Kwahiyo kwakua msiba ni wa Arusha na wanao fariji wawe wa urusha.kwani Arusha hakuna wasanii? hizo nyimbo mnazotaka zikishaimbwa wazazi na walezi ndio watapata watoto wao?? acheni SIASA ktk MSIBA
Waombolezaji wa post wamegeukia malimbano.update ndo zmefka kikomo jaman?
Kweliii! Ata amolapa sijamuona au ana nauri?Tumepatwa na msiba ila cha kushangaa sijaona wasanii wetu kutunga wimbo wa maombolezo ni watu wa ajabu sana nyie wasanii. mnashindwa hata kutunga nyimbo za maombolezo kumbukeni mulipo pata matatizo kama kutekwa tulikuwa pamoja
Mkewe kafanyiwa IVF walivyoenda marekani...sasa hivi yuko south analea mimbaOoh nilikua sijui kama hana mtoto
Kwahiyo hana vyeti na pia hana mtoto, okay sawa.
acheni hzo nyimbo nying tu zimetungwa na kuimbwa na wasanii weng tu,wakiwemo bongofleva artists na gospel,sema hamjaskiza radio.au mlitaka wapige live pale uwanjani,wakat watu wakiomboleza?Kweliii! Ata amolapa sijamuona au ana nauri?
Tulitegemea ilo,,,Vp cocochanel hujamuona hapo mkuu
Watarudi naye kule nini!
Mkuu una mambo ya kitoto kweli aisée!AYI MAMA MWANANGU.
Kilio hiki kilio, siwezi kukizuia,
Siyo langu kusudio, kalele kuwapigia,
Sababu kuna tukio, lafanya miye kulia,
Ayi mwenzenu mwanangu, leo ametangulia.
Machozi jama machozi, sina yameniishia,
Ila mwenzenu majonzi, bado yamenizidia,
Hata kusema siwezi,nabaki nagugumia,
Ayi mwenzenu mwanangu, leo ametangulia.
Msiba huu msiba, wenzangu nawaambia,
Umekuwa kama mwiba, kooni ulonasia,
Jama wanipa adhaba, nashindwa ivumilia,
Ayi mwenzenu mwanangu, leo ametangulia.
Mkaja ule mkaja, bado naukumbukia,
Damu nyingi zilovuja, mwana nikijazalia,
Musidhani naleleja, uchungu 'menirudia,
Ayi mwenzenu mwanangu, leo ametangulia.
Ajali hizi ajali, hadi lini Tanzania?
Lawama kwa serikali, kwa macho kuwafumbia,
Madereva makatili, leseni kuwaachia,
Ayi mwenzenu mwanangu, leo ametangulia.
Mkanda jama mkanda, mwana hakuutumia,
Dereva pamwe na konda, lawama nawatupia,
Wangewafunga mikanda, kabla ya gia kutia,
Ayi mwenzenu mwanangu, leo ametangulia.
Milanga jama milanga, miongo karne pia,
Izidi mbele kusonga, mwana ulipo sikia,
Hakuna wa kunipinga, moyoni utasalia,
Ayi mwenzenu mwanangu, leo ametangulia.
Tamati sasa tamati, wino umeniishia,
Nilivyo nusu kaputi, kifo ninasubiria,
Nasema haya kwa dhati, duniya nawaachia,
Ayi mwenzenu mwanangu, leo ametangulia.
...t...a...m...a...t...i..
Share shairi hili mara nyingi uwezavyo.
Mpumzike kwa Amani watoto wetu.
07 Meyi 2017 Jumapili 12:29Pm
[HASHTAG]#JiniKinyonga[/HASHTAG]
Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
Call/whatsp 0622845394 Morogoro.