Yaliyojiri katika mjadala wa huduma na changamoto za Saratani ya Watoto katika club house ya JamiiForums

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
1632929134421.png


KUSHIRIKI MJADALA HUU TAFADHALI GUSA LINK HII HAPA CHINI

Mjadala huu unamulika huduma ya saratani kwa watoto pamoja na changamoto mbalimbali. Baadhi ya mambo muhimu yaliyozungumziwa na wataalamu.

Dkt. Shakilu: Saratani kwa Watoto haina tofauti kama inavyowapata Wakubwa. Mwili huzalisha Seli ambazo hukua kwa haraka kuliko kawaida na kuzalisha uvimbe

Chembechembe hai za Saratani hujenga uwezo wa kuepuka Kinga ya Mwili (zinakiuka Mabadiliko ya Vinasaba) na kusambaa Mwilini

Dkt. Shakilu: Kwa Watoto wadogo Saratani nyingi hutokea kwa bahati mbaya yaani hakuna sababu ya moja kwa moja ya kueleza kwanini Mtoto amepata Saratani

Tofauti na kwa wakubwa huwa kuna sababu ikiwemo uvutaji wa Sigara na mengineyo

Dkt. Shakilu: Maambukizi ya VVU kwa Watoto pia huwaweka baadhi ya Watoto kuwa katika hatari ya kupata Saratani

Sababu nyingine ni kuwa kwenye sehemu zenye Mazingira ya mionzi au 'heavy metals'. Lakini kwa Watoto wengi ni ngumu kufahamu sababu za moja kwa moja wao kupata Saratani

Dkt. Shakilu: Pia kuna aina fulani za Saratani huwashambuliwa Watu kutokana na asili yao ya Ngozi

Kwa takwimu za Marekani Leukemia huwashambua Watoto wengi wenye Ngozi nyeupe (Wazungu) kuliko wenye Ngozi nyeusi (asili ya Kiafrika)

Dkt. Shakilu: Kwa Nchi zinazoendelea tuna changamoto ya kuwa na Watoto wengi wanaopata Saratani kuliko Nchi zilizoendelea kutokana na kuwa tuna idadi kubwa ya Watoto na Vijana

Kwa Tanzania, Watoto wengi wanapata Saratani ya Damu, Figo, Jicho na Saratani ya matezi

Dkt. Shakilu: Kuna Saratani tunashindwa kuzigundua kutokana na uhaba wa Vifaa vilivyopo

Kugundua Saratani ya Ubongo ni lazima Mgonjwa awekwe kwenye mashine Maalum ambapo hapa kwetu inapatikana kwenye hospitali chache. Hivyo wengi hufariki kabla ya kugundulika

Dkt. Shakilu: Saratani ya Damu inafanana kwa dalili na malara kwa hiyo hutibiwa Malaria kutokana na kushindwa kupima saratani zilizopo

Kwa sababu hiyo wanapofariki huandikwa kama wamekufa kwa Malaria lakini inakuwa ni saratani iliyosababisha kifo

Dkt. Shakilu: Changamoto kubwa ya Watu kutogundulika mapema kwa Watoto ni kwasababu baadhi ya Saratani dalili zake zinafanana na Magonjwa mengine ya Watoto

Kikubwa ni sisi kuboresha huduma zetu ili tuweze kuwagundua mapema Watoto wanaoumwa

Dkt. Heronima: Bugando huduma za Saratani zilianza 2007 na kipindi hicho tulikuwa tunapokea Watoto chini ya 100. Hata hivyo wengi walikuwa wakipelekwa Muhimbili wakifuata huduma bora zaidi

Kwa sasa kila wiki tunapata Watoto 5 - 7. Saratani tunazozipata zinatofautia Kijiografia

Dkt. Heronima: Kwa Watoto Uchunguzi umejitahidi kuboreshwa ambapo walichunguza kwanini Saratani ya Lymphoma inatokea sana ambapo walibaini sababu mojawapo ni uwepo wa Malaria

Dkt. Shakilu: Kwa Saratani ambazo hazileti uvimbe ni kuangalia endapo Mtoto anapata Dalili za mara kwa mara yaani zinazojirudia au aliyetibiwa lakini hapati nafuu ni muhimu awekwe kwenye kundi la kuangaliwa kwa uwezekano wa kuwa na Saratani

Dkt. Esther: Kwa kanda ya kasikazini watoto wanaongoza kupata saratani ya damu na saratani ya matezi

Saratabi ambazo zinaongoza zinategemea sana maeneo ambayo mtu anatokea. Mwaka 2017 KCMC ilipokea watoto 200 waliokuwa na saratani

Dkt. Esther: Tuligundua asilimia 70 ya Wagonjwa ambao walikuja wakiwa na Saratani tayari walikuwa wametibiwa kwa Mitishamba au kwenda kwa Waganga

Hali hii inafanya wengi wachelewe kufika kupata Matibabu kutokana na Watanzania wengi kuwa na mazoea ya kupenda Mitishamba

Dkt. Lulu: Hapa Tanzania huduma za kuhudumia Saratani ya Watoto zimeimarika sana tofauti na hapo Nyuma

Kwa Nchi nyingi Watoto wenye Saratani hipata huduma ktk Idara ya Watoto na sio kwenye Taasisi za Saratani kama Watu wazima. Saratani hutibiwa kwa Dawa, upasuaji na mionzi

Dkt. Lulu: Saratani inaweza kutibiwa kwa namna tatu ambayo ni dawa tiba, upasuaji na mionzi

Zamani huduma ya mionzi ilikuwa Ocean Road lakini kwa sasa viko vituo vingine vinavyoanza kutoa tiba ya mionzi

Dkt. Lulu: Zamani huduma ya mionzi ilikuwa Ocean Road lakini kwa sasa vipo Vituo vingine vinavyoanza kutoa tiba ya mionzi

Kugundua Saratani unahitaji vipimo na vifaa vya hali ya juu ambapo kuna vipimo vya kuchukua kinyama au uroto. Pia unaweza kuhitaji MRI au CT-Scan

Dkt. Lulu: Kuna tatizo la uelewa na imani potofu kuhusu saratani za watoto ambalo lipo kwa ngazi ya jamii na watoa huduma za afya

Wengi wanadhani saratani ni kurogwa au saratani haziponi ambapo pia wahudumu wa afya hushindwa kugundua na kuwapa watoto rufaa mapema

Dkt. Lulu: Changamoto huwa watoto hufika kwenye matibabu wakiwa wamechelewa ambapo 80% huwa 'advanced stage'

Saratani ni suala la muda, ukichelewa inasambaa na linakuwa tatizo kubwa. Tunategemea vituo vinavyosambaza mikoani vitasaidia kuwafikisha watoto mapema

Dkt. Lulu Chirande: Hakuna Serikali inaweza kugharamia tiba ya Saratani 100%. Hata Bima za Afya haziwezi kulipia tiba

Nchi zinazoendelea tuna nafasi ya kutengeneza huduma zilizo bora. 60% ya Watoto wanasumbuliwa na Saratani ambapo asilimia nyingi wapo katika nchi zinazoendelea
 
Aisee kumbe saratani inaweza kutibika kwa dawa. Mimi nilikuwa najua unapigwa mionzi au kukatwa viungo tu
 
Lengo hapa ni kuchangisha pesa tu, kuweni wawazi, itasaidia kupoteza muda kuzunguka mbuyu, wekeni hiyo account number tuchangie, basi. Msiwe kama madalali wa chanjo wanaolazimisha tuchome chanjo kumbe lengo ni wanataka kupiga pesa za mkopo
 
Lengo hapa ni kuchangisha pesa tu, kuweni wawazi, itasaidia kupoteza muda kuzunguka mbuyu, wekeni hiyo account number tuchangie, basi. Msiwe kama madalali wa chanjo wanaolazimisha tuchome chanjo kumbe lengo ni wanataka kupiga pesa za mkopo
Duuuh nipo hapa nafatilia mjadala, naona umejikita kutoa ufafanuzi na mambo ya msingi kuhusu saratani ya watoto. Huenda unalosema ni sawa lakini naamini umejaji bila kufuatilia mjadala.
 
Duuuh nipo hapa nafatilia mjadala, naona umejikita kutoa ufafanuzi na mambo ya msingi kuhusu saratani ya watoto. Huenda unalosema ni sawa lakini naamini umejaji bila kufuatilia mjadala.
Ifike mahala tuokoe muda, mnahitaji pesa kununua vifaa tiba basi be straight, wekeni akaunti namba ya kuchangia, wadau tuchangie, basi, hakuna mtoto mdogo hapa
 
Ifike mahala tuokoe muda, mnahitaji pesa kununua vifaa tiba basi be straight, wekeni akaunti namba ya kuchangia, wadau tuchangie, basi, hakuna mtoto mdogo hapa
Nafikiri suala la vifaa tiba ni muhimu kwa mazingira ya nchi yetu. Wapo wagonjwa wengi wanavihitaji mahospitali. Ni vyema kama kuna nafasi ya kuchangia mimi na wewe tufanye hivyo bila hata kusubiri kupewa namba za kuchangia. m
 
Back
Top Bottom