Valuhwanoswela
JF-Expert Member
- Jun 27, 2019
- 1,229
- 1,125
CHADEMA walikuwa na Gazeti la Tanzania Daima lingesaidia sana kutufikishia habari za Uchaguzi lakini siku hizi halionekani, kuna Tv binafsi nyingi sana nchini lakini zote zinaonyesha matangazo toka TBC tu. Tatizo ni Awamu ya Tano iliyoingia madarakani kwa makosa ilitumia kila mbinu haramu kuendeleza makosa badala ya kurekabisha yasirudiwe tena matokeo yake hata hayo matangazo ya TBC wengi hatuangalii tena. Uchaguzi wa mwaka huu ni muhimu sana lakini kwa sababu ya Serikali kuminya uhuru wa vyombo habari na wanahabari, kampeni za mwaka huu zimepoa sana utadhani siyo Uchaguzi Mkuu. Hii inatia wasiwasi huenda watu wengi wasijitokeze kupiga kura na kuruhusu figisufigisu kuingiza viongozi wabovu madarakani.Asante sana Mkuu Molemo , kiukweli tungefaidi sana kama Watanzania tungepata fursa ya kushuhudia live kuputia TV, mikutano yote ya Tundu Lissu, kama tunavyo ishuhudia mikutano ya mgombea wetu Magufuli, ili Watanzania tuwapime tuamue tunamchagua nani!.
Nakumbuka hili niliwahi kushauri Chadema lakini hamsikii...
Elections 2015 - Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni ...
Nilisema
P