehe Ngapi.
Shahidi: Ilikuwa tarehe 04 Mwezi wa Saba Mwaka Jana
MTOBESYA: wakati unaelezea (Kusoma) unakumbuka Kielelezo ulipata wasaa wakujua Urio alishiriki Vipi katika swala hili?
Shahidi: sijaelewa Vizuri
MTOBESYA: Statement hii ambayo unasema uliandika unakumbuka Urio alishiriki namna gani?
Shahidi: naomba Jaji anisomee anapoparejea
Jaji: labda tuweke, Ushiriki wa urio ulikuwa Vipi
Shahidi: Urio ameshiriki kwa kuwatafuta Vijana, ameshiriki kuwapatia nauli na ameshiriki Kutafuta Vijana waliofukuzwa Jeshi
Mtobesya: Umesema kwenye Maelezo alifanya hayo Tarehe ngapi
Shahidi: Sikumbuki tarehe
MTOBESYA: sasa nije kwenye Maelezo uliyoyachukua, kwa ajili ya Kumbukumbu Unakubaliana na Mimi Kuwa kuna namna tatu za Kuchukuliwa Maelezo. moja, Kwa Anateyetaka Kuchukuliwa Maelezo kuomba Karatasi na kalamu na kuandika Mwenyewe. Pili, kwa anayehojiwa kuongozwa Tatu, kwa njia ya Maswali na Majibu Wewe ukichagua Njia gani?
Shahidi: Mimi nilitumia Maswali na Majibu
Mtobesya: naomba niishie hapa
Wakili Malya: naomba Kielelezo (Statement) Mahakama inampatia John Malya
Wakili Malya: Unasimu ya mkononi
Shahidi: Ndiyo
Wakili Malya: unaweza kututajia EMEI namba ya Simu yako
Shahidi: Hapana Siwezi
Wakili Malya: kwanini..?
Shahidi: Sijaamua kuishika
Wakili Malya: Una ya mtu yoyote wa Karibu yako unayoikumbuka
Shahidi: Hapana
Wakili Malya: sasa Katika maelezo Adam alikutajia EMEI namba Kutoka wapi
Shahidi: Alikuwa na kikaratasi
Wakili Malya: Ulizungumza kwamba Mshtakiwa alikuwa na kikaratasi?
Shahidi: Sikuzungumza
Wakili Malya: ni sahihi unapoandika Maelezo unaandika kwa usahihi kabisa
Shahidi: Sahihi Kabisa
Wakili Malya: kwa uelewa wako Unapotaja Sheria, kwa Mbele Mwaka Unatajwa, Maana ya Kuwa na Miaka katika Sheria.
Shahidi: Mimi siyo Mwanasheria
Wakili Malya: Nafahamu wewe siyo Mwanasheria ila Umeandika Mwenyewe Vifungu Vya Sheria ili Mtu ajue Haki yake
Shahidi: Ndiyo nafahamu. Sasa Unatoa somo
Wakili Malya: Kwa hiyo wewe Unaweza kuandika Mwaka wowote tu.
Shahidi: am not aware of It
Wakili Malya: kwa hiyo wewe Unaweza Kuandika Sheria na Mwaka ukaweka Wowote tu
Shahidi: Hapana naweka na Sheria
Wakili Malya: na Mwaka kama imefanyika amendment Zake? Sasa Kwa Maelezo hayo uliyoyashika Tusomee hapa.
Shahidi: Cap 20 REV 2018
Wakili Malya: sasa hiyo Sheria Hakuna. Wewe umechukua Maelezo ya Onyo kwa Sheria ambayo haipo, Unasemaje kwa hilo
Shahidi: Hiyo ni Typing Error kwa sababu imechapwa. Ile niliyoandika kwa Mkono wangu huenda sikuandika hivi.
WAKILI mallya: wakati unaisoma hapa Mahakamani Ulisema hapa kwamba hii siyo au ulikariri ukawa unaisoma tu Hapa
Shahidi: kwenye eneo hili Onyo Chini ya Kifungu Cap Rev 2002 badala Ya kusomeka 2018.
Wakili Malya: kwa hiyo ulipaswa Kusomeka Vinginevyo siyo hiyo
Shahidi: Ndiyo
MALYA: ushawahi Kusikia Kiongozi wa Polisi Liberatus Barrow aliuwawa
Shahidi: Ndiyo Wakili Malya: aliuwawa?
Shahidi: Ndiyo WAKILI
Mallya: waliomuua Walikamatwa Ndiyo
Shahidi: Ndiyo
WAKILI mallya: walishitakiwa na Makosa gani?
SHAHIDI: mauaji
WAKILI mallya: Lakini Kumdhuru Sabaya ni Ugaidi?
Shahidi: kuleta Vurugu kwenye Masoko, Kukata Miti Barabara, Kuzia Magari yasipite ni Vitendo vingeleta hofu na Wasiwasi Vitendo hivi Vinaashiria ni Vitendo Vya Ugaidi.
Wakili Mallya: umerudi Viongozi sana Ukimtoa lengai Ole Sabaya Kiongozi Mwingine nani..?
Shahidi: ni Maelezo ya Adam Kasekwa, Siyo ya kwangu
Wakili Mallya: ulipomkamatia Adamoo Moshi na Kilichokufanya usichukue Maelezo Moshi ni sababu zipi
Shahidi: Sababu za Kiupelelezi
Mallya: wakati Unatoka Moshi ulipitia Njia ipi ya Chalinze au Bagamoyo
Shahidi: Msata
Mallya: ulitoka Msata kwenda Central Njia kuna Mbweni na Oysterbay kwanini uliamua kwenda Central
Shahidi: Sababu za Maelezo na Pili Ndipo kesi ilipofunguliwa
Wakili Mallya: Wewe kwa sasa ni RPC KINONDONI Je unafahamu kuwa Kinondoni inajitegemea
Shahidi: Ndiyo, zikiwa Chini ya Kanda Maalum Dar es Salaam
Wakili Mallya: ulieza Mahakama Kwanini Huyu achukuliwe Maelezo Temeke Mkoa Mwingine wa Kipolisi na kwanini hakusafirishwa kama wenzie kuja Mkoa wa Ilala
Shahidi: Hapana sikueleza
Wakili Mallya: umesema Yalifunguliwa Majalada mawili
Shahidi: Ndiyo
Wakili Mallya: nani alifungua hayo Majalada Shahidi: Inspector swila
Wakili Mallya: Umemtaja Sabaya, Alikuwa Mkuu wa Wilaya wa wapi Vile?
Shahidi: Hai
Wakili Mallya: je pale Hai Pana Ofisi ya Mkuu wa upelelezi?
Shahidi: Ndiyo
WAKILI: mallya Je Kilimanjaro Kuna Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi?
Shahidi: Ndiyo
Wakili Mallya: Ni hayo tu
JAJI: naomba Tubreak Kwa Lisa limoja Tutarudi hapa Saa 7 na Dakika 20
Jaji anatoka
Mpaka sasa saa saba na nusu, Jaji hajaingia.
Mahakama imerejea
Wakili Robert Kidando anaomba Kumtambulisha Wakili Nasorro Katuga
Jaji: nilipo Break tulikuwa tumemaliza Maswali ya Dodoso ya Wakili wa Mshitakiwa wa Pili, Nipo sahihi..? Wawakili wa Pande zote Mbili wanaitikia, NDIYO
Jaji: namruhusu Wakili wa Mshtakiwa wa tatu aendelee,
WAKILI MATATA
Matata: Shahidi Ni sahihi kwamba Maagizo ya Kushughulika na Kesi hii ulipewa na DCI
Shahidi: Ndiyo
Matata: Ni kweli kwamba Urio ndiye aliyekupa Taarifa kuwa kuna Makomandoo amewatafuta kuwapeleka kwa Mbowe, kusaidizana naye kutenda Uhalifu. Shahidi: Kweli
Matata: Urio huyo huyo ndiye alikupa Taarifa kwamba alikuwa anatoa fedha za Kuwawezesha Makomandoo
Shahidi: Ndiyo
MATATA: na Ukasema Mambo hayo yote yangefanyika Mwaka Jana Kuanzia Mwezi wa Saba.
MATATA: nitakosea Nikisema Mbowe Kuwapa Fedha Makomandoo Yalifanyika Mwaka Jana
Shahidi: Kweli
Matata: Utakubaliana na Mimi Mbowe amekamatiwa Mwaka huu Mwezi wa Saba Shahidi: Kweli
Shahidi: Ndiyo
Matata: amekamatwa akiwa Mwanza
Shahidi: Ndiyo
MATATA: Mbowe alishiriki Uchaguzi Mwaka Jana akigombea Jimbo la Hai?
Shahidi: Kweli
Matata: Kwa Nyakati tofauti Mbowe amekuwa nchini
Shahidi: Kweli
Matata: Leo Umeeleza Mahakama Kwamba hamkumkamata kwa sababu mlikuwa Mnafanya Upelelezi na Uchunguzi wa Ki-Forensic
Shahidi: Kweli
MATATA: Utakubaliana na Mimi kwamba huo Uchunguzi Umeisha lini
Shahidi: Nimeeleza Mahakama
MATATA: Utakubaliana na Mimi Kwamba huo Uchunguzi wa Kiforensic Ulikuwa Unahusu nini
Shahidi: nimeeleza
Matata: Wakati unahojiwa na Wakili umeeleza huo Uchunguzi wa Kiforensic ulihusisha nini
Shahidi: Nilieleza Kwamba ni Vifaa Vya Electronics
MATATA: nikisema Mbowe Mmemkamata Mwanza 21 July 2020 kwa sababu ya kutaka Kufanya Kongamano la Katiba nitakuwa Nimekosea
Shahidi: Si kweli, Utakuwa Umekosea
MATATA: Mheshimiwa Jaji ni hayo tu
Jaji: Wakili wa Mshtakiwa wa Nne
Peter Kibatala: Asante Mheshimiwa Jaji
Kibatala: Shahidi Katika Statement Uliyosoma kuna Mambo yanamgusa Mshtakiwa wa Nne
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Kwanini huwa tunataka Kifungu Mahususi kinacho mpa Haki zake Mshitakiwa katika Caution Statement.?
Shahidi: Ni takwa la Kisheria
Kibatala: kwa hiyo unafahamu kuwa kuna matakwa yake ili zoezi likamilike kuwa la Kisheria
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unafahamu Kuwa unapokosea Kifungu cha Sheria Jambo Lote linakufa.
Shahidi: Inategemea
Kibatala: Ukikosea Sheria yenyewe?
Shahidi: inaweza kuwa Fatal
Kibatala: Sheria katika Kielelezo P1 imepatiwa au Imekosewa
Shahidi: slip of the pen
Kibatala: hiyo Slip of the pen Mpaka Mawakili wanakuongoza Kwa Mujibu wa "Oxygen Principle" kwamba turekebishe hata kwa pen
Shahidi: Hapana
Kibatala: Unafahamu Kuwa Kukiri Kwa Mshitakiwa kunapaswa Kuongozane na Vitu Vingine
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je umetaja hapa Mahakamani vielelezo gani Vingine kama vinaunga Mkono Kukiri Kwa Mshtakiwa wa Pili?
Shahidi: Maelezo yake
Kibatala: ndiyo hayo Maelezo Yanatakiwa yafungwe Mkono na Premises zingine tuorodhesheee
Shahidi: Maelezo ya Luteni Denis, Kuhusu Kukata Miti na Kutaka Kufanya Vurugu.
Kibatala: Umemueleza Jaji sehemu yoyote kwamba ulienda huko Morogoro Mpaka Iringa Kuona Miti iliyotakiwa kukatwa.?
Shahidi: Hapana Wala sijaenda
Kibatala: Umetaja Maandamano yalitakiwa kufanyika wapi hadi wapi
Shahidi: Hapana sijasema
Kibatala: Kuhusu Mwanza Pia Maandamano yalitakiwa yaanze Point gani hadi Point gani tarehe fulani?
Shahidi: Sijamwambia
Kibatala: Kuhusu Kilimanjaro ulitaja sehemu yoyote?
Shahidi: Hapana sijamwambia
Kibatala: Umemtaja Mheshimiwa Jaji Maandamano yalitakiwa kuanzia wapi hadi wapi na ajenda ya maandamano
Shahidi: nilisema ili Kuonekana Nchi haitawaliki
Kibatala: Kuna sehemu umemwambia Jaji tarehe ya Maandamano
Shahidi: Hapana
Kibatala: Umezungumzia kuwa alipanga kuwepo yeye personally
Shahidi: Sikusema
Kibatala: ulitaja Vituo vilivyotakiwa Kuchomwa
Shahidi: Ndiyo nilivitaja
Kibatala: ndiyo Mwambie Mheshimiwa Jaji ulitaja wapi na wapi
Shahidi: Nakumbuka nilitaja Big Bon Kariakoo, Big Bon Sinza na Total Morroco
Kibatala: Unakumbuka Upo Chino ya Kiapo, Maana kazi yangu ni Kuuliza Maswali swala la Uongo au La! wanajua watu wengine
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je baada ya planning Huko Moshi Je washitakiwa walifanikiwa Kuja Dar es Salaam Kuja kutekeleza hilo
Shahidi: Walikuwa Baada ya Kuwakamata
Kibatala: Nauliza Mshitakiwa wa Nne alitoa Maagizo Moshi akaja Dar es Salaam Kuja Kutekeleza hayo Maagizo
Shahidi: Dar es Salaam tuliwakamata kabla hawajatekeleza.
Kibatala: Mliwakamata na nini ambacho Mtu anaweza Kukihusisha na Ulipuaji wa Vituo Vya mafuta
Shahidi: kwa Upande wa Kuchoma Vituo Vya Mafuta sikuwakamata na Kitu chochote
Kibatala: Uliwakamata na Kifaa gani kinachohusisha Kukata Miti
Shahidi: Sikuwakamata na Kifaa chochote
Kibatala: Mshitakiwa wangu wa Nne ulimkamata na Kipeperushi cha Maandamano?
Shahidi: Hapana
Kibatala: we Polisi Mzoefu Miaka 18 ya Upelelezi Kazini, najua Siyo Mwanasheria ila Unasimamia Sheria je Unafahamu Mtu anapokiri anatakiwa kukiri Kila Kipengele anachoshitakiwa
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Ulizungumza Chochote Kuhusu Mshitakiwa Mbowe kuwapo Morogoro kati ya Tarehe 1 May na 20 August 2020
Shahidi: Sikuzungumza
Kibatala: Ulizungumza Katika ya Tarehe 01¬May 2020 na 20 August 2020 kuwa washitakiwa watatu walikuwa Arusha
Shahidi: Ndiyo nilizungumza ila siyo Leo
Kibatala: kwa ufahamu wako kama Mpelelezi Mkuu umewahi Kugundua kuwa Freeman Mbowe na Watuhumiwa wenzake Mkoani Morogoro
Shahidi: na Mbowe Hapana
Kibatala: Waliwahi Kukutana Mkoa wa Arusha
Shahidi: Sijafahamu
KIBATALA: Waliwahi Kukutana Mkoani Dar es Salaam
Shahidi: walikuja Dar es Salaam, walikuwa Pamoja Tarehe 26 July 2020.
Kibatala: hayo yapo katika maelezo ya Kukiri uliyoyasoma?
Shahidi: Yapo Ndiyo
Kibatala: Naomba Mahakama nimkabidhi P1 anitafutie eneo hilo
Jaji: tutajie kurasa
Shahidi: "Kesho yake tulirudi Dar es Salaam, Tukiwa na Mheshimiwa Mbowe na wanachana Wengine ambao sikuwafahamu" That Means walikutana
Kibatala: Sitaki tafsiri yako, Tusomee ambao Mshtakiwa amesema walikutana
Jaji: nafikiri kuna sehemu hamkutani, nafikiri anatafsiri kuwa kuna Wakati walikuwa wote Dar es Salaam, We unamaanisha nini?
Kibatala: "Hati ya Mashitaka inasema walikuwa wamekaa Kikao, Nitafutie alipokiri kuwa walikaa Kikao"
Shahidi: hiyo specifically Kikao sikueleza
Kibatala: ooohhhh Sasa Umeelewa
Kibatala: Sheria inayounda Shitaka Unatakiwa kuitamka kikamilifu ili haki za Mshitakiwa ziwe zimekamilika, Unafahamu..?
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Je unafahamu sub section mbili zote zinazozungumzi hilo
Shahidi: hiyo ni Mpaka Niperuzi
Kibatala: aahhhhhh Sawa Ngoja nimpatie Sheria
JAJI: anacheka, Sasa atafahamu Vipi kuwa yenyewe
Kibatala: nawapa kwanza Kaka zangu Mawakili wa Serikali waithibitishe
Wakili wa Serikali: Ndiyo yenyewe
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Iwapo Maelezo ya Onyo ulitaja Kifungu cha Sheria cha Kwanza na Cha Pili (Subsection)
Shahidi: Subsection Sikutaja
Kibatala: Kwa ufahamu wako wewe Kutokutaja Subsection zinakuja zimeathirika au hazijaathirika
Shahidi: Hiyo ni Curable Irregularity
Kibatala: ulitoa ufafanuzi huo Kwa Jaji ili afanye hiyo CURE
Shahidi: sikutoa Kibatala: Hawa Washitakiwa 2 wanashitakiwa Kushiriki Vitendo, Mkutano wa Kuongea Vitendo Vya kigaidi Ndiyo Hati ya Mashitaka inavyosema.
Shahidi: Sahamani naomba Niione
Kibatala: Ooh Sawa hii hapa
Kimya Kinatawala Shahidi anasoma
Wakili wa Serikali: Sahamani Mheshimiwa Jaji na sisi kabla ajajibu tunaomba tuione
Kibatala: Ooohh sawa Mheshimiwa Jaji wanahaki hiyo
Wakili wa Serikali: Ndiyo yenyewe Mheshimiwa
Jaji Shahidi: Ndiyo yenyewe
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kuwa Iwapo alishiriki Mkutano, Ugaidi ilikuwa sehemu ya Maelezo yako ya Onyo.
Shahidi: Nilimuonya kwa Vitendo
Kibatala: Ulimuonya kwa Meeting au hukuonya
Shahidi: Si Kumuonya
Kibatala: Terrorists Meeting ni Shitaka Namba ngapi
Shahidi: 4
Kibatala: Ndiyo ambalo hukumuonya Adamoo
Shahidi: Ndiyo sikumuonya
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kama Ulimuonya kwa Kupatikana na Mali
Shahidi: Kwa Vitendo Vya kigaidi
Kibatala: Twende Shitaka la Tano, kwa Kupatikana kwa hiyo Mali, Si bado tunakubaliana kuwa kunapaswa Kuungana na Mambo Mengine si Tuna kubaliana
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama Ulifanya Forensic ya DNA au Finger Prints kuwa ni Kweli ilikuwa Chini ya Umiliki wake
Shahidi: hapo unazungumzia kumilili..?
Kibatala: Ulizungumzia Kuhusu kwamba Umefanya Uchunguzi wa Finger Prints
Shahidi: Hapana Siku fanya Finger Prints
Kibatala: hii Kesi tangu ianze kuanzia kuwakamata na Muanze Upelelezi ni muda gani
Shahidi: Miezi 08
Kibatala: Kwa hiyo kwa Miezi 08 hamjawahi Kufanya Finger Prints
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unakubaliana na Mimi Kuwa DNA ni Njia ya Kisasa Ya kuthibitisha Umiliki, na Jinai
SHAHIDI: ndiyo
KIBATALA: Umezungumzia Chochote Kuhusu DNA analysis
Shahidi: Hapana Mheshimiwa
Kibatala: Umemwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa Adamoo amepata wapi hii Bunduki
Shahidi: Adamoo hakusema
Kibatala: Nikiangalia Kielelezo Cha Mahojiano nitaona Hilo swali?
Shahidi: Hapana Nilimuuliza Kama Mimi tu
Kibatala: Wakati anakamatwa Adamoo alikwambia walikuwa na Moses Lijenje, Je alikwambia wakati wa Mahojiano ya Kisheria au Nje Ya Kisheria
Shahidi: kivipi
Kibatala: Uliipata baada ya Kumuhoji Adamoo..?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulimuhoji kwa mdomo AU kwa Maandishi
Shahidi: kwa Mdomo
Kibatala: Unakubaliana na Mimi kwamba hilo kitendo cha Kumuhoji Adamoo hutakiwi Kukifanya kwa Mujibu wa Sheria
Shahidi: nilikuwa namuhoji Kupata upelelezi
Kibatala: Unakubaliana na Mimi kwa Mujibu PGO ulipaswa kwanza Umpe haki zake Mshitakiwa wa 2 wakati Mpo Moshi
Shahidi: Usichanganye Vitu
Kibatala: Miye nakuhoji unachosema wewe, Kwamba Unakubaliana kuwa kuna Mahojiano Yalifanyika Moshi
Shahidi: Ndiyo nilifanya Mahojiano ya Mdomo
Kibatala: lakini Mliwasafirisha kutoka Moshi Kuja Dar es Salaam Kuja Kuwahoji.?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: ilikuwa Muda gani
Shahidi: Muda uleule
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji pia kama Ulimuhoji Mohammed Ling'wenya Akiwa Moshi kuhusu Moses Lijenje
Shahidi: Ndiyo nilimuoji pia na Maelezo ni yaleyele
Kibatala: nimesikia kuwa Leo Umemtaja Kakobe kuwa ndiyo Moses Lijenje
Shahidi: kwa Maelezo yao Ndiyo WAMESEMA hivyo.
Kibatala: Shahidi nakukabidhi Maelezo hayo ya Kielelezo ya P1 kuwa Adamoo anasema KAKOBE ndiyo Moses Lijenje
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Sikumbuki kama niliandika
JAJI: Kibatala Umemwambia atumie muda Mwingi iwezekanavyo kutafuta hilo, nakukumbusha Muda ni wa Mahakama.
Kibatala: Mheshimiwa Jaji samahani sana nilipigiwa, Kama ningekuwa mwangalifu ningesema Kwa Ruhusa ya Mahakama
Kibatala: Nitafutie sehemu katika Maelezo kuwa Mshitakiwa wa Pili amekiri Bastola ni ya kwake
Shahidi: Hakuna Mheshimiwa Jaji
Kibatala: Nitafutie katika Maelezo ambayo Mshtakiwa amekiri kuwa Bastola hiyo alitaka kutumia kumdhuru Sabaya, Kutumia kwenye Maandamano au Kutumia Kukata Miti
Shahidi: Hilo Mheshimiwa Jajo hakuna
Kibatala: Nitafutie Mstari au haya yoyote ambayo Mshtakiwa wa pili anasema kuwa uniform za JWTZ walitaka kuzitumia kwa ajili ya Ugaidi
Shahidi: Hakuna kwa sababu Mshitakiwa sikumkuta na Uniforms
Shahidi: Uliza Maswali Sensible Bwana
Mawakili wa Utetezi Wote wananyanyuka
KIBATALA: No No No No Kaeni Mwacheni
Kibatala: Nataka Useme kama Kuna sehemu katika maelezo kuna sehemu umesema kuhusu Uniform
Shahidi: Hapana
Kibatala: Nina Swali la Lijenje kijinga ila Nivumilie Je kuna sehemu kuna Maelezo ya Nyongeza? Kuhusu Kuchukua Sampuli za Miandiko
Shahidi: Hatukua na haja hiyo
Kibatala: Kwa hiyo Mshitakiwa wa Pili hakuna anapozungumza kuhusu Mwandiko
Shahidi: Hakuna
KIBATALA: Naona Umeokoa muda sasa
Kibatala: Iliwachukua muda gani Kuwashitaki wakina Malima Mpaka Mkagundua kuwa hapakuwa na Ushahidi wa kutosha.
Shahidi: Tuliwashitaki Mwishoni Mwa Mwaka Jana
Kibatala: Ikumbushe Mahakama Mteja wangu tangu Mumkamate anamuda gani Vile
Shahidi: Kama Miezi 4
Kibatala: Fedha zilitumwa katika Ushahidi wa Mshitakiwa wa Nne kwenda kwa watu wengine
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na Rekodi za SMS za Mshitakiwa zipo sehemu ya Ushahidi? Nazungumzia Mshitakiwa wa Nne
Shahidi: Hapana hakuna
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa Ulichukua Device za Watoto wa Mheshimiwa Mbowe
Shahidi: Ndiyo nilichukua Kibatala: Mpaka Leo Unazo
Shahidi: walizidai nikatoa Maelekezo
Kibatala: Mpaka Leo unaongea Wamerudishiwa au bado?
Shahidi: sijui nilitoa Maelekezo
Kibatala: lakini wewe Ndiyo Mkuu wa Uangalizi
Shahidi: Kwa sauti ya Hasira anasema SIYO MUANGALIZI
Kibatala: Umeeleza Makamani Kuhusu Kumtaarifu Sabaya
Shahidi: Hiyo sikusema
Kibatala: Je hapa Mahakamani Umetoa Taarifa kuwa Uliwapa Taarifa kuwa Kuna Jambo Zito kama hilo Kwenye Kamati za Ulinzi na Usalama
Shahidi: Hapana Sikuwapa
Kibatala: Je, wewe Binafsi umeshawahi Kumuhabarisha Rais Samia Suluhu kuhusu Kesi hii
Shahidi: Hapana
Kibatala: Je unataarifa kwamba Washitakiwa wameshafungwa na Kuchukuliwa hata kabla ya Kesi Kuanza
Shahidi: Unamaana gani Kuuliza swali Kama hilo
Kibatala: Maana najua Mimi, We Jibu swali
Shahidi: Sijui
Kibatala: Umeongelea hapa Kuhusu ya Battle Confusion
Shahidi: Mimi siyo Practitioner
Kibatala: Wewe Mpaka unamuhoji Mshitakiwa ambaye anarekodi ya Kuumwa Ugonjwa kama huo
Shahidi: alikuwa ananijibu Vizuri na Kwamba alikuwa ameshapona.
Kibatala: umesema akiwa anaondoka Chalinze yeye akijua anaenda Moshi kufanya VIP PROTECTION
Shahidi: Mheshimiwa labda sasa tusomewe
Kibatala: anasoma "Nilienda hadi Nyumbani nikaambiwa Kuna Kazi ya VIP protection, ambayo anajua zaidi Luteni Urio"
Shahidi: Ndiyo lakini siyo Maelezo yote.
Kibatala: Tafuta Katika Statement hiyo Mshtakiwa anapo Sema Kuwa Urio alikuwa anamtafuta Kwa Vitendo Vya Ugaidi
Shahidi: Hakuna Sehemu ambayo Adamoo amesema hayo
Kibatala: hata Huko Mbele kuna sehemu amesema Urio alimtafuta kwa ajili ya Kutenda Vitendo Vya Ugaidi?
Shahidi: Hapana lakini walikutana na Mbowe
Kibatala: Sijakuuliza kuhusu Mbowe nimekuuliza kuhusu Urio
Shahidi: Sasa Usinibane Kuniuliza Maswali ambayo siwezi Kutoa Maelezo Alikuwa anaficha ficha
Kibatala: Wewe ndiye Umesema Urio alikuwa Willing Informer Leo amekuwa Mtu wa kuficha ficha tena.?
Shahidi: Usiniulize kuhusu URIO mimi
Kibatala: Kwanini sasa Nisikuulize Kuhusu URIO, Wewe Ndiye umemleta Urio Mahakamani.
JAJI: kibatala Unamchanganya sana Shahidi, Kumleta maana pia Kumbeba
Kibatala: sahamani Mheshimiwa Jaji kama kaelewa hivyo
Kibatala: Unakubaliana na mimi, Mpaka wanaenda Moshi Mlinzi wa Mheshimiwa Mbowe alikuwa ni Willy
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mshitakiwa wa Pili ameenda Moshi 26 /07 /2020. Wakati Mashitaka yenu yanasema tangu Mwezi 05 alikuwa ameshiriki Vitendo Vya Ugaidi
Shahidi: Miye sijui hayo
Kibatala: Unakubaliana na Mimi kwamba Mpaka Mshitakiwa wa pili anaenda Moshi alikuwa hajui Mambo ya Ugaidi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: kuna sehemu inayosema kwamba tulienda naye kwenye Kikao Cha Chama wakarudi. Je kuna sehemu inafafanua kuwa walirudi wapi?
Shahidi: Hapana hakuna, ila Mwenye akili timamu anajua walirudi wapi
Kibatala: Miye sina Akili timamu
Kibatala: kitendo cha Mkuu wa Wilaya kushusha Bendera za Chadema inaruhusiwa Kisheria?
Shahidi: Hapana hairuhusiwi
Kibatala: Kwamba Kufanya Preventive measures kwa Kuzuia Mtu kushusha Bendera za Chadema ni Ugaidi huo
Shahidi: Nimeshatoa Maelezo kuwa Jinai haiwezi Kuzuiwa na Jinai
Kibatala: Jibu swali Langu, Sasa swali langu halikuwa hivyo
Kibatala: Je Kitendo cha Kuzuia kwamba wasishushe, Mbele ya Mungu ni Ugaidi
Shahidi: halikuwa hivyo
Kibatala: hapa kuna Maelezo kuwa "Ametisha Wapiga Kura, amefanya hujuma na Kutisha Wapiga kura, ikiwemo Kuiba Kura" haya Umeyaandika wewe Je uliyaamini au huyaaamini Haya Maneno
Shahidi: Mimi sijui Sasa
inaweza Kuwa sijaamini
Kibatala: tutatakiwa Kuhoji wengine kama wewe uliyeandika Maelezo huyaaamini wao wametoa wapi Nguvu ya Kuleta Mahakamani
Shahidi: Mheshimiwa Sijazungumzia
Kibatala: Huyo ambaye alikuwa ampatie Ling'wenya Spray ya Sumu umezungumzia hapa, huyo Mtu
Shahidi: sijamzungumzia, Lakini upelelezi Unaendelea
Kibatala: kwa hiyo kuna Siku unaweza Kutuletea Mtuhumiwa Mwingine
Shahidi: Ndiyo inawezekana
Kibatala: Okey Mwenye Mahakama anasikia unachosema
Kibatala: Kuna sehemu inasema "Baada ya Kumfikisha Mheshimiwa Nyumbani Kwake" katika hiyo Statement Uliyorekodi ametajwa au hakutajwa
Shahidi: huyo atakuwa ni Mheshimiwa Mbowe
Kibatala: Nakuuliza hapo Kwenye Statement huyo Mheshimiwa ametajwa?
Shahidi: hajatajwa
Kibatala: tulikuwa na Mohammed Je hapo kwenye Statement Mohammed ametajwa kuwa ni Mohammed Nani
Shahidi: sijataka
Kibatala: Kitendo Cha kwamba tulipewa pesa Kwenda Kununua Nguo ili Kumpokea Tundu Lissu, Je kutumia hizo pesa Kununua Nguo ni Kosa la Jinai
Shahidi: Lengo halikuwa hilo
Kibatala: Mimi sitaki Lengo nauliza Mlichoandika hapa
Shahidi: Lengo haswa lilikuwa ni Kufanya uhalifu, hii ilikuwa Kama incentives
Kibatala: hiyo incentives ndiyo walipanga Kununua Nguo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kuna sehemu ambayo amekiri kwamba Hiyo pesa ilikuwa kwa ajili ya Kutenda Ugaidi
Shahidi: Hapana
Kibatala: "Kesho tukaenda Kumpokea Lissu, Mimi na Mohammed Je huyo Mohammed ametajwa ni nani?
Shahidi: Sikutaja ila atakuwa ni Mohammed Ling'wenya
Kibatala: Ndiyo ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa Uligundua kuwa ni Mohammed Ling'wenya.?
Shahidi: Hapana sikusema
Kibatala: na hii 78,000 ya nauli inajumuishwa kama pesa ya kufadhili Ugaidi..?
Shahidi: Inawezekana ikawemo
Kibatala: Wewe Upelelezi wako Uligundua nini
Shahidi: Imo
Kibatala: Kuna Mahala Mshitakiwa anasema pesa ilitumika Kwenda Kununua Spray ya Sumu
Shahidi: Hapana
Kibatala: Kuna Mahala popote Mshitakiwa anasema alipewa Pesa na Mbowe kwa ajili ya Kufadhili Maandamano
SHAHIDI: Hapana
Kibatala: Kuna Mahala Popote Mshitakiwa alikiri Kuwa alifika Arusha..?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Kuna Mahala Popote kwamba Mshitakiwa anakiri alipewa Pesa Kwenda Kumdhuru Sabaya
Shahidi: Hapana
Kibatala: Kuna Mahala Mshitakiwa wa pili amekiri kuwa alishawahi Kwenda Arusha
Shahidi: Kwenye Maelezo haya Hakuna Sehemu kama hiyo
Kibatala: Katika Maelezo Mshitakiwa alikuwa na Kete za Madawa ya Kulevya 52 Je yanatosha Humu?
Shahidi: Sikutaja 52
JAJI: tujielekeze Katika hii Kesi
Kibatala: Katika hayo Madawa DNA analysis ilifanyika
Shahidi: Hapana Kibatala: finger prints ilifanyika.?
Shahidi: haikufanyika
Kibatala: Huyu Moses Lijenje yupo wapi? tunapomzungumzia leo
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: hata Kama amekufa hufahamu
Shahidi: sifahamu
Kibatala: Mpaka wakati huu unapozungumza hujawahi kuhangaika Kujua yupo wapi?
Shahidi: Hapana sijahangaika
Kibatala: Ulishawahi Kuuliza Jeshi Kuhusu Uwepo wa Moses Lijenje
Shahidi: Sasa Mtu kafukuzwa, Jeshi litajuaje?
Kibatala: ndiyo Ni Jibu swali Langu hata Kama la kijinga
JAJI: halipaswi Kuwa swali la Kijinga, anaweza Kilipuuza au Mimi nisiandike likija la Kijinga
Kibatala: Asante Mheshimiwa Jaji ni la Msingi
Kibatala: Shahidi Uliwashirikisha Jeshi Kuhusu Lijenje
Shahidi: Ndiyo tuliwashirikisha
Kibatala: Nimeona umezungumzia kuhusu Uniforms Za Jeshi, Una utaalamu wa Kujua Uniform za Jeshi?
Shahidi: hata Nikiona naweza Kujua hili Jeshi la Wapi, Yemen, Nepal au India.
Kibatala: Je unafahamu Kuwa Nguo za Jeshi zimetungiwa Kanuni
Shahidi: hilo sifahamu
Kibatala: Kama hufahamu Kanuni unajua wapi Mambo ya Nguo za Jeshi
Shahidi: Kwa Kuona
Kibatala: kwa kuwa Leo Upo Ngoja Nikuulize, Je unajua kuwa Mtuhumiwa wa Kwanza alitekwa Kwenye Daladala akiwa na Maafisa wa zamani wa Jeshi Nyuma yake na Mbele yake akawekwa Mtu Kati, Yeye akaomba wasimdhuru wala wasimpige wakayamalize Polisi.
Shahidi: hayo ya kwako
Kibatala: umesema mara ya kwanza Mshitakiwa wa Kwanza alichuliwa Maelezo akiwa wapi.?
Shahidi: Chang'ombe
Kibatala: Unafahamu nini Kuhusu Kupeleka Mshitakiwa Tazara
Shahidi: Miye Mambo ya Tazara siyajui
Kibatala: kwa hiyo tukienda Kwenye Detention Register tunaweza Kuwa na Kuwa alikuwa Chang'ombe
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unafahamu Detention Register ili iwe Genuine Unatakiwa ionekane Vipi nje na Ndani
Shahidi: Hapana sifahamu
Kibatala: Kwanini hufahamu na wewe ni Afisa wa Polisi kwa Muda wa Miaka 18.
Shahidi: kuna Maswali unataka Kunibana na Mimi nakwepa.
Kibatala: mimi kazi yangu Kuuliza Maswali tu, Wenyewe walikaa wataamua, tumeambiwa tukuulize kila kitu kwa sababu hatuna Uhakika kama utakuja tena
Shahidi: Ndiyo basi Unilishe maneno
Kibatala: Wewe Kwa uzoefu wako Kuna Kesi yoyote ile ambayo mnataarifa jambazi anataka Kuvamia Benki A, B, C na Mkamuacha Jambazi azurure Mtaani? ipo?
Shahidi: Ndiyo Ipo
Kibatala: umeitolea Ushahidi hapa Mahakamani?
Shahidi: Hapana
Kibatala: kabla ya Kumkamata Mbowe katika Kongamano la Katiba Mwanza, mlikuwa mnajua kuwa Mbowe anasafiri Nje ya Nchi.
Shahidi: Ndiyo tulikuwa tunajua
Kibatala: Wewe Mtu Mzima Inaingia akilini Mtu ana kesi ya Ugaidi mnampeleleza Mkamruhusu asafiri Mpaka arudi Mwenyewe
Shahidi: Ndiyo inawezekana tulikuwa tuna Mpelelezi Ndani na Nje ya Nchi.
Kibatala: Ulishawahi Kutaarifu Mamlaka zingine nje ya Nchi kuwa anayekuja Ni Gaidi
Shahidi: Hapana hakuwa Flight Risk
Kibatala: umesikiliza Mahojiano ya BBC na Rais Samia
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Rais wa Nchi amesema alipokuwa BBC kuwa Freeman Mbowe alichelewa Kukamatwa kwa sababu alikimbia Nje ya Nchi
Shahidi: Naomba Jaji aniruhusu Kujibu hilo swali.
Kibatala: Mimi nahitaji hilo Jibu, Labda Mahakama inizuie, Lakini Mimi nataka Unijibu.
Wakili wa Serikali: OBJECTION, Mheshimiwa Jaji naomba tuangalie Sheria kama zinaruhusu au Kutubana.
Wakili wa Serikali 02: MAJIBU anayotaka ni Kuhusu Mahojiano, aulizwe Maswali ambayo yeye yanamhusu.
JAJI: Peter kwa hoja hizo Unasemaje Kibatala: Mheshimiwa Jaji samahani Sana, Tulifungua Kesi ya kikatiba namba 21 ya Mwaka 2021 Wakalamikiwa walikuwa DPP, na Mwanasheria Mkuu. JAJI mgeta akasema hivi; Mahakama yake inafungwa haiwezi Kuingilia Kesi hiyo, na Kama kuna hoja anaomba Ziwasilishwe katika kesi ya Jinai inayoendelea Katika Mahakama Kuu.
Jaji: Sasa huyu amekuja Kama Executive Order au Kama Shahidi
Kibatala: Ikumbukwe Mahakama ipo Majaribuni pia kwamba sasa Rais ameshasema
Jaji: Naona Shahidi unamtreat kama Shahidi anayekuja Kuwakilisha Muhimili, Wakati tumemuapisha kuja Kutoa Ushahidi Kwenye Jambo alilolifanya
Kibatala: Kama hutojali uamuzi Ule tumekatia Rufaa, Mimi ukiniambia hapa Siyo Mahali pake nitatumia hiyo Statement.
Jaji: Mengine yote unaweza Kumuuliza, lakini tusimuilize Swali ambalo kasema Mtu Mwingine.
Kibatala: Nauliza kama Forum hapa Ikifungwa tukienda Kwingine wasisiseme hatukulileta hapa.
Jaji: Hatuwezi Kusema kwa hii Trial Mlango pia Umefumgwa, Nafahamu kwamba mnamashahidi mnaweza Kuwaleta mkawahoji kuhusu Kauli hizo.
Kibatala: Je Shahidi Unafahamu kuwa Freeman Mbowe alikimbia Nchi kwa Kukwepa tuhuma za Ugaidi
Shahidi: Hilo si fahamu Kibatala: Unakubali kuwa ulikwepo wakati Mnampekua Freeman Mbowe
Shahidi: Mi nilikuwa Nje tu zoezi lilisimamamiwa na Superitendent Mwakabonga
Kibatala: ilikuwa saa ngapi.? Shahidi: ilikuwa saa 3 Mpaka saa 4
Kibatala: kwa ufahamu wako Sheria Inasemaje Kuhusu Kupekuliwa Usiku.
Shahidi: Nikuulize wewe Kibatala:
Kibatala Shahidi Mbona swali lipo Fair
Shahidi: Tunaruhusiwa kupekua hata Usiku.
Kibatala: uliwahi Kumkamata na Kumpekua Mbowe Kabla
Shahidi: Hapana Kibatala: kwa hiyo ni Mwaka Mmoja
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: ile situation Report ambayo Makamanda wanabadilishana Taarifa na Makamanda wengine Kipolisi inaitwaje
Shahidi: Situational Report
Kibatala: Sasa tuambie kuwa Mpaka Kamanda Wa Mwanza anamkamata Mbowe
Shahidi: Mimi sikwepo nilikuwa Busy, Sikuwa najua kilichotokea Mwanza
Kibatala: kwa hiyo Kibona Hakukwambia lolote kuhusu tulio la Mwamza
Shahidi: kwanza sisi tuna riport kwa IGP siwezi Kujua kinachotokea kwa Mkoa Mwingine.
Kibatala: Maelezo hayo uliyatoa Kwenye Ushahidi
Shahidi: Hapana
Kibatala: Kwanini ulimtamkia Mshitakiwa Freeman Mbowe kuwa "wewe si Unajifanya Unajua Sana Katiba Mpya, Sasa tunakupa Kesi ya ugaidi Safari hii hutoki"
Shahidi: Hayo ni Maneno wameyapanga kwa Maslahi yao wenyewe kama Unavyosema Nipo Chini ya Kiapo, hapa Pia Quran ipo.
Kibatala: Kiongozi gani Mwingine wa Upinzani Ushawahi Kumkamata
Shahidi: Sijawahi
Kibatala: Lissu Je
Shahidi: Sijawahi Kumkamata ila Niliwahi Kushughulika n a kesi zake
Kibatala: Ngapi.?
Shahidi: Mbili
Kibatala: ni hayo tu Mheshimiwa jaji
Mndeme: Shahidi Unafahamu kuna Sheria ya Vyama Vya siasa
Shahidi: Nafahamu
Mndeme: unafahamu kuwa inaruhusu Mkutano na maandamano
Shahidi: Nafahamu
MNDEME: unafahamu Maandamano ni Kosa au Siyo Kosa
Shahidi: Yakiwa na Kibali siyo Kosa
Mndeme: utakubaliana Kutofautiana Kisiasa Siyo Kosa la Jinai
Shahidi: Ndiyo
Mndeme: Kutoipenda Serikali ni Maoni ya kisiasa.
Shahidi: ni Maoni ya Mtu Binafsi
Mndeme: kwa hiyo hatakuichukia Serikali ni Maoni Binafsi
Shahidi: Inategemea na Mtu
Mndeme: ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.
Wakili wa Serikali: Naomba Tuahirishe hadi Kesho Asubuhi Saa 3 ilituweze Kumalizia
Jaji yupo Kimya Na Mahakama Ipo Kimya kidogo Bado shahidi Yupo Kizimbami
Jaji: Upande wa Utetezi mnasemaje
Kibatala: Hatuna Pingamizi lakini tunaomba Kesho Waje na Shahidi Mwingine kwa kuwa Re examination hata Ikiwa ndefu haitozidi Masaa 2 tukianza Saa 3 Asubuhi
Jaji: sawa, ikiwezekana mje na Shahidi Mwingine.
Jaji: basi Maombi ya ahirisho yamekubaliwa kama ambavyo yameombwa na Upande wa Jamhuri na hayajapingwa na Utetezi. Basi tunahairisha Mpaka kesho saa tatu tutakapo endelea na Shahidi Namba Moja na baada ya Shahidi namba Moja tunategemea Kuendelea na Shahidi namba 2.
Jaji: Washitakiwa wataendelea Kuwa Ndani Mpaka hapo Kesho.
Jaji: ananyanyuka.
Policeccm ni waliofeli frm 4,yani hawajawahi kua na akili na haitatokea wawe na akili,watu wanaishi kwenye mabanda ya bati na bata zao...ni watu wenye roho mbaya,wachafu,wauaji,wezi,majambazina pesa walizokuwa wanapewa kwa ajili ya ujira wao ndo inashangaza zaidi eti watu waue Sabaya, walipue kila mahali afu wanapewa laki2, laki na 50 hadi haziwatoshi wanaenda kubana matumizi kwa dada ake mbowe!!!
Hao ni wale uvccm njaa team mcherengwa,wanaoishi kwa kuombaombaSasa kama shahidi wa kwanza anayetarajiwa kupigilia msumari katika kesi ushahidi wake ni huo wa kakipande cha karatasi, amekiri kabisa hana Fingerprints, wala DNA, hao mashahidi wengine 18 watakuja na vielelezi gani kama sio kutupotezea muda tu?
Pelekeni kesi haraka mtoe hukumu acheni kutupotezea muda. Mpelelezi mwaka mzima unakuja na kielelezo hiki kama ushahidi? oneni aibu!
Hayo yalipaswa kua miongoni mwa maswali yanayoulizwa na mawakili wa utetezi.Cha ajabu maswali wanayo uliza
Kesi Ikiwa mbaya na Mbowe akifungwa ni furaha kwako na familia yako .MUNGU atakuwa amejibu maombi yako.Familia yako itaishi vizuri ,familia yako haitokaa ihangaike ki uchumi Wala kiafya maana mbaya na mchawi MBOWE aliyekuwa anazuia ajira ,aliyekuwa anazuia maisha Bora atakuwa amefungwa.Ni hulka ya sisi binadamu kujifariji hata mambo yanapokuwa magumu. Ukweli ni kuwa kesi hii ni mbaya kwa Mbowe. Kwa ushahidi huu kuchomoka ni ngumu.
either tuamue kuamini ushahidi ni wauongo au ushahidi niwaukweli.....Je tunajuaje ushahidi ni wauongo au waukweli?..... huyo Urio aliyetajwa naye yupo kwenye kutoa ushahidi?,
Figure za hela zinazotajwa wahusika kupewa mbona hazilingani na kazi tunayoambiwa walipewa?..
Sijaona mahala popote wahusika wanapewa kazi kwa makubaliano fulani, Je wahusika waliahidiwa nini baada ya hiyo kazi ya hatari?...hivi mtu anaweza tu kufanya kazi ya hatari kama hiyo bure?...maswali ni mengi ngoja tuendelee kujiuliza..