The Sheriff
JF-Expert Member
- Oct 10, 2019
- 617
- 1,799
Leo tarehe 22/11/2021 kesi ya Mwenyekiti wa CHEDEMA Freeman Mbowe inaendelea baada ya kuahirishwa siku siku ya Ijumaa, tarehe 18 Novemba, 2021.
Kujua kesi ilipoishia, soma: Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe - Novemba 18, 2021. Kesi imeahirishwa hadi Novemba 22, 2021
Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
=========
UPDATES:
JAJI AMEINGIA MAHAKAMANI
Kesi imetajwa..
Wakili wa Serikali Pius Hilla Anatambulisha Jopo la Mawakili wa Serikali
Esther Martin
Nassoro Katuga
Jenitreza Kitali
Tulimanywa Majige
Ignasi Mwinuka
Wakili Peter Kibatala anatambulisha Jopo la Mawakili wa Utetezi
Nashon Nkungu
John Malya
Dickson Matata
Seleman Matauka
Sisty Aloyce
Maria Mushi
Khadija Aron
Jaji anaita Majina ya Washtakiwa wote wanne,
Wanaitika
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Shauri limekuja kwa ajili ya Kupokea Uamuzi na Tupo tayari Kuendelea na Shauri..
Kibatala: sisi pia Mh Jaji Shauri lilikuwa kwa ajili ya Uamuzi Mdogo kwa Ruhusa yako tupo tayari Kuendelea na Shauri
Jaji anaandika Kidogo
Jaji: tarehe 18 November Mahakama hii ilihairisha Kesi hii wakati Shahidi akiwa anatoa Ushahidi Wake
Mahakama inatoa Uamuzi kama ninavyosoma Sasa. Wakati Wa Shauri Hili Dodo Shahidi alikuwa anatoa Ushahidi Kuhusu Kuchukuliwa Maelezo ya Onyo
Shahidi aliomba kutoa Kielelezo ambacho ni Detention Register ambayo alitumia Siku anawapokea Watuhumiwa Namba 2 na Namba 3. Walipo fikishwa kwake na Shahidi namba 1 na Shahidi namba 4. Kwa Maana ACP KINGAI na ASP Jumanne, Wakati anakitoa, Upande wa Utetezi walipinga
Kwamba 1. palikuwa hakuna Disposal Order 2. Mahakama ilikuwa inazuia kwa sababu ilishakijadili Functus Officio 3. KWA issue Estoppel Kwamba Jambo ambalo Limeshajadilowa Mahakamani Upande wa Mashitaka Wanazuiwa Kurudisha tena Mahakamani
Upande wa Utetezi waliwakilishwa na Jeremiah Mtobesya na Peter Kibatala, Kwa Upande wa Mashtaka Waliwakilishwa na Abdallah Chavula na Pius Hilla. Kwa Kutokurudia Mahakama itazungumza Kwa pamoja Hoja zote.
Jaji: Kwa kuanza Upande wa Utetezi walisema Kwamba Hakuna Disposal Order Kwa kupitia Kifungu cha 353, Wakasema Kwamba Kwa Mahakama Kutoa Kielelezo ni Njia Pekee ya DISPOSAL ORDER, Na Kwamba Kielelezo ambacho Kinaombwa Kuingia kilishatolewa Mahakamami na Kutolewa
Na Kwamba Jaji alikwepo au aliyemrithi hakuna Sehemu yoyote ambayo wametoa Mahakamani Disposal Order, Na Kwamba suala la Kutoa Kielelezo Mahakamani linatakiwa Kuwa Shirikishi na Lifuate Taratibu za Utawala na tatu lazima Utoaji wa Disposal Order Ufanyike kwenye Mwenendo wa Wazi
Naibu Msajili Kutoa Kielelezo pasipo Amri ya Mahakama, Ni Kukiuka Misingi na wakaomba basi Mahakama Isipokee. Wakasema haitoshi Palipaswa kuwa na Register Ya DISPOSAL Ambapo kwa Mujibu wa Muongozo wa Jaji Mkuu Unavyosema. Na Mahakama iangalie Katika Muongozo Katika Sehemu ya 4:4
Jaji: Na Hoja ya Pili kuhusu Mahakama Kuwa Funtus officio, Wakiomba kwamba Kwa sababu Mahakama Ilisha toa Maamuzi, Katika kesi Ndogo ndani ya Shitaka Kubwa basi Mahakama Ione kwamba pale ambapo Mahakama Ilisha toa a Maamuzi awezi Tena Kujadili Kuhusu Kielelezo hicho
Na Kwa sababu Mahakama Ilisha letewa Kielelezo hicho na ikakikataa, Na Kwamba Shahidi Namba Moja Alisha letewa na Kwa ajili ya a Utambuzi haijalishi, Wakaomba Mahakama ireje Kesi mbalimbali, Theresia Zackaria Vs Oscar Ukurasa wa Nne, NBC & IMMA ADVOCATE Vs....ya Mahakama ya Rufaa
Issue ya Estoppel Kwamba waliomba Mahakama ione kwamba Upande wa Mashtaka Hauwezi Kuleta Jambo hilo Kisheria, Estoppel Asili yake ni Madai lakini iliingizwa Kwenye a kesi za Jinai, Kwa kesi ISSA TOJO Mbele ya Jaji Mkuu wa wakati huo Jaji Samata,
Alisema Kwamba Kanuni ya Estoppel Ni sehemu za Sheria zetu. Na wakasisitiza Kupitia kesi ya JULIUS MICHAEL Vs JAMHURI. Ambapo Mahakama Ilipolewa na Kufanya Maamuzi. Ambapo Mahakama ili Ombwa Kurejea Kurasa wa 6 Mpaka 9. Waliomba Mahakama Ione kwamba Swala la Upoowa
Detention Register Lilishajadiliwa na alitakiwi Kuletwa Tena Mahakamani. Lengo la Kanuni hiyo ni Kufanya Mfumo wetu wa Jinai Kuwa Mfumo uliokamilika. Na Kwamba Mshtakiwa asiitwe tena Mahakamani. Kulinda Heshima Ya Mahakama na suala la Uchumi..
Kwa Maana hiyo wakaomba Mahakama Kuona kwamba Kanuni ya Estoppel Inaizuia Kuleta tena Mahakamani, Wakaomba Mahakama is Ipokee Detention Register, Na Upande wa Mashtaka Na wao walianza kwa Kupinga, Kwamba Mapingamizi yaliyoletwa yamekosewa yametafsiriwa Vibaya
Jaji: Kwamba suala la Upokelewaji wa Kielelezo ni Vigezo Vitatu vinatumika. Vya Relevance, Competence and Materiality. Kwa Upande wa Mashtaka walisema Kwamba Shahidi alisema wazi ni wapi alipotoa Kielelezo hicho. Hata Maamuzi ya Mahakama Ya wakati huo yalihusu Shahidi Kutokujenga
Misingi na Kwamba Kielelezo Hicho akijawahi Kitamkwa Kwamba ni Incompetent. Hoja ya Pili ilikuwa ni Detention Register ilikuwa inatolewa kwa ajili ya a Utambuzi wakati sasa Kinatolewa Kwa ajili ya Kielelezo. Kuhusiana na Maamuzi ya a kesi ya OSCAR na THERESIA wamesema hawana
Shida na Maamuzi hayo na Kwamba Maamuzi hayo kwenye kesi hii ni Distinguishable. Kwamba Mahakama Iliamua Kanuni ya Funtus Officio ni Kanuni iliyokuwa Inatumika Kwenye Sheria kesi. Kama Kesi ya KAMURI Vs JAMHURI ambapo Kwa Maoni yao wanasema Mashauri hayo ya natengeneza Kanuni kwa
Jinsi gani Kanuni ya Funtus Officio inaweza Kutumika ambapo ni Mashauri yanayo kuwa yamekwishamalizika. Wakaomba turejee Kesi ya THERESIA kuwa Distinguishable. Na tukija Issue Estoppel Walikiri kwamba ni Kanuni za Sheria zetu na Wakapinga kwamba ipo tofauti Kwenye kesi hii..
Wakasema issue Estoppel Inaweza Kutumika Pale ambapo Kesi iliyopo inafanana kabisa na Kesi iliyokwisha, Kwenye Uamuzi wa Mahakama Hii wanasema ujikite katika Shahidi Kushindwa Kujenga Misingi. Na Kwamba Shauri linapswa Kufika Mwisho.. Na Kwa Shauri hili bado haijafika Mwisho
Kwamba Detention Register Ilikataliwa kwenye Shauri hili hili, Na Kwamba Sababu ya a Kukataa Detention Register Ilikuwa haijafika Mwisho na Kwamba Khakuna namna ambapo Shauri Dogo litatengenishwa na Kesi Mama. Issue Estoppel Kama Swala la Kisheria lina Kosa asifa kwa Sababu
Shauri Halikufika Mwisho. Pia haliweI Kuwepo Sababu hata Malengo ya Kwa nini ilikataliwa mara ya kwanza ni tofauti na Sasa. Na suala la Tatu kuhusiana na DISPOSAL ORDER Kama Ilivyo kuwa imesemwa na Upande wa Utetezi..
Jaji: Wamesema Kwamba Amri ya kuachia Kielelezo inatolewa baada ya Shauri Kufika Mwisho. Na Kwamba Kielelezo hakikuombwa Kurudishwa Kwa wenyewe Bali Malengo yalikuwa ni Kukirudisha Mahakamani. Kwamba Malengo yake yameandikwa kwenye Barua hiyo na Naibu Msajili
Na Kwamba wanaomba Mahakama Ione kwamba Kanuni inayohitaji Kuwepo Kwa Amri ya Kuachia Kielelezo Haiwezi Kutumika Katika Shauri hili. Kwa Mujibu wa Kesi ya KONDO GEDE Vs JAMHURI. Inaelezea kwamba Mahakama inaweza Kutumia suala la Mdomo.
Wakaomba Mahakama Ipokee Kielelezo Kwa sababu ambazo wamezieleza. Kuhusiana na Ukweli Kwamba Naibu Msajili hana Uwezo wa Kutoa Kielelezo, Shahidi ameeleza namna gani alipata Kielelezo. Wakaomba Mahakama imuamini Shahidi. Kwa sababu Shahidi anaaminika.
Uombwaji wa Kielelezo Uliombwa Kwa Makusudi Ya Kurudi Mahakamani na Siyo Kurudi kwa Mwenyewe. Kama rejea Ya Kesi ya GANDI, Mahakama itumie Sheria kesi hii. Kwamba Maombi yalikuwa ni Upokelewaji wa Kielelezo. Mahakama ijikite Katika Kanuni za Upokelewaji Wa Kielelezo ambazo ni Competence, Relevance na Materiality. Na Kwamba Maamuzi ya a Mahakama ya lisema kwamba Kielelezo kinaweza Kuna mbwa kwa Njia ya Utawala. Kwa Upande wa Utetezi walipata Muda wa Kufanya Rejoinder. Wakasema Kwamba Kesi Ndogo iliyopo katika kesi Kubwa inajitegemea Kabisa.
Jaji: Kwa Sheria na Utaratibu uliopo pale ambapo Mahakama Unahitaji Kufanya Kesi Ndogo, inaondoka Kabisa katika Kesi Kubwa. Mwenendo Wa Kesi Ndogo katika kesi kubwa ni Suala la Factual Exercise, Suala la Kutafuta ukweli. Kwamba Suala la Kuthibitisha kwamba Maelezo ya Mshtakiwa yalichukuliwa kwa Njia halalali ni Wajibu wa Upande wa Mashtaka Na Upande wa Utetezi wanao Wajibu pia.
Jambo la Tatu ni kwamba Mahakama Ilishawahi Kufanya Kesi Ndogo kwa Mshtakiwa Wa Pili. Na Kwamba Swala la Amri kama ambavyo inatajwa katika Kifungu cha 353 ni Jambo la Msingi katika Kueleza Mnyororo kama. Ulifuta Utaratibu, Wakiendelea Kueleza tofauti kati ya Kesi Ndogo katika kesi Kubwa, na wakaeleza Namna ambavyo Mashahidi wanapewa Utambulisho tofauti. Na Kwamba Kwa Sababu ni Kesi tofauti basi Waliomba Kesi tofauti.
Wakaomba Mahakama ifuatilie na Kusoma Guidelines ambayo imewekwa na Mahakama kuhusu Kushughulika na Kielelezo hicho. Mahakama isome Mwanzo hadi Mwisho Namna ya Mahakama Kushughulika na Kielelezo Hiko..
Jaji: Kwamba Quorum Ya Exhibit Register Inapaswa Amri ya Mahakama Ione Imetolewa na Imetolewa na nani. Na Kwamba Kesi ya DEGE ni Irrelevant. Upande wa Mashtaka Wameangalia Kama Jambo la Kielelezo tu lakini wao wanaangalia Admissibility. Na Kwamba Mahakama inabanwa Kuendelea Kushughulika na suala hilo kupitia Funtus officio. Issue Siyo Conclusivity ya kesi Bali hata Jambo ambalo Lipo Mbele ya Mahakama. Kesi ya Gandhi haihusiani na Kutoa Kielelezo kinyemela na Kesi hiyo ni Distinguishable.
Kwamba Kesi ya Julius Michael na wenzake ndiyo Inajielezea yenyewe, Mahakama Ione inabanwa na Maamuzi yake, Wakaendelea Kusema Hoja walizoleta kwamba Kukosekana kwa Amri ya a Mahakamani, Funtus Officio na Issue Estoppel Kwa sababu hizo Wakaomba Mahakama Ikatae Kielelezo hiko
Na Hizo ndiyo zilikuwa Hoja za pande zote mbili, Na Hoja zote zimenisaidia Kufikia Uamuzi. Siku ya tarehe 19 Mwezi wa September Wakati anatoa Ushahidi Wake Mahakamani aliomba Kutoa Ushahidi Wake Mahakamani. Aliomba Kutoa Kielelezo hicho.
Jaji: Shahidi Aliomba Kutoa Kielelezo hicho, Maombi hayo yalikuwa yamekataliwa. Na Hoja zilikuwa kwamba Shahidi Hakuwa amejenga Misingi wa Namna gani ambapo Kielelezo Kimemfikia. Na namna kilivyotunzwa.
Mahakama Ilitoa Uamuzi wa Kukubali Pingamizi na Kwamba Mahakama Uliona Kweli Shahidi Hakuwa amejenga Misingi. Na Kwamba Mahakama Uliona Kwamba Kielelezo hicho hakikikuwa kimetolewa na Utawala na Njia Nyingine za Kuleta Kielelezo
Kielelezo hicho Kilikataliwa Mahakamani. Ambapo Upande Wa Mashtaka Wakaomba Kielelezo hicho Kwa Ofisi ya naibu Msajili. Naibu Msajili aliwapatia Kielelezo hicho. Na Kwa sababu Shahidi aliomba kutoa Kielelezo Ndiyo Kikapingwa na Upande wa Utetezi.
Jaji: Hoja ya Funtus Officio inaweza Kuathiri Maamuzi ya Mahakama. Na Kwa sababu hiyo naanza na Jambo hili. Kwa sababu hii na Tizama Maamuzi na hoja zilizoletwa. Na rejea Mashauri yote yaliyoletwa Mbele Ya Mahakama.
Maamuzi ya KISOPO MEDARD dhidi ya Waziri wa Ardhi Maamuzi yanakubali kuwa Yanatumika katika Mfumo wetu wa Sheria, Mahakama Imeombwa Irejee eneo linalosomeka hivi, Kwenye Mambo ya Mwenendo Wa Mahakama Kama Maamuzi yalishajulikana basi Inazuiwa Kuyajadili tena.
Na kesi ya OSCAR RWECHUNGURA kama ambavyo nimekwisha Kusema Kwamba Mahakama Ilikuwa Inazuiwa na Kanuni hiyo ya Funtus Officio, kwa hiyo siyo Sawa Hakimu Mkazi Kukubali Kupokea suala hilo katika Mahakama ya Wilaya.
Na katika Kesi ya IMMA ADVOCATE Pia, Kesi ya MWIGURO COSMAS, Pia Kesi ya MAHURI dhidi Ya JAMHURI. Ambapo Iliamua kwamba Katika Mazingira hayo inajitokeza ni Wakati gani Hakimu anakuwa Funtus officio na hawezi Kuendelea na Shauri Mbele yake.
Jaji: Ambapo Iliamua kwamba Katika Mazingira hayo inajitokeza ni Wakati gani Hakimu anakuwa Funtus officio na hawezi Kuendelea na Shauri Mbele yake. Pia Mahakama ya Tanzania SELEMAN Vs SMZ Mahakama Ilisema Kwamba Mahakama Inakuwa Funtus Officio
Maamuzi yote haya ni nayo ya rejea ni wazi kuwa ni Mashauri ambayo imefikisha Mahakama Mwisho. Kwa Upande wa Utetezi Wamesema Siyo lazima Kesi iwe imefika Mwisho. Nakubalina nao lakini inategemea ni Jambo gani.
Jaji: Kwa sababu hiyo Mahakama hii inajiuliza kwamba Je Jambo la Kuijadili Register Ilikuwa inafikisha Mahakama Mwisho? Jibu ni Hapana.. Kielelezo Kinaweza Kutolewa Mahakamani Kwa ajili ya Utambuzi.. Na Inapotolewa kama Utambuzi basi ni tofauti inapopokelewa kwa ajili ya Ushahidi
Kielelezo kinapoitwa kwa ajili ya Utambuzi Kimakosa hadhi ya Mahakama Kutumia kama Kielelezo. Katika mazingira Mengi ambapo Mahakama Imepokea Kielelezo anapokuwa Shahidi ambaye ni Competent anakitumia.
Mahakama Inaona kwamba suala La Kutolewa Kielelezo na Shahidi Hakuwa inafikisha Mahakama Mwisho. Kwa Sheria Kesi nilizozitaja hapo Juu ili Mahakama Iwe Funtus Officio Mambo haya lazima yatimie.
Jaji: MAHAKAMA inakuwa Funtus officio Ikithibitika kwamba Jambo Lililopo Mbele ya Mahakama limesha zungumzwa na Kutolewa Maamuzi. Kwamba Jambo hilo linatakiwa liwe limeimaliza Kesi Kwa Kumkuta Mshtakiwa Ana hatia au Kuitisha Jambo lolote.
Amri hiyo ambayo inakuwa imeinyima Mahakama, inatakiwa iwe na Matokeo ya kufikisha Kesi Mwisho. Ukiangalia Kimantiki Kielelezo mbacho Kimetolewa Baada ya Kielelezo hicho Kukataliwa Kilikuwa Katika suala la Utambuzi Na kwamba Upokelewaji wake siyo Wa Mwisho basi hata Kupokelewa kwake siyo Jambo la Msingi, Hoja ya FUNTUS OFFICIO naitupilia mbali kwa Sababu nilizo eleza.
Jaji: Suala Zima La ISSUE ESTOPPEL ni sehemu ya Sheria zetu, nakubaliana na Maamuzi ya Mahakama kuu. Kwamba ilikusudi ziweze Kutumia ya Issue Estoppel Lazima Mambo haya yawepo
Pale ambapo Jambo limesha amriwa na Mahakama, Maamuzi yalifikiwa kwa manufaa ya Mshtakiwa, Kwamba Maamuzi yakifikisha Mahakama Mwisho. Kwa sababu hiyo ndiyo inatengeneza Falsafa ya Issue Estoppel.
Ni Kuhakikisha kwamba Mshtakiwa Haitwi tena, Pili Kulinda Mfumo unaotambulika katika Mfumo jinai. Kulinda Hadhi ya Taasisi na suala la Kiuchumi. Kama ambavyo imeelezwa Mwanzo. Suala la Detention Register Ilishaletwa Mahakamani na Mahakama ikaikataa.
Kwa Sababu hiyo ilikataliwa, Je Mahakama inajiuliza Je Mahakama inazuiwa? Mahakama Inazingatia Hoja zote za Utetezi na Upande wa Mashtaka. Hakuna Ubishi Kwamba suala la Detention Register Ililetwa kwa ajili ya Utambuzi na Shahidi Alishindwa Kujenga Misingi ya Kielelezo hicho.
Na Kwamba Kukataliwa kwake halikuwa imelifikisha Mwisho Shauri hilo, kama ambavyo Nimeeleza katika Sheria Kesi, Ili Mahakama Iweze Kufikia Maamuzi Ilikuona Kama Issue ya Estoppel inahusika lazima Mahakama Ione kama yanafanana, Katika Context na Substance yake.
Jaji: Katika Shauri Mbali lipo Mbele ya Mahakama hii Utolewaji wa Kielelezo hicho hata Kama Kingepokelewa Isingefika Mwisho. Kielelezo hicho Kilikuwa bado lazima kitolewe na Shahidi ambaye ni Competent. Kama Kupokelewa hakuweziKufikia Mwisho wa Shauri lake.
Mahakama Inaona kwamba Issue ya Estoppel haiwezi Kuwepo, Suala linalobakia ni Kuwepo au Kutowepo Kwa DISPOSAL ORDER. Mahakama Imeelekezwa Kutumia Kifungu cha 353 na Mwongozo wa Mahakama. Na Kwamba Mahakama Imeelekezwa Kwamba bila a Kuwepo Kwa DISPOSAL ORDER, Basi Utolewaji Wa Barua ya Naibu Msajili hakuwezi Kuhalilisha Suala hilo.. Mahakama Imezingatia Hoja zote. Mahakama Inaona kwamba zuala Zima La Upokelewaji wa Kielelezo Mahakamani, Ni Kwa Mujibu wa Sheria, Na Baada Ya Kielelezo Kupokelewa inabaki kuwa Chini ya Mahakama
Jaji: Imeelezwa Vizuri Kwenye Mwongozo wa Mahakama, Mahakama Imefuata kifungu 353(3) kinasema Kwamba Bila Kuathiri Kifungu cha Kwanza nza, Mahakama ikiona Inafaa, Kitu ambacho Kimetolewa Mahakamani kitolewe Na Kurudishwa Mahakamani Kwa Ushahidi.
Kwa Masharti itakayokuwa imeweka. Ni wazi Kwamba Kumbe Kielelezo Kinapokuwa Christmas ni ya Mahakama, Kwamba pale Kielelezo Kinapokuwa Kinatoa Kinapswa Kitolewa kwa Amri ya Mahakama, Nakubaliana na Upande wa Utetezi, Na Kwamba Mahakama inapokiwa imekipokea Kielelezo hicho haihusiki na Kutunza Kielelezo hicho, Ni Jukumu la Hakimu Mfawidhi na Naibu Msajili. Mwongozo Unasema Kwamba watamteua atakaye tunza. Kanuni inampa Naibu Msajili na Hakimu Mfawidhi Uwezo wa Kudhibiti Vielelezo.
Jaji: Kwamba Naibu Msajili ana jukumu ya Kukagua Register ya Vielelezo. Kwa kusudi la Kujiridhisha, Lakini Suala la Kutoa Kielelezo Mahakamani, Sura ya Nne inasema Kwamba Utoaji wa Vielelezo Unafanyika Mwisho Baada ya Shauri Kufika au Rufaa Kukata Katika Shauri hilo
Kama Mwenendo wa Jinai Unavyosema, Ni Msimamo Wa Sheria Kama ambavyo Mahakama Iliamua Katika kesi ya SIAYO, Vielelezo vinatakiwa Vitoke ambapoa Shauri LIMEFIKA Mwisho, Kwamba KATIKA MWONGOZO sehemu Ya Nne inasema Kwamba
Pamoja na Kanuni hiyo Kielelezo Kinaweza Kutoka Mapema Wakati Shauri linaendelea, Kama ambavyo Kifungu cha 353(1), Kwamba Mahakama itatoa Amri ya Kuachiwa kwa Kielelezo, Mpaka Pale Mahakama Itakapokuwa unahitaji Kielelezo hicho.
Mahakama inaweza Kutoa Amri ya Kutoa Kielelezo Pale ambapo Shauri LIMEFIKA Mwisho au Rufaa imefika Mwisho. Mahakama Katika Amri yake inayohusu Disposal Order inahusu Kama Kielelezo Kurudi kwa Mwenyewe, Kielelezo Kiharibiwe, Au Kurudi Serikalini
Jaji: Mahakama U+itasema kwamba ni Kielelezo Gani kiharibiwe Kila Mwisho Mwezi,, Na Mwisho ni kwamba pale ambapo Kielelezo Kinatakiwa kuharibiwa Notisi utolewe Siku 30 kabla kwa Mshtakiwa, Ofisi ya Upelelezi, ofisi ya Mwanasheria. Hiyo ndiyo namna Kielelezo Kinapswa Kitolewe
Mahakama hii inakubaliana na Upande Wa Utetezi kwamba Naibu Msajili hana Mamlaka ya Kutoa Kielelezo, Mamlaka yake ni Kusimamia pale Kielelezo Kinapokuwa Kwenye Chumba Cha Kielelezo. Kusimamia Utolewaji au Kuharibiwa kwa Kielelezo hicho.
Jaji: Kwa namna hiyo basi ni Kweli Kwamba Kielelezo hakiwezi Kutolewa pasipo Amri ya Mahakama. Hata hivyo Mahakama inatakiwa Ijielekeze Katika Sheria Kesi hiyo. Mahakama inatakiwa Kusema Kwamba Kielelezo Kurudi Kwa Mwenyewe, au Kiharibiwe, au Kurudishwa Serikalini
Mahakama haina Mamlaka ya Kutolea Amri nje ya Kazi hizo Juu. Barua ilivyoandikwa Kwa Naibu Msajili Haikuwa imeeleza Mambo hayo hapo Juu. Mahakama Ina maoni kwamba halikuwa Muafaka kwa Kutolea Amri ya kuteketeza
Lakini Naibu Msajili ametajwa Kwamba ana uwezo wa Kutunza Kielelezo, Na Kwamba Kielelezo Kinacho takiwa kwa kesi zaidi ya Moja au Mahakama Moja, Mahakama zaidi ya Moja. Kutokana na hali hiyo basi ni wazi Siyo Kila wakati Kwamba Kila Wakati Kielelezo Kinapokuwa Kutumika Kinatakiwa
Kiwe na Amri ya Mahakama, Kwamba Kinaweza Kutumika Kwa Kesi au Mahakama Zaidi ya moja bila Amri ya Mahakama, Kwamba Naibu Msajili atakuwa ananoti kwenye Register yake Movement ya Kielelezo hicho, KIELELEZO SIYO LAZIMA PAWE NA AMRI YA MAHAKAMA.
Jaji: Nimeona Kwamba Siyo lazima Kielelezo hicho kuwa na Amri ya Mahakamani, Kwa sababu hiyo naitupilia Mbali Sababu zote tatu za Mapingamizi ya Kuzuia Kielelezo hicho, NATOA AMRI
Mawakili wa pande zote mbili Wanasimama na Kukaa
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Kufuatilia Maamuzi ya Mahakama naomba Sasa Shahidi aruhusiwe Kuendelea Kutoa Ushahidi Wake
Jaji: Upande wa Utetezi Kuna Hoja yoyote
Kibatala: Hakuna, Endelea
Jaji: Kwa Mujibu wa Utaratibu Kielelezo Kinatakiwa Kisomwe
Wakili wa Serikali: tunaomba sasa tupewe P2 ilishahidi aweze Kusoma
Jaji: Tunaomba Shahidi asome Maeneo ambayo ni Relevant tu
Mallya: Sawa tu
Wakili wa Serikali: Ushahidi wako umesema tarehe 07 August 2020 ulipokea Watuhumiwa walioletwa na Kingai na ACP jumanne, Twende Kwenye eneo ulilowaingiza na utusomee
Shahidi: amemaliza kukifafanua Kitabu cha Mahabusu
Wakili wa Serikali: Mtu huyu aliyetolewa alirejea Saa ngapi
Shahidi: Saa 5 na Dakika 6
Wakili wa Serikali: anaonekana namba Ngapi
Shahidi: Namba 401
Wakili wa Serikali: Wakati anaingia hii mara ya Pili, Alikuwa na Hali gani
Shahidi: Physical Condition ni Good
Wakili wa Serikali: Baada ya Kuingia Tarehe 07 August 2020 saa Tano, ni lini tena alitoka
Shahidi: alitoka tena Tarehe 08 August 2020, Majira ya Sa 4 na Dakika 05 Asubuhi
Wakili wa Serikali: nani alimtoa
Shahidi: Inspector Mahita
Wakili wa Serikali: Sababu za Kumtoa
Shahidi: Nje kwa Upelelezi
Wakili wa Serikali: Mtu Mwingine uliyepokea ni nani
Shahidi: Adam Kasekwa
Wakili wa Serikali: anasema Entry namba Ngapi
Shahidi: 393
Wakili wa Serikali: aliingizwa Saa ngapi
Shahidi: 07 August 2020, Saa 12 na Dakika 9
Wakili wa Serikali: baada ya kumuingiza ni lini alitoka tena
Shahidi: 07 August 2020 Saa 11 na Dakika 11
Wakili wa Serikali: Kwa Mujibu wa Kitabu kuna Entry ya Lesheni
Shahidi: Leseni Supply anatakiwa apewe Asubuhi Mchana na jioni, Kwa Mujibu wa Kitabu Mtuhumiwa amepewa Chakula Asubuhi, Mchana na Jioni
Wakili wa Serikali: Taarifa za Kwenye Kitabu ni za Kituo gani Shahidi Taarifa za Central Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Watu hao uliowapokea hapa Mahakamani Wapo?
Shahidi: Wapo kwenye Kizimba cha Washtakiwa
Wakili wa Serikali: Ifahamishe Mahakama yupi ni yupi
Shahidi: hawa wawili wa Kati kati, Wapili kutoka Kulia ni Adam na huyu Mwingine ni Mohammed Abdilah Ling'wenya
Wakili wa Serikali: Uliwapokea wapi
Shahidi: Dar es Salaam, Central
Wakili wa Serikali: Lini
Shahidi: Tarehe 07 August 2020
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji hatuna Serikali swali lingine kwa Shahidi, Tumemaliza Examination In-chief
Nashon Nkungu: Shahidi Unafahamu Kwamba Washtakiwa Wanasema hawajawahi Kuonana na wewe na hawajawahi Kufika Central Da es Salaam?
Shahidi: Sifahamu Kama Wanasema hivyo
Nashon: Unafahamu kuhusu Station Diary
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Nashon: na ni Duty ya CRO
Shahidi: Sahihi
Nashon: Mheshimiwa Jaji naomba Kupatiwa Exhibit P2
Nashon: ni Sahihi Kabisa kwamba Askari anayekuja na anayetoka lazima wasainishane kwenye Station Diary
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: ni sahihi Kwamba inatajwa kwamba Nimemkabidhi, pamoja na Silaha na Majina ya Mahabusu
Shahidi: Nafahamu kwamba nitakwa la Kisheria
Nashon: na Kutaja Watuhumiwa na mali
Shahidi: Kwenye suala la Watuhumiwa sijafahamu
Nashon: uoni kwamba Station Diary Ingekuwa ya Muhimu Kuwepo Mahakamani
Shahidi: Siyo ya Umuhimu
Nashon: Pale Kituo cha Central Police Dar es Salaam, palikuwa na Askari Wengine wakati Wakina Kingai wanatoka MOSHI
Shahidi: Ndiyo palikuwa na Askari Wengine
Nashon: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Katika Askari Waliokuwepo Kituoni Hapakuwa na Askari Wengine ambao wangewachukua Maelezo Watuhumiwa?
Shahidi: Sikusema
Nashon: Je ulipata Kufahamu kama Kuna Ndugu au Wakili Waliokwepo wakati wanachukuliwa Maelezo
Shahidi: Hapana
Nashon: Je, kuna Ndugu au Mawakili walikuja kuwatembelea Washitakiwa
Shahidi: Hakuna
Mallya: Kwamba Kwa Madai yako ulikuwa Central Siku ya 07 August 2020
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kwamba Wakati huo ulikuwa umefanya Kazi kwa Muda gani
Shahidi: Mwaka 2014 Mpaka 2020
Mallya: Pale CRO Ulikaa mara ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Mallya: Kwa hiyo Ulishawahi Kufanya Kazi za General Duties Mara kadhaa
Shahidi: Sahihi
Mallya: Kwa huo Mwezi wa Saba pia Ulikaa pale CRO
Shahidi: Ndiyo, lakini Sikumbuki Mara ngapi
Mallya: Umesema Ushawahi Kufanya kazi Central, Nitafuti e Sehemu Nyingine Kwenye hicho Kitabu ambapo ukishawahi Kufanya Majukumu hayo
Shahidi: Tarehe 02 August 2020
Mallya: Mheshimiwa Jaji Utaangalia Wakati Unafanya Uamuzi Kwenye Serial Namba 184
Mallya: Wakati Unaandika wakati wa Kumtoa Mtu, Sababu inakuwa kweli au lah
Shahidi: Wakati amemtoa
Mallya: interest yangu Entry inayomuhusu Mshitakiwa Wa Pili, Wakati anamtoa aliandika nini
Shahidi: Nje kwa Upelelezi
Mallya: Jumanne anasema kwamba alimtoa Kwa sababu ya mahojiano, we umeandika sababu ya upelelezi
Shahidi: Ndiyo mahojiano ni sehemu ya upelelezi Mallya Kwa hiyo ni kitu kimoja, hicho
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Soma hapa na hapa..
Shahidi: NJE KWA UPELELEZI, NJE KWA MAHOJIANO
Mallya: Sasa ni kitu Kimoja
Shahidi: Hapana, Upelelezi ni Broad na Mahojiano ni Specific
Mallya: Kwa Uelewa kwako Wewe Maana yake nini
Shahidi: Mchakato unaotumika Kuanzia Kesi Imefunguliwa Mpaka Pale inapofikishwa Mahakamani
Mallya: Walikwambia Wanawatoa kwa Jambo gani
Shahidi: Mmoja kwa ajili ya Upelelezi na Mmoja kwa ajili ya Mahojiano
Mallya: aliyemtoa Mshitakiwa wa 3 ni nani
Shahidi: Inspector Mahita
Wakili wa Serikali: OBJECTION Kuhusu Utaratibu, unampomhoji Mtu, Basi Inukuliwe Maneno sahihi, Wakili azuiliwe Kuweka Maneno kwa Shahidi ambaye hayupo huku
Kibatala: OBJECTION tulishawahi Kuweka Utaratibu humu kwamba Objection itafanyika kwa Majibu siyo Maswali
Jaji: Una Kifungu cha Sheria Kinacho Kataza hilo
Wakili wa Serikali: naomba Dakika 1
Wakili wa Serikali: Sijakipata Kifungu Moja kwa Moja ila Mheshimiwa Jaji unapokuwa unamuhoji Shahidi Kwamba Fulani Alishasema kifu fulani hairuhusiwi na wewe unajua hilo
Jaji: Kanuni za cross Examination inasemaje
Mallya: Maswali ambayo yanamdhalilisha Shahidi, Maswali anayoulizwa Shahidi hapa hayamlengi Shahidi
Mallya: Sababu alizomtoa Mtuhumiwa Mahabus Central Ni pamoja na Kwenda Kumpiga
Shahidi: Hapana kwa ajili ya Upelelezi
Mallya: Ulikutwa na Diary hapa Mahakamani, na Jaji akasema wewe ni VIOLATOR
Shahidi: Mheshimiwa Jaji, Entry Namba 396 sababu ya Kumtoa, Tarehe na Muda na Mtu aliyemtoa Mtuhumiwa no. Tofauti na Kalamu iliyotumika au Mwandiko wangu uliotumika Kumuingiza Mtuhumiwa.
Mallya: Ulipata Kueleza Mahakamani?
Shahidi: Hapana
Mallya: Vifupi Vya Maneno kwenye Detention Register Mnaandika wenyewe au Ni kwa Mujibu wa Sheria
Shahidi: Mujibu wa PGO
Mallya: Ngoja nikuonyeshe PGO, naona DAR ES SALAAM kwamba CDS ni nini.
Shahidi: Inawekezakana ni Chuo Cha Polisi
Mallya: nakuonyesha Vituo Vya Polisi Vyote Tanzania na Vifupi Vyake Nionyeshe Walipo andika CENTRAL ni CDS
Shahidi: Anakodoa kwa Muda mrefu..
Mallya: nimetafuta sijaona, Sijui kama utapata Muda wa Kutosha
Shahidi: Mimi sijaona humu
Mallya: Sasa sisi ili tuamini kwamba hiki kitabu kitoke DSM Polisi Central tulitaka tuone kiandikwe ni POLICE CENTRAL DAR ES SALAAM au Kifupi Chake, Kwa Sababu kuna Kimoja Hakipo Sahihi
Shahidi: Detention Register ipo sahihi
Mallya: mie nataka nijue Kipi Hakipo Sahihi
Jaji: sasa katika ya PGO na DETENTION REGISTER kipi Kipo sahihi
Shahidi: siwezi Kusema Kwamba PGO Haipo sahihi
Jaji: Swali ni Kwamba Kipi hakiko sahihi
Shahidi: Hakuna ambacho Hakipo Sahihi
Mallya: Sasa Kuna Diary yako ulikamatwa nayo Mahakamani
Shahidi: sijakamatwa nayo
Shahidi: Niliandika Siku ya Kwanza kuja Kutoa Ushahidi Tarehe 20 September
Jaji: Ndiyo Siku uliyoandika
Shahidi: Hapana Kabla ya Siku ya Kuja Kutoa Ushahidi
Mallya: Kwa Uwezo wa Pale Central na rasilimali zake Ukoje
Shahidi: Hayo sasa Watakuwa Kuzungumzia watu wa Utawala
Mallya: Kwa Ufahamu Wako wewe Ukishawa Kuishiwa Karatasi Pale Central za Kuandikia Maelezo
Shahidi: Hapana
Dickson Matata: Nitakuhoji Maswali Machache Kutokana Maelezo uliyoyatoa Hapa Mahakamani, Kutokana ana Wateja wetu Kupinga kwamba hawakuwa hi Kuandika Maelezo na hawajawahi Kufika Central Dar es Salaam. ulisema Kituo chako Cha Kwanza Kuanza Kazi ni wapi
Shahidi: Msimbazi
Matata: Msimbazi ipo wapi
Shahidi: Wilaya ya Kipolisi Kariakoo
Matata: Kuna sehemu yoyote ulitaja Kiongozi uliyewahi Kufanya naye kazi Pale Msimbazi
Shahidi: Sijazungumzia
Matata: Ukiachana na Kutaja Majina yako na Force Namba zako, Kuna Ushahidi wowote Umeonyesha kwamba Uliwahi Kufanya kazi Central Police Dar es Salaam
Shahidi: Ndiyo nimeleta Detention Register Yenye Muandiko wangu Mimi
Matata: Kuna Kitu chochote umeleta Mahakamani mabpo kwa Kuangalia DR tunaweza Kusema huu ni Mwandiko wako
Shahidi: Kimya
Matata: twende sasa Kwenye DR, Mheshimiwa Jaji namuonyesha Kuanzia Entry namba 393
Matata: Nenda tarehe Saba, Kuna Sahihi yako hapo Kwenye hizo Entry?
Shahidi: Hakuna
Matata: Kuna sehemu Yoyote yenye Force Namba yako hapo?
Shahidi: Hakuna
Matata: nikisema Mtu yoyote anaweza Kuandika, kilichoandikwa hapa nitakuwa nakosea
Shahidi: utakuwa unakosea
Matata: Kuna Kitu Kingine chochote kinachoonyesha kwamba Detention Register Imetoka Polisi Central Dar es Salaam Na siyo Mbweni
Shahidi: Kitu Pekee ni hiyo CD
Matata: ni sahihi Kwamba Mwaka huu Ndiyo umeanza Kufanya kazi Oysterbay Polisi
Shahidi: Ndiyo Mwaka huu
Matata: Pale Central Mmesema Mnatumia CD. Je, Oysterbay Mnatumia nini?
Shahidi: OB
Matata: hiyo OB inatoka inatokana na nini
Matata: PGO namba 05 ndiyo inazungumzia Vifupisho Vya Vituo Vya Polisi. Hebu Soma haoa
Shahidi: Oysterbay Inasema ni OYB
Matata: Kuna Kitabu au Mwongozo Umekuja nao hapa Unaonyesha Oysterbay ni OB na siyo OYB?
Shahidi: Hapana
Shahidi: Kimya
Kibatala: ile Diary Uliyo kuwa nayo Kwenye Kizimba, sehemu Mahususi ambazo zinahusika na Kesi hii zimeingia Kama Kielelezo Cha Mahakama namba 1
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Siku hiyo ulikuwa wapi
Shahidi: Sikumbuki nilikuwa wapi
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Vitu vilivyochukuliwa kwenye Diary Yako vinahusiana na Kesi hii na Ushahidi wako Shahidi: Ndiyo Vinahusiana
Kibatala: na Unafahamu Kwamba Mahakama Imechukua Kurasa Kwenye Diary Yako Kabla ya wewe Kuja Kutoa Ushahidi Leo
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je Ulifafanua kwa Jaji Wakati wa Kuongozwa na Wakili wa Serikali Kwamba Kuna Kidhibiti namba Moja Mule Kuna 1,2,3 na Maana yake ni nini
Shahidi: sijafafanua
Kibatala: kwa sababu hujafafanua, Je unafahamu Kwamba ulifafanua wakati wa Re Examination
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Basi Kama hufahamu, mkijaribu tutasimama
Kibatala: Shika Kielelezo namba P1 Muonyeshe Mheshimiwa Jaji, Ni wapi Pameandikwa CENTRAL POLICE STATION DAR ES SALAAM
Shahidi: Hakuna
Kibatala: kwa hiyo ili Mahakama iijue Kwamba Kielelezo hiki Ni Cha Central lazima iingie Kwenye Details za Ndani
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mojawapo ya Vifaa kazi Vya Utambuzi ni PGO
Shahidi: Ndiyo PGO
Kibatala: Kingine kipi
Shahidi: miongozo ya Jeshi la Polisi huwa Inatolewa
Kibatala: Ni lini umefahamu Kwamba Unakuja Kutoa Ushahidi wa Kesi Ndogo ya Mohammed Ling'wenya
Shahidi: Sikumbuki Tarehe, ila kama Siku 13 Nyuma
Kibatala: Toka unapokea Summons, ni lini Ulifanya Maandalizi ya Kuleta Muongozo
Shahidi: sijaleta Muongozo
Kibatala: Kuna Mtu yoyote alikuzuia kuleta
Shahidi: Hapana
Kibatala: Kingine ni Kitu gani
Shahidi: Police auxiliary Act
Kibatala: Kifungu gani
Shahidi: Kimya
Kibatala: Katika Kielelezo P1 hapo Katikakati ni nini hicho
Shahidi: Mheshimiwa Jaji ni pini iliyodondokea kwa Bahati Mbaya katika Ukurasa unaowahusu Washtakiwa hawa
Kibatala: Ulifafanua kuhusu hiyo pini
Shahidi: SiKufafanua
Kibatala: hiyo tarehe 07 August 2020 ulipokea Zamu kutoka kwa nani na nani
Shahidi: aliyepokea Zamu ni Afande Fatuma
Kibatala: Kwahiyo wewe humfahamu hata Askari Mmoja kati ya wale uliowapokea
Shahidi: Siwakumbuki
Kibatala: Ulipotoka Duty uliwakabidhi Askari nani na nani
Shahidi: aliwakabidhi Afande Fatuma, miye siwajui
Kibatala: Imakama Maana yake nini
Shahidi: Miye sikumbuki
Kibatala: Kuna Mpango Kazi Unaonyesha Askari Fulani anakaa wapi na nani anaenda wapi
Shahidi: Ndiyo upo
Kibatala: na wewe Mpaka Unakuja Kutoa Ushahidi, hujaleta sehemu ya Mpango kazi
Shahidi: Kimya
Kibatala: Unamfahamu Mtu anaitwa Lembrus Mchome
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: anasema Kwamba Mwaka Jana Mwezi wa Tano Ulimpokea Oysterbay Polisi Ukiwa CRO
Shahidi: Simkumbuki
Kibatala: ana sababu gani za kukusingizia
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: hiyo Siku ya tare 07 August 2020, Wakati Unampokea Mohammed Abdilah Ling'wenya alikuwa na Karatasi yoyote
Shahidi: Sikumkuta na Chochote
Kibatala: Wakati Unaongozwa ulipata Kuzungumzia Kuhusu Seizure Certificate
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Je Exhibit zinatunzwa wapi kama Mtu akikutwa navyo
Shahidi: Kwa Mtunza Vielelezo
Kibatala: Walikuongoza Kuzungumzia Kuhusu Vielelezo vya Mohammed Ling'wenya
Shahidi: Kimya
Kibatala: Mtunza Vielelezo anaitwa nani
Shahidi: Sikumbuki ni Siku Nyingi sana
Kibatala: ulisema Mohammed Ling'wenya alichukuliwa Maelezo Kwenye Ofisi ya OCS, umesema kwa Jaji nani alifungua Mlango
Shahidi: Sikusema Kibatala: Ulimweleza Jaji Kuwa OCS alikuwepo wapi
Shahidi: Sikusema
Kibatala: nani alikuwa Custodian wa Detention Register
Shahidi: mimi
Kibatala: Wakati unasema Ulimsindikiza ASP Jumanne, ulisema Detention Register Ulimuachia nani
Shahidi:
Kibatala: Kuna sehemu nilisikia Unasema Ulitambua Barua ya Naibu Msajili kwa Sababu ya Sahihi yake, we Unaifahamu Sahihi ya Naibu Msajili?
Shahidi: Siyo Familiar Sana
Kibatala: Wakati Barua hii inasainiwa ulikuwepo
Shahidi: Sikuwepo
Kibatala: Wakati Mnapeana Barua hii Sisi tulishirikishwa?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji sehemu gani katika hii Barua umesaini Kwamba Ulipokea wewe
Shahidi: sijasaini
Kibatala: nilisikia Kuna sehemu Walikusainisha Je Umekuja na hicho Kitabu Ulichosaini
Shahidi: Hapana
Kibatala: Soma hii Barua ilivyoandikwa Kwa naibu Msajili, Kuna Jina lako
Shahidi: Hapana
Kibatala: Sasa Naibu Msajili alijuaje wewe unahitaji Kielelezo
Shahidi: Sijui yeye
Kibatala: Soma kwenye Barua Mlipeana Kielelezo gani
Shahidi: TP 1
Kibatala: Unafahamu Kwamba Kwa Mujibu wa Jaji Mkuu, Vielelezo Vyote vinatakiwa kuanza na P na siyo TP
Kibatala: Unajua kwa nini tulipinga hii Barua Kupokelewa
Kibatala: tulipinga Mahakama Kuitwa kama Shahidi Kibatala: kwa Ruhusa Ya Mahakama, kesi Inayomuhusu Mohammed Ling'wenya, alitolewa Nje kwa nini
Shahidi: Kwa Upelelezi
Kibatala: Eleza Sasa ni Wapi ulifafanua kwamba Nje kwa Upelelezi ina Manisha nini
Shahidi: Sikumbuki
Shahidi: Kimya
Kibatala: Nje kwa Upelelezi na Nje kwa Mahojiano ni sawa
Shahidi: Hazifanani lakini ni Kitu Kimoja
Kibatala: Unafahamu Kwamba Kidhibiti Kinatakiwa kijielezee chenyewe
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Kuna PPR namba, Mueleze Mheshimiwa Jaji Maana yake nini
Shahidi: Kimya
Kibatala: Je Nakala ya Ling'wenya Ya Seizure Certificate for na fall Kwenye PPR namba
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Ulitoa Ufafanuzi hapa Kwenye Kitabu Kuna DASH Kwenye PPR namba
Shahidi: Ndiyo ipo
Kibatala: Ulitoa Ufafanuzi Kwa Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba hii Detention Register inaishia lini
Shahidi: Tarehe 12 August
Kibatala: Kama Mke wa Ling'wenya alikuja Polisi Central Station alikuja Polisi Station, kwa Kitabu hiki angeambiwa yupo wapi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: kama Mke wa Ling'wenya Alikuja Central na haukumuona kwenye Daftari itakuwa nini?
Shahidi: Sijui
Kibatala: Nimesikia Kwamba Mnaulizana na Mallya kuhusu Mwandiko. Je, Ulitoa Kitu Kingine Chenye Mwandiko wako tuweze Kulinganisha?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Physical Condition ni sawa na Health Conditions?
Shahidi: ni Tofauti
Kibatala: Wakati unaweka Entry za Ling'wenya Kingai na Timu yake walikuwepo
Shahidi: Kingai alikuwa mbali ila timu yake walikuwepo
Kibatala: ulifanya Upekuzi Maungoni kwa Ling'wenya
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Nani alikwepo
Shahidi: Afande Fatuma
Kibatala: Kwa hiyo ni Ushahidi Wako Kwamba Ulifanya Upekuzi Wako Mbele ya Afande Fatuma
Shahidi: Ndiyo Nilifanya
Kibatala: Shahidi wako Mwingine ni nani
Shahidi: TIMU nzima iliyokuwa CRO
Kibatala: Majina ya Ling'wenya uliyapata Kutoka kwa nani
Shahidi: Kwa wao wenyewe
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kulikuwa na Alternative Facilities za Kuwasiliana na ndugu zake Ling'wenya?
Shahidi: Hapa Sijamwambia
Kibatala: Unaifahamu station Diary
Shahidi: Ndiyo PF 51
Kibatala: Umetoa hapa Mahakamani
Shahidi: Sijaja na Station Diary
Kibatala: ulitaja kwa Mheshimiwa Jaji Kwamba nani alikupa DR
Shahidi: Sikutaja
Kibatala: Ulitaja Mtu aliyekupa
Shahidi: Sikutaja
Kibatala: Kwani hii ni Mali yako au Mali ya Jeshi la Polisi
Shahidi: Mali ya Jeshi la Police
Kibatala: Entry ya Ling'wenya Ipo wapi
Shahidi: 392
Kibatala: Na Imeacha Kutumika lini
Shahidi: 12 August 2020
Kibatala: Fungua Entry namba 208.. Tarehe ngapi?
Shahidi: hapasomeki
Kibatala: Mie nakwambia Mwaka 2021
Shahidi: Hapana Hapasomeki
Kibatala: Miye na kwambia Mwaka 2021
Shahidi: Hapana Hapasomeki
Kibatala: Fungua tena Entry 114
Shahidi: 30 July 2021
Kibatala: Entry 113
Shahidi: Haisomeki
Kibatala: Fungua Entry namba 156, 03 August 2021
Kibatala: Unafahamu Kwamba hiki Kielelezo kinapimwa pia Kwa Uongo wake
Kibatala: Nakuonyesha Entry inayomuhusu Ling'wenya, Aliingia Saa 06:07hrs, Wakati anatoka 08:10, kuna au hakuna Hours?
Shahidi: Hakuna Hours
Kibatala: wakati Unaongozwa na Hila ulifafanua Shahidi Sikumbuki
Kibatala: Katika Entry ya Ling'wenya Kuna Dole Gumba, Mwambie Mheshimiwa Jaji Kama Ulifafanua Kuwa Dole Gumba la Nani
Shahidi: Sikufafanua
Kibatala: Mheshimiwa Jaji sina swali lingine naomba Kurudisha Kielelezo namba P2
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Tumekaa Mfukilizo tangu Asubuhi, Ikikupendeza tunaomba tupate Health Break Jaji Utetezi
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Sisi tunapinga, Tunapinga Tunahisi Muda huo utatumika Kumfundisha majibu Shahidi
Wakili wa Serikali: Hoja iliyotumika ni tuhuma Jaji: kasema ana wasiwasi tu
Wakili wa Serikali: Basi tunaomba tupate Health Break
Jaji: Wote tulikwepo humu ndani na Hasa Mimi, mimi napata Ugumu kumfungia Sehemu asifundishwe Majibu
Mallya: tusaidie, najitolea Kukaa naye na nitakula naye
Jaji: basi naelekeza Hilla, Mallya na Shahidi Mkae pamoja
Mallya: Pius Hilla tujawahi Kula pamoja
Jaji: basi Leo Mtakula pamoja kwa Amri ya Mahakama
Jaji: na Kama Watachukua Nusu saa basi Break iwe lisaa lizima
Jaji anatoka
Jaji amerejea
Mahakamani Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa tena
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Ikupendeze Mheshimiwa Jaji, uwakilishi Upande wa Jamhuri Una marekebisho Kidogo
Tungeomba Mahakama Iridhie Kuwaingiza Kwenye Quorum Wakili wa Serikali Robert Kidando na Wakili wa Serikali Abdallah Chavula, Wengine tupo Kama tulivyo kuwa awali..
Wakili Peter Kibatala: Kwa Upande wa Utetezi Quorum ipo kama tulivyo kuwa awali na tupo tayari Kuendelea
Wakili wa Serikali, Pius Hilla: Shahidi Sasa Nitakuuliza Maswali Kwa ajili ya Ufafanuzi Kufuatiwa na yale waliyokuuliza Mawakili Wasomi
Wakili wa Serikali: Umeulizwa Kwamba Washitakiwa Wakana Kwamba Hawajafikishwa Central hebu fafanua hufahamu nini
Shahidi: sikuwa nafahamu kama, Lakini Mimi ndiye niliyewapokea na Nikawa Detain.
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Kuwa Supplied na Kielelezo Cha Mahakama.
Wakili wa Serikali: Shahidi Uliulizwa Swali hukusiana na hawa Watuhumiwa Kutolewa Nje, Kwa Mahojiano na Kwa Upelelezi, Ifafanulie Mahakama
Uliposema Kwamba Mahojiano ni sehemu ya Upelelezi
Shahidi: Upelelezi Unajumuisha Kuwa Mtuhumiwa alitolewa atahojiwa, atarekodiwa naninavyo fahamu Mimi Mahojiano ni pale Mtuhumiwa anapotolewa Nje Specific kwa kwenda Kuhojiwa
Wakili wa Serikali: Ukasema Kwa Kusoma Kuna Utofauti, Je Utofauti wake nini
Shahidi: Kwamba Mahojiano ni tofauti na Upelelezi lakini Mahojiano ni Sehemu ya Upelelezi
Wakili wa Serikali: Kuna Swali Mallya alikuuliza Kwamba Mahita aliwatoa watuhumiwa kwenda Kuwapiga, Ukasema Siyo Kweli, Je Ulimaanisha nini
Shahidi: Kwa sababu Afande Mahita hakumtoa Kwa Sababu ya Kumpiga na Kupiga siyo Sehemu ya Upelelezi
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Maswali Mengi Mengi Kuhusiana na Abbreviation CDS na CD ukaonyeshwa na PGO Ukasema DR haina Makosa na PGO haina Makosa, Je Kule Central CD ni Kifupisho cha Neno gani
Shahidi: CD Kifupisho cha CENTRAL DAR ES SALAAM, haipatikani Kwenye Kifupisho cha Kituo chochote pale Tanzania Nzima WS: Uliulizwa pia Kuwa Kituo chako Cha Kazi Msimbazi na pia Kitu gani Kinathibitishwa Kwamba Ulifanya Central
Shahidi: Kwa hapa ni D. R ambayo Kifupisho chake uwezi kukioata Sehemu Yoyote Tanzania na Kwamba Mimi ndiye niliyejaza
Wakili wa Serikali: Ulionyeshwa Specific Kwenye Entry namba 393 Ukasema Hakuna Sahihi yangu wala Jina langu, Je Ni kitu gani Kitaonyesha wewe Umewahi Kufanya kazi Central
Shahidi: Entry Inaonyesha Mtuhumiwa alichukuliwa na Afande Kingai
Wakili wa Serikali: Nini Kinaonyesha Kwamba Ulikwepo Siku Ile
Shahidi: Uwepo Wa Mwandiko wangu
Wakili wa Serikali: Kwenye swali hilohilo Ujafafanua Kwamba Siyo Mtu yoyote anaweza a kuandika hicho kitabu
Shahidi: Siyo watu wote waweza...
Wakili wa Serikali: Jikite kwenye Entry namba 393
Shahidi: Siyo Mtu yoyote anaweza Kupata namba ya Kesi, Kupata details za Watuhumiwa
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali hapa kuhusiana na PIN kukutwa Katikati, Ukajibu kwamba HAIKWEPO. Ifafanulie Mahakama haikwepo Wakati gani
Shahidi: Wakati natoa Ushahidi Mara ya kwanza
Kibatala: OBJECTION swali lilikuwa alifafanua au hakufafanua..
Wakili wa Serikali: PIUS HILLA Mheshimiwa Jajiiye nilisikia Jibu la Pin haikwepo na Nataka Kufafanua
Jaji: alitoa hilo Jibu lakini wakili akasema halitaki
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali Ukasema Huku fafanua, kwakuwa PIN ndiyo Umeonyeshwa Ieleze Mahakama ni Pin ya namna gani
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Ni Kipande cha Pin ipo Katikati katika Ukurasa WA Mohammed Ling'wenya, Ndiyo Maana Nika fafanua haikuwepo.. Mheshimiwa Jaji naomba Kupewa P1, (Barua).. Mheshimiwa Jaji naomba Kumuonyesha shahidi
Wakili wa Serikali: Kwa Mujibu wa hiyo Barua ni Kitu gani unaitambua
Shahidi: nilikuwa namkabidhi wa Detention Register
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Shahidi Ulicho kuwa unakabidhiwa kwa Mujibu wa hiyo Barua ni Kitu gani
Shahidi: Detention Register
Wakili wa Serikali: Lipo swali lingine Uliulizwa Kuhusiana na Physical Condition Na Ukasema Hakuna Entry ya Health Condition, Ukasema Kwenye D. R hakuna Sehemu ya Health Conditions ulikuwa unamaanisha nini
Shahidi: sehemu tuliokuwa tunatumia Physical condition Kuandika kwenye Detention Register
Wakili wa Serikali: aliuliza wakili kwamba Mtu aliye kutishia akiwepo atakuwa na hofu
Shahidi: Ndiyo aliuliza kwamba Mtu aliye kutishia akiwepo Tishio Kinaendelea? Nikajibu ndiyo
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusu D. R Ukasema DR ni Mali ya Polisi, Ulimwambia kuwa Unamanisha nini
Shahidi: Nilienda Kumuomba Mkuu wa Kituo, Kwamba Natakiwa kutoa Ushahidi, akanisainisha kwenye Station Diary
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Hatuna Maswali
Jaji: Shahidi Nakushukuru Kwa Ushahidi Wak
Jaji: Kuna Shahidi Mwingine?
Wakili wa Serikali: Pius Hilla Kwa Leo Hatuna Shahidi Mheshimiwa Jaji, ambaye yupo tayari Kuingia Kwenye Kizimba cha Ushahidi, Tunaomba Usikilizwaji uhairishwe kwa Leo hadi Kesho Tarehe 23 November 2021 ambapo tutaleta Shahidi Mwingine
Jaji: Utetezi
Kibatala: hatuna pingamizi Mhe. Jaji ukizingatia na muda
Jaji: Kufuatia maombi ya hairisho Mahakama inahairisha mpaka kesho saa 3 asubuhi, upande wa mashtaka wanaelekezwa kuleta mashahidi, watuhumiwa wataendelea Kuwa chini ya magereza mpaka kesho asubuhi saa 3 Jaji anatoka
Kujua kesi ilipoishia, soma: Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe - Novemba 18, 2021. Kesi imeahirishwa hadi Novemba 22, 2021
Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
=========
UPDATES:
JAJI AMEINGIA MAHAKAMANI
Kesi imetajwa..
Wakili wa Serikali Pius Hilla Anatambulisha Jopo la Mawakili wa Serikali
Esther Martin
Nassoro Katuga
Jenitreza Kitali
Tulimanywa Majige
Ignasi Mwinuka
Wakili Peter Kibatala anatambulisha Jopo la Mawakili wa Utetezi
Nashon Nkungu
John Malya
Dickson Matata
Seleman Matauka
Sisty Aloyce
Maria Mushi
Khadija Aron
Jaji anaita Majina ya Washtakiwa wote wanne,
Wanaitika
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Shauri limekuja kwa ajili ya Kupokea Uamuzi na Tupo tayari Kuendelea na Shauri..
Kibatala: sisi pia Mh Jaji Shauri lilikuwa kwa ajili ya Uamuzi Mdogo kwa Ruhusa yako tupo tayari Kuendelea na Shauri
Jaji anaandika Kidogo
Jaji: tarehe 18 November Mahakama hii ilihairisha Kesi hii wakati Shahidi akiwa anatoa Ushahidi Wake
Mahakama inatoa Uamuzi kama ninavyosoma Sasa. Wakati Wa Shauri Hili Dodo Shahidi alikuwa anatoa Ushahidi Kuhusu Kuchukuliwa Maelezo ya Onyo
Shahidi aliomba kutoa Kielelezo ambacho ni Detention Register ambayo alitumia Siku anawapokea Watuhumiwa Namba 2 na Namba 3. Walipo fikishwa kwake na Shahidi namba 1 na Shahidi namba 4. Kwa Maana ACP KINGAI na ASP Jumanne, Wakati anakitoa, Upande wa Utetezi walipinga
Kwamba 1. palikuwa hakuna Disposal Order 2. Mahakama ilikuwa inazuia kwa sababu ilishakijadili Functus Officio 3. KWA issue Estoppel Kwamba Jambo ambalo Limeshajadilowa Mahakamani Upande wa Mashitaka Wanazuiwa Kurudisha tena Mahakamani
Upande wa Utetezi waliwakilishwa na Jeremiah Mtobesya na Peter Kibatala, Kwa Upande wa Mashtaka Waliwakilishwa na Abdallah Chavula na Pius Hilla. Kwa Kutokurudia Mahakama itazungumza Kwa pamoja Hoja zote.
Jaji: Kwa kuanza Upande wa Utetezi walisema Kwamba Hakuna Disposal Order Kwa kupitia Kifungu cha 353, Wakasema Kwamba Kwa Mahakama Kutoa Kielelezo ni Njia Pekee ya DISPOSAL ORDER, Na Kwamba Kielelezo ambacho Kinaombwa Kuingia kilishatolewa Mahakamami na Kutolewa
Na Kwamba Jaji alikwepo au aliyemrithi hakuna Sehemu yoyote ambayo wametoa Mahakamani Disposal Order, Na Kwamba suala la Kutoa Kielelezo Mahakamani linatakiwa Kuwa Shirikishi na Lifuate Taratibu za Utawala na tatu lazima Utoaji wa Disposal Order Ufanyike kwenye Mwenendo wa Wazi
Naibu Msajili Kutoa Kielelezo pasipo Amri ya Mahakama, Ni Kukiuka Misingi na wakaomba basi Mahakama Isipokee. Wakasema haitoshi Palipaswa kuwa na Register Ya DISPOSAL Ambapo kwa Mujibu wa Muongozo wa Jaji Mkuu Unavyosema. Na Mahakama iangalie Katika Muongozo Katika Sehemu ya 4:4
Jaji: Na Hoja ya Pili kuhusu Mahakama Kuwa Funtus officio, Wakiomba kwamba Kwa sababu Mahakama Ilisha toa Maamuzi, Katika kesi Ndogo ndani ya Shitaka Kubwa basi Mahakama Ione kwamba pale ambapo Mahakama Ilisha toa a Maamuzi awezi Tena Kujadili Kuhusu Kielelezo hicho
Na Kwa sababu Mahakama Ilisha letewa Kielelezo hicho na ikakikataa, Na Kwamba Shahidi Namba Moja Alisha letewa na Kwa ajili ya a Utambuzi haijalishi, Wakaomba Mahakama ireje Kesi mbalimbali, Theresia Zackaria Vs Oscar Ukurasa wa Nne, NBC & IMMA ADVOCATE Vs....ya Mahakama ya Rufaa
Issue ya Estoppel Kwamba waliomba Mahakama ione kwamba Upande wa Mashtaka Hauwezi Kuleta Jambo hilo Kisheria, Estoppel Asili yake ni Madai lakini iliingizwa Kwenye a kesi za Jinai, Kwa kesi ISSA TOJO Mbele ya Jaji Mkuu wa wakati huo Jaji Samata,
Alisema Kwamba Kanuni ya Estoppel Ni sehemu za Sheria zetu. Na wakasisitiza Kupitia kesi ya JULIUS MICHAEL Vs JAMHURI. Ambapo Mahakama Ilipolewa na Kufanya Maamuzi. Ambapo Mahakama ili Ombwa Kurejea Kurasa wa 6 Mpaka 9. Waliomba Mahakama Ione kwamba Swala la Upoowa
Detention Register Lilishajadiliwa na alitakiwi Kuletwa Tena Mahakamani. Lengo la Kanuni hiyo ni Kufanya Mfumo wetu wa Jinai Kuwa Mfumo uliokamilika. Na Kwamba Mshtakiwa asiitwe tena Mahakamani. Kulinda Heshima Ya Mahakama na suala la Uchumi..
Kwa Maana hiyo wakaomba Mahakama Kuona kwamba Kanuni ya Estoppel Inaizuia Kuleta tena Mahakamani, Wakaomba Mahakama is Ipokee Detention Register, Na Upande wa Mashtaka Na wao walianza kwa Kupinga, Kwamba Mapingamizi yaliyoletwa yamekosewa yametafsiriwa Vibaya
Jaji: Kwamba suala la Upokelewaji wa Kielelezo ni Vigezo Vitatu vinatumika. Vya Relevance, Competence and Materiality. Kwa Upande wa Mashtaka walisema Kwamba Shahidi alisema wazi ni wapi alipotoa Kielelezo hicho. Hata Maamuzi ya Mahakama Ya wakati huo yalihusu Shahidi Kutokujenga
Misingi na Kwamba Kielelezo Hicho akijawahi Kitamkwa Kwamba ni Incompetent. Hoja ya Pili ilikuwa ni Detention Register ilikuwa inatolewa kwa ajili ya a Utambuzi wakati sasa Kinatolewa Kwa ajili ya Kielelezo. Kuhusiana na Maamuzi ya a kesi ya OSCAR na THERESIA wamesema hawana
Shida na Maamuzi hayo na Kwamba Maamuzi hayo kwenye kesi hii ni Distinguishable. Kwamba Mahakama Iliamua Kanuni ya Funtus Officio ni Kanuni iliyokuwa Inatumika Kwenye Sheria kesi. Kama Kesi ya KAMURI Vs JAMHURI ambapo Kwa Maoni yao wanasema Mashauri hayo ya natengeneza Kanuni kwa
Jinsi gani Kanuni ya Funtus Officio inaweza Kutumika ambapo ni Mashauri yanayo kuwa yamekwishamalizika. Wakaomba turejee Kesi ya THERESIA kuwa Distinguishable. Na tukija Issue Estoppel Walikiri kwamba ni Kanuni za Sheria zetu na Wakapinga kwamba ipo tofauti Kwenye kesi hii..
Wakasema issue Estoppel Inaweza Kutumika Pale ambapo Kesi iliyopo inafanana kabisa na Kesi iliyokwisha, Kwenye Uamuzi wa Mahakama Hii wanasema ujikite katika Shahidi Kushindwa Kujenga Misingi. Na Kwamba Shauri linapswa Kufika Mwisho.. Na Kwa Shauri hili bado haijafika Mwisho
Kwamba Detention Register Ilikataliwa kwenye Shauri hili hili, Na Kwamba Sababu ya a Kukataa Detention Register Ilikuwa haijafika Mwisho na Kwamba Khakuna namna ambapo Shauri Dogo litatengenishwa na Kesi Mama. Issue Estoppel Kama Swala la Kisheria lina Kosa asifa kwa Sababu
Shauri Halikufika Mwisho. Pia haliweI Kuwepo Sababu hata Malengo ya Kwa nini ilikataliwa mara ya kwanza ni tofauti na Sasa. Na suala la Tatu kuhusiana na DISPOSAL ORDER Kama Ilivyo kuwa imesemwa na Upande wa Utetezi..
Jaji: Wamesema Kwamba Amri ya kuachia Kielelezo inatolewa baada ya Shauri Kufika Mwisho. Na Kwamba Kielelezo hakikuombwa Kurudishwa Kwa wenyewe Bali Malengo yalikuwa ni Kukirudisha Mahakamani. Kwamba Malengo yake yameandikwa kwenye Barua hiyo na Naibu Msajili
Na Kwamba wanaomba Mahakama Ione kwamba Kanuni inayohitaji Kuwepo Kwa Amri ya Kuachia Kielelezo Haiwezi Kutumika Katika Shauri hili. Kwa Mujibu wa Kesi ya KONDO GEDE Vs JAMHURI. Inaelezea kwamba Mahakama inaweza Kutumia suala la Mdomo.
Wakaomba Mahakama Ipokee Kielelezo Kwa sababu ambazo wamezieleza. Kuhusiana na Ukweli Kwamba Naibu Msajili hana Uwezo wa Kutoa Kielelezo, Shahidi ameeleza namna gani alipata Kielelezo. Wakaomba Mahakama imuamini Shahidi. Kwa sababu Shahidi anaaminika.
Uombwaji wa Kielelezo Uliombwa Kwa Makusudi Ya Kurudi Mahakamani na Siyo Kurudi kwa Mwenyewe. Kama rejea Ya Kesi ya GANDI, Mahakama itumie Sheria kesi hii. Kwamba Maombi yalikuwa ni Upokelewaji wa Kielelezo. Mahakama ijikite Katika Kanuni za Upokelewaji Wa Kielelezo ambazo ni Competence, Relevance na Materiality. Na Kwamba Maamuzi ya a Mahakama ya lisema kwamba Kielelezo kinaweza Kuna mbwa kwa Njia ya Utawala. Kwa Upande wa Utetezi walipata Muda wa Kufanya Rejoinder. Wakasema Kwamba Kesi Ndogo iliyopo katika kesi Kubwa inajitegemea Kabisa.
Jaji: Kwa Sheria na Utaratibu uliopo pale ambapo Mahakama Unahitaji Kufanya Kesi Ndogo, inaondoka Kabisa katika Kesi Kubwa. Mwenendo Wa Kesi Ndogo katika kesi kubwa ni Suala la Factual Exercise, Suala la Kutafuta ukweli. Kwamba Suala la Kuthibitisha kwamba Maelezo ya Mshtakiwa yalichukuliwa kwa Njia halalali ni Wajibu wa Upande wa Mashtaka Na Upande wa Utetezi wanao Wajibu pia.
Jambo la Tatu ni kwamba Mahakama Ilishawahi Kufanya Kesi Ndogo kwa Mshtakiwa Wa Pili. Na Kwamba Swala la Amri kama ambavyo inatajwa katika Kifungu cha 353 ni Jambo la Msingi katika Kueleza Mnyororo kama. Ulifuta Utaratibu, Wakiendelea Kueleza tofauti kati ya Kesi Ndogo katika kesi Kubwa, na wakaeleza Namna ambavyo Mashahidi wanapewa Utambulisho tofauti. Na Kwamba Kwa Sababu ni Kesi tofauti basi Waliomba Kesi tofauti.
Wakaomba Mahakama ifuatilie na Kusoma Guidelines ambayo imewekwa na Mahakama kuhusu Kushughulika na Kielelezo hicho. Mahakama isome Mwanzo hadi Mwisho Namna ya Mahakama Kushughulika na Kielelezo Hiko..
Jaji: Kwamba Quorum Ya Exhibit Register Inapaswa Amri ya Mahakama Ione Imetolewa na Imetolewa na nani. Na Kwamba Kesi ya DEGE ni Irrelevant. Upande wa Mashtaka Wameangalia Kama Jambo la Kielelezo tu lakini wao wanaangalia Admissibility. Na Kwamba Mahakama inabanwa Kuendelea Kushughulika na suala hilo kupitia Funtus officio. Issue Siyo Conclusivity ya kesi Bali hata Jambo ambalo Lipo Mbele ya Mahakama. Kesi ya Gandhi haihusiani na Kutoa Kielelezo kinyemela na Kesi hiyo ni Distinguishable.
Kwamba Kesi ya Julius Michael na wenzake ndiyo Inajielezea yenyewe, Mahakama Ione inabanwa na Maamuzi yake, Wakaendelea Kusema Hoja walizoleta kwamba Kukosekana kwa Amri ya a Mahakamani, Funtus Officio na Issue Estoppel Kwa sababu hizo Wakaomba Mahakama Ikatae Kielelezo hiko
Na Hizo ndiyo zilikuwa Hoja za pande zote mbili, Na Hoja zote zimenisaidia Kufikia Uamuzi. Siku ya tarehe 19 Mwezi wa September Wakati anatoa Ushahidi Wake Mahakamani aliomba Kutoa Ushahidi Wake Mahakamani. Aliomba Kutoa Kielelezo hicho.
Jaji: Shahidi Aliomba Kutoa Kielelezo hicho, Maombi hayo yalikuwa yamekataliwa. Na Hoja zilikuwa kwamba Shahidi Hakuwa amejenga Misingi wa Namna gani ambapo Kielelezo Kimemfikia. Na namna kilivyotunzwa.
Mahakama Ilitoa Uamuzi wa Kukubali Pingamizi na Kwamba Mahakama Uliona Kweli Shahidi Hakuwa amejenga Misingi. Na Kwamba Mahakama Uliona Kwamba Kielelezo hicho hakikikuwa kimetolewa na Utawala na Njia Nyingine za Kuleta Kielelezo
Kielelezo hicho Kilikataliwa Mahakamani. Ambapo Upande Wa Mashtaka Wakaomba Kielelezo hicho Kwa Ofisi ya naibu Msajili. Naibu Msajili aliwapatia Kielelezo hicho. Na Kwa sababu Shahidi aliomba kutoa Kielelezo Ndiyo Kikapingwa na Upande wa Utetezi.
Jaji: Hoja ya Funtus Officio inaweza Kuathiri Maamuzi ya Mahakama. Na Kwa sababu hiyo naanza na Jambo hili. Kwa sababu hii na Tizama Maamuzi na hoja zilizoletwa. Na rejea Mashauri yote yaliyoletwa Mbele Ya Mahakama.
Maamuzi ya KISOPO MEDARD dhidi ya Waziri wa Ardhi Maamuzi yanakubali kuwa Yanatumika katika Mfumo wetu wa Sheria, Mahakama Imeombwa Irejee eneo linalosomeka hivi, Kwenye Mambo ya Mwenendo Wa Mahakama Kama Maamuzi yalishajulikana basi Inazuiwa Kuyajadili tena.
Na kesi ya OSCAR RWECHUNGURA kama ambavyo nimekwisha Kusema Kwamba Mahakama Ilikuwa Inazuiwa na Kanuni hiyo ya Funtus Officio, kwa hiyo siyo Sawa Hakimu Mkazi Kukubali Kupokea suala hilo katika Mahakama ya Wilaya.
Na katika Kesi ya IMMA ADVOCATE Pia, Kesi ya MWIGURO COSMAS, Pia Kesi ya MAHURI dhidi Ya JAMHURI. Ambapo Iliamua kwamba Katika Mazingira hayo inajitokeza ni Wakati gani Hakimu anakuwa Funtus officio na hawezi Kuendelea na Shauri Mbele yake.
Jaji: Ambapo Iliamua kwamba Katika Mazingira hayo inajitokeza ni Wakati gani Hakimu anakuwa Funtus officio na hawezi Kuendelea na Shauri Mbele yake. Pia Mahakama ya Tanzania SELEMAN Vs SMZ Mahakama Ilisema Kwamba Mahakama Inakuwa Funtus Officio
Maamuzi yote haya ni nayo ya rejea ni wazi kuwa ni Mashauri ambayo imefikisha Mahakama Mwisho. Kwa Upande wa Utetezi Wamesema Siyo lazima Kesi iwe imefika Mwisho. Nakubalina nao lakini inategemea ni Jambo gani.
Jaji: Kwa sababu hiyo Mahakama hii inajiuliza kwamba Je Jambo la Kuijadili Register Ilikuwa inafikisha Mahakama Mwisho? Jibu ni Hapana.. Kielelezo Kinaweza Kutolewa Mahakamani Kwa ajili ya Utambuzi.. Na Inapotolewa kama Utambuzi basi ni tofauti inapopokelewa kwa ajili ya Ushahidi
Kielelezo kinapoitwa kwa ajili ya Utambuzi Kimakosa hadhi ya Mahakama Kutumia kama Kielelezo. Katika mazingira Mengi ambapo Mahakama Imepokea Kielelezo anapokuwa Shahidi ambaye ni Competent anakitumia.
Mahakama Inaona kwamba suala La Kutolewa Kielelezo na Shahidi Hakuwa inafikisha Mahakama Mwisho. Kwa Sheria Kesi nilizozitaja hapo Juu ili Mahakama Iwe Funtus Officio Mambo haya lazima yatimie.
Jaji: MAHAKAMA inakuwa Funtus officio Ikithibitika kwamba Jambo Lililopo Mbele ya Mahakama limesha zungumzwa na Kutolewa Maamuzi. Kwamba Jambo hilo linatakiwa liwe limeimaliza Kesi Kwa Kumkuta Mshtakiwa Ana hatia au Kuitisha Jambo lolote.
Amri hiyo ambayo inakuwa imeinyima Mahakama, inatakiwa iwe na Matokeo ya kufikisha Kesi Mwisho. Ukiangalia Kimantiki Kielelezo mbacho Kimetolewa Baada ya Kielelezo hicho Kukataliwa Kilikuwa Katika suala la Utambuzi Na kwamba Upokelewaji wake siyo Wa Mwisho basi hata Kupokelewa kwake siyo Jambo la Msingi, Hoja ya FUNTUS OFFICIO naitupilia mbali kwa Sababu nilizo eleza.
Jaji: Suala Zima La ISSUE ESTOPPEL ni sehemu ya Sheria zetu, nakubaliana na Maamuzi ya Mahakama kuu. Kwamba ilikusudi ziweze Kutumia ya Issue Estoppel Lazima Mambo haya yawepo
Pale ambapo Jambo limesha amriwa na Mahakama, Maamuzi yalifikiwa kwa manufaa ya Mshtakiwa, Kwamba Maamuzi yakifikisha Mahakama Mwisho. Kwa sababu hiyo ndiyo inatengeneza Falsafa ya Issue Estoppel.
Ni Kuhakikisha kwamba Mshtakiwa Haitwi tena, Pili Kulinda Mfumo unaotambulika katika Mfumo jinai. Kulinda Hadhi ya Taasisi na suala la Kiuchumi. Kama ambavyo imeelezwa Mwanzo. Suala la Detention Register Ilishaletwa Mahakamani na Mahakama ikaikataa.
Kwa Sababu hiyo ilikataliwa, Je Mahakama inajiuliza Je Mahakama inazuiwa? Mahakama Inazingatia Hoja zote za Utetezi na Upande wa Mashtaka. Hakuna Ubishi Kwamba suala la Detention Register Ililetwa kwa ajili ya Utambuzi na Shahidi Alishindwa Kujenga Misingi ya Kielelezo hicho.
Na Kwamba Kukataliwa kwake halikuwa imelifikisha Mwisho Shauri hilo, kama ambavyo Nimeeleza katika Sheria Kesi, Ili Mahakama Iweze Kufikia Maamuzi Ilikuona Kama Issue ya Estoppel inahusika lazima Mahakama Ione kama yanafanana, Katika Context na Substance yake.
Jaji: Katika Shauri Mbali lipo Mbele ya Mahakama hii Utolewaji wa Kielelezo hicho hata Kama Kingepokelewa Isingefika Mwisho. Kielelezo hicho Kilikuwa bado lazima kitolewe na Shahidi ambaye ni Competent. Kama Kupokelewa hakuweziKufikia Mwisho wa Shauri lake.
Mahakama Inaona kwamba Issue ya Estoppel haiwezi Kuwepo, Suala linalobakia ni Kuwepo au Kutowepo Kwa DISPOSAL ORDER. Mahakama Imeelekezwa Kutumia Kifungu cha 353 na Mwongozo wa Mahakama. Na Kwamba Mahakama Imeelekezwa Kwamba bila a Kuwepo Kwa DISPOSAL ORDER, Basi Utolewaji Wa Barua ya Naibu Msajili hakuwezi Kuhalilisha Suala hilo.. Mahakama Imezingatia Hoja zote. Mahakama Inaona kwamba zuala Zima La Upokelewaji wa Kielelezo Mahakamani, Ni Kwa Mujibu wa Sheria, Na Baada Ya Kielelezo Kupokelewa inabaki kuwa Chini ya Mahakama
Jaji: Imeelezwa Vizuri Kwenye Mwongozo wa Mahakama, Mahakama Imefuata kifungu 353(3) kinasema Kwamba Bila Kuathiri Kifungu cha Kwanza nza, Mahakama ikiona Inafaa, Kitu ambacho Kimetolewa Mahakamani kitolewe Na Kurudishwa Mahakamani Kwa Ushahidi.
Kwa Masharti itakayokuwa imeweka. Ni wazi Kwamba Kumbe Kielelezo Kinapokuwa Christmas ni ya Mahakama, Kwamba pale Kielelezo Kinapokuwa Kinatoa Kinapswa Kitolewa kwa Amri ya Mahakama, Nakubaliana na Upande wa Utetezi, Na Kwamba Mahakama inapokiwa imekipokea Kielelezo hicho haihusiki na Kutunza Kielelezo hicho, Ni Jukumu la Hakimu Mfawidhi na Naibu Msajili. Mwongozo Unasema Kwamba watamteua atakaye tunza. Kanuni inampa Naibu Msajili na Hakimu Mfawidhi Uwezo wa Kudhibiti Vielelezo.
Jaji: Kwamba Naibu Msajili ana jukumu ya Kukagua Register ya Vielelezo. Kwa kusudi la Kujiridhisha, Lakini Suala la Kutoa Kielelezo Mahakamani, Sura ya Nne inasema Kwamba Utoaji wa Vielelezo Unafanyika Mwisho Baada ya Shauri Kufika au Rufaa Kukata Katika Shauri hilo
Kama Mwenendo wa Jinai Unavyosema, Ni Msimamo Wa Sheria Kama ambavyo Mahakama Iliamua Katika kesi ya SIAYO, Vielelezo vinatakiwa Vitoke ambapoa Shauri LIMEFIKA Mwisho, Kwamba KATIKA MWONGOZO sehemu Ya Nne inasema Kwamba
Pamoja na Kanuni hiyo Kielelezo Kinaweza Kutoka Mapema Wakati Shauri linaendelea, Kama ambavyo Kifungu cha 353(1), Kwamba Mahakama itatoa Amri ya Kuachiwa kwa Kielelezo, Mpaka Pale Mahakama Itakapokuwa unahitaji Kielelezo hicho.
Mahakama inaweza Kutoa Amri ya Kutoa Kielelezo Pale ambapo Shauri LIMEFIKA Mwisho au Rufaa imefika Mwisho. Mahakama Katika Amri yake inayohusu Disposal Order inahusu Kama Kielelezo Kurudi kwa Mwenyewe, Kielelezo Kiharibiwe, Au Kurudi Serikalini
Jaji: Mahakama U+itasema kwamba ni Kielelezo Gani kiharibiwe Kila Mwisho Mwezi,, Na Mwisho ni kwamba pale ambapo Kielelezo Kinatakiwa kuharibiwa Notisi utolewe Siku 30 kabla kwa Mshtakiwa, Ofisi ya Upelelezi, ofisi ya Mwanasheria. Hiyo ndiyo namna Kielelezo Kinapswa Kitolewe
Mahakama hii inakubaliana na Upande Wa Utetezi kwamba Naibu Msajili hana Mamlaka ya Kutoa Kielelezo, Mamlaka yake ni Kusimamia pale Kielelezo Kinapokuwa Kwenye Chumba Cha Kielelezo. Kusimamia Utolewaji au Kuharibiwa kwa Kielelezo hicho.
Jaji: Kwa namna hiyo basi ni Kweli Kwamba Kielelezo hakiwezi Kutolewa pasipo Amri ya Mahakama. Hata hivyo Mahakama inatakiwa Ijielekeze Katika Sheria Kesi hiyo. Mahakama inatakiwa Kusema Kwamba Kielelezo Kurudi Kwa Mwenyewe, au Kiharibiwe, au Kurudishwa Serikalini
Mahakama haina Mamlaka ya Kutolea Amri nje ya Kazi hizo Juu. Barua ilivyoandikwa Kwa Naibu Msajili Haikuwa imeeleza Mambo hayo hapo Juu. Mahakama Ina maoni kwamba halikuwa Muafaka kwa Kutolea Amri ya kuteketeza
Lakini Naibu Msajili ametajwa Kwamba ana uwezo wa Kutunza Kielelezo, Na Kwamba Kielelezo Kinacho takiwa kwa kesi zaidi ya Moja au Mahakama Moja, Mahakama zaidi ya Moja. Kutokana na hali hiyo basi ni wazi Siyo Kila wakati Kwamba Kila Wakati Kielelezo Kinapokuwa Kutumika Kinatakiwa
Kiwe na Amri ya Mahakama, Kwamba Kinaweza Kutumika Kwa Kesi au Mahakama Zaidi ya moja bila Amri ya Mahakama, Kwamba Naibu Msajili atakuwa ananoti kwenye Register yake Movement ya Kielelezo hicho, KIELELEZO SIYO LAZIMA PAWE NA AMRI YA MAHAKAMA.
Jaji: Nimeona Kwamba Siyo lazima Kielelezo hicho kuwa na Amri ya Mahakamani, Kwa sababu hiyo naitupilia Mbali Sababu zote tatu za Mapingamizi ya Kuzuia Kielelezo hicho, NATOA AMRI
Mawakili wa pande zote mbili Wanasimama na Kukaa
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Kufuatilia Maamuzi ya Mahakama naomba Sasa Shahidi aruhusiwe Kuendelea Kutoa Ushahidi Wake
Jaji: Upande wa Utetezi Kuna Hoja yoyote
Kibatala: Hakuna, Endelea
Jaji: Kwa Mujibu wa Utaratibu Kielelezo Kinatakiwa Kisomwe
Wakili wa Serikali: tunaomba sasa tupewe P2 ilishahidi aweze Kusoma
Jaji: Tunaomba Shahidi asome Maeneo ambayo ni Relevant tu
Mallya: Sawa tu
Wakili wa Serikali: Ushahidi wako umesema tarehe 07 August 2020 ulipokea Watuhumiwa walioletwa na Kingai na ACP jumanne, Twende Kwenye eneo ulilowaingiza na utusomee
Shahidi: amemaliza kukifafanua Kitabu cha Mahabusu
Wakili wa Serikali: Mtu huyu aliyetolewa alirejea Saa ngapi
Shahidi: Saa 5 na Dakika 6
Wakili wa Serikali: anaonekana namba Ngapi
Shahidi: Namba 401
Wakili wa Serikali: Wakati anaingia hii mara ya Pili, Alikuwa na Hali gani
Shahidi: Physical Condition ni Good
Wakili wa Serikali: Baada ya Kuingia Tarehe 07 August 2020 saa Tano, ni lini tena alitoka
Shahidi: alitoka tena Tarehe 08 August 2020, Majira ya Sa 4 na Dakika 05 Asubuhi
Wakili wa Serikali: nani alimtoa
Shahidi: Inspector Mahita
Wakili wa Serikali: Sababu za Kumtoa
Shahidi: Nje kwa Upelelezi
Wakili wa Serikali: Mtu Mwingine uliyepokea ni nani
Shahidi: Adam Kasekwa
Wakili wa Serikali: anasema Entry namba Ngapi
Shahidi: 393
Wakili wa Serikali: aliingizwa Saa ngapi
Shahidi: 07 August 2020, Saa 12 na Dakika 9
Wakili wa Serikali: baada ya kumuingiza ni lini alitoka tena
Shahidi: 07 August 2020 Saa 11 na Dakika 11
Wakili wa Serikali: Kwa Mujibu wa Kitabu kuna Entry ya Lesheni
Shahidi: Leseni Supply anatakiwa apewe Asubuhi Mchana na jioni, Kwa Mujibu wa Kitabu Mtuhumiwa amepewa Chakula Asubuhi, Mchana na Jioni
Wakili wa Serikali: Taarifa za Kwenye Kitabu ni za Kituo gani Shahidi Taarifa za Central Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Watu hao uliowapokea hapa Mahakamani Wapo?
Shahidi: Wapo kwenye Kizimba cha Washtakiwa
Wakili wa Serikali: Ifahamishe Mahakama yupi ni yupi
Shahidi: hawa wawili wa Kati kati, Wapili kutoka Kulia ni Adam na huyu Mwingine ni Mohammed Abdilah Ling'wenya
Wakili wa Serikali: Uliwapokea wapi
Shahidi: Dar es Salaam, Central
Wakili wa Serikali: Lini
Shahidi: Tarehe 07 August 2020
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji hatuna Serikali swali lingine kwa Shahidi, Tumemaliza Examination In-chief
Nashon Nkungu: Shahidi Unafahamu Kwamba Washtakiwa Wanasema hawajawahi Kuonana na wewe na hawajawahi Kufika Central Da es Salaam?
Shahidi: Sifahamu Kama Wanasema hivyo
Nashon: Unafahamu kuhusu Station Diary
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Nashon: na ni Duty ya CRO
Shahidi: Sahihi
Nashon: Mheshimiwa Jaji naomba Kupatiwa Exhibit P2
Nashon: ni Sahihi Kabisa kwamba Askari anayekuja na anayetoka lazima wasainishane kwenye Station Diary
Shahidi: Ni sahihi
Nashon: ni sahihi Kwamba inatajwa kwamba Nimemkabidhi, pamoja na Silaha na Majina ya Mahabusu
Shahidi: Nafahamu kwamba nitakwa la Kisheria
Nashon: na Kutaja Watuhumiwa na mali
Shahidi: Kwenye suala la Watuhumiwa sijafahamu
Nashon: uoni kwamba Station Diary Ingekuwa ya Muhimu Kuwepo Mahakamani
Shahidi: Siyo ya Umuhimu
Nashon: Pale Kituo cha Central Police Dar es Salaam, palikuwa na Askari Wengine wakati Wakina Kingai wanatoka MOSHI
Shahidi: Ndiyo palikuwa na Askari Wengine
Nashon: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Katika Askari Waliokuwepo Kituoni Hapakuwa na Askari Wengine ambao wangewachukua Maelezo Watuhumiwa?
Shahidi: Sikusema
Nashon: Je ulipata Kufahamu kama Kuna Ndugu au Wakili Waliokwepo wakati wanachukuliwa Maelezo
Shahidi: Hapana
Nashon: Je, kuna Ndugu au Mawakili walikuja kuwatembelea Washitakiwa
Shahidi: Hakuna
Mallya: Kwamba Kwa Madai yako ulikuwa Central Siku ya 07 August 2020
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kwamba Wakati huo ulikuwa umefanya Kazi kwa Muda gani
Shahidi: Mwaka 2014 Mpaka 2020
Mallya: Pale CRO Ulikaa mara ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Mallya: Kwa hiyo Ulishawahi Kufanya Kazi za General Duties Mara kadhaa
Shahidi: Sahihi
Mallya: Kwa huo Mwezi wa Saba pia Ulikaa pale CRO
Shahidi: Ndiyo, lakini Sikumbuki Mara ngapi
Mallya: Umesema Ushawahi Kufanya kazi Central, Nitafuti e Sehemu Nyingine Kwenye hicho Kitabu ambapo ukishawahi Kufanya Majukumu hayo
Shahidi: Tarehe 02 August 2020
Mallya: Mheshimiwa Jaji Utaangalia Wakati Unafanya Uamuzi Kwenye Serial Namba 184
Mallya: Wakati Unaandika wakati wa Kumtoa Mtu, Sababu inakuwa kweli au lah
Shahidi: Wakati amemtoa
Mallya: interest yangu Entry inayomuhusu Mshitakiwa Wa Pili, Wakati anamtoa aliandika nini
Shahidi: Nje kwa Upelelezi
Mallya: Jumanne anasema kwamba alimtoa Kwa sababu ya mahojiano, we umeandika sababu ya upelelezi
Shahidi: Ndiyo mahojiano ni sehemu ya upelelezi Mallya Kwa hiyo ni kitu kimoja, hicho
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Soma hapa na hapa..
Shahidi: NJE KWA UPELELEZI, NJE KWA MAHOJIANO
Mallya: Sasa ni kitu Kimoja
Shahidi: Hapana, Upelelezi ni Broad na Mahojiano ni Specific
Mallya: Kwa Uelewa kwako Wewe Maana yake nini
Shahidi: Mchakato unaotumika Kuanzia Kesi Imefunguliwa Mpaka Pale inapofikishwa Mahakamani
Mallya: Walikwambia Wanawatoa kwa Jambo gani
Shahidi: Mmoja kwa ajili ya Upelelezi na Mmoja kwa ajili ya Mahojiano
Mallya: aliyemtoa Mshitakiwa wa 3 ni nani
Shahidi: Inspector Mahita
Wakili wa Serikali: OBJECTION Kuhusu Utaratibu, unampomhoji Mtu, Basi Inukuliwe Maneno sahihi, Wakili azuiliwe Kuweka Maneno kwa Shahidi ambaye hayupo huku
Kibatala: OBJECTION tulishawahi Kuweka Utaratibu humu kwamba Objection itafanyika kwa Majibu siyo Maswali
Jaji: Una Kifungu cha Sheria Kinacho Kataza hilo
Wakili wa Serikali: naomba Dakika 1
Wakili wa Serikali: Sijakipata Kifungu Moja kwa Moja ila Mheshimiwa Jaji unapokuwa unamuhoji Shahidi Kwamba Fulani Alishasema kifu fulani hairuhusiwi na wewe unajua hilo
Jaji: Kanuni za cross Examination inasemaje
Mallya: Maswali ambayo yanamdhalilisha Shahidi, Maswali anayoulizwa Shahidi hapa hayamlengi Shahidi
Mallya: Sababu alizomtoa Mtuhumiwa Mahabus Central Ni pamoja na Kwenda Kumpiga
Shahidi: Hapana kwa ajili ya Upelelezi
Mallya: Ulikutwa na Diary hapa Mahakamani, na Jaji akasema wewe ni VIOLATOR
Shahidi: Mheshimiwa Jaji, Entry Namba 396 sababu ya Kumtoa, Tarehe na Muda na Mtu aliyemtoa Mtuhumiwa no. Tofauti na Kalamu iliyotumika au Mwandiko wangu uliotumika Kumuingiza Mtuhumiwa.
Mallya: Ulipata Kueleza Mahakamani?
Shahidi: Hapana
Mallya: Vifupi Vya Maneno kwenye Detention Register Mnaandika wenyewe au Ni kwa Mujibu wa Sheria
Shahidi: Mujibu wa PGO
Mallya: Ngoja nikuonyeshe PGO, naona DAR ES SALAAM kwamba CDS ni nini.
Shahidi: Inawekezakana ni Chuo Cha Polisi
Mallya: nakuonyesha Vituo Vya Polisi Vyote Tanzania na Vifupi Vyake Nionyeshe Walipo andika CENTRAL ni CDS
Shahidi: Anakodoa kwa Muda mrefu..
Mallya: nimetafuta sijaona, Sijui kama utapata Muda wa Kutosha
Shahidi: Mimi sijaona humu
Mallya: Sasa sisi ili tuamini kwamba hiki kitabu kitoke DSM Polisi Central tulitaka tuone kiandikwe ni POLICE CENTRAL DAR ES SALAAM au Kifupi Chake, Kwa Sababu kuna Kimoja Hakipo Sahihi
Shahidi: Detention Register ipo sahihi
Mallya: mie nataka nijue Kipi Hakipo Sahihi
Jaji: sasa katika ya PGO na DETENTION REGISTER kipi Kipo sahihi
Shahidi: siwezi Kusema Kwamba PGO Haipo sahihi
Jaji: Swali ni Kwamba Kipi hakiko sahihi
Shahidi: Hakuna ambacho Hakipo Sahihi
Mallya: Sasa Kuna Diary yako ulikamatwa nayo Mahakamani
Shahidi: sijakamatwa nayo
Shahidi: Niliandika Siku ya Kwanza kuja Kutoa Ushahidi Tarehe 20 September
Jaji: Ndiyo Siku uliyoandika
Shahidi: Hapana Kabla ya Siku ya Kuja Kutoa Ushahidi
Mallya: Kwa Uwezo wa Pale Central na rasilimali zake Ukoje
Shahidi: Hayo sasa Watakuwa Kuzungumzia watu wa Utawala
Mallya: Kwa Ufahamu Wako wewe Ukishawa Kuishiwa Karatasi Pale Central za Kuandikia Maelezo
Shahidi: Hapana
Dickson Matata: Nitakuhoji Maswali Machache Kutokana Maelezo uliyoyatoa Hapa Mahakamani, Kutokana ana Wateja wetu Kupinga kwamba hawakuwa hi Kuandika Maelezo na hawajawahi Kufika Central Dar es Salaam. ulisema Kituo chako Cha Kwanza Kuanza Kazi ni wapi
Shahidi: Msimbazi
Matata: Msimbazi ipo wapi
Shahidi: Wilaya ya Kipolisi Kariakoo
Matata: Kuna sehemu yoyote ulitaja Kiongozi uliyewahi Kufanya naye kazi Pale Msimbazi
Shahidi: Sijazungumzia
Matata: Ukiachana na Kutaja Majina yako na Force Namba zako, Kuna Ushahidi wowote Umeonyesha kwamba Uliwahi Kufanya kazi Central Police Dar es Salaam
Shahidi: Ndiyo nimeleta Detention Register Yenye Muandiko wangu Mimi
Matata: Kuna Kitu chochote umeleta Mahakamani mabpo kwa Kuangalia DR tunaweza Kusema huu ni Mwandiko wako
Shahidi: Kimya
Matata: twende sasa Kwenye DR, Mheshimiwa Jaji namuonyesha Kuanzia Entry namba 393
Matata: Nenda tarehe Saba, Kuna Sahihi yako hapo Kwenye hizo Entry?
Shahidi: Hakuna
Matata: Kuna sehemu Yoyote yenye Force Namba yako hapo?
Shahidi: Hakuna
Matata: nikisema Mtu yoyote anaweza Kuandika, kilichoandikwa hapa nitakuwa nakosea
Shahidi: utakuwa unakosea
Matata: Kuna Kitu Kingine chochote kinachoonyesha kwamba Detention Register Imetoka Polisi Central Dar es Salaam Na siyo Mbweni
Shahidi: Kitu Pekee ni hiyo CD
Matata: ni sahihi Kwamba Mwaka huu Ndiyo umeanza Kufanya kazi Oysterbay Polisi
Shahidi: Ndiyo Mwaka huu
Matata: Pale Central Mmesema Mnatumia CD. Je, Oysterbay Mnatumia nini?
Shahidi: OB
Matata: hiyo OB inatoka inatokana na nini
Matata: PGO namba 05 ndiyo inazungumzia Vifupisho Vya Vituo Vya Polisi. Hebu Soma haoa
Shahidi: Oysterbay Inasema ni OYB
Matata: Kuna Kitabu au Mwongozo Umekuja nao hapa Unaonyesha Oysterbay ni OB na siyo OYB?
Shahidi: Hapana
Shahidi: Kimya
Kibatala: ile Diary Uliyo kuwa nayo Kwenye Kizimba, sehemu Mahususi ambazo zinahusika na Kesi hii zimeingia Kama Kielelezo Cha Mahakama namba 1
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Siku hiyo ulikuwa wapi
Shahidi: Sikumbuki nilikuwa wapi
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Vitu vilivyochukuliwa kwenye Diary Yako vinahusiana na Kesi hii na Ushahidi wako Shahidi: Ndiyo Vinahusiana
Kibatala: na Unafahamu Kwamba Mahakama Imechukua Kurasa Kwenye Diary Yako Kabla ya wewe Kuja Kutoa Ushahidi Leo
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je Ulifafanua kwa Jaji Wakati wa Kuongozwa na Wakili wa Serikali Kwamba Kuna Kidhibiti namba Moja Mule Kuna 1,2,3 na Maana yake ni nini
Shahidi: sijafafanua
Kibatala: kwa sababu hujafafanua, Je unafahamu Kwamba ulifafanua wakati wa Re Examination
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Basi Kama hufahamu, mkijaribu tutasimama
Kibatala: Shika Kielelezo namba P1 Muonyeshe Mheshimiwa Jaji, Ni wapi Pameandikwa CENTRAL POLICE STATION DAR ES SALAAM
Shahidi: Hakuna
Kibatala: kwa hiyo ili Mahakama iijue Kwamba Kielelezo hiki Ni Cha Central lazima iingie Kwenye Details za Ndani
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mojawapo ya Vifaa kazi Vya Utambuzi ni PGO
Shahidi: Ndiyo PGO
Kibatala: Kingine kipi
Shahidi: miongozo ya Jeshi la Polisi huwa Inatolewa
Kibatala: Ni lini umefahamu Kwamba Unakuja Kutoa Ushahidi wa Kesi Ndogo ya Mohammed Ling'wenya
Shahidi: Sikumbuki Tarehe, ila kama Siku 13 Nyuma
Kibatala: Toka unapokea Summons, ni lini Ulifanya Maandalizi ya Kuleta Muongozo
Shahidi: sijaleta Muongozo
Kibatala: Kuna Mtu yoyote alikuzuia kuleta
Shahidi: Hapana
Kibatala: Kingine ni Kitu gani
Shahidi: Police auxiliary Act
Kibatala: Kifungu gani
Shahidi: Kimya
Kibatala: Katika Kielelezo P1 hapo Katikakati ni nini hicho
Shahidi: Mheshimiwa Jaji ni pini iliyodondokea kwa Bahati Mbaya katika Ukurasa unaowahusu Washtakiwa hawa
Kibatala: Ulifafanua kuhusu hiyo pini
Shahidi: SiKufafanua
Kibatala: hiyo tarehe 07 August 2020 ulipokea Zamu kutoka kwa nani na nani
Shahidi: aliyepokea Zamu ni Afande Fatuma
Kibatala: Kwahiyo wewe humfahamu hata Askari Mmoja kati ya wale uliowapokea
Shahidi: Siwakumbuki
Kibatala: Ulipotoka Duty uliwakabidhi Askari nani na nani
Shahidi: aliwakabidhi Afande Fatuma, miye siwajui
Kibatala: Imakama Maana yake nini
Shahidi: Miye sikumbuki
Kibatala: Kuna Mpango Kazi Unaonyesha Askari Fulani anakaa wapi na nani anaenda wapi
Shahidi: Ndiyo upo
Kibatala: na wewe Mpaka Unakuja Kutoa Ushahidi, hujaleta sehemu ya Mpango kazi
Shahidi: Kimya
Kibatala: Unamfahamu Mtu anaitwa Lembrus Mchome
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: anasema Kwamba Mwaka Jana Mwezi wa Tano Ulimpokea Oysterbay Polisi Ukiwa CRO
Shahidi: Simkumbuki
Kibatala: ana sababu gani za kukusingizia
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: hiyo Siku ya tare 07 August 2020, Wakati Unampokea Mohammed Abdilah Ling'wenya alikuwa na Karatasi yoyote
Shahidi: Sikumkuta na Chochote
Kibatala: Wakati Unaongozwa ulipata Kuzungumzia Kuhusu Seizure Certificate
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Je Exhibit zinatunzwa wapi kama Mtu akikutwa navyo
Shahidi: Kwa Mtunza Vielelezo
Kibatala: Walikuongoza Kuzungumzia Kuhusu Vielelezo vya Mohammed Ling'wenya
Shahidi: Kimya
Kibatala: Mtunza Vielelezo anaitwa nani
Shahidi: Sikumbuki ni Siku Nyingi sana
Kibatala: ulisema Mohammed Ling'wenya alichukuliwa Maelezo Kwenye Ofisi ya OCS, umesema kwa Jaji nani alifungua Mlango
Shahidi: Sikusema Kibatala: Ulimweleza Jaji Kuwa OCS alikuwepo wapi
Shahidi: Sikusema
Kibatala: nani alikuwa Custodian wa Detention Register
Shahidi: mimi
Kibatala: Wakati unasema Ulimsindikiza ASP Jumanne, ulisema Detention Register Ulimuachia nani
Shahidi:
Kibatala: Kuna sehemu nilisikia Unasema Ulitambua Barua ya Naibu Msajili kwa Sababu ya Sahihi yake, we Unaifahamu Sahihi ya Naibu Msajili?
Shahidi: Siyo Familiar Sana
Kibatala: Wakati Barua hii inasainiwa ulikuwepo
Shahidi: Sikuwepo
Kibatala: Wakati Mnapeana Barua hii Sisi tulishirikishwa?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji sehemu gani katika hii Barua umesaini Kwamba Ulipokea wewe
Shahidi: sijasaini
Kibatala: nilisikia Kuna sehemu Walikusainisha Je Umekuja na hicho Kitabu Ulichosaini
Shahidi: Hapana
Kibatala: Soma hii Barua ilivyoandikwa Kwa naibu Msajili, Kuna Jina lako
Shahidi: Hapana
Kibatala: Sasa Naibu Msajili alijuaje wewe unahitaji Kielelezo
Shahidi: Sijui yeye
Kibatala: Soma kwenye Barua Mlipeana Kielelezo gani
Shahidi: TP 1
Kibatala: Unafahamu Kwamba Kwa Mujibu wa Jaji Mkuu, Vielelezo Vyote vinatakiwa kuanza na P na siyo TP
Kibatala: Unajua kwa nini tulipinga hii Barua Kupokelewa
Kibatala: tulipinga Mahakama Kuitwa kama Shahidi Kibatala: kwa Ruhusa Ya Mahakama, kesi Inayomuhusu Mohammed Ling'wenya, alitolewa Nje kwa nini
Shahidi: Kwa Upelelezi
Kibatala: Eleza Sasa ni Wapi ulifafanua kwamba Nje kwa Upelelezi ina Manisha nini
Shahidi: Sikumbuki
Shahidi: Kimya
Kibatala: Nje kwa Upelelezi na Nje kwa Mahojiano ni sawa
Shahidi: Hazifanani lakini ni Kitu Kimoja
Kibatala: Unafahamu Kwamba Kidhibiti Kinatakiwa kijielezee chenyewe
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Kuna PPR namba, Mueleze Mheshimiwa Jaji Maana yake nini
Shahidi: Kimya
Kibatala: Je Nakala ya Ling'wenya Ya Seizure Certificate for na fall Kwenye PPR namba
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Ulitoa Ufafanuzi hapa Kwenye Kitabu Kuna DASH Kwenye PPR namba
Shahidi: Ndiyo ipo
Kibatala: Ulitoa Ufafanuzi Kwa Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba hii Detention Register inaishia lini
Shahidi: Tarehe 12 August
Kibatala: Kama Mke wa Ling'wenya alikuja Polisi Central Station alikuja Polisi Station, kwa Kitabu hiki angeambiwa yupo wapi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: kama Mke wa Ling'wenya Alikuja Central na haukumuona kwenye Daftari itakuwa nini?
Shahidi: Sijui
Kibatala: Nimesikia Kwamba Mnaulizana na Mallya kuhusu Mwandiko. Je, Ulitoa Kitu Kingine Chenye Mwandiko wako tuweze Kulinganisha?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Physical Condition ni sawa na Health Conditions?
Shahidi: ni Tofauti
Kibatala: Wakati unaweka Entry za Ling'wenya Kingai na Timu yake walikuwepo
Shahidi: Kingai alikuwa mbali ila timu yake walikuwepo
Kibatala: ulifanya Upekuzi Maungoni kwa Ling'wenya
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Nani alikwepo
Shahidi: Afande Fatuma
Kibatala: Kwa hiyo ni Ushahidi Wako Kwamba Ulifanya Upekuzi Wako Mbele ya Afande Fatuma
Shahidi: Ndiyo Nilifanya
Kibatala: Shahidi wako Mwingine ni nani
Shahidi: TIMU nzima iliyokuwa CRO
Kibatala: Majina ya Ling'wenya uliyapata Kutoka kwa nani
Shahidi: Kwa wao wenyewe
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kulikuwa na Alternative Facilities za Kuwasiliana na ndugu zake Ling'wenya?
Shahidi: Hapa Sijamwambia
Kibatala: Unaifahamu station Diary
Shahidi: Ndiyo PF 51
Kibatala: Umetoa hapa Mahakamani
Shahidi: Sijaja na Station Diary
Kibatala: ulitaja kwa Mheshimiwa Jaji Kwamba nani alikupa DR
Shahidi: Sikutaja
Kibatala: Ulitaja Mtu aliyekupa
Shahidi: Sikutaja
Kibatala: Kwani hii ni Mali yako au Mali ya Jeshi la Polisi
Shahidi: Mali ya Jeshi la Police
Kibatala: Entry ya Ling'wenya Ipo wapi
Shahidi: 392
Kibatala: Na Imeacha Kutumika lini
Shahidi: 12 August 2020
Kibatala: Fungua Entry namba 208.. Tarehe ngapi?
Shahidi: hapasomeki
Kibatala: Mie nakwambia Mwaka 2021
Shahidi: Hapana Hapasomeki
Kibatala: Miye na kwambia Mwaka 2021
Shahidi: Hapana Hapasomeki
Kibatala: Fungua tena Entry 114
Shahidi: 30 July 2021
Kibatala: Entry 113
Shahidi: Haisomeki
Kibatala: Fungua Entry namba 156, 03 August 2021
Kibatala: Unafahamu Kwamba hiki Kielelezo kinapimwa pia Kwa Uongo wake
Kibatala: Nakuonyesha Entry inayomuhusu Ling'wenya, Aliingia Saa 06:07hrs, Wakati anatoka 08:10, kuna au hakuna Hours?
Shahidi: Hakuna Hours
Kibatala: wakati Unaongozwa na Hila ulifafanua Shahidi Sikumbuki
Kibatala: Katika Entry ya Ling'wenya Kuna Dole Gumba, Mwambie Mheshimiwa Jaji Kama Ulifafanua Kuwa Dole Gumba la Nani
Shahidi: Sikufafanua
Kibatala: Mheshimiwa Jaji sina swali lingine naomba Kurudisha Kielelezo namba P2
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Tumekaa Mfukilizo tangu Asubuhi, Ikikupendeza tunaomba tupate Health Break Jaji Utetezi
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Sisi tunapinga, Tunapinga Tunahisi Muda huo utatumika Kumfundisha majibu Shahidi
Wakili wa Serikali: Hoja iliyotumika ni tuhuma Jaji: kasema ana wasiwasi tu
Wakili wa Serikali: Basi tunaomba tupate Health Break
Jaji: Wote tulikwepo humu ndani na Hasa Mimi, mimi napata Ugumu kumfungia Sehemu asifundishwe Majibu
Mallya: tusaidie, najitolea Kukaa naye na nitakula naye
Jaji: basi naelekeza Hilla, Mallya na Shahidi Mkae pamoja
Mallya: Pius Hilla tujawahi Kula pamoja
Jaji: basi Leo Mtakula pamoja kwa Amri ya Mahakama
Jaji: na Kama Watachukua Nusu saa basi Break iwe lisaa lizima
Jaji anatoka
Jaji amerejea
Mahakamani Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa tena
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Ikupendeze Mheshimiwa Jaji, uwakilishi Upande wa Jamhuri Una marekebisho Kidogo
Tungeomba Mahakama Iridhie Kuwaingiza Kwenye Quorum Wakili wa Serikali Robert Kidando na Wakili wa Serikali Abdallah Chavula, Wengine tupo Kama tulivyo kuwa awali..
Wakili Peter Kibatala: Kwa Upande wa Utetezi Quorum ipo kama tulivyo kuwa awali na tupo tayari Kuendelea
Wakili wa Serikali, Pius Hilla: Shahidi Sasa Nitakuuliza Maswali Kwa ajili ya Ufafanuzi Kufuatiwa na yale waliyokuuliza Mawakili Wasomi
Wakili wa Serikali: Umeulizwa Kwamba Washitakiwa Wakana Kwamba Hawajafikishwa Central hebu fafanua hufahamu nini
Shahidi: sikuwa nafahamu kama, Lakini Mimi ndiye niliyewapokea na Nikawa Detain.
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Kuwa Supplied na Kielelezo Cha Mahakama.
Wakili wa Serikali: Shahidi Uliulizwa Swali hukusiana na hawa Watuhumiwa Kutolewa Nje, Kwa Mahojiano na Kwa Upelelezi, Ifafanulie Mahakama
Uliposema Kwamba Mahojiano ni sehemu ya Upelelezi
Shahidi: Upelelezi Unajumuisha Kuwa Mtuhumiwa alitolewa atahojiwa, atarekodiwa naninavyo fahamu Mimi Mahojiano ni pale Mtuhumiwa anapotolewa Nje Specific kwa kwenda Kuhojiwa
Wakili wa Serikali: Ukasema Kwa Kusoma Kuna Utofauti, Je Utofauti wake nini
Shahidi: Kwamba Mahojiano ni tofauti na Upelelezi lakini Mahojiano ni Sehemu ya Upelelezi
Wakili wa Serikali: Kuna Swali Mallya alikuuliza Kwamba Mahita aliwatoa watuhumiwa kwenda Kuwapiga, Ukasema Siyo Kweli, Je Ulimaanisha nini
Shahidi: Kwa sababu Afande Mahita hakumtoa Kwa Sababu ya Kumpiga na Kupiga siyo Sehemu ya Upelelezi
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Maswali Mengi Mengi Kuhusiana na Abbreviation CDS na CD ukaonyeshwa na PGO Ukasema DR haina Makosa na PGO haina Makosa, Je Kule Central CD ni Kifupisho cha Neno gani
Shahidi: CD Kifupisho cha CENTRAL DAR ES SALAAM, haipatikani Kwenye Kifupisho cha Kituo chochote pale Tanzania Nzima WS: Uliulizwa pia Kuwa Kituo chako Cha Kazi Msimbazi na pia Kitu gani Kinathibitishwa Kwamba Ulifanya Central
Shahidi: Kwa hapa ni D. R ambayo Kifupisho chake uwezi kukioata Sehemu Yoyote Tanzania na Kwamba Mimi ndiye niliyejaza
Wakili wa Serikali: Ulionyeshwa Specific Kwenye Entry namba 393 Ukasema Hakuna Sahihi yangu wala Jina langu, Je Ni kitu gani Kitaonyesha wewe Umewahi Kufanya kazi Central
Shahidi: Entry Inaonyesha Mtuhumiwa alichukuliwa na Afande Kingai
Wakili wa Serikali: Nini Kinaonyesha Kwamba Ulikwepo Siku Ile
Shahidi: Uwepo Wa Mwandiko wangu
Wakili wa Serikali: Kwenye swali hilohilo Ujafafanua Kwamba Siyo Mtu yoyote anaweza a kuandika hicho kitabu
Shahidi: Siyo watu wote waweza...
Wakili wa Serikali: Jikite kwenye Entry namba 393
Shahidi: Siyo Mtu yoyote anaweza Kupata namba ya Kesi, Kupata details za Watuhumiwa
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali hapa kuhusiana na PIN kukutwa Katikati, Ukajibu kwamba HAIKWEPO. Ifafanulie Mahakama haikwepo Wakati gani
Shahidi: Wakati natoa Ushahidi Mara ya kwanza
Kibatala: OBJECTION swali lilikuwa alifafanua au hakufafanua..
Wakili wa Serikali: PIUS HILLA Mheshimiwa Jajiiye nilisikia Jibu la Pin haikwepo na Nataka Kufafanua
Jaji: alitoa hilo Jibu lakini wakili akasema halitaki
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali Ukasema Huku fafanua, kwakuwa PIN ndiyo Umeonyeshwa Ieleze Mahakama ni Pin ya namna gani
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Ni Kipande cha Pin ipo Katikati katika Ukurasa WA Mohammed Ling'wenya, Ndiyo Maana Nika fafanua haikuwepo.. Mheshimiwa Jaji naomba Kupewa P1, (Barua).. Mheshimiwa Jaji naomba Kumuonyesha shahidi
Wakili wa Serikali: Kwa Mujibu wa hiyo Barua ni Kitu gani unaitambua
Shahidi: nilikuwa namkabidhi wa Detention Register
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Shahidi Ulicho kuwa unakabidhiwa kwa Mujibu wa hiyo Barua ni Kitu gani
Shahidi: Detention Register
Wakili wa Serikali: Lipo swali lingine Uliulizwa Kuhusiana na Physical Condition Na Ukasema Hakuna Entry ya Health Condition, Ukasema Kwenye D. R hakuna Sehemu ya Health Conditions ulikuwa unamaanisha nini
Shahidi: sehemu tuliokuwa tunatumia Physical condition Kuandika kwenye Detention Register
Wakili wa Serikali: aliuliza wakili kwamba Mtu aliye kutishia akiwepo atakuwa na hofu
Shahidi: Ndiyo aliuliza kwamba Mtu aliye kutishia akiwepo Tishio Kinaendelea? Nikajibu ndiyo
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusu D. R Ukasema DR ni Mali ya Polisi, Ulimwambia kuwa Unamanisha nini
Shahidi: Nilienda Kumuomba Mkuu wa Kituo, Kwamba Natakiwa kutoa Ushahidi, akanisainisha kwenye Station Diary
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Hatuna Maswali
Jaji: Shahidi Nakushukuru Kwa Ushahidi Wak
Jaji: Kuna Shahidi Mwingine?
Wakili wa Serikali: Pius Hilla Kwa Leo Hatuna Shahidi Mheshimiwa Jaji, ambaye yupo tayari Kuingia Kwenye Kizimba cha Ushahidi, Tunaomba Usikilizwaji uhairishwe kwa Leo hadi Kesho Tarehe 23 November 2021 ambapo tutaleta Shahidi Mwingine
Jaji: Utetezi
Kibatala: hatuna pingamizi Mhe. Jaji ukizingatia na muda
Jaji: Kufuatia maombi ya hairisho Mahakama inahairisha mpaka kesho saa 3 asubuhi, upande wa mashtaka wanaelekezwa kuleta mashahidi, watuhumiwa wataendelea Kuwa chini ya magereza mpaka kesho asubuhi saa 3 Jaji anatoka