Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,813
- 4,544
Salaam Wakuu,
Leo tarehe 16/11/2021 kesi ya Mwenyekiti wa CHEDEMA Freeman Mbowe inaendelea.
Kujua jana kesi ilipoishia, soma: Yaliyojiri kesi ya Freeman Mbowe na wenzake Nov 15,2021
Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
UPDATES;
- Jaji ameingia Mahakamani..
- Kesi inatajwa..
Wakili wa Serikali: Robert Kidando anatambulisha Jopo la Mawakili wa Serikali..
1. Jenitreza Kitali
2. Abdallah Chavula
3. Pius Hilla
4. Nassoro Katuga
5. Esther Martin
6. Tulimanywa Majige
7. Ignasi Mwinuka
Wakili Peter Kibatala anatambulisha Jopo la Mawakili wa Utetezi..
1. Jeremiah Mtobesya
2. John Mallya
3. Seleman Matauka
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Uamuzi Mdogo
Peter Kibatala Mheshimiwa Jaji na sisi tupo tayari Kupokea Malekezo
Jaji: Jana nilihairisha shauri Jana Jioni, nikasema Nitasoma uamuzi leo... Lakini kutokana na wingi wa hoja naomba muda zaidi mpaka kesho.. Nikakamilishe kuandika uamuzi... Naomba radhi kwa hairisho hili ambalo hatukulitarajia wote..
- Mawakili wa pande zote wanasimama kukubaliana
Jaji: kama nilivyosema kwamba nahairisha shauri mpaka Kesho, UPANDE WA MASHTAKA MTAMLETA SHAHIDI ATAKAA KIZIMBANI NA ATAENDELEA KUTOA USHAHIDI Nahairisha mpaka kesho saa 3 asubuhi.
- Jaji anatoka!
Kooooooooooortiiiiiiiiii..
===
Kesi ya ugaidi inayomkabili mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu imeahirishwa hadi kesho kutokana na kutokukamilika kuandikwa uamuzi kuhusu uhalali wa shahidi wa Jamhuri anayedaiwa kupanda kizimbana akiwa na diary, simu na kalamu
Akitoa uamuzi huo leo Jumanne Novemba 16, 2021 Jaji Joachim Tiganga amesema ameshindwa kukamilisha kuandika uamuzi huo kutokana na wingi wa hoja zilizotolewa na mawakili wa pande zote.
Jana yaliibuka malumbano ya kisheria katika mahakama hiyo kuhusiana na uhalali wa shahidi kupanda kizimbani akiwa na diary, simu na kalamu.
Upande wa utetezi unadai kuwa shahidi huo alikuwa anatumia vifaa hivyo wakati akitoa ushahidi wake Ijumaa, jambo wanalosisitiza kuwa ni kinyume cha sheria na utaratibu.
Chanzo: Mwananchi
Leo tarehe 16/11/2021 kesi ya Mwenyekiti wa CHEDEMA Freeman Mbowe inaendelea.
Kujua jana kesi ilipoishia, soma: Yaliyojiri kesi ya Freeman Mbowe na wenzake Nov 15,2021
Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
UPDATES;
- Jaji ameingia Mahakamani..
- Kesi inatajwa..
Wakili wa Serikali: Robert Kidando anatambulisha Jopo la Mawakili wa Serikali..
1. Jenitreza Kitali
2. Abdallah Chavula
3. Pius Hilla
4. Nassoro Katuga
5. Esther Martin
6. Tulimanywa Majige
7. Ignasi Mwinuka
Wakili Peter Kibatala anatambulisha Jopo la Mawakili wa Utetezi..
1. Jeremiah Mtobesya
2. John Mallya
3. Seleman Matauka
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Uamuzi Mdogo
Peter Kibatala Mheshimiwa Jaji na sisi tupo tayari Kupokea Malekezo
Jaji: Jana nilihairisha shauri Jana Jioni, nikasema Nitasoma uamuzi leo... Lakini kutokana na wingi wa hoja naomba muda zaidi mpaka kesho.. Nikakamilishe kuandika uamuzi... Naomba radhi kwa hairisho hili ambalo hatukulitarajia wote..
- Mawakili wa pande zote wanasimama kukubaliana
Jaji: kama nilivyosema kwamba nahairisha shauri mpaka Kesho, UPANDE WA MASHTAKA MTAMLETA SHAHIDI ATAKAA KIZIMBANI NA ATAENDELEA KUTOA USHAHIDI Nahairisha mpaka kesho saa 3 asubuhi.
- Jaji anatoka!
Kooooooooooortiiiiiiiiii..
===
Kesi ya ugaidi inayomkabili mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu imeahirishwa hadi kesho kutokana na kutokukamilika kuandikwa uamuzi kuhusu uhalali wa shahidi wa Jamhuri anayedaiwa kupanda kizimbana akiwa na diary, simu na kalamu
Akitoa uamuzi huo leo Jumanne Novemba 16, 2021 Jaji Joachim Tiganga amesema ameshindwa kukamilisha kuandika uamuzi huo kutokana na wingi wa hoja zilizotolewa na mawakili wa pande zote.
Jana yaliibuka malumbano ya kisheria katika mahakama hiyo kuhusiana na uhalali wa shahidi kupanda kizimbani akiwa na diary, simu na kalamu.
Upande wa utetezi unadai kuwa shahidi huo alikuwa anatumia vifaa hivyo wakati akitoa ushahidi wake Ijumaa, jambo wanalosisitiza kuwa ni kinyume cha sheria na utaratibu.
Chanzo: Mwananchi