Heshima kwa wote.

Nafuatilia hii kesi ya Mbowe na wenzake watatu najikuta nacheka na kusikitika kwa wakati mmoja.

Mosi Magaidi wanampango wa kwenda kulipua vituo vya mafuta na kukata Miti hawana Mabomu wala mapanga au Cheingso.

Pili katika hati ya mashtaka hakuna ushahidi kwamba walikuwa na mkutano au kulikuwa na ushahidi wa kilichopangwa na kupangika.

Tatu kulikuwa na mpango wa kumdhuru Sabaya lakini hakuna aina yoyote ya silaha iliyokamatwa kama kielelezo

Aina hii ya kesi ipo Tanganyika pekee yake yaani Polisi anaweza kukamata na kuandaa mashtaka bila ushahidi wenye mashiko na ukakaa mahabusu muda wa kutosha.

Ipo haja Police wetu kurejea upya darasani na kujifunza namna bora ya kuandaa mashtaka, kupeleleza na hatimaye kupelekea kesi Mahakamani, kinyume chake ni kupoteza fedha za walipa kodi buuure.

2977025_AIgmal.jpg
Wenyewe wanaoifahamu vyema kesi hii wanakwambia hivi:

1. "Mbowe siyo Malaika", wakionyesha wanajuwa mengi yaliyopangwa na Mbowe na wenzake, yatakayowashangaza watu yatakapotolewa mahakamani.

2. Mwingine katangazia dunia kabisa, kwamba "washiriki wenzake tayari yalishahukumiwa na wanatumikia vifungo vyao. Mbowe pekee yake hakuhukumiwa kwa vile alikimbia na kwenda kujificha Nairobi." Kwa hiyo ni zamu yake Mbowe kupata haki yake mahakamani!

Na ushahidi wenyewe utakaomweka hatiani, ndio huo ambao umewasilishwa mahakamani na shahidi wa kwanza wa Jamhuri.

Hawa watu wote hawaoni hata haya, soni, aibu mbele za watu wengine wenye akili timamu, wenye uwezo wa kufikiri. Hivi kweli inahitaji mtu ajue sheria kama msomi wa fani hiyo kuweza kuona yanayoendelea kwenye mahakama hii?

Tukiweka pembeni uovu wa matakwa yao, tunaloweza kusema hapa ni jinsi nchi yetu ilivyoporomoka, hata katika ule uwezo wa kutunga uongo tu unaoweza angalau kuonekana kama una ukweli ndani yake.
Lakini hawa wakubwa hili siyo tatizo kwao, maadam wanao uwezo wa maguvu, kufanya lolote wanalojisikia wanaweza kulifanya.

Ikiwapendeza, Mbowe anaweza kuendelea kukaa ndani kwa muda wote wakati hawa wakiendelea kuwa madarakani kwa nguvu.

Wakati huo huo, tusiwasahau wahusika kama DCI, ambaye anaruhusu kesi kama hii kwenda mahakamani!

Nchi hii tumefika pabaya sana sasa!
 
magaidi watatu walipanga kulipua sheli nchi nzima kwa laki 6. tuuite nini kama sio ushuzi
Bora Hitler mpango wake ungefanikiwa tu, Africa yote iwe shamba la katani. Ugaidi unafadhiliwa kwa laki 6??? Wakati hiyo haitoshi hata kuwa mahari ya demu aliyekuwa mlezi wa wana kitaa. Kmmae walahi
 
Uneona eh? Halafu polisi wanaochunguza jambo wasilojua litafanyika lini hawatoi taarifa kwa kamati za ulinzi za wilaya/mikoa, OCD au RPC wa maeneo husika!! Wanajua mpaka vituo vitakavyolipuliwa lakini wasiwataarifu wamiliki wala kuvifunga! Sababu ni rahisi, walikuwa wanajua jambo hili halipo. La sivyo wangechukua tahadhari! Watu wanamshutumu Kibatala lakini anajaribu kujenga narrative kuwa swala la ugaidi ni la kufikirika zaidi kuliko kupangwa!!

Binafsi ninadhani itakuwa interesting kupata kumsikia Dennis Urio. Yeye hasa ndio shahidi muhimu. Imenishangaza Kingai kusema Adamoo mpaka anakwenda Moshi alikuwa hajui habari za Ugaidi - akiwa huko kabla ya kuonana na Mbowe alikamatwa. Kwanini anashitakiwa kwa jambo ambalo hakuhusika nalo???
Ni vitu ambavyo havi make sense kabisa yaan unaona wamejiandaa tu kunyanyasa hakuna mtuhumiwa apo ni basi na CHIEF HANGAYA naye katulia anafikiri dunia hii ni yake, yaan matukio hatarishi kiasi iko yanapangwa na watu wanne nchi nzima afu mkubwa wao wanamwacha huru adi uchunguzi unakamilika baada ya mwaka ndo anakuja kukamatwa, muda woote huo hajafanya tukio hata moja
 
Tuweke akiba ya maneno. Hata Ile kesi ndogo Kwa macho ya wengi ilikuwa jaji asipokee kile kilelezo lakini Jaji siyani alikipokea kile kielelezo na akajiyoa kusikiliza kesi. Mbaya zaidi hakukuwa na cha kumfanya.

Kwa hiyo huo ushahidi wa Kingai tuuangalie Kwa jicho la tahadhali sana. Ikumbukwe hawa majaji hawaaminiki tena.
Mkuu 'Mzee Chayai', ilibidi nitafakari kidogo kuhusu uamzi wa Siyayi (hawa watu naona sana hata kuwapa hadhi zao za 'Jaji), pengine nawe ukiangalia kutoka upande huo, itakulazimu uuone mwanga kama nilivyouona mimi.

Yule Siyayi angekubaliana na upande wa utetezi, maana yake kesi ingeishia hapo, au siyo? Naona yeye aliona hana ubavu huo, na hasa baada ya kupewa cheo kama rushwa kwake.

Sasa sijui tena hapa, na ushahidi huu unaoendelea kutolewa mahakamani kwenye kesi ya msingi, kama bado huyu aliyepewa zigo bado ataona haijalishi uwepo wa sheria!
 
RPC Kingai ameeleza hatua kwa hatua bila kuacha shaka jinsi Freeman Mbowe alivyopanga kumuuwa aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai Ole Lengai Sabaya kwa kutumia perfume ya sumu kwa madai kuwa Sabaya alikuwa anatishia nafasi ya Mbowe kuendelea kuwa mbunge wa jimbo la Hai.

=======

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Ramadhani Kingai akisoma maelezo ya mshtakiwa wa pili katika kesi ya uhujumu uchumi, Adam Kasekwa amesema mtuhumiwa huyo alisema Freeman Mbowe alipanga kumdhuru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya.

Katika ushahidi alioutoa leo, Oktoba 26, 2021 katika Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Kingai amesoma maelezo ya mtuhumiwa huyo kwamba Mbowe alisema Sabaya anahatarisha nafasi yake ya kuendelea kuwa mbunge wa Hai.

Ifuatayo ni sehemu ya maelezo ya mshtakiwa Adamu kama yalivyosomwa na RPC Kingai:

“Mbowe alituelekeza tufuatilie nyendo zake na tumdhuru kwa spray ya sumu. Ling'wenya alifuatilia mtu wa kupata sumu. Tarehe 27 tulirudi Dar na magari mawili pamoja na Mbowe na mlinzi wake.

“Baada ya kufika Dar tulifikishwa Mikocheni mimi na Ling'wenya tulipewa Sh200,000 tujiandae. Baadaye tulipewa nauli turudi Moshi. Agosti Mosi saa 11 alfajiri Mbowe alituita akasema tutekeleze maelekezo ya kumdhuru Sabaya.

“Akituonesha picha ya Sabaya na maeneo anauyopenda kutembelea. Alituelekeza baada ya kazi ya Sabaya turudi Dar kutekeleza kazi nyingine nyeti kulipua vituo vya mafuta na kushinikiza maandamano ili Serikaki ionekane imeshindwa maana inatuchukia sisi wapinzani.

“Yeye aliondoka kurudi Dar sisi tukabaki kutekeleza kumdhuru Sabaya Tarehe 3 Agosti tulienda eneo la Rao Madukani kwa dada yake Ling'wenya ili kubana matumizi maana Mheshimiwa alituachia Sh150,000

“Tulikamatwa na askari tukituhumiwa kukutwa na dawa za kulevya na kupanga njama za ugaidi. Tuhuma hizo ni za kweli na pia kukutwa na silaha ni za kweli na nilikutwa na simu yangu ya Itel.

“Nilisaini hati ya kuchukuliwa mali na askari nao wakasaini. Nikachukuliwa kwenda Central Moshi. Uthibitisho haya maelezo ni ya kweli kwa saini.

“Muda wa kumaliza kuandika maelezo hayo ilkiuwa ni saa 3".

Wakili wa Serikali Mwandamizi SSA Kidando alimtaka ACP Kingai aelezee alichoelezwa na mshtakiwa huyo wa pili Adamu.

ACP Kingai :Alikiri kukutana na wenzake kwa ajili kwenda kwa Mbowe, alikiri kupewa nauli kwenda Moshi kukutana na Mbowe, alikiri kuwepo Moshi tarehe 24 -26 Julai 2020, alikiri kuwepo yeye na wenzake wawili akiwemo Ling'wenya na mtu mwingine.

“Alikiri tarehe 25 usiku kufanya mkutano yeye na Ling'wenya, Moses Lujenje maarufu Kakobe, Hassan Bwire na Freeman Mbowe"

SSA Kidando: Nini kiliendelea?

ACP Kingai: Alikiri kwenye mkutano alielekezwa na Mbowe kumdhuru DC Sabaya kwa njia yoyote ile.

SSA Kidando: Kitu gani kingine alikueleza?

ACP Kingai: Shahidi pia alikiri kupewa pesa na Mbowe Sh150,000 kukidhi mahitaji hapo Moshi, alikiri Agosti Mosi 2020 alfajiri Mbowe aliwaita tena na kuwapa maelekezo, kwamba wahakikishe wanayafanyia kazi.

“Kumdhuru Sabaya na ili wawe na uhakika Mbowe aliwaonyesha picha ya Sabaya kupitia simu yake, aliwalekeza wamalize kazi hiyo ya Moshi halafu warudi Dar kufanya kazi nyingine nyeti.

“Alitaja kazi hiyo kwamba walipanga wakalipue vituo vya mafuta, lakini pia kufanya vurugu kwenye masoko na maeno ya watu wengi”.
 
We vipi tena? Gaidi linaelekea kutiwa kwenye mnyororo wa chuma
Good for you.Personally nakujua na yaliyokupata nayajua.Tatizo mnajisahau mnapokuwa mnaandika.Kama hujajifunza kwa pigo Mungu alilokupa linalokuja utakuja kusimulia time will tell.

Narudia tena acha kuchuma laana ,wasimulie wenzako kilicho kupata.
 
Good for you.Personally nakujua na yaliyokupata nayajua.Tatizo mnajisahau mnapokuwa mnaandika.Kama hujajifunza kwa pigo Mungu alilokupa linalokuja utakuja kusimulia time will tell.

Narudia tena acha kuchuma laana ,wasimulie wenzako kilicho kupata.
ndio style yako ya kunichokoza?
 
Yaani magufuli amuache Mbowe.
Kwa hisia tu magufuli angeshamuweka ndani kitambo ushahidi ungemkutia ndani.
Kama aliweza waweka ndani wazee wa escrow bila ushahidi alishindwa vipi kumuweka Mbowe ndani
 
CCM wakishirikiana na kina kingai wameitunga hii kesi na ndiyo maana ina mapengo mengi mno.

Ukiwa Jaji wa haki kabisa hakuna haja na kusikiliza hii kitu, wastage of country resources.
 
Back
Top Bottom