Uchaguzi 2020 Yaliyojiri Katika Mapokezi na Mkutano Mkubwa wa hadhara wa Tundu Lissu Mjini Bukoba

Asante sana Mkuu Molemo , kiukweli tungefaidi sana kama Watanzania tungepata fursa ya kushuhudia live kuputia TV, mikutano yote ya Tundu Lissu, kama tunavyo ishuhudia mikutano ya mgombea wetu Magufuli, ili Watanzania tuwapime tuamue tunamchagua nani!.

Nakumbuka hili niliwahi kushauri Chadema lakini hamsikii...
Elections 2015 - Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni ...
Nilisema

P
CHADEMA walikuwa na Gazeti la Tanzania Daima lingesaidia sana kutufikishia habari za Uchaguzi lakini siku hizi halionekani, kuna Tv binafsi nyingi sana nchini lakini zote zinaonyesha matangazo toka TBC tu. Tatizo ni Awamu ya Tano iliyoingia madarakani kwa makosa ilitumia kila mbinu haramu kuendeleza makosa badala ya kurekabisha yasirudiwe tena matokeo yake hata hayo matangazo ya TBC wengi hatuangalii tena. Uchaguzi wa mwaka huu ni muhimu sana lakini kwa sababu ya Serikali kuminya uhuru wa vyombo habari na wanahabari, kampeni za mwaka huu zimepoa sana utadhani siyo Uchaguzi Mkuu. Hii inatia wasiwasi huenda watu wengi wasijitokeze kupiga kura na kuruhusu figisufigisu kuingiza viongozi wabovu madarakani.
 
CHADEMA walikuwa na Gazeti la Tanzania Daima lingesaidia sana kutufikishia habari za Uchaguzi lakini siku hizi halionekani, kuna Tv binafsi nyingi sana nchini lakini zote zinaonyesha matangazo toka TBC tu. Tatizo ni Awamu ya Tano iliyoingia madarakani kwa makosa ilitumia kila mbinu haramu kuendeleza makosa badala ya kurekabisha yasirudiwe tena matokeo yake hata hayo matangazo ya TBC wengi hatuangalii tena. Uchaguzi wa mwaka huu ni muhimu sana lakini kwa sababu ya Serikali kuminya uhuru wa vyombo habari na wanahabari, kampeni za mwaka huu zimepoa sana utadhani siyo Uchaguzi Mkuu. Hii inatia wasiwasi huenda watu wengi wasijitokeze kupiga kura na kuruhusu figisufigisu kuingiza viongozi wabovu madarakani.
Kina Mayala wanjifanya hawayajui haya
 
Nadhani mambo yakienda sawa itakuwa kesho
Jitahidini sana mfike, huko pia kuna kura nyingi sana tu. Jiwe alishatutenga na anafanya makusudi kulipa kisasi kwa kunyimwa ubunge mara zote alizogombea pale.

Halafu ile si ngome ya chama chochote, anayewekwa akizingua anachezea kichapo. Hivyo kwakuwa jiwe na mbunge wake wamezingua nafasi ipo wazi
 
CHADEMA walikuwa na Gazeti la Tanzania Daima lingesaidia sana kutufikishia habari za Uchaguzi lakini siku hizi halionekani, kuna Tv binafsi nyingi sana nchini lakini zote zinaonyesha matangazo toka TBC tu. Tatizo ni Awamu ya Tano iliyoingia madarakani kwa makosa ilitumia kila mbinu haramu kuendeleza makosa badala ya kurekabisha yasirudiwe tena matokeo yake hata hayo matangazo ya TBC wengi hatuangalii tena. Uchaguzi wa mwaka huu ni muhimu sana lakini kwa sababu ya Serikali kuminya uhuru wa vyombo habari na wanahabari, kampeni za mwaka huu zimepoa sana utadhani siyo Uchaguzi Mkuu. Hii inatia wasiwasi huenda watu wengi wasijitokeze kupiga kura na kuruhusu figisufigisu kuingiza viongozi wabovu madarakani.
Tanzania Daima Jiwe alilifungia Mwaka mzima
 
Nashangaa kwa nini hajadekiwa barabara kama ilivyokuwa kwa Lowassa!

Uzuri wa siasa za upinzani Tanzania, wagombea Urais huingia kwenye uchaguzi kwa mbwebwe na baada ya uchaguzi huanza kupotea polepole!

Tanzania kuna vituko!
Najua mnamlaumu sana aliyekosea shabaha. Hii mikikimikiki anayoleta Lisu isingekuwepo....Ulikuwa Devil advocate wa kudai Upinzani umekufa...sasa chupi zinawabana..
 
Kiasili, Magufuli siyo mwanademokrasia. Analazimishwa tu. Ingekuwa ni matakwa yake, angefuta achaguzi, na yeye kujitangaza kuwa ni Rais, na yeyote ambaye angehoji apelekewe askari wenye silaha.

Hivyo tusitegemee maendeleo ya demokrasia wala maendeleo ya watu, kama Magufuli ataendelea kuwa Rais.

Mifano mingi ipo inayothibitisha hulka ya Rais Magufuli. Hata akiamua kukudhalilisha, hataki hata ujitetee, yeye akuseme, akusimange, akutukane, hata kama ni kwa kukuonea, wewe unyamaze tu kimya au uitikie, 'sawa mheshimiwa Rais'. Viongozi wa namna hiyo ni hatari sana kwa Taifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Najua mnamlaumu sana aliyekosea shabaha. Hii mikikimikiki anayoleta Lisu isingekuwepo....Ulikuwa Devil advocate wa kudai Upinzani umekufa...sasa chupi zinawabana..
Na kweli namshangaa hata haoni aibu kuja kuchangia hapa wakati ana maandiko yake mengi hapa ya kutabiri kifo Cha Upinzani

Hata huyo Pascal Mayalla alikuwa anajiapiza hapa kwamba Mbowe kaua Chadema
 
Mgombea Urais kupitia Chadema Tundu Lissu leo anatarajiwa kuingia kwa kishindo kikubwa mjini Bukoba.

Mji wa Bukoba ambao ni ngome Kuu ya Chadema unatarajiwa kuzizima Leo wakati shujaa huyo atakapokanyaga viunga vya mji huo.

Mgombea Ubunge wa Bukoba Mjini mwenye ushawishi mkubwa Chief Kalumuna amewaalika wananchi wote wa Bukoba kumlaki na kumsindikiza kwa maandamano makubwa mgombea huyo wa Urais atakapowasili Hadi katika viwanja vya Gymkhana.

Wachunguzi wa siasa za Bukoba wanasema huenda Leo mji wa Bukoba ukavunja Rekodi ya Mapokezi iliyowekwa na miji ya Tunduma, Mbeya na Mwanza.

Mpaka Sasa kila dalili zinaonyesha mgombea Urais kupitia Chadema Tundu Lissu ana Uhakika wa kushinda kwa zaidi ya asilimia 60%

Kabla ya kuingia Bukoba Mjini Lissu atahutubia mikutano katika miji ya Karagwe na Misenyi

Yaliyojiri
Kama ilivyotarajiwa Lissu amewasili Bukoba Mjini majors ya saa 10 jioni na kulakiwa na umati mkubwa wa watu waliojipanga majiani huku msafara ikiongozwa na bodaboda zaidi ya Mia tano.

Akihutubia halaiki hiyo ya watu Lissu kwa maneno yake mwenyewe amesema kwa Sasa Bukoba ndiyo inayoshikilia Rekodi ya Mapokezi.

Pamoja na mambo mengine kwa Mara nyingine Lissu amelaani vikali sheria Kandamizi ya Mafao ya wastaafu inayozuia Fao la Kujitoa na kupunguza Mafao ya Wafanyakazi maskini wanapostaafu.

Lissu amesema ole wao Wafanyakazi wakiichagua CCM kwani Sheria hii iliyojaa hila na uovu ilaanza kutumiia mwakani.

Lissu ameahidi Wafanyakazi kufutilia mbali sheria hii isiyojali Haki za watu endapo wananchi wakimchagua kuwa Rais wao.
View attachment 1576775
View attachment 1577480
View attachment 1577481
View attachment 1577482
View attachment 1577499
View attachment 1577500
View attachment 1577501
View attachment 1577502
This ia terrible.....ni haki Jpm alielie kweli. Eti tunachakata za 2014😂😂
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom